Jinsi ya kuepuka kumwonea mwenzako wivu mbaya

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Mtu mmoja aliomba, "Mungu, naomba unibariki mimi na mke wangu na mtoto wangu John na mke wake. Sisi wanne tu, na si zaidi"

Hiyo inatoa picha jinsi binadamu alivyo mbinafsi kwa asili. Ndiyo maana watu wengine hupika kiwango cha ustaarabu wa mtu kwa kuangalia kiwango ambacho amefanikiwa kuushinda ubinafsi.

Kwa kuwa ubinafsi ni hali ya kawaida ya binadamu, nitakujulisha njia mbili zinazoweza kukusaidia kuushinda:

1. Kuwa na bidii kufuatilia upande chanya wa mtu. Ukiwa "focused" kutafuta madhaifu yake, utayapata mengi sana. Lakini ukiamua kuyatafuta mema yake, utayaona.

Hakuna mtu ambaye ni mbaya tu asiyekuwa na upande mzuri, na hutakutana na binadamu aliye mkamilifu bila madhaifu yoyote.

2. Sifia mema yake
Kwa mfano, hata kama ni mpinzani wako wa kisiasa au kibiashara, anapofanya vizuri na hata kukushinda, sifia mafanikio yake bila kujali kama hatapata taarifa kuwa ulimsifia. Ukikwepa kusifiwa mafanikio yake, unaweza ukaingia kwenye mtego wa kumwonea wivu na kujikuta unaamza kumpigia majungu.

Hizo ni mbinu chache nizijuazo. Naamini kuna wana JF wanaofahamu mbinu nzuri na bora zaidi!

Karibuni!
 
Hapa umepiga mule mule na nimekuelewa sana. Hii ni muhimu sana hasa katika mahusiano/ndoa. Tafuta mema ya mwenza wako na uyapalilie hayo maana hayo mema (hata kama ni machache) ndiyo yatakuja kugeuka na kuwa nguzo- mama ambayo kwayo uhusiano wenu wote utaweza kujiegemeza na kusimama.
 
Njia ya kujiepusha na wivu pindi unapoona mtu kafanikiwa
sema: Mashaallah
Maana yake: Mungu amependa.
 
Ubinafsi unatija pia, kuna mda inabidi kukubaliana na walimwengu huwezi wabadilisha. Hakuna siku utakua sawa maisha yako yote. So tuishi nao hivyohivyo tu.
 
Kila mtu ana njia ya kuepukana na wivu ,

Wengine utasikia ni friiimasoni yuleπŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†


Wengine utasikia ni mpigo πŸ€”πŸ€”πŸ€”



Wengine utasikia vya urithiπŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„


Wengine utasikia "tutaviacha Duniani huku yeye anapata shida DunianiπŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†

Mimi nasema kuepuka wivu panga malengo Yako mwenyewe usiangalizie kwa jilani alafu fanya kazi sana, ukiangalia kwa jilani mana ake jilani ndio atakuwa kipimo chako, Sasa yeye ana kazi na kipato tofauti na wewe, hata kama mna kazi Moja amini matumizi mtakuwa tofauti,so utaumia na kuishia kuwa na wivu
 
"Whatever you praise, you increase!" - M. R. Emerson.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…