jinsi ya kuwadhibiti watu tuliowajiri ktk biashara zetu wasituibie.

jinsi ya kuwadhibiti watu tuliowajiri ktk biashara zetu wasituibie.


Mkuu usimamie vipi?
- Mfano unamagari ya Biashara mabasi uwe unayaendesha mwenyewe? au uwe kondact wa mabasi yote? utasimamia biashara yako lakini huwezi simamia katika operation zote,

- Hakuna biashara ambayo utakua nayo wasikuibie wakiamua,

- Labuda uwe na TAX NA WEWE NDO DREVA NA WEWE NDO KONDACTA NA WEWE NDO UNAJAZA MAFUTA NA WEWE NDO UNAPELEKA GARI GEREJI

- Wahindi huwa wanasimamia maduka yao asubuhi hadi jioni lakini wanaibiwa wakiwa hapo hapo, sasa wewe unaongelea usimamizi wa aina gani?

- Wafanyakazi wako hata sekunde 50 zinatosha kukuibia na wala hawahitaji saa nzima, kitendo hata cha kwenda chooni kinatosha wao kukuibia,


- NA WIZI UKO KATIKA VITU VINGI SANA MKUU NA SI KWENYE PESA TU
- wanaweza kukuibia pesa sawa
- Watakuibia bidhaa zako
- Watakuibia katika manunuzi
- Watakuibia katika matengenezo
- Watakuibia muda

NILAZIMA UWAJENGEE UWEZO WAFANYAKAZI WAKO NA UWAPE ELIMU YA KUTOSHA NA UWALIPE VIZURI NA KUWAPA STAHIKI ZINGINE,


Komando,

Sio lazima usimamie mwenyewe. Unapofanya biashara yoyote kipimo ni pesa unayopata. Kama unazo taxi, waambie madereva wako kuwa ikifika jioni unataka kiasi fulani. Na akishindwa kutimiza masharti haya kwa kipindi fulani mfukuze kazi.

Vilevile kama wewe unaogopa kufanya biashara kwa sababu kuna aina nyingi za wizi, tafuta kazi ya kuajiliwa. Kwani biashara ina risks zake.
 
Kipapai ni dawa tosha,
Kama ni mwanaume basi akigusa tu anageuka Mlupo
 
hebu twende na mfano wa guest house ya vyumba 21
una chaji kila chumba sh 10000......

na umeajili watu wa tatu wasimamizi na wasafishaji

na imetokea umesafiri wiki mbili

utawezaje kuzuia wasikuibie?

mkuu hapa nadhan ndio teknolojia inaweza kusaidia kudhibiti.
cctv camera na mashine za cash register zinaweza kusaidia.
 
TATIZO LA WATANZANIA BIASHARA ZETU NI PROFIT ORIENTEDSANA, TUNAANGALIA FAIDA TU NA SI KITU KINGINE,

UAMINIFU MDOGO KWA WAFANYA KAZI HUSABABISHWA NA

1. Elimu- kutowapa elimu ya jinsi ya kusimamia vyema biashara

2. Malipo duni- Wafanya kazi wengi sana wanapunjwa, mwajiri yeyeanaangali faida pekee haangalii wafanya kazi wake wanaishi vipi

3. Marupurup/ motivation

MOJA YA NJIA ZA KUFANYA

1. Elimu- Wafundishe kwanza jinsi ya kusimamia mradi wako, wape elimuya wiki moja kama huwezi kutoa elimu ajiri watalaamu watoe elimu hiyo,wafundishe kwamba hiyo biashara ndo itakayo walisha wao so kadri wanavyosimamia vyema na kupata faida ndo na wao watakavyo nufaika

2. Malipo- Jitahidi sana kuwalipa vizuri wafanya kazi wako- usiangaliefaida tu na kuwalipa wafanya kazi wako elifu 60 wakati maisha yenyewe ndo haya,jitahidi kuwalipa vyema, usiangalie tu kwenye kumake super profiti wakatiwafanya kazi wako wakiwa na maisha magumu sana hapo ni lazima wakuibie sana

