Mbona easy. Take this simple stapes
1. Chukua karanga zile za mafuta ( maarufu kama karanga za lishe) zilizomenywa tayari
2. Zichambue vizuri na chagua zenye ukubwa sawa
3. Kama unataka ziwe na ladha ya chumvi, basi zichanganye na maji yenye chumvi kiasi (kisha zianike juani zikauke)
4. Chukua sufuria kisha tia mchanga ndani yake. Pasha kwenye jiko (mi huwa natumia jiko la mkaa-for best results)
5. Mchanga ukishapata joto kiasi, weka karanga zako kisha rusharusha sufuria ili karanga zijichanganye na mchanga wa moto. ANGALIZO TUMIA MOTO WENYE JOTO LA WASTANI, ILI ZISIUNGUE
6 Endelea kuzigeuza kwa kurusharusha sufuria (AFTER 30 SECONDS TO 1 MINUTE), mpaka utakapoona karanga zimeanza kuiva.
N:B Karanga zikianza kuiva utasikia zinanukia, na hata ukipukucha punje utaona zinamenyeka kutoka katika layer yake kiurahisi
7. Epua sufuria kisha mwaga mchanganyiko wa karanga na mchanga katika sakafu au sinia
8. Zitoe karanga zako ziweke kwenye ungo.
9. Zisugue kwenye ungo kutoa layer yake, kisha pembua maganda (layers) na zibaki karanga tu
10. Saga karanga zako kwenye mashine ya kusagia karanga(ina fanana na ile ya kusagia nyama au viungo vya sambusa) mpaka karanga zako ziwe laini kabisa mithili ya blueband.
Weka katika chombo safi kwa ajili ya matumizi yako. Waweza kutumia kama bread spread maana huwa ni laini sana. Pia waweza kutumia kama kiungo cha mboga za majani. (MI HUWA NATUMIA PIA KWA MAPISHI YA SAMAKI WAKAVU/WALIOKAANGWA AU DAGAA WALIOKAANGWA) Inanoga pia
N:B Mchanganyiko huo hukaa muda mrefu pasipo kuharibika au kuchacha. Pia kadiri mchanganyiko unavyokaa hujichuja mafuta, ambayo pia ni kiungo kizuri kwa mboga hasa za majani.
ENJOY