Mazoezi gani mkuu muda wote nipo job vyakula vya mafuta kuacha hilo lipo ndani ya uwezo wangu tuendelee wangu
Mazoezi ni mengi sana, na si lazima kwenda GYM.
Utakaporudi nyumbani kutoka kazini, muda tosha wa kufanya mazoezi unapatikana. Ni wewe mwenyewe kujiwekea ratiba.
Chumbani panatosha, na Mazoezi ya tumbo ni mengi sana, ngoja nikupe haya mepesi kwanza.
Unachotakiwa kufanya ukiwa chumbani au hata sebuleni ni wewe tu na maamuzi yako, muombe mtu wa kukuzuia miguu yako huku wewe ukiwa umekaa kitako, kisha anza kulala kinyume nyume kidogo, ukishafika chini jinyanyue tena.
Na hii si lazima uwe na mtu hata peke ako, tafuta sehemu ambayo utapenyeza miguu yako ili uweze kujinyanyua na kujirudisha taratibu, na vilevile ukishazoea uwe unajinyanyua kiubavubavu kisha ukijirudisha unajirudisha kwa kanuni ile ile ulioanza nayo, yaani unajirudisha kwa kujiweka sawa, na ukijinyanyua tena unaendelea kiubavubavu ukijirudisha kama nilivyoelezea hapo.
Sasa kwa vile wewe itakuwa ni mara ya kwanza inabidi usiende raundi nyingi, fanya hata kumi kumi kisha unapumzika japo dakika mbili au tatu kisha unaendelea.
Na kwa mtu kama wewe ambae hufanyi mazoezi siku ya pili utajisikia sana maumivu ya tumbo, usiogope inabidi uendelee kila siku mpaka utakapozoea hutohisi maumivu tena, na pia kuwa na utaratibu wa kujiwekea mapumziko japo kwa wiki mara moja, unajiwekea siku moja ambayo unapumzika/hufanyi mazoezi.
Na pia uwe unakunywa sana maji.
Na cha nyongeza, siri ya mazoezi ya tumbo mwanzoni tegemea kuharisha, na wala usiogope kama hali hiyo itakutokea, wewe endelea na mazoezi. Inategemea na tumbo la mtu waweza kuharisha au kutoharisha ila maumivu ya tumbo lazima, usiogope jiandae.
Ruka sana kamba, inasaidia sana kukufanya uwe mwepesi na kupunguza mafuta ya mwili kwa kiasi kikubwa.
Haya maelezo ninayoyatoa naona kama hayatoshi vile, ungekuwa karibu na mimi ningekupa mazoezi ya kutosha na nakuahidi baada ya wiki mbili tu ungeanza kuona mabadiliko