Jinsi ya kupika rosti la mayai ya kuchemsha

Jinsi ya kupika rosti la mayai ya kuchemsha

Nimeipenda sana. Ila ukiweka picha itaongeza mvuto wa uzi.
 
nipo farkhina nilikuwa kwenye shangwe za birthday yangu jana, japo nilitegemea bonge la keki toka kwako

Owh happy birthday labda nimechelewa kuku wish....hope ulifurahia vizur

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Tenaaaa, sio kila siku nyama kumbe ht mayai kwa roast yanaenda.

Asante kwa pishi
 
nipo farkhina nilikuwa kwenye shangwe za birthday yangu jana, japo nilitegemea bonge la keki toka kwako

Angel alikua wap kwani ....yy ndo alikua aliteremshe bongezz la cake sote tupate vijipande...lol
 
Owh happy birthday labda nimechelewa kuku wish....hope ulifurahia vizur

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums

kikubwa ilikuwa kumshukuru Mungu kwa kuniweka hai na kunilinda, kiukweli nilifunga siku ya jana nikiwakumbuka yatima wajane na wagonjwa tuliozaliwa siku moja ambao hawakuweza kuifurahia siku yao ya kuzaliwa
 

Attachments

  • 1401723682639.jpg
    1401723682639.jpg
    43.7 KB · Views: 225
Last edited by a moderator:
Asante kwa pishi
Kichuo zaid ila tulikua hatuwek nazi
Tamu na wali
 
Kuna sehemu nililiona ili pishi nikajaribu kulipika aisee ni tamu asikwambie mtu, hii ni kwa wale wenzangu na mimi wanaopenda kujaribu jaribu mapishiii.

MAHITAJI
1: Mayai Manne.
2: Nyanya tatu.
3:kitunguu maji kimoja.
4😛ilipili hoho moja.
5: karoti moja.
6: nyanya chungu(KAMA UKIPENDA) tatu.
7: Nazi moja. 8: Mafuta ya kupikia chupa moja.
9: Chumvi upendavyo.

JINSI YA KUANDAA
1; Chemsha mayai yako kwa dakika 15, yakisha iva yaepue yaache yapoe halafu yamenye.
2; Weka mafuta ya kula kwenye moto wa wastani yakisha pata moto weka mayai yako ambao umeyamenya na yakapoa yaache mpaka yawe na rangi ya kahawia ila yasikaukeee halafu yaepue ili yajichuje mafuta.
4; katakata nyanya, karoti,nyanya chungu, kitunguu maji na pilipili hoho.
5: kuna nazi yako halafu chuja matui mawili kama unavyounga maharage.
6: weka sufuria jikoni weka na mafuta kidogo ya kuungia mboga halafu weka kitunguu maji kiache mpaka kiwe kahawia halafu weka karoti nazo kaanga mpaka zibadilike rangi kidogo halafu weka pilipili hoho kaanga kidogo halafu uweke nyanya na nyanya chungu halafu funika mpaka ziive kidogo (usisahau kuweka chumvi kwenye huo mchanganyiko).

7: mchuzi ukishaiva iva weka mayai yako ambayo ulishayakaanga halafu weka tui jepesi halafu piga piga mpaka liive(lichemke) likishaiva weka tui bubu nalo piga piga mpaka nalo liive (lichemke) likishaiva likisha iva epua.

Mboga yako ipo tayari kuliwa unaweza kula na kitu chochoteee. Karibuni.....

Mafuta ya kupikia chupa moja?! Are you serious?!
 
Hapa nimejaribu kwa nazi ya Azam...Sema nahofia naweza poteza funguo...Tumbo limeshangaa sana...THANKS GUYS FOR PROCEDURES...cto acha kujaribu...
 
Back
Top Bottom