Kifo kipo karibu sana na mwanadamu hata zaidi ya umbali kati ya unyayo wake na sori ya kiatu chake.....hapa nina maanisha kuwa maisha ya mwanadamu hapa duniani ni mafupi sana...kiasi kwamba hamna sababu ya kujivuna kuishi maisha mazuri na ya anasa hapa duniani kwani wakati wake ni mdogo sana.....
Vile vile kwa kuwa kufa ni lazima na kuishi ni bahati...basi hakuna sababu ya kukiogopa kifo...kwani uoga wako , wasi wasi wako na hofu yako havitakusaidia siku yako itakapotimia...suluhu pekee ni kujiandaa na kifo mahala popote na wakati wowote kwani haijulikani siku wala saa ambayo mwanadamu atanyakuliwa.....
Na njia pekee ya kuijiandaa na kifo kufanya yale ambayo yanampendeza MUNGUM wakati wote na kuyaacha yale aliyoyakataza.....
AMEN...