Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.

Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.

Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.

Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.

Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.

Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.

Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.

Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.

Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.

Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.

"Habari?" Tukionana.

"Asante." Tukiagana.

Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.

Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.

Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.

Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.

Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.

Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.

Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.

Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"

Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.

Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.

Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.

Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?

Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.

Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.

Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.

Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.

Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.

Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.

Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.

Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.

Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.

Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.

Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.

Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.

Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.

Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.

Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.

Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.

Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!

Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?

Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.

***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
Antonia Antonnia
 
Man! Wife wake amechip in ghafla sana, na pia watoto wake hawachezi nje na watoto wengine wala hajawakanya chochote kuhusu jirani mtata, kama vile wasije wakaingia nyumbani kwa big iwe mvua iwe jua!? Anyway ni hadithi hii, labda tusishupaze sana shingo
Unataka umwone na mtoto akiwa anacheza? [emoji1] Aisee, kama kuna tukio litamhusisha nitamtaja kama hamna hutokaa umwone kamwe ili nikupe wewe wasaa wa kuiandika familia yako vizuri hapa.
 
Ko steve utakomea hii moja au ndo utadondosha one for the road to mbonji!
 
Ko steve utakomea hii moja au ndo utadondosha one for the road to mbonji!
Dah....itabidi adondoshe hata mbili au tatu tena maana hii tumeisubir kwa muda mrefu sana aisee
 
Mkuu ongeza japo moja aisee mwanzoni nilijua ile mifurushi big wanakunya ndani wanaenda kumwaga nikachukulia poa maana ilikua ndo zangu kipindi flan chuga maji kisoda bas ile mifuko laini ya zamani ilikoma. Kwangu ilikua kila ukiingia kunanuka puu mbaya sjui nlikua nawaza nn mbaya zaid akija mama yeyo nae anafanya yake tunamix tunavizia mtaa umepoa tunaenda kutupa nje mbali kidogo sitasahau mtego niliowekewa na kunaswa mpk nikahama saa kumi usiku sjui naenda wapi life la kukosa ela mtu unakuwa nusu mwehu
Wewe ulikuwa ni mchafu tu.
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 09



KATIKATI ya usiku mke wangu alianza kuongea mwenyewe, mwanzoni nilidhani ni masikio yangu pengine yanasikia vibaya lakini nilipofungua macho kutazama nilibaini kile nilichokisikia kilikuwa ni kweli, mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa usingizini, maongezi ambayo kwa muda kidogo sikufahamu anachokimaanisha.

Kidogo, nikiwa namtazama na kumskiza, akakurupuka toka usingizini, aliponikuta namtazama akakurupuka tena zaidi kabla ya kutulia. Alikuwa ameparwa na hofu sana, macho ameyatoa akihema. Nilimuuliza ni nini kimemsibu lakini kabla hajaniambia kitu alinyoosha mkono wake kwenye swichi akawasha taa alafu akaniambia kwa kunong’ona, “kuna mtu mlangoni.” Akarudia tena akiwa amenishika mkono, “kuna mtu mlangoni.”

Nikatoka kwenda sebuleni kutazama, niliwasha taa nikaufungua mlango lakini huko sikuona kitu. Nilipogeuza uso kumtazama mke wangu nilimwona akiwa amesimama kwenye mlango wa chumbani ananitazama kwa macho ya hofu, nikamwambia hamna mtu hapa mlangoni wala koridoni kisha nikarejea naye chumbani, huko hakutaka tuzime taa abadan, alisema anaogopa sana.

Aliniambia alisikia mtu mwenye sauti kama ya kwake akiwa anagonga na kubisha hodi vilevile kama alivyokuwa anabisha hodi muda ule kwenye mlango wa BIGI. Alijaribu kuniamsha lakini sikuamka, punde kidogo ndo’ akasikia mlango unafunguliwa sebuleni.

Kwa kumtuliza, nikamwambia hiyo ni ndoto tu na jambo hilo ameliota maana alikuwa akilifikiria sana, cha muhimu apuuzie kisha alale hamna chochote kitakachotokea, kishingo upande akalala lakini akinisisitiza tena nisizime taa. Kama baada ya lisaa hivi akapitiwa na usingizi, lakini hakukucha mpaka asubuhi akawa anashtuka shtuka, si kwa kuota tena bali kwa uoga wake binafsi. Alikuja kulala kwa amani jua lilipomea.

Siku hiyo kama nilivyokuwa nimepanga, nilienda kumwona Tarimo kule hospitali, huko nikakutana na ndugu yuleyule ambaye nilimkuta siku ile kule Mwananyamala, ndugu huyo alikuwa pamoja na mke wa Tarimo, niliongea naye mambo kadha wa kadha kumhusu mgonjwa na nilipoona ni vema nikondoka zangu kurejea nyumbani. Nilipofika, hata sikupoa, nikapata taarifa kuwa mtoto wa Bembela, yule mwanamke mama ntilie, alizidiwa hoi bin taabani akafanya kuwahishwa hospitali ya Massana!

