Jinsi ya connect simu yako na Computer/ laptop kwa kutumia Xender

Vincenzo Jr

Platinum Member
Joined
Sep 23, 2020
Posts
24,262
Reaction score
58,728
1. Washa hotspot yako ili uweze kuunga simu yako na computer/ laptop hii ni free haihitaji kuwa na data/ bando kwenye simu yako

2.ingia kwenye Xender yako gusa neno Connect to PC itakupeleka sehemu hii hapo picha ya pili kwa chini


3.Kuna number hapo kwenye steps 3 izo ni web address unatakiwa uandike kwenye browser ya PC yako

4. Ingia kwenye web browser ya Pc. (Tumia Microsoft Edge).

Ingiza ile web address [192.168.....] bila kukosea hata nucta kwenye Microsoft edge.

Hizi utaziandika sehemu ya kusearch address juu.

Kisha utabonyeza "Enter"

utaletewa notification ya kuruhusu Pc ku-access simu yako

5.Utaingia kwenye simu kisha utaruhusu kwa kubonyeza "Accept"

Kisha itakuwa imesha-connect.

6. Hapo ishakuwa connected kama unataka kuweka picha utaweka kwenye picha kama unataka kuweka movie utaweka kwenye movie kama kwenye audio ni audio

Muhimu:

Kumbuka process zote hizi hazitumiii Mb's wala bundle la aina yeyote, hivyo unapoconnect Hotspot ya simu yako na Pc hakikisha uwe umezima data ya simu yako.

Na ukiconnect Pc yako itakwambia "wifi connected without network"

_____________

Tulia, soma steps taratibu✌️
Picha za juu credit by me
Picha za chini
Credit by njiwa flow
 
Hii njia nimeitumia sana, ni namna gani naweza unganisha simu yote kabisa, maana yangu kuwa kila nachofanya kwenye simu kiwe projected kwenye Pc?
 
Njia ngumu sana hiyo ya Xender... The easiest way ni kutumia FTP Server kushare files za simu yako na PC yaani hauhitaji hata MB au chanzo cha data chochote zaidi ya WiFi na Hotspot


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…