Jinsi ya kutunza na kuimarisha Afya ya Akili ya Mtoto wako

Jinsi ya kutunza na kuimarisha Afya ya Akili ya Mtoto wako

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Uhusiano Imara na wenye nguvu sio tu unakufanya kuwa Binadamu bora bali pia husaidia kukuimarisha Kihisia. Wakati wa kujenga uhusiano na Watoto wako, waambie unawapenda mara kwa mara

Ni muhimu kila Siku utenge muda wa kuzungumza na kumsikiliza Mtoto. Ikiwa mtoto wako anataka kuzungumza nawe, sikiliza na umsikilize kikamilifu. Pia, mhimize kujenga Uhusiano mzuri na Familia na Marafiki

Epuka kufoka na kumpa vitisho: Watoto wanapokosea, usipige kelele, badala yake waeleweshe ni nini kimekwenda vibaya kisha uwaoneshe njia sahihi. Kuwatisha kunaweza kuwa na athari za muda mrefu.

Kuza nidhamu: Watoto wanahitaji fursa ya kuchunguza na kukuza ujuzi mpya na uhuru. Wakati huo huo, watoto wanahitaji kujifunza kwamba tabia fulani hazikubaliki na kwamba wanawajibika kwa matokeo ya matendo yao. Sitawisha nidhamu na adabu kwa watoto wako katika umri mdogo ili kuwafanya kuwa wanadamu wazuri.
 
Naomba nifahamu kama una mtoto kwanza then ujibu unamfanyiaga hayo mwisho tuhaidi hautaacha kumfanyia mpaka atapofikia umri wa akili yake sawa sawa ( tegemezi/pevuko)
 
Back
Top Bottom