3. Motivation/ malupulupu- Jitahidi sana kuwapa vitu vingine vya ziadamfano
- Kuwatoa wakaenda hata kutembelea kambuga fulani
- Tenga pesa ya matibabu yao na familia zao
- Kila mwaka uwe unatoa zawadi kwa mfanya kazi bora, zawadi iwe yamaana lakini si zawadi uchwara
- Sometime Biashara yako ikiruhusu wasaide hata katika kusomesha watotowao kwa kuwaambia utatoa kiwango fulani cha pesa
- Uwe unawasiliza mara kwa mara shida zao na kuwasaidia kutatua hizoshida zao
UKIFANYA HAYO WATAKUWA NA MOYO NA KAZI KWA SABABU WANAJUA JINSI GANIUNAVYO WAJALI SANA

asante kwa ushauri mkuu.
Ila mkuu kwanza hii inabidi iwe ni biashara kubwa yenye kuingiza pesa ya maana,si kila mfanyabiashara anaweza kuyafanya haya kwa wafanyakazi wake.
Na pia,hata ukifanya hivi,siku zote wafanyakazi wakipata mwanya wa kupata cha ziada wataiba tu.
Katika hali halisi mim naona hii sio dawa ya kudhibiti wizi.
 
theoretically yes, kiuhalisia mkuu umepotea vibaya sana. Njia pekee ya kuzuia wizi ni wewe mwenyewe kuwa karibu sana na kazi zako, hakikisha unakula nao sahani moja kwa kila step within your business area and you must be very sensitive to detect possible frauds. Weka sheria kali kwa wafanyakazi wako wote na hakikisha kila mfanyakazi anazifuata hapa swala la kuchekacheka ondoa kabisa and you must be cruel inapobidi.
Weka records nzuri ya stock uliyonayo na uwe unafanya inspection daily/twice a week ili kudetect kama kuna loss.

indirect theft: huu wizi unawaliza wengi sana siku hizi bila kujijua na zaidi wenye maduka/suppliers utakuta mfanyakazi wako anaingiza bidhaa zake sawa na zakwako zilizopo stock na kuziuza kupitia biashara yako, matokeo yake unaona wateja wengi lakini quantity yako inatoka kidogo. Hii kitu unaweza ukaidetect kwa kufanya ka intelijesia kako utakachoona katakufaa kutokana na nature ya biashara yako. Mimi nilimshauri ndugu yangu afanye inspection ya kushitukiza na nikamwambia akikuta bidhaa zisizo za kwake achukue uamuzi mgumu wa kujibinafsishia zile bidhaa na kweli alifanya nilichomwambia na alikuta mzigo usio wake wa sh 4.2m.. alimfukuza yule mfanyakazi haraka na tangu siku hiyo haka katabia kalikoma

Njia nyingine ninayoipenda ni mind games, katika wafanyakazi wako 10 weka watatu wawe kama informers wako kukuletea taarifa za ubadhilifu wa baadhi ya wenzao, make sure hawatambuani (muaminishe kila mtu hiyo ni kazi yake pekee)na wape bonus of around 40%, akikuletea taarifa nyingi zaidi muongezee tena bonus ili awe encouraged zaidi.. this should be repeated and reviewed..

NOTE: ITAKUSAIDIA KUPUNGUZA

mkuu ushauri wako ni mzuri asante,ila hapo pakuwa mkatili patanishinda ni bora nimuondoe mtu kuliko aendelee kunisaidia huku nikimfanyia ukatili kama njia ya kumdhibiti,naona hiyo ndo itafanya waniibie bila hata huruma.
 