Yule jirani, mwanamke ambaye nilimdhania kuwa ni yeye ndiye alimpa maneno Bembela jana yake, alirejea majira ya jioni akitokea hospitali alipokuwapo na Bembela na mgonjwa akatuambia yale yaliyokuwa yamejiri, mtoto yule aliamka akiwa na homa kali tangu asubuhi na kutwa akilalamika mwili mzima unamuuma. Alimpatia dawa za kutuliza maumivu akidhani atapoa lakini kadiri muda ulivyoenda hakupata nafuu, ikambidi ampigie simu mama yake aje upesi waende hospitali. Maneno mengine aliyoyasema niliamini ni chumvi tu ya kwetu waswahili, sikuyatilia sana maanani mpaka pale kesho yake asubuhi mimi mwenyewe nilipopata kupitia hospitali ya Massana baada ya kupata upenyo mdogo kazini majira ya mchana, muda wa lunch. Hospitali hiyo haikuwa mbali na eneo ninapofanyia kazi, yaani hapo GOIG, hivyo haikuniwia ugumu kufika upesi kisha nikaendelea na mambo yangu mengine.

Hapo hospitali nilimkuta Bembela akiwa na mwanae kitandani anampatia chakula. Mtoto huyo alionekana hana nguvu, amevalia khanga aliyoifunga shingoni na uso wake unaugulia maumivu. Mwanamke yule, yaani Bembela, akanieleza ya kwamba usiku wa kuamkia siku ile mwanaye alikuwa anasumbuka sana na ndotoni, na mara mbili alikurupuka akisema kuna mtu anampiga, mtu asiyemwona, kwa maelezo hayo akaamini mwanaye anaota yale yaliyotokea siku ile.

Asubuhi ilipowasili, aliondoka kwenda kuendelea na shughuli zake za kawaida, hakuona kama jambo lile ni ishu kubwa, lakini ajabu majira ya baadae ndipo alipigiwa simu na shoga yake akaambiwa hali ya mtoto imekuwa mbaya, aliporejea akamkuta mtoto amevimba na baadhi ya sehemu zake za mwili zimevilia damu, kama haitoshi homa yake ilipanda sana na tena anatapika damu mara kwa mara. Jambo hilo likamshtua maana mpaka anaondoka ile asubuhi hakupata kuona kama kuna cha ajabu kumhusu mwanaye.

Mtoto alipimwa ikabainika ana majeraha ya ndani, lakini pia maumivu yake makali, kwa mujibu wa daktari, hayakusababishwa na kitu kingine isipokuwa kipigo, swala hilo likafanya daktari amtake Bembela kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kwanza kwa kuhofia huenda mtoto yule alikuwa ni mhanga wa ukatili wa majumbani, naye akafanya hivyo lakini akiwa tayari ameshamkabidhi mtoto kwa ajili ya huduma. Lakini ajabu ni kwamba sisi sote tulikuwa tunafahamu kilichomtokea mtoto yule, tukio lililomtokea halikuwa cha kiasi hicho cha kumtia hali mbaya namna ile, hayo mambo ya kuvilia na kutapika damu yalikuwa yanashangaza sana.

Nilipomaliza kumwona mgonjwa nikaenda nyumbani na huko nikaeleza kwa wengine hali ya mtoto. Kesho yake, jumatatu, asubuhi nikiwa kazini nikapigiwa simu kuwa mtoto yule amefariki usiku, hivyo nyumbani kuna msiba. Jambo hilo likanishtua sana kwani sikutegemea kama lingetokea haraka hivyo, ndio mtoto yule alikuwa anaumwa lakini sikudhani kwa jinsi nilivyomwona siku ile basi angelifariki usiku wake. Wenyeji wa yale maeneo watakuwa wanaukumbuka msiba huu vema.

Msiba huo ulipelekwa nyumbani kwa wakina Bembela, maeneo ya Mbezi Mwisho, huko kwa wazazi wake. Wapangaji wote walihidhuria huo msiba isipokuwa bwana BIGI na familia yake. Hakuna aliyepata kuwaona mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. Baadae, kwasababu ya kutokuwepo ama kushinda nyumbani muda mrefu wa siku, nilikuja kupata taarifa kuwa maafisa wa polisi walifika pale nyumbani kuwahoji baadhi ya watu kuhusu kesi ile ya mtoto. Walihitaji kuonana na bwana BIGI na familia yake lakini hakuwapo hata mmoja, wakaomba mawasiliano ya hao watu lakini hamna hata mtu mmoja alokuwa nayo, wengine walidhani mimi ningelikuwa nayo kwasababu ya yale madhali ya kipindi kile kuja naye na pikipiki lakini hata mimi sikuwahi kuwa nayo, basi wakachukua namba ya mwenye nyumba kisha wakajiondokea.

