Jinsi ya kuongeza mauzo kupitia mtandao kwa gharama ndogo

Jinsi ya kuongeza mauzo kupitia mtandao kwa gharama ndogo

Jerry10

Member
Joined
Jan 2, 2013
Posts
22
Reaction score
5
Mtandao wa intaneti umekuwa sehemu ya maisha ya watu wengi kwa maisha ya sasa. Tanzania nayo inaongezeko kubwa la watumiaji wa intaneti, hususani kupitia simu za mkononi na 'tablet' computers.

Idadi kubwa ya watu hutumia mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter na Instagram. Zaidi ya yote wanatumia sana tovuti kama Google au Bing kutafuta taarifa, bidhaa au huduma mbali mbali kwenye mtandao.

Ili uweze kufanikiwa kuuza kwenye biashara yako ni myhimu ukapatikana kwenye mtandao ili uweze kufaidi hili ongezeko la watumiaji wa mtandao wa intaneti. Hapa chini nitaelezea mambo ya muhimu unayotakiwa kufanya.

1. Tengeneza tovuti.

Kitu cha kwanza ni kutengeneza tovuti ya biashara yako ambayo wateja wako wanaweza kupata taarifa muhimu kuhusu bidhaa, huduma na bei zako wakaki wowote, bila kufika hapo biashara yako ilipo. Pia unaweza kuuza bidhaa kupitia kwenye tovuti yako. Tovuti ni kitu cha muhimu sana kwa biashara yako iwe biashara kubwa au biashara ndogo. Kwani tovuti haitamwambia mteja kwamba hii ni kampuni ndogo. Zaidi sana unaweza ukawa na tovuti nzuru kuliko kampuni kubwa.

2. Jiunge na mitandao ya kijamii kama Facebook, Twitter au Linkedin. Mitandao ya kijamii ni njia nzuri ya kuwa karibu na wateja wako. Na ni rahisi zaidi kwa biashara ndogo ambazo haziwezi kumudu gharama za kuendesha tovuti.

3. Iboreshe tovuti yako iweze kupatikana kirahisi kwenye 'search engine' kama Google. Ukitengeneza tovuti haishii hapo tu, unatakiwa kuhakikisha kwamba wakati wote inapatika kirahisi na ikiwezekana ikatokea juu mtu anapotafuta huduma au bidhaa unazouza. Hii itasaidia kuongeza idadi ya watu wanaoingia kwenye tovuti yako.

4. Rahisisha manunuzi au mawasiliano kwenye tovuti yako. Umeshakuwa na tovuti yako, mitandao ya kijamii na umefanikiwa kupata watu wengi kwenye tovuti yako lakini wananunua? Wanakutafuta? Au wanatalii halafu wanaondoka. Hii ni mbaya kwani hata Google wanaweza kuishushaa tovuti yako kwenye orodha ikawekwa chini kwani inaoneka kama vile watu wakija kwenye tovuti yako hawapati wanachokitafuta.

5. Linda tovuti au biashara yako na maoni mabaya kwenye mtandao.
Watu wanapo 'comment' vibaya kuhusu biashara yako wanakupunguzia nafasi ya kupata wateja wapya. Hivyo basi utatakiwa uipiganie biashara yako kwenye mtandano.

Unaweza ukafanya hivyo mwenyewe au kama una kazi nyingi ukatafuta mtaalamu akakusaidia.

Jeremiah Ngalla ni mtaaalamu wa masuala ya kutangaza kwenye mtandano pamoja na kutengeza tovuti zenye viwango vya kukubalika na Google. Amekwisha saidia baadhi ya biashara kupata wateja kupitia mtandao wa intaneti.

Email yake ni jrmhngalla@gmail.com
Linkedin kupitia tz.linkedin.com/in/jeremiahngalla
+255 688 199 349.
 
mnatengenezea bei gani na je ukiwa na website kuna gharama zozote za uendesha kwenye hiyo website??
 
Safi sana. Binafsi nimejitangaza kupitia mtandaoni na sasa napiga kazi nchini na nje ya nchi. Mimi ni mbunifu Wa nembo/logo
LOGO DESIGNER
 
mnatengenezea bei gani na je ukiwa na website kuna gharama zozote za uendesha kwenye hiyo website??

Bei zetu ni kuanzia Tshs 300,000 pamoja na kuihost kwa mwaka mmoja.

Gharama za ziada zinakuja pale ambapo unataka kuiboresha tovuti yako kwa kuweka taarifa mpya mara kwa mara na kuifuatilia kuhakikisha kwamba inapata watu wa kutosha.
 
Tuonyeshe website uliyowai kutengeneza. Maneno mazuri na namba za simu hazitoshi.
 
Back
Top Bottom