Queen kumthibiti moja kwa moja asikuibie kabisa ni kazi saana lazima utaibiwa tu kwa kiwango fulani, na hii hutegemea na Biashara. Kwa mtu ambae ana biashara nyingi ambazo hawezi manage mwenyewe mara nyingi ni nzuri sana kua makini sana katika wafanya kazi.... Lets say Una wafanya kazi 10. Katika maeneo matano tofauti, ni lazima uwe na mtu ambae ni Msaidizi. Na tokana na kwamba wafanyakazi wengi twaajiri ambao sio proffessionals inatakiwa huyo mtu umjenge kuweza kusaidia kuendesha hizo biashara zako.

Katika hao kumi lazima atakuepo mtu ambae yupo trust worthty, ana bidii, yupo sharp, ana nidhamu na aijua kazi kuliko wenzie.... If at any means unaona hakuna katika hilo kundi mtu wa namna hio; then Nakushauri unaajiri mara moja. Ukisha mpata wa sampuri hio... Invest kwake kumkosha Psychologically and physically. Hakikisha wampa mshahara wa kutosha, marupu rupu, na wamtreat kama rafiki mwenye mipaka (asikuzoee kuvuka mpaka heshima iwe pale pale!) hakikisha wamfundisha kazi hasa upande wa Management ya biashara zako vizuri na muoneshe kua Unamuamini saana (Hakikisha unamuamini kwa % 50 tu!); Huyu mtu atakusaidia kuweza endesha biashara na wewe huku aki pointi penye matatizoa na madhaifu.... na mwaweza work as partners hali ni mfanya kazi wako. Mara nyiingi hii technique ni nzuri for from experience na observation watu wa namna hii huwa hadi wachungu kwa wafanya kazi wenzao. Hapo tayari yeye anakusaidia kuthibiti wenzie wa chini yake (Maadamu tu asiwanyanyase).

Kuweza kumdhibiti anaekusaidia kuendeha biashara na wale chini yake ni kujua vema Biashara yako.... Ukijua Biashara yako fika hata kama utaibiwa ni katika kiwango cha chini sana. Which can not be escaped. Hii itakusaidia hata unapo pata dharula ya kusafiri nje kidogo ya mji ama matatizo kama misiba ikitokea....

asante dearest.
Kipengele cha kutokuanao rafiki sana inabidi nikifanyia kazi,mim nimezidisha sana matani na urafiki na wafanyakazi wangu.Kumbe ni tatizo nitalishughulikia na kufuata pia yote uliyoshauri.
 

Mkuu usimamie vipi?
- Mfano unamagari ya Biashara mabasi uwe unayaendesha mwenyewe? au uwe kondact wa mabasi yote? utasimamia biashara yako lakini huwezi simamia katika operation zote,

- Hakuna biashara ambayo utakua nayo wasikuibie wakiamua,

- Labuda uwe na TAX NA WEWE NDO DREVA NA WEWE NDO KONDACTA NA WEWE NDO UNAJAZA MAFUTA NA WEWE NDO UNAPELEKA GARI GEREJI

- Wahindi huwa wanasimamia maduka yao asubuhi hadi jioni lakini wanaibiwa wakiwa hapo hapo, sasa wewe unaongelea usimamizi wa aina gani?

- Wafanyakazi wako hata sekunde 50 zinatosha kukuibia na wala hawahitaji saa nzima, kitendo hata cha kwenda chooni kinatosha wao kukuibia,


- NA WIZI UKO KATIKA VITU VINGI SANA MKUU NA SI KWENYE PESA TU
- wanaweza kukuibia pesa sawa
- Watakuibia bidhaa zako
- Watakuibia katika manunuzi
- Watakuibia katika matengenezo
- Watakuibia muda

NILAZIMA UWAJENGEE UWEZO WAFANYAKAZI WAKO NA UWAPE ELIMU YA KUTOSHA NA UWALIPE VIZURI NA KUWAPA STAHIKI ZINGINE,

mkuu umeongea sawa,elimu na mshahara mzuri kulingana na kipato cha biashara ni muhimu,lakini huwezi tu kutegemea kufanya hivyo ukaamin kwamba hawatakuibia.Kama kuna nafasi za kuiba wataiba tu.Bado elimu na mshagara mzuri sio mbinu yakuwadhibiti.
 
