Kalpana
JF-Expert Member
- Jun 16, 2017
- 32,603
- 62,269
Ni balaa mnoooNimeithibitisha hapa napoishi aisee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni balaa mnoooNimeithibitisha hapa napoishi aisee
Naam mkuu ndo naisoma hapa saiv
[emoji23][emoji23]Ukianza kusoma stori unaweza kudhani jamaa alikua na jirani mchawi kumbe alikua na jirani anaeacha mlango wazi na kumfanya jaamaa aogope pikipiki yake kuibiwa
Huo ni mtungi wa gesi na pipe zakeHii mimba ina miezi mingapi??
Dondosha namba 8Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 07
Nilitazama ndani ya kiroba kile pasipo kujali harufu yake kali iliyonifanya nizibe pua, ndani yake nikakuta nywele nyingi, sikujua ni nywele za nini na za wapi ila zilikuwa nywele ndefundefu za usinga, nguo zilizojifinyangafinyanga na nyama zilizokuwa zinatoa harufu … nyama ya nini hii? Nilijiuliza nikipekua, kidogo nikakutana na kichwa cha mbuzi, kichwa hicho kilikuwa na pembe fupi ambazo zimengushiwa uzi mwekundu, kukibinua kichwa hicho kukikagua na kukitazama vema mara nikasikia kitu kimedondoka mguuni pangu, nikapatwa na hofu kubwa, niliangaza upesi kwa tochi ya simu nikaona sarafu ya hamsini iko chini, sarafu hiyo ni mpya kama imetoka benki muda huu.
Niliichukua sarafu hiyo nikaiweka mfukoni kisha nikaendelea kupekuapekua kiroba kile kwa kijiti, nywele nyingi nisizozeielewa pamoja na manyoyamanyoya ambayo niliamini ni ya mbuzi yule yalijaa humo, kabla sijamaliza zoezi hilo nikasikia sauti za wanaume wakiwa wanateta, wanaume hao walikuwa wanakuja kutokea upande ule wa bar nilikotokea.
Nilitazama upande huo nikaona mwanga wa tochi ukimulikamulika, na pia nikasikia vishindo vya miguu vikisogea kwa upesi, basi haraka nikaona ni vema nikajificha kwani nikionekana hapo hakuna mtu atakayenielewa kuwa mimi ni mshuhudiaji tu, niliona hilo ni wazo bora kwasababu kama ningejaribu kukimbia ama kurejea katika njia yangu basi wangenikuta kabla sijafanikisha hilo na basi wangehisi kuna kitu kinaendelea na mimi humo korongoni.
Nikajibana nyuma ya mti nikatulia tuli niwezavyo, nikawasikia watu wale wakijongea na kujongea karibu huku wanaongeaongea, tochi yao kali inamulika hapa na pale, mwendo wao wa upesi sana.
Majamaa wale walipofika mahali fulani katikati ya korongo lile, katika kumulikamulika kwao huku na kule, wakamulika kile kiroba nilichokuwa nakipekua, nikamsikia mmoja akisema;
“Oya, nini kile?”
Nilitazama nikiwa hapo nyuma ya mti, nikaona kile kichwa cha mbuzi. Sijui akili yangu ilikuwa wapi, kumbe kile kichwa nilikitupia chini nikakiacha papo hapo, sasa kichwa hicho kilikuwa kimesimama chini kikitazamia kule njiani! Nikahamaki na moyo wangu. Niliogopa watu wale wasije kwa karibu kukitazama kwani wakifanya hivyo tu basi ningekuwa nimekwisha. Japo sikuwa kwa ukaribu mkubwa lakini uwezekano wa kuniona nilipojibana ulikuwa ni mkubwa pia.
Mwingine akamjibu mwenziwe: “Mbona kama kichwa cha mbuzi?” Walimulikamulika maeneo hayo ya karibu huku wakiwa wanaongeaongea kuhusu korongo lile, mimi akili yangu ikiwa inaomba tu wasije wakasogea upande wangu, muda si mrefu wakakata shauri wakaondoka kuendelea na safari yao, hiyo ndo’ ikawa ahueni yangu.