Baadae mimi nikiwa nipo nyumbani naambiwa hayo yaliyotokea, ndipo simu yangu inaita akipiga mwenye nyumba. Bwana huyo akaniambia ametafutwa na polisi anatakiwa atoe taarifa za bwana BIGI na ubaya ni kwamba yeye hana chochote kwani hakuwahi kupeana makaratasi yoyote na yule bwana, aliniuliza kama ninayo namba yake nikamwambia sina, mimi nilimshafikishia BIGI ule ujumbe wake kuhusu mkataba muda mrefu tu hivyo sikufahamu kama muda wote huo hawakupata kuonana, basi yule bwana aka-panick sana, alihofia atawaambia nini polisi wakamwelewa na vipi kama BIGI hatopatikana tena?

Zilipita siku kadhaa, kama mbili au tatu hivi, baadae nikaja kusikia tetesi kwa watu kuwa mtoto yule marehemu kabla ya kukumbana na kifo chake aliendelea kulalamika akiwa pale hospitali ya kwamba maumivu yanamzidi na kumzidi. Ni kana kwamba aliendelea kupigwa na kupigwa lakini alokuwa anampiga haonekani. Zoezi hilo lilidumu kwa muda kidogo tu akapoteza maisha.

Tetesi hizo zilisambaa sana pale nyumbani na zikajenga hofu kubwa kumhusu bwana BIGI, wengine wakarejea kauli ya Bembela akiwa pale mlangoni mwa BIGI kuwa kauli hiyo imemponza, na wengine wakasema bwana huyo hatokuja kurejea tena pale alipokuwa anaishi, kwamba ametoroka baada ya kufanya tukio.

Basi bwana, kama mchezo hivi, siku hiyo nikiwa natoka kazini na pikipiki, nikamwona bwana BIGI akiwa anashuka na begi lake mgongoni mwelekeo wake ni kule nyumbani. Sikujua kwamba ndo alikuwa anarejea nyumbani kutoka safari au alikuwapo tu hapa mjini, na kama anarejea kutoka safari mbona alikuwapo mwenyewe ingali pale nyumbani kwa maelezo ya majirani na polisi familia yake nzima haikuwapo? Au waliongea pasi na uhakika?

Nilimsalimu na kumtaka apande tumalizie safari yetu lakini alikataa, kabla ya kuachana nikamwambia anatafutwa sana na mwenye nyumba kuhusu swala lile la mkataba basi afanye namna wawasiliane, akaniambia anajua kila kitu, na anajua pia polisi wanamhitaji.

Baada ya hapo sikupata kuonana na bwana huyo kwa muda wa siku kadhaa, nilikuja kusikia polisi walionana naye na pia walimwona mtoto wake, yule mwenye utindio, lakini hamna cha maana na kikubwa kilichojiri. Kwa maneno ya yule shoga yake Bembela , maneno ambayo alipata kumwambia mke wangu, Bembela alikuwa amesafiri kwenda mkoani kuonana na mtaalam. Mwanamke huyo , yaani Bembela, hakupata kuwa sawa tena tangu tukio lile la mwanae na aliamini kabisa lina mkono wa mtu.

Lakini mbali na mwanamke huyo, hata mimi mwenyewe mke wangu hakupata kuwa sawa tena tangu siku ile. Hali ambayo ilikuja kupelekea hata baadae mimba yake kuharibika, hili ntakuja kulieleza hapo mbele, lakini punde kama siku chache mbele ya lile tukio, mke wangu alianza kuona siku zake pamoja na kuwa mjamzito.



***
Aiseh inasikitisha
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 09



KATIKATI ya usiku mke wangu alianza kuongea mwenyewe, mwanzoni nilidhani ni masikio yangu pengine yanasikia vibaya lakini nilipofungua macho kutazama nilibaini kile nilichokisikia kilikuwa ni kweli, mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa usingizini, maongezi ambayo kwa muda kidogo sikufahamu anachokimaanisha.

Kidogo, nikiwa namtazama na kumskiza, akakurupuka toka usingizini, aliponikuta namtazama akakurupuka tena zaidi kabla ya kutulia. Alikuwa ameparwa na hofu sana, macho ameyatoa akihema. Nilimuuliza ni nini kimemsibu lakini kabla hajaniambia kitu alinyoosha mkono wake kwenye swichi akawasha taa alafu akaniambia kwa kunong’ona, “kuna mtu mlangoni.” Akarudia tena akiwa amenishika mkono, “kuna mtu mlangoni.”