Bibie ume raise very important point kwenye biashara kwani biashara ina element mbili

Mapato (faida) na Matumizi, plus hasara ikiwemo uwizi wa aina mbalimbali

Kuhus kudhibiti wafanyakazi naomba nikupe mfano wangu sijui unafanya biashara gani

a. Fahamu kwa uhakika margin ya mapato ya siku (average) hii inatokana na wewe kukaa kwenye sehemu ya biashara hiyo kwa muda wa kutosha..then hiyo inakuwa benchmark ya ku-detect uwizi ikiwa faida (mapato yamepungua sana kwa siku kadhaa...STUKA

b.Hakikisha wafanyakazi wako wanalipwa on time (hata kama kuna nini? very impotant) hata kama uko kwenye difficulties wafanya kazi stahili zao zipatikana haraka iwezekanavyo na waone kuwa kweli owner anajali stahili zao in case manager wao wanawazengua

c. Internal infomer na external field visit, internal atakusaidia kupata uwizi na mawazo ya wafanyakazi kuhusu biashara yako na kazi, external visit ni kama auditing ya mara kwa mara bila taarifa..

d. Angalia sana usifukuze wafanyakazi wako (ni hatari) wafanyakazi wakishajua kuwa hapa turnover ni kubwa wanajua owner ni mnoko kwa hiyo wanakula haraka..(hapa na concur na yule jamaa aliyeshauri elimu na uhakika kuwa hii kazi ni kudumu kwake na kwako..

nitaendelee...
 
mkuu hapa nadhan ndio teknolojia inaweza kusaidia kudhibiti.
cctv camera na mashine za cash register zinaweza kusaidia.
CCTV guest? utakimbiwa na wateja woote. Any way control measures inategemea aina ya biashara na u need more than one offcourse. Na measures zinaanza tangu unapo hire, treatment ya wafanyakazi wakiwa kazini na separation wanapoacha kazi.

Waajiri wengi wa bongo huwafanya wafanyakai wao kuwa watumwa, hali inayofanya wakate tamaa na wasiheshimu kazi kwani waweza kuwa fired bila notice. Wafanye wafanyakazi wako wapende biashara na kuona kama ni yao. Incentive kama kuwapeleka short courses na zawadi ya sikukuu yaweza kusaidia.

Matumizi ya tekinolojia kama computer na cctv yaweza kusaidia lakini inategemea aina ya biashara na jinsi ulivyodesign mfumo wa utendaji kazi .

Separation of responsibilities pia ni muhimu. kwa mfano kwenye guest waweza kuwa na cashier na house keeper.Keshia anapokea fedha tu na house keeper anatunza funguo na ku update room status. kila mmoja ana keep daily recods zake. wewe utakua una verify kwa kumatch the two records.

Wabongo wooote ni wezi, hata mimi ni mwizi.
 
