Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
JIONI MOJA NA BI. TITI NYUMBANI KWAKE UPANGA MIAKA YA 1980
Nimewakuta watoto hawa leo asubuhi hapa Ikwiriri, Rufijib wanaitazama picha ya Bi. Titi nikawaomba tupige picha mimi na wao na Bi. Titi.
Watoto hawa wamenikumbusha siku moja jioni moja kiasancha miaka 30 iliyopita nilipokwenda nyumbani kwa Bi. Titi Upanga.
Miadi hii alikuwa kanipangia Bwana Ally Sykes na nilimuimba anipangie ili nimhoji Bi. Titi kuhusu historia yake na mchango wake katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hapa Upanga nilipomkuta Bi. Titi alivyokuwa alikuwa tofauti sana na Bi. Titi niliyemuona Temeke nyumbani kwake kabla miaka michache iliyopita.
Tulikwenda mimi na wenzangu Temeke kwa Bi. Titi kwenye harusi.
Siku ile pale Temeke Bi. Titi hakuwa kachangamka kama nilivyomuona pale nyumbani kwake Upanga.
Hii ilikuwa mara yangu ya pili kufika pale nyumbani kwa Bi. Titi Upanga.
Mara ya kwanza nilifika pale Upanga nyumbani kwake ni siku alipofanya Maulid kushukuru kurudishiwa nyumba yake hiyo iliyotaifishwa na serikali katika miaka ya 1970.
Nyumba yake hii alirudishiwa na Rais Ali Hassan Mwinyi.
Maulid yale yalihudhuriwa na watu.wengi wa kimjini na Tewa Said Tewa alikuwapo na mkewe Bi. Zainab bint Maulid.
Hawa watoto niliowakuta katikati ya mji wa Ikwirir kwenye bango la Bi. Titi lilinikumbusha Bi. Titi nilipokwenda nyumbani kwake mara kwa nia ya kufanya mazungumzo kuhusu maisha yake nikamkuta kakaa na wajukuu zake wakiwa na furaha kubwa.
Bi. Titi huku akicheka aliniambia, "Bwana Mohamed huna jipya wewe utakaloandika kuhusu mimi ambalo bado halijaandikwa na waandishi."
Lakini akaniambia kitu ambacho kwa hakika kwangu kilikuwa kipya sikupata kukisikia popote.
"Sikiliza Bwana Mohamed nenda Arusha kwa Ismail Bayumi kamuulize nini tulifanya Mombasa."
Huu ukawa ndiyo mwisho wa mazungunzo yetu nikawa nimebaki pale kumaliza soda yangu na yeye akawa amekaa chini na wajukuu zake wanaangalia senema ya "Cinderella."
Wajukuu zake wakawa wanacheka wanasema, "Cinderella," yeye anawaambia, "Huyo ni "Kisonoko."
Nilikwenda Arusha kwa Ismail Bayumi na yeye ndiye akanieleza nini Bi. Titi alifanya alipokwenda Mombasa kama mgeni wa TANU Club kwa minajili ya kufanya kampeni Waingereza wamtoe Jomo Kenyatta kifungoni.
Historia hii nikaiandika katika kitabu cha Abdul Sykes.
Picha ya kwanza ni bango likitangaza Tamasha la Bi. Titi, Ismail Bayumi na picha ya mwisho mwandishi akamkabidhi Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Mohamed Omar Mchengerwa kitabu cha Abdul Sykes.
Nimewakuta watoto hawa leo asubuhi hapa Ikwiriri, Rufijib wanaitazama picha ya Bi. Titi nikawaomba tupige picha mimi na wao na Bi. Titi.
Watoto hawa wamenikumbusha siku moja jioni moja kiasancha miaka 30 iliyopita nilipokwenda nyumbani kwa Bi. Titi Upanga.
Miadi hii alikuwa kanipangia Bwana Ally Sykes na nilimuimba anipangie ili nimhoji Bi. Titi kuhusu historia yake na mchango wake katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
Hapa Upanga nilipomkuta Bi. Titi alivyokuwa alikuwa tofauti sana na Bi. Titi niliyemuona Temeke nyumbani kwake kabla miaka michache iliyopita.
Tulikwenda mimi na wenzangu Temeke kwa Bi. Titi kwenye harusi.
Siku ile pale Temeke Bi. Titi hakuwa kachangamka kama nilivyomuona pale nyumbani kwake Upanga.
Hii ilikuwa mara yangu ya pili kufika pale nyumbani kwa Bi. Titi Upanga.
Mara ya kwanza nilifika pale Upanga nyumbani kwake ni siku alipofanya Maulid kushukuru kurudishiwa nyumba yake hiyo iliyotaifishwa na serikali katika miaka ya 1970.
Nyumba yake hii alirudishiwa na Rais Ali Hassan Mwinyi.
Maulid yale yalihudhuriwa na watu.wengi wa kimjini na Tewa Said Tewa alikuwapo na mkewe Bi. Zainab bint Maulid.
Hawa watoto niliowakuta katikati ya mji wa Ikwirir kwenye bango la Bi. Titi lilinikumbusha Bi. Titi nilipokwenda nyumbani kwake mara kwa nia ya kufanya mazungumzo kuhusu maisha yake nikamkuta kakaa na wajukuu zake wakiwa na furaha kubwa.
Bi. Titi huku akicheka aliniambia, "Bwana Mohamed huna jipya wewe utakaloandika kuhusu mimi ambalo bado halijaandikwa na waandishi."
Lakini akaniambia kitu ambacho kwa hakika kwangu kilikuwa kipya sikupata kukisikia popote.
"Sikiliza Bwana Mohamed nenda Arusha kwa Ismail Bayumi kamuulize nini tulifanya Mombasa."
Huu ukawa ndiyo mwisho wa mazungunzo yetu nikawa nimebaki pale kumaliza soda yangu na yeye akawa amekaa chini na wajukuu zake wanaangalia senema ya "Cinderella."
Wajukuu zake wakawa wanacheka wanasema, "Cinderella," yeye anawaambia, "Huyo ni "Kisonoko."
Nilikwenda Arusha kwa Ismail Bayumi na yeye ndiye akanieleza nini Bi. Titi alifanya alipokwenda Mombasa kama mgeni wa TANU Club kwa minajili ya kufanya kampeni Waingereza wamtoe Jomo Kenyatta kifungoni.
Historia hii nikaiandika katika kitabu cha Abdul Sykes.
Picha ya kwanza ni bango likitangaza Tamasha la Bi. Titi, Ismail Bayumi na picha ya mwisho mwandishi akamkabidhi Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Mohamed Omar Mchengerwa kitabu cha Abdul Sykes.