Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata huyo mfanyakazi si unaweza kumuasili badala ya kwenda huko vituoni? Kuasili kwenyewe unaweza fanya rasmi kwa kujaza makaratasi au isivyo rasmi kwa kumchukulia huyo mfanyakazi kama mwanao. Where is that BIG mistake?
mhhhSema jamaa alikuwa anaaminiwa sana na mama mwenye nyumba hivyo alikuwa ana vijisent sana.
Kuna wafanyakazi...heri ukutane na shetani... ...Kivipi
Acha roho mbaya kwani wakiwasomesha kuna shida gani?Big mistake !
Kama ni Mfanyakazi mpe stahiki yake, mlipie NSSF kila mwezi pamoja na Bima ya Afya basi hayo mengine siyo kazi yako, kama unataka mtoto nenda kaasili Vituo wapo watoto wengi wenye mahitaji, ...
Acha roho mbaya kwani wakiwasomesha kuna shida gani?
Wewe una toho ya WIZI weweHuyo inawezekana amefanya kama mradi huku akipokea fedha kwa mabeberu.
Hii chai ni ya tangawizi itakua.Hakika hapa duniani kuna binadamu wanatabia njema sana!
Jirani yangu pamoja na mkewe! Wana maisha ya kawaida kabisa kama yangu ya kipato cha kati!
Wakiishiwa hela wananiazima, vivyo nami nawaazima vyao nikiishiwa. Tuna maisha ya kawaida sana!
Lakini Jirani Siku zote hapo kwake haishi kupokea vijana wa kazi za ndani wa kike na kiume kwa siku zote tulizofahamiana!
Vijana hao alikuwa akinitambulisha kuwa ni watoto wa kaka na Dada zake (ndugu) wamekuja kumtembelea!
Sikuwahi kuhisi hata siku kuwa wale ni wafanyakazi!
Style yake ya maisha anavyoishi nao! anawahudumia kila kitu kama watoto wake wa kuzaa! Mke wake pia anapika nao chakula kwa zamu!
Kiufupi huwezi kabisa kujua yupi ni mtoto na yupi ni mfanyakazi!
Cha ajabu zaidi mfanyakazi akitimiza mwaka anamwandikisha chuo, (private sponsored) anasomesha kuanzia ngazi ya chini hadi degree, na ada anawalipia vizuri!
Na likizo wanarudi kama watoto wa pale!! Mmoja anaoingia chuo ndipo huagiza mfanyakazi mwingine mpya! Hivyo hivyo!
Wakati jirani yangu akifanya hivi! Mimi na Mke wangu tuko kwenye ugomvi mkubwa kwasababu kafumania meseji za house girl wangu navyomtafuna! Ndoa iko mashakani hadi majirani wameingia kusuruhuhishwa!
Ndipo huyu jamaa jirani kaamua kunisihi kuniambia kuwa hawa watoto tunatakiwa kuwahudumia na kuwasaidia kama watoto wetu! Siyo vizuri kuwarubuni kabisa!
Kaniambia hadi hivi leo, kashasomesha house girl watatu na boy mmoja (jumla wanne) na sasa kuna mwingine wa tano juzi katoka kuchukua form pale magogoni!
Ananisihi sana, badala ya kuwageuza wake, niwaone kama watoto wangu! Niwasaidie wafikie malengo!
Hakika nimesikia maumivu makubwa sana kwa tabia na moyo wa kipekee alionao jilani yangu!
Hakika nimemuelewa jirani yangu ni mtu wa kipekee sana!
Natamka wazi sitamtaka wala kumtamani house girl teeena! Hata akiwa na matako makubwa kama behewa! Sithubutu!
Nitafanya kama jirani yangu alivyo kuanzia sasa, hata kama iwe elimu ndogo ya ufundi chelehani nitasomesha ili nipande mbegu njema!
BadoHamjamroga kweli kwa wivu wenu Wa kiswahili