Ndugu zangu wote waliopata mkopo na wale waliokosa kwanza kabisa nipende kwa pamoja sote tumshukuru Mwenyezi Mungu kwani ana mipango na sisi wanadamu aijalishi umepata mkopo au la. Basi ndugu zangu bila kuwachosha nilete yangu yalo moyoni na atakayeweza kunipa mawazo, maoni na msaada mwingine naomba atupie hapa. Mimi ni kijana niliyezaliwa katika kijiji kidogo nikiwa mtoto wa 17 kati ya watoto 30 wa baba yangu nikimaanisha kuwa kuna wakubwa zangu wasio na uwezo mzuri kiuchumi 16 na wadogo zangu ambao pengine wananitegemea 12. Kutokana na hali hiyo ya familia niliamua kukimbilia kutafuta elimu ambayo itakuwa ni mkombozi kwangu na hata familia na jamii kwa ujumla. Basi kwa neema ya Mungu nilifanikiwa kufaulu kidato cha nne kwa kupata dalaja la kwanza (16 ) na baadae kujiunga kidato cha tano na cha sita nikafaulu kwa dalaja la kwanza (9) basi kama ilivyo furaha ya wengi hata mimi mwenzenu mimefanikiwa kuchaguliwa Bachelor of science in nursing university of Dodoma na kupata mkopo 4,032,500/= lakini baada ya kusikia kuwa mtu anapopata GPA kali mfano 5 inakuwa ni lahisi kutoka kielimu na pengine kubakizwa chuoni kuwa assistance lecturer nimekuja kwenu wa jf na great thinkers muweze kunipa/kutupa mawazo au ushauri sisi sote ili kuepukana na supplementary, kuto disco na hatimae kupata GPA kali hili kuweza kukomboa familia kama yangu na zaidi kupata elimu ambayo itakuwa ya manufaa kwa jamii na wala si elimu ya kukariri ukizingatiwa nitadili na afya ya binadamu. ASANTE KWA KUNISIKILIZA , NAKARIBISHA MAWAZO/ Ushauri WENU.
Kihalali:
Fanya assignents vizuri.
Usipitwe na quiz hata yenye max1,uwe unajizoeza kusoma kwa uelewa lecturer anapofundisha somo fulani. Uwe unapunguza mzigo wa notes ambazo hazijasomwa ,kwa kupitia kidogo kidogo na siyo 'fayatingisha' karibu na mtihani. Kikubwa ni uelewa..na kupangilia muda wako na ratiba yako vizuri. Na yote yanawezekana ukimtanguliza mbele 'MUNGU MWAMINIFU',kwa Kila jambo,katika Masomo na Maisha yako.
Rule 1: Go do what you are supposed to do, not what you want to do.
Rule 2: Rule 1 shall always prevail, mutatis mutandis!
Ahsante, masomo mema.
Rule 1: Go do what you are supposed to do, not what you want to do.
Rule 2: Rule 1 shall always prevail, mutatis mutandis!
Ahsante, masomo mema.
bro mm cjaelewa maana ya madesa, naomba nifafanulie vzur
kaka asante sana iyo tutorial ndo nimechanganya na assistance ki ukweli ushauri wako mzuri sana ingewezekana ningeprint page lakini naomba unisaidia hapo namba 5. Kuhusu boo control maana huku nyumbani familia nzima wanafanya sherehe wakisema boom likiwa linaingia natuma hata laki 250 kwa ajili ya wadogo zangu huku wakisisitiza kuwa health related fields zote huwa wanaongezewa hata motisha je kwa wale wazoefu inawezekana nikajibana vip ili niweze kusatisfy pande zote nyumbani na mi mwenyewe.
shall apply to all you are responsible for hapo chuo...thats masomo.asante kaka ila hiyo mutandis sijailewa.
Yeah mkuu.Nimeipenda hii....hiyo mutatis mutandis bila shaka ni kama cetiris paribus
Nimeipenda hii....hiyo mutatis mutandis bila shaka ni kama cetiris paribus
Obviously GPA ya 5 hutapata, kulingana na historia yako...lakini komaa, piga msuli kama wa form six, tafuta discussion groups za watu wenye akili timamu..epuka vitu kama hivyo hapo kwenye red, hudhuria vipindi vyote na ukae mbele..zaidi sana mtangulize Mungu,,atakutuliza akili
Huu ushauri mzuri sana ndugu...nimepata kitu na mimi hapo
zamani kule o level nilikuwa nikidharau marks au masomo fulani ila kaka umenikumbusha Mungu anisaidie sitakosa hata kwenye 1+[_]=2