FORCE NAMBA
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 937
- 327
Nimeipenda hiyooo!!!!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimejaribu kupita njia zote but nikianza kuroot inaishia 16% alafu inafeli na kuniambia "no strategy now". Msaada wapi nakoseaJinsi ya ku root simu yako ya Android.
Utangulizi:
Simu zetu za Android zimekua sehemu ya Maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia katika Mawasiliano, Kuhifadhi kumbukumbu za muhimu, burudani, biashara, nk. Haya yote hufanywa na Program ambazo huwekwa kwenye mfumo wa simu (Operating System). Programu hizo hubeba maaginzo maalum (Set of instructions) ambazo humwezesha mtumiaji kufanyia mambo mbalimbali kutegemea program hio. Mfano wa program muhimu kwenye simu ni kama vile Opera Mini (humwezesha mtumiaji kufungua kurasa mbalimbali za Intaneti), Calculator, nk.
Program hizo huwekwa sio tu kwenye simu, bali hata vifaa vingine kama vile Computer. Mtumiaji wa Simu au Computer ndie anaeamua program ya kuweka kutegemeana na matumizi yake. Katika miongo michache iliopita zimetengenezwa program nyingi mpya na zenye maboresho makubwa na ya kisasa. Ubunifu uliopo katika program mbalimbali unaleta ukuaji katika Nyanja mbalimbali katika maisha yetu ya kila siku. Program hizi pia zimeleta urahisi na ufanisi. Mfano Calculator, Saa, Vitabu Vitakatifu (Biblia na Kuran), Kamusi, Camera, nk.. vyote vimetengenezewa PROGRAM na kuwa rahisi kuvitumia katika simu muda wowote, mahali popote.
SASA TUJE KWENYE MADA;
Android ni Mfumo wa simu (Operating System) ambao unaboreshwa siku hadi siku. Mfumo huu una majina tofauti kutegeana na toleo lake. Haya ni Matoleo (Versions) mbalimbali ya Android kuanzia ya kwanza mpaka ya mwisho;
1. Cupcake (1.5)
2. Donut (1.6)
3. Éclair (2.0 2.1)
4. Froyo (2.2 2.2.3)
5. Gingerread (2.3 2.3.7)
6. Honeycomb (3.0 3.2.6)
7. Ice Cream Sandwich (4.0 4.0.4)
8. Jelly Bean (4.1 4.3.1)
9. KitKat (4.4 4.4.4)
10. Lollipop (5.0 5.1.1)
Matoleo haya huboreshwa kadri yanavyozidi kutolewa. Kujua toleo la simu yako nenda Settings About phone Android Version. Ukikuta Jelly Bean, KitKat au Lollipop hongeara! kwani unatumia matoleo ya mwisho yalioboreshwa!!
Mfumo huu wa Android unafaa kufanyiwa settings mbalimbali na kuwekewa Program mbalimbali ili kumfanya mtumiaji aifurahie simu yake kwa asilimia 100, lakini shida huja kwamba sio kila PROGRAM inayowekwa katika mfumo huu wa Android inakubali kufanya kazi!! Wapo watengenezaji wengi wa program (Software Designers) ulimwenguni. Sasa watengenezaji wa mfumo huu wa Android wamezuia Program ambazo hazijatoka kwao zisifanye kazi kwenye mfumo huo kwa sababu za kimaslahi.
HAPA SASA TUTAPATA KUELEWA MAANA YA KU ROOT kua ni kuifanya simu ikubali Program zilizozuiwa na watengenezaji wa Android (Android Developers). Ukishai root simu yako sasa utakua na uwezo wa kuweka program zinazohitaji root permission kwenye simu yako.
JINSI YA KU ROOT SIMU YAKO.
Kuna aina za simu ni rahisi sana ku root, lakini nyingine zinahitaji utafiti wa kina na muda wa kutosha. Zipo program nyingi sana zinazoweza kutusaidia zoezi hili. Mojawapo ya Program ambazo zinajulikana sana kwa ku root simu ni kama vile KingRoot, Vroot, Kingoapp Root, SRSRoot, Framaroot, Root Master, z4root, Universal root, Easy root, nk.. Baadhi ya Program hizi zitahitaji Computer, nyingine hazihitaji.