kwa mfano huo unaweza fanya hivi, hao watatu wote umekosea kuwafanya wawe wasimamizi. Hata kama wote ni wasimamizi ni lazima kuwe na msimamizi mkuu ambao wengine watareport kwake.
Pili, katika kugawa majukumu angalia usije ukampa mtu majukumu ya yeye kuwa na control ya kila kitu. Kwa mfano, unaweza kuta katika biashara mtu huyo huyo anaetunza fedha na kuidhinisha malipo ndio huyo huyo anaehusika na kwenda kupurchase vitu na pengine hata yeye ndio anavikeep hivyo vitu. Hapo lazima uibiwe maana kwenye kutenga fungu la manunuzi atajipangia mwenyewe, kwenye manunuzi anaweza foji risiti na kwenye store anaweza kufoji records. Jaribu kuweka mgawanyo mzuri wa majukumu katika namna ambayo haileti mkanganyiko wa kimaslahi.
Tengeneza mbinu za kuwamotivate, mfano. Kama unajua guest house yako inaingiza maximum laki 2 kwa siku, unaweza waambia siku watakayoingiza zaidi ya laki 2 watapata bonus ya % fulani kwa wale ambao wapo incharge siku hiyo. Au kama watu watakuwa wanakula hapo hapo then wakataka wapelekewe vyakula vyumbani... Unaweza kuwacharge amount ya hiyo huduma ya mpaka mchumbani then hizo hela zikawa ni marupu rupu ya watu wa jikoni.
Unaweza kubuni mbinu nyingi za kuwafanya wafanyakazi wako wakawapunguza kuiba au kuacha kabisa.

Kutumia teknolojia hapa ndio kikomo cha wizi. Kama una guest weka milango inayofunguka kwa kadi, chumba hakifunguki bila login details na mambo mengine muhimu kwenye software kukamilika. Hata kama haupo hawawezi kuuza vyumba bila funguo, actuially hata umeme chumbani hautowaka kama hujaanza kuingiza details kwenye computer...
Kudhibiti wizi inahitaji clever approach. Na hizi zinavary kwa kila aina ya biashara.
 
CCTV guest? utakimbiwa na wateja woote. Any way control measures inategemea aina ya biashara na u need more than one offcourse. Na measures zinaanza tangu unapo hire, treatment ya wafanyakazi wakiwa kazini na separation wanapoacha kazi.

Waajiri wengi wa bongo huwafanya wafanyakai wao kuwa watumwa, hali inayofanya wakate tamaa na wasiheshimu kazi kwani waweza kuwa fired bila notice. Wafanye wafanyakazi wako wapende biashara na kuona kama ni yao. Incentive kama kuwapeleka short courses na zawadi ya sikukuu yaweza kusaidia.

Matumizi ya tekinolojia kama computer na cctv yaweza kusaidia lakini inategemea aina ya biashara na jinsi ulivyodesign mfumo wa utendaji kazi .

Separation of responsibilities pia ni muhimu. kwa mfano kwenye guest waweza kuwa na cashier na house keeper.Keshia anapokea fedha tu na house keeper anatunza funguo na ku update room status. kila mmoja ana keep daily recods zake. wewe utakua una verify kwa kumatch the two records.

Wabongo wooote ni wezi, hata mimi ni mwizi.

mkuu nashukuru kwa ushauri.
cctv guest inaweza kutumika mapokezi bila ya wateja kufahamu kuwa ipo pale.Kumbuka hata ktk mahoteli makubwa ambayo watu pia huyatumia kwa mambo yanayofanyika guest kuna cctv cameras,cha msingi ni kuhakikisha matukio yanayorekodiwa yanaheshimiwa kwa aidha mim mmiliki tu ndiye ninayeweza kuona kilichorekodiwa na sio kila mtu.
 
Kutumia teknolojia hapa ndio kikomo cha wizi. Kama una guest weka milango inayofunguka kwa kadi, chumba hakifunguki bila login details na mambo mengine muhimu kwenye software kukamilika. Hata kama haupo hawawezi kuuza vyumba bila funguo, actuially hata umeme chumbani hautowaka kama hujaanza kuingiza details kwenye computer...
Kudhibiti wizi inahitaji clever approach. Na hizi zinavary kwa kila aina ya biashara.

wazo zuri sana mkuu lakini hii inahitaji mtu uwe na uwezo wa kuweka hiyo teknolojia maana sidhani kama ni ya bei rahisi.Kwa hizi guest za kawaida kawaida sidhani kama wataweza kumudu hizi gharama.
asante kwa wazo lako.
 
Back
Top Bottom