Mabwana wale wakawa wameenda wakiwa wemeniachia funzo kubwa kwani nilihisi nimevuka sana mipaka na sikutakiwa kabisa kufanya yale niliyoyafanya. Vipi kama ningeonekana hapo na watu wakanishuku na kunidhuru kwa ulozi?
Nilitoka nikaenda nyumbani moja kwa moja, hakukuwa na kingine siku hiyo, nilijilaza na kwa msaada wa pombe nilizokunywa siku hiyo nikapitiwa na usingizi mapema ya saa saba, hiyo kwangu ilikuwa ni mapema maana si kawaida yangu. Kesho yake nikaendelea na mambo yangu mengine huku nikiwa najaribu kuona ratiba yangu itakuaje hapo karibuni ili nikapate kumtembelea bwana Tarimo kule Muhimbili.
Ikapita siku na masiku, bado sikwenda kumtazama mgonjwa, kila nilipojifaragua na ratiba ya kazi sikufanikiwa kabisa kupata upenyo hata weekend nilihisi uchovu, kiasi kwamba yule jirani niliyeagana naye kwenda pamoja hospitali akajiendea mwenyewe. Bwana huyo aliendea siku tatu tu baada ya siku ile ya Mwananyamala, mimi nikaapa mwisho wa wiki ijayo, yaani weekend nyingine inayofuata, haswa Jumapili, lazima nitaenda kumwona bwana yule kumjulia hali, kwahiyo kwa wakati wote huo nilikuwa naulizia tu na kupewa habari za mgonjwa toka kwenye vinywa vya watu wengine.
Nakumbuka vema, ilipofika siku ya Jumamosi, yani bado siku moja kwenda kumtembelea mgonjwa kama nilivyopanga, nikiwa nipo nyumbani pamoja na familia majira ya asubuhi, tulisikia tangazo la kipaza sauti likikatiza katika mitaa yetu, kwa mara ya kwanza nikadhani ni watu wa kuuza sumu za panya, mende, kunguni na viroboto maana nao siku hizi wamerahisisha kazi zao kwa vipaza sauti lakini kitambo kidogo tangazo hilo lilifika karibu nikalisikia vema, lilikuwa ni tangazo la kukumbusha kikao cha mtaa wa Mashuka, wito ukitolewa na mwenyekiti.
Kwa mujibu wa tangazo hilo, kikao kilikuwa kinafanyika kuanzia saa kumi jioni kwenye kiuwanja fulani kidogo ambacho kilikuwepo upande wa kushoto mita chache tu tangu ukiacha njia pana iliyosakafiwa kama unatokea kituo cha Kontena kushuka zaidi kule Mashuka. Kiwanja hiko hakikuwa rasmi, kilikuwa kipo tu katika ‘saiti’ ambayo haikumaliziwa, nyumba fulani hivi ambayo ni kama ilitelekezwa kwa muda kidogo.
Agenda kuu ya kikao hiko ilikuwa ni kujadili kuhusu kumaliziwa kwa barabara ile ya sakafu tokea pale ilipokuwa imeishia, mbele kidogo ya geti la lile ghorofa la bweni la Saint Joseph, iende mpaka mwisho kabisa wa Mashuka, yani njia zima kusiwe na vumbi.
Tangazo hilo kwangu likawa ndo’ mara ya kwanza kulisikia lakini nilipouliza, ‘wife’ akaniambia ni siku ya tatu sasa linapita lakini kwasababu majira yake yalikuwa ni mchana, muda ambao mimi sipo home, ndo’ maana sikupata kulisikia.
Basi baada ya hilo tangazo, nilikaa hapo nyumbani mpaka majira ya mchana nikatoka kwenda Goba centre kwenye mnada. Siku ya Jumamosi kulikuwa na mnada hapo na mimi nilikuwa napendelea kwenda kwasababu ya kuchukua vitu vingi vya ndani kwa bei nzuri kuliko kuchuuza kidogokidogo.
Nilienda huko nikafanya kila kilichonipeleka, wakati wa kurudi, kama kawaida, nilipofika kituo cha Kontena nilishuka na barabara ile iliyosakafiwa kuelekea nyumbani kule Mashuka. Nilipomaliza barabara hiyo nikashika njia ya vumbi, kidogo mbele, pale kwenye kile kiwanja nikakuta tayari watu wameanza kusogeasogea, hapo pamewekwa viti kadhaa vya plastiki tayari kwaajili ya kikao.
Mimi nikanyookea nyumbani kwanza kutua mizigo na kuoga kabisa, kisha nikarejea kujumuika na wale watu wa kwenye kikao. Nilikuta tayari wameshaanza.
Kuhusu ile barabara, nilichosikia kwa maneno ya mwenyekiti, ilikuwa ipo katika mpango wa kuendelea kujengwa kumaliziwa lakini changamoto iliyoibuka ni kwamba kuna baadhi ya makazi ya watu na hata pia magenge yamebana hifadhi hiyo ya barabara, haswa huko Mashuka kwa chini, na watu hao si kwamba wamevamia ama wametenda kosa, la hasha, yale ni maeneo yao kabisa kwa haki hivyo kikao kiliitwa ili pajadiliwe na ikiwezekana watu hao waombwe kutoa sehemu ndogo za maeneo yao kwaajili ya kukamilisha mradi wa barabara ile ilosakafiwa.
Kitendo cha serikali ya mtaa kukaa kimya muda mrefu bila kuiendeleza ile barabara, kuliibua minong’ono kwamba pesa iliyotengwa huenda ilishapigwa, kwasababu hiyo kikao cha kuweka mambo wazi kilikuwa ni muhimu.
Watu wakajadiliana na wakakubaliana, wengine waliokuwa wamiliki wa maeneo husika wakiwa pale, mwisho wa siku ikaadhimiwa mwenyekiti atatengeneza pendekezo rasmi na litafikishwa kwa walengwa, lakini wachache waliokuwepo pale wao waliridhia kabisa kugawa maeneo yao alimradi maendeleo yapite.
Baada ya swala hilo kumalizika mwenyekiti alitoa fursa kwa watu kuuliza ajenda zingine muhimu mbali na ile iliyojadiliwa, katika uwanja huo ndipo mjumbe akaibuka na yale ya kule korongoni juu ya namna gani watu wameligeuza kuwa dampo lisilokuwa rasmi. Mjumbe huyo alieleza kuwa korongo hilo limegeuka kuwa kero kubwa ya harufu kwenye baadhi ya maeneo kitendo ambacho ni hatarishi kwa milipuko ya magonjwa haswa kipindi cha mvua.
Swala hilo likaibua mengine, kuna wajumbe wakasimama na kuituhumu pia shule ya St. Joseph wakisema shule hiyo imekuwa ikielekezea uchafu wake wa machemba kule kwenye lile korongo. Punde chemba zao zinapojaa basi wanazifungulia kumwagia korongoni na ndo’ maana halijawahi kuonekana gari lolote la kunyonya maji machafu hapo shuleni tangu kuanza kwake kwa shughuli.
Basi swala hilo mwenyekiti akaahidi kulifanyia kazi lakini pia akapiga marufuku kwa mtu yeyote kutupa taka kule korongoni na endapo yeyote akikamatwa basi atawajibishwa. Katika kutimiza hilo, tena likijumuishwa na swala la wezi majira ya usiku wa manane ambalo kumbe lilishawahi kuongelewa kwenye vikao vya nyuma, mwenyekiti pamoja na wajumbe wakaazimia kuwe na ulinzi shirikishi katika maeneo yale japokuwa mimi mpaka naondoka kikaoni haikuelezwa wazi oparesheni hiyo itaanza rasmi lini.
Nilishika njia ya kurejea nyumbani, nikajikuta napatana na majirani wenzangu wawili wa kuongozana nao, majirani hao nao walikuwa katika kile kikao hivyo tuliongozana kwa pamoja tukiyajadili yale yaliyozungumzwa kikaoni, mwelekeo wetu ukiwa mmoja, hapo majira sasa yakiwa yanaelekea kuwa giza la saa moja.
Kufika getini tulipokelewa na sauti ya kilio cha mtoto, mtoto ambaye mimi sikumfahamu ni nani kwa sauti yake hiyo. Tuliingia ndani tukakuta wanawake wawili wakiwa wanahangaika na mtoto mmoja wa kike anayeishi humu ndani, mtoto wa kama miaka kumi hivi kwa makadirio, ambaye alikuwa analia kwa machozi mengi huku amejishika kichwa.
Mtoto huyo nilipomtazama vema, kwa upande wake ule wa pili, alikuwa anavuja damu kichwani, juu kidogo ya sikio lake la kushoto. Mkono wake ulioshika hilo jeraha ulikuwa umelowa damu vidoleni.
Kabla sijafanya jambo, nikamwona ‘wife’ anakuja kwa kasi akitokea nyumba kubwa, amevalia khanga kiunoni na kifuani, akasema: “Hamna mtu ndani, yupo yule mtoto peke yake. Nimegonga na kuita lakini kimya, mlango ameufunga kwa ndani.”
Katika maongezi yalojiri hapo nikabaini kuwa yule mtoto wa BIGI ndiye aliyemjeruhi mtoto huyo kisha akakimbilia ndani na kujifungia, lakini zaidi katika maongezi hayo nikabaini kuwa mtoto yule wa BIGI kumbe hakuwa mtoto mzima kama wengine bali ana matatizo makubwa ya akili. Hata muda huo tukiwa tunazungumza na kumpatia huduma mtoto yule aliyejeruhiwa, yeye alikuwa dirishani akitutazama. Mimi nilimwona.
Lakini zaidi ya yote, nilijikuta napoteza yale yote niliyokuwa nayajenga kwaajili ya usalama wa familia yangu … si jingine bali jambo la kutokutaka kuwahusisha kwenye lolote lile kuhusu mwenendo wa yule jirani.
***
Ila pole Sana mi hizi hazinitishi kabisa, Tena Kuna mavitabu ni hatarii[emoji16][emoji16][emoji16] mkuu Napokaa usiku mnene panatisha kngesee
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Story tamu sana. Wanaokosoa achana nao. Mimi hata ukisema BIG alikua pacha wako sina tatzo,cha msingi stori inaenda[emoji28]
Namba nane ipe tena watu wanasubiri ep ya 11?Dondosha namba 8
Kweli kabisa, niliwahi soma kitabu cha mama yangu anakula nyama za watu, ilikuwa ni hatar nyakati za usiku aiseeIla pole Sana mi hizi hazinitishi kabisa, Tena Kuna mavitabu ni hatarii
Tafuta kazi ya kufanya dogoKuwa na kazi binafsi,kulipwa au kutokulipwa haisuiani na nilichoandika unless hujanielewa nilichoandika
Hiyo roho mbaya ndio uchawi wenyewe.Hiv kwann karibu kila mtu mwenye via viashiria vya uchawi lazma awe na roho mbaya, au ndo sheria zao zipo hvo
Sijui huko mbele kukoje ila kuanzia sehemu ya 07 unaandika visivyo na ulazima. Kiufupi unalazimisha sasaJirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 08
Baada ya mtoto yule kupata huduma ya kadiri ilivyowezekana, kila mtu aliendelea na shughuli yake. Kasheshe ilikuja baadae kwenye majira ya saa nne hivi, nikiwa natazama marudio ya habari kwenye runinga, nilisikia kelele na zogo, kelele ambazo zilikuwa zinaita huko nje ya nyumba kubwa. Kelele hizo hazikudumu kwa muda mrefu huko nje mara zikajongea ndani hivyo nikazidi kuzisikia kwa ukaribu, nikatambua kulikuwa na ugomvi, ugomvi ulosababishwa na kipigo cha mtoto yule kwani aliyekuwa anaongea hapo kwa ukali alikuwa ni mama wa yule mtoto tuliyemkuta analia akivuja damu.
Mama huyo, sisi tulizoea kumuita Bembela, sijui kama lilikuwa jina lake halisi au lah, alikuwa ni mwanamke anayejihusisha na shughuli za mama n’tilie pale Goba kontena, nyuma ya kituo cha mwelekeo wa kwenda Goba centre, kabla hapajabomolewa na ile kampeni ya serikali ya kusafisha vituo hivi vya madaladala kwa kuwaondoa watu wanaohusika na uchuuzi wa bidhaa ndogondogo katika mfumo usokuwa rasmi.
Hapo, akiwa pamoja na wamama wengine kama wawili hivi achilia mbali mabanda mawili ya chips, walikuwa wanauza chakula mpaka majira ya usiku wa saa tatu hivi au saa nne, nahisi inategemea na mauzo ya siku hiyo kama chakula kitaisha mapema au lah. Mimi mara kwa mara nilikuwa nikipata chakula kwake haswa nikiwa mwenyewe nyumbani, so nikitoka kazini napitia kwake nakula kisha nashuka zangu nyumbani. Kwasababu alikuwa ananifahamu, alikuwa ananizingatia sana kwenye huduma na chakula.
Kwa makutano hayo machachemachache, story za hapa na pale haswa tukikutana zaidi katika mazingira yake ya kazi, nilipata kumjua Bembela kama mwanamke mmoja mpambanaji sana. Mungu ambariki huko aliko. Kwa kupitia shughuli za mikono yake alikuwa analipia kodi ya pango na anamsomemsha mwanaye. Bembela alikuwa ni ‘single mother’. Lakini mbali na hapo alikuwa ni mwanamke mmoja mwongeaji mno, kuongea kwake si kazi, na kama ungepata kula kwake basi ungelichukua sekunde chache sana kujua haiba yake hiyo. Sauti yake ni kali na anapenda kusema hili na lile hapa na pale.
Basi kitambo kidogo tu, mimi nikiwa hapo sebuleni nilisikia mlango fulani unabamizwa bum-bum-bum, kwa ukali, kisha sauti ya Bembela ikanguruma, “haya nyie mabondia, tokeni nje tupigane!” Nikajua swala hili sio la mchezo., wakati huo nikawa nasikia na majirani wengine kwa mbali wakiwa wanaongeaongea huko nje.
Kidogo tena Bembela akaubamiza mlango kwa fasheni ileile, bum-bum-bum-bum, alafu akaropoka; “nasema tokeni, nyie si mnajifanya mtoto wenu ni bondia, haya nimemleta huyu aendelee kumpiga.”
Nikatambua Bembela amekuja hapo kwa shari kamili na si nusu shari. Amekuja hapo kuwasha moto, si kuuzima. Aliendelea kuubamiza mlango na kuongea kwa nguvu akisema namna gani anavyomlelea na kumpambania mwanaye kwa tabu alafu mtu anakuja na kumjeruhi kiurahisi. Akaenda mbele zaidi akiuliza kama jirani huyo anaujua uchungu aloupata akijifungua mtoto huyo, lakini maneno yote hayo hayakusaidia kitu kwani mlango aliokuwa anaufokea na kuubamiza hakufunguliwa kamwe. Zaidi sisi majirani, ambao kwa namna moja ama nyingine ndo’ tulikuwa tunaathirika na makelele yake majira yale ya usiku ndo’ tulitoka kumtuliza jazba na kumsihi atumie njia nyingine ya stara.
Bembela aling’aka, “hapana, hawa hawana ustaarabu na ndo’ maana hawastahili ustaarabu vilevile! Wanajua kabisa mtoto wao alichokifanya, wanashindwa kuja kuomba radhi au kuongea na mimi? Maana yake nini kama sio wamedhamiria? Ndo maana nimemleta huyu mtoto hapa waendelee kumpiga!”
Mwanamke huyo alikuwa anaongea kwa mikono mingi mno na vidole vya majigambo. Dera lake amelibana na mtandio kiunoni. Uso wake umefura kweli, anaongea huku mdomo ukienda pembeni, lakini kama ungemsikiliza vema Bembela ungebaini kulikuwa na presha fulani ambayo alipewa na mwanamke mwenzake wa jirani, mmoja wa wanawake tuliowakuta wakiwa na mtoto yule wakati sisi tunatokea kwenye mkutano, maana Bembela alisema muda wote huo wazazi wa yule mtoto hawakufanya jambo lolote pamoja na kwamba waligongewa na kuambiwa, sasa muda wote upi ingali yeye alikuwa amerejea kazini muda si mrefu? Hivyo bila shaka alikuwa amepewa maneno juu ya yale yaliyotokea na nilimjua vema mtu huyo aliyemwambia kwani naye alikuwa akiongezea nyama katika maneno hapa na pale.
Mwanamke huyo katika moja ya kuthibitisha hoja yake, alimuuliza mke wangu ambaye alikuwa amesimama kwenye kingo ya mlango, eti mama fulani hukuwagongea mlango saa ile kuwaita? Walitoka?
Basi zogo lile lilidumu kwa muda kidogo hapo pasipo kuzaa matunda yoyote kwani mhusika hakupata kuonekana mpaka mwisho wake, matokeo yake kwenye majira ya kama saa sita hivi, kila mtu alirudi kwenye makazi yake usiku ukazidi kusonga mbele, lakini kisa kile cha mtoto wa BIGI na mapigano yake ndo’ ulikuwa mwanzo mzuri kabisa kwa watu wasiokuwa na maisha ya usiku mkubwa kuanza kuinyooshea kidole familia ile lakini kwa ambao walikuwa na desturi ya kulala kesho yake kama mimi na ambao walikuwa wanapata kuwa macho mara kadhaa kwenye usiku mkubwa kama Tarimo, ile haikuwa ‘breaking news’ bali tu mwendelezo wake.
Ni tokea hapo, ndipo niligundua hisia za udadisi zilizopo ndani ya mke wangu zikaanza kumea kwa kasi, kitu ambacho mimi binafsi nilikihofia sana kutokana na hali aliyokuwa nayo muda huo, ujauzito wa takribani miezi mitano au sita hivi kama niko sahihi. Usiku huo, baada ya lile zogo na kabla ya yeye kwenda kulala, alinieleza vizuri vyote vilivyojiri mpaka kupelekea tukio lile la mapigano na watoto kuumizana.
Aliniambia katika majira yale ya jioni, yeye alikuwa nje anaanua nguo za mtoto alizopata kuzifua asubuhi yake. Akiwa katika zoezi hilo, kama ilivyo kawaida ya weekend, watoto wengi walikuwa wanazungukazunguka wakicheza huku na kule ikiwemo mtoto yule wa Bembela lakini kwasababu ya majira kuanza kuwatupa mkono, yaani jua kuanza kuzama, jirani mmoja mwanamke, yule ambaye mimi nilihisi ndo’ alimpa maneno Bembela, alianza kuwasihi watoto wale kuacha michezo warejee majumbani mwao kwani giza lishaingia, ni hatari kucheza muda huo kwasababu wanaweza kusababisha ajali na majeraha.
Basi watoto wakapungua, wengi wao wakirejea ndani mwao na wale wa mbali wakaanza safari, hapo wakabakia mtoto wa Bembela na mtoto wa huyo mama jirani. Bembela yeye tofauti na wengine hakuwa na mzazi wa kumwita muda huo wala wa kwenda kukaa naye ndani, mama yake yuko shughulini mpaka majira ya usiku wa saa tatu au nne, kwasababu hiyo basi mtoto huyo alifurahia kupata angalau ‘kampani’ ya mtoto mmoja aliyebaki naye, watoto hao wakawa wapo kibarazani wanachezea ile midoli ya kike.
‘Wife’ aliendelea kuanua nguo zake na alipomaliza alibaini nguo zile hazikuwa timilifu, kwa mujibu wake kuna nguo mbili za mtoto hakuziona, kwasababu hiyo alienda kwenye moja ya mlango wa mtu ambaye naye alifua siku ile na kuanika kumuuliza kama amekosea kwenye kuanua akabeba na nguo zake. Alipotoka huko, japokuwa hizo nguo hakupata kuziona, alirejea akakuta pale kibarazani kuna watoto watatu, mmoja wa kiume ameongezeka, mtoto huyo alikuwa amemwona kwa mara ya pili sasa tangu wamehamia pale na siku hiyo ndo’ alipata kumwona kwa ukaribu alipokatiza kupeleka nguo ndani, mtoto huyo alikuwa anachekacheka mdomo wake ukichuruza udenda, hapo ndo’ akajua hakuwa mzima wa akili na huenda hiyo ndo’ sababu wazazi wake wanamfungia sana ndani, ni ngumu sana kumwona nje.
Alipeleka nguo zake ndani, lakini kitambo kidogo akiwa anazikunja nguo hizo akasikia sauti kali ya mtoto analia pale nje, alitoka upesi kwenda kutazama, alipofungua mlango akamkuta mtoto yule mwenye matatizo ya akili akiwa amesimama mlangoni kwao anatazama nje kwa kuchungulia. Alimwendea mtoto anayelia nje akamkuta mtoto yule wa Bembela ameshikilia kichwa chake anavuja damu, hapo ndipo yakaendelea na mengine mpaka sisi kuwakuta pale wakati tunatoka kwenye kile kikao.
Aliponieleza yote hayo, mimi nikatokea kuamini labda mtoto yule alikuwapo mwenyewe nyumbani na ndio maana aliufunga mlango hivyo hakukuwa na mtu mwingine wa kutoka nje kuja kumwona majeruhi, swala hilo mke wangu akakataa, yeye aliamini kulikuwa na mtu mule ndani kwani kuna muda fulani wakati anatazama maharage jikoni alisikia sauti ya mwanaume ikifoka kidogo mule ndani kwahiyo aliamini kabisa baba yumo.
Pale mimi nilipokuwa naishi, ‘wife’ na hata wanawake wengine wa ile nyumba kubwa walikuwa na utaratibu wa kupikia kwenye majiko mawili ya mkaa yaliyokuwa yanakaa koridoni, majiko hayo yalikuwa yanasaidia kwenye kutunza gesi kwa kutumika kama mbadala wa kupikia vitu vya muda mrefu mathalani maharage na njugu mawe. Majiko hayo yalikuwa hapo muda wote, hamna aliyethubutu kupikia jiko la mkaa ndani mwake.
Basi baada ya maongezi hayo mimi nilibaki sebuleni peke yangu. Nilikaa hapo mpaka majira yangu ya kawaida nilipoanza kuhisi kichwa change kizito ndipo nikaenda kujilaza.
Niliamini kabisa usiku huo na makeke yake ulikuwa umeshapita, lakini muda kidogo mbele kama baada ya lisaa limoja hivi mimi kuwapo kitandani, nikagundua kumbe usiku ule bado ulikuwa na mimi. Usiku ule ulikuwa haujamaliza mambo yake.
***
Yeah vitu ka hizo ndo angalau ninaweza kustuka ila bado SanaKweli kabisa, niliwahi soma kitabu cha mama yangu anakula nyama za watu, ilikuwa ni hatar nyakati za usiku aisee
Yes, inavyoendelea anaharibuInachosha unaandika vitu havina hata maana , mpaka mtu unaburuza Aya nyingine
Mfano kulikuwa Kuna haja gani ya kufafanua umama ntilie wa bembela? Kuwa anauzia sehemu Fulani sijui anauza mpaka saa sita za usiku mara kubomolewa vibanda duuh!
Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
sasa s uachane nayoSijui huko mbele kukoje ila kuanzia sehemu ya 07 unaandika visivyo na ulazima. Kiufupi unalazimisha sasa