Nikatoka kwenda sebuleni kutazama, niliwasha taa nikaufungua mlango lakini huko sikuona kitu. Nilipogeuza uso kumtazama mke wangu nilimwona akiwa amesimama kwenye mlango wa chumbani ananitazama kwa macho ya hofu, nikamwambia hamna mtu hapa mlangoni wala koridoni kisha nikarejea naye chumbani, huko hakutaka tuzime taa abadan, alisema anaogopa sana.

Aliniambia alisikia mtu mwenye sauti kama ya kwake akiwa anagonga na kubisha hodi vilevile kama alivyokuwa anabisha hodi muda ule kwenye mlango wa BIGI. Alijaribu kuniamsha lakini sikuamka, punde kidogo ndo’ akasikia mlango unafunguliwa sebuleni.

Kwa kumtuliza, nikamwambia hiyo ni ndoto tu na jambo hilo ameliota maana alikuwa akilifikiria sana, cha muhimu apuuzie kisha alale hamna chochote kitakachotokea, kishingo upande akalala lakini akinisisitiza tena nisizime taa. Kama baada ya lisaa hivi akapitiwa na usingizi, lakini hakukucha mpaka asubuhi akawa anashtuka shtuka, si kwa kuota tena bali kwa uoga wake binafsi. Alikuja kulala kwa amani jua lilipomea.

Siku hiyo kama nilivyokuwa nimepanga, nilienda kumwona Tarimo kule hospitali, huko nikakutana na ndugu yuleyule ambaye nilimkuta siku ile kule Mwananyamala, ndugu huyo alikuwa pamoja na mke wa Tarimo, niliongea naye mambo kadha wa kadha kumhusu mgonjwa na nilipoona ni vema nikondoka zangu kurejea nyumbani. Nilipofika, hata sikupoa, nikapata taarifa kuwa mtoto wa Bembela, yule mwanamke mama ntilie, alizidiwa hoi bin taabani akafanya kuwahishwa hospitali ya Massana!

Yule jirani, mwanamke ambaye nilimdhania kuwa ni yeye ndiye alimpa maneno Bembela jana yake, alirejea majira ya jioni akitokea hospitali alipokuwapo na Bembela na mgonjwa akatuambia yale yaliyokuwa yamejiri, mtoto yule aliamka akiwa na homa kali tangu asubuhi na kutwa akilalamika mwili mzima unamuuma. Alimpatia dawa za kutuliza maumivu akidhani atapoa lakini kadiri muda ulivyoenda hakupata nafuu, ikambidi ampigie simu mama yake aje upesi waende hospitali. Maneno mengine aliyoyasema niliamini ni chumvi tu ya kwetu waswahili, sikuyatilia sana maanani mpaka pale kesho yake asubuhi mimi mwenyewe nilipopata kupitia hospitali ya Massana baada ya kupata upenyo mdogo kazini majira ya mchana, muda wa lunch. Hospitali hiyo haikuwa mbali na eneo ninapofanyia kazi, yaani hapo GOIG, hivyo haikuniwia ugumu kufika upesi kisha nikaendelea na mambo yangu mengine.

Hapo hospitali nilimkuta Bembela akiwa na mwanae kitandani anampatia chakula. Mtoto huyo alionekana hana nguvu, amevalia khanga aliyoifunga shingoni na uso wake unaugulia maumivu. Mwanamke yule, yaani Bembela, akanieleza ya kwamba usiku wa kuamkia siku ile mwanaye alikuwa anasumbuka sana na ndotoni, na mara mbili alikurupuka akisema kuna mtu anampiga, mtu asiyemwona, kwa maelezo hayo akaamini mwanaye anaota yale yaliyotokea siku ile.

Asubuhi ilipowasili, aliondoka kwenda kuendelea na shughuli zake za kawaida, hakuona kama jambo lile ni ishu kubwa, lakini ajabu majira ya baadae ndipo alipigiwa simu na shoga yake akaambiwa hali ya mtoto imekuwa mbaya, aliporejea akamkuta mtoto amevimba na baadhi ya sehemu zake za mwili zimevilia damu, kama haitoshi homa yake ilipanda sana na tena anatapika damu mara kwa mara. Jambo hilo likamshtua maana mpaka anaondoka ile asubuhi hakupata kuona kama kuna cha ajabu kumhusu mwanaye.

Mtoto alipimwa ikabainika ana majeraha ya ndani, lakini pia maumivu yake makali, kwa mujibu wa daktari, hayakusababishwa na kitu kingine isipokuwa kipigo, swala hilo likafanya daktari amtake Bembela kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kwanza kwa kuhofia huenda mtoto yule alikuwa