Katika Makala hii tutaelekeza kwa kutumia Program iitwayi KingRoot ambayo inakubali kufanikisha zoezi hili kwenye asilimia kubwa ya simu za Android. Program hii haihitaji Computer. Kuipata nenda Google kisha I isearch na kui download. Kwa msaada uliza
Maandalizi:
(i) Charge Simu yako, angalao ijae kwa 50%
(ii) Wezesha Developer Options kwenye simu yako. Menu hii imefichwa kwa watumiaji wa kawaida. Sisi tunataka kutumia simu zetu kwa 100%. Sasa kuifichua nenda Settings>About phone>Build number. Baadhi ya simu (LG na HTC) nenda Settings>About phone>Software information>Build number. Ukishafika kwenye Build number gusa hapo mara saba (tap 7 times) mpaka uambiwe You are now a Developer
(iii) Sasa nenda Settings>Developer options>USB debugging. Weka tiki hapo (kama haipo)
(iv) Nenda settings>Security>Unknown Sources. Weka tiki hapo (Kama haipo).
Hapo maandalizi yatakua ni tayari. Sasa download KingRoot 4.0 (or above) kwa kui search kwenye Google kisha Install kwenye simu yako. Baada ya ku install gusa Open. Baada ya hapo KingRoot itafunguka na itaitambua simu yako automaticallyModel ya Simu na Toleo lake. (Mf. Model: H6 Android 4.4.2). Kama simu yako haijawahi kuwa rooted utaona Root access is unavailable. Chini gusa START ROOT. Hapo KingRoot itakua inakomboa simu yako kutoka kwenye kifungo cha maisha kuwa na subira zoezi hilo litachukua muda kidogo (sio Zaidi ya dak 6) mpaka utakapoona ROOT SUCCSSFULLT DONE!!!!! YOU ARE NOW A SUPERUSER !!!!!
--
Ili kuhakikisha kama simu yako imeshakuwa rooted, nenda PlayStore kisha download Root Checker. Ukishai Install na kuifungua gusa VERIFY ROOT. Ukiona Congratulations! Root access is properly installed on this Device HAPO KILA KITU TAYARI!!!!!
FAIDA ZA KU ROOT SIMU:
1. Utaweza ku update toleo la mfumo wa simu yako (Kuflash). Mfano kama unatomia Android 4.4.2 (KitKat) unaweza kui update kwenda Android 5.0 (Lollipop) Simu ya Android haiwezi kuflashiwa bila kuwa rooted!
2. Hua inatokea simu kuibiwa. Wewe unaesoma Makala hii usiibe simu ya Android siku hizi (ukiokota mtafute mwenye nayo). Nitafute nikupe story!! Sasa zipo program nyingi za ku track simu yako wakati imeibiwa lakini nyingi huondoka kwenye System ya simu yako baada ya kufanyiwa Factory reset au kuflashiwa. Kama ume root simu yako, zipo Program za kuitafuta simu yako ambazo hata mtuhumiwa aiflash au aireset .BADO ITAKUWEPO TU! Mfano wa Program hizo ni Cerberus.
3. Utakua na uwezo wa kuweka Program nyingi na nzuri za kuifanya simu yako iwe fasta na kuboresha muonekano (performance and appearance). Pia kuna program za kutunzia chaji, Kuzuia matangazo kutoka Google (mf. AdAway), n.k . ambazo hazitafanya kazi bila root
ZINGATIA:
Rooting inaweza kuharibu kabisa simu yako na kuifanya isiwake tena!! (Mimi hapa sitahusika kwa lolote). Usiogope, hii huwatokea wale wanaokurupuka na kutofuata maelekezo. Mimi binafsi nishairoot simu yangu na za Marafiki zangu zisizopungua 20 bila madhara yoyote kutokea. Fanya utafiti kwanza ni program gani sahihi ku root simu yako, omba ushauri, ..
Pia Rooting inaharibu Warranty ya simu yako. Kama ulipewa Warranty uliponunua simu yako na ukaikuta na tatizo, ukiirudisha haitakubalika. Aidha, inawezekana pia kuunroot
HITIMISHO:
Kwa yeyote ambae ni mdadisi na mtafiti, anaependa kusaidiwa na Technologia, kuna ulazima wa kuroot simu yake. Baada ya Makala hii, wale woote ambao tutaenda sambamba tutaanza kupitia Programs nyingi ambazo zinahitaji Root Permission. Mie natumia Tecno H6, baada ya kui root nimeifanyia Settings nyingi sana na ninaitumia katika mambo mengi sana!! ROOTING imeniwezesha hata kubadilisha muonekano wa maandishi system nzima!!
Makala na:
Athanas Chriss
0757413078 (Whtsp tu)
Mpigie AthanasNimejaribu kupita njia zote but nikianza kuroot inaishia 16% alafu inafeli na kuniambia "no strategy now". Msaada wapi nakosea
Program 10 za muhimu ambazo kila mtumiaji waPia nilikuwa naomba kujua apps gani ambazo naweza kuzipata baada ya Ku root simu,ambapo awali nilikuwa siwezi kuzipata
Mimi nimekopi na kupaste.This is good education. Big up mkuu
Hata kama umecopy na kupaste mkuu, sharing good information ndio cha muhimu sana. Wangapi wanapata vitu wanakaa navyo kimya?Mimi nimekopi na kupaste.
Thanks to Athanas
MKUU mbona hizo link zako zinazingua, sana sana naitaka hiyo nova launcherProgram 10 za muhimu ambazo kila mtumiaji wa
Simu ya android alie MTAFITI anapaswa kua nazo:
1. Blackmart 0.99 (Rooted devices only)- Kwa ajili
ya ku download Paid Android Apps
# Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!118&authkey=!AFiTDD2xyqstI-U&ith
int=file%2capk
2. FMWhatsapp 2.12 - Altenative Whatsapp App
(Tumia Whatsapp 2 mpaka 3 za namba tofauti
kwenye simu moja)
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!127&authkey=!AH2xem5Fo-jDZNY&ith
int=file%2capk
3. GBWhatsapp - Altenative Whatsapp App
(Tumia Whatsapp 2 mpaka 3 za namba tofauti
kwenye simu moja)
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!122&authkey=!AL8lUrPTIdDVTsI&ith
int=file%2capk
4. Lucky Patcher 5.9.5 (Rooted devices only) -
Kwa ajili ya kufanya Program iwe 'System app',
kutoa Google ads kwenye Program flan,
ku'crack' apk file, ku unistall System apps, nk
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!128&authkey=!AAwtBlVJzIQSU-U&ith
int=file%2capk
5. Nova Launcher 4.0.1 Prime (Works best in
rooted Devices) - Best Android Launcher I ever
met!
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!148&authkey=!AAnJrCIaHHQBL1w&ith
int=file%2capk
6. RAMExpander 3.19 (Rooted devices only) - Kwa
ajili ya kuongeza RAM ya Simu kutoka kwenye
SD Card
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!123&authkey=!APdamHpO3gsGuTI&ith
int=file%2capk
7. Tubemate 2.2.6 - Kwa ajili ya ku download
Video za Youtube
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!117&authkey=!ALvbo3iGe3xGN5Q&ith
int=file%2capk
8. Switchme 2.1.32 (Rooted devices only) -
Kwaajili ya kutengeneza Profile tofauti za Mfumo
mzima wa Android...
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!153&authkey=!AI0GtUCbAnyqmIU&ith
int=file%2capk
9. Rashr (Flash tools) (Rooted devices only) -
Ku unlock bootloader, ku flash ROMs na .zip
files kwenda kwenye OS
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!152&authkey=!ADY75n8sqbHnnsI&ith
int=file%2capk
10. System App Removal (Rooted devices only) -
Kwa ajili ya ku uninstall Sysyem Apps
#Downloadlink
https://onedrive.live.com/redir?resid=360E
C7743B8A3A62!155&authkey=!AGfNB9lF3CI1syo&ith
int=file%2capk
Kusoma makala jinsi ya Ku root simu, fungua
hapa:-
https://m.facebook.com/story.php?story_
fbid=520754191429717&id=135063953332078
Usisahau ku like ukurasa wetu kwa Updates zaidi:-
https://mobile.facebook.com/Mobile-Phone-Tips-
Tricks-More-135063953332078/
Tunaomba Radhi kwa kutokuzingatia kigezo cha
Lugha.
Regards....
Athanas Chriss 0757413078
hahaaaa ngoja nsubr kutoka kwakoNiliwai kutembelea makala moja about rooting..bahati mbaya makala ilijaa maneno magumu ya kiingereza. Na kama unavyojua English hata Magufuli hawez...nilishindwa kuelewa.
Sasa leoo nimeinyaka. Ntafanya iko kitu rooting!! Mkiona sionekani humu ujue imezima.
Mtafte Athanas kwenye simuMKUU mbona hizo link zako zinazingua, sana sana naitaka hiyo nova launcher
Pamoja sana ndgThank u ulieleta huu uzi kwa kiswahili
Soma Makala yangu hii:Am wait for good answer