Lile ni balaa....huwa nalipikaga home.
Unatakiwa:
Papai bichi sana au embe mbichi.
Pilipili mbuzi zile ndefu, changanya kijani na nyekundu ili kuvutia sambaro lako.
Vitunguu maji.
Vitunguu saumu.
Curry powder au Garam masala.
Nyanya maji.
Tangawizi kiduchu.
Uwatu mzima au uliosagwa.
Mbegu za giligilani nzima (si lazima sana)
Ndimu ( si lazima sana)
Pilipili manga ya unga ( si lazima sana)
Steps:
Unachukua papai bichi kabisa au embe mbichi na pilipili mbuzi zile ndefu nyekundu au za kijani.
Unachukua papai bichi au embe mbichi kisha unakata pieces ndogo ndogo kiurefu, waweza menya maganda au usimenye.
Pilipili mbuzi unazipasua katikati kiurefu.
Halafu vyote kwa pamoja unaanika juani au kama una oven unazi-bake kidogo.
Baada ya hapo unaweka mafuta jikoni, unaweka kitunguu maji, kitunguu saumu, tangawizi kidogo sana....curry powder, garam masala, pilipili manga kidogo.
kama huna hivo vitu....weka kitunguu saumu na masala tu.
Mchanganyiko wako ukiwa umekolea, weka nyanya na uwatu, uwatu mzuri ni ule ulionunua na kuusaga mwenyewe
Acha vichemke kisha weka papai lako au embe pamoja na pilipili kisha funika.
Baada ya muda koroga kisha weka mbegu za mgagani, usizitwange, weka nzima nzima.
Kama huna mbegu hizo si lazima ila uwatu lazima uweke.
Kisha ziache zichemke mpaka uone zimeanza kutoa rojo na uwatu kunukia.
Epua sambaro lako.
Hapa kuna mawili, kama utaweka ndimu, ndimu wekea chini usiweke ndimu wakati sambaro iko jikoni.
Kama hutaki ndimu, liepue sambaro lako na lisave kwa wali, pilau, au biriani.
Karibu
talnam
Iko siku tutakutana kwa Sele bonge, ndo mitaa ya home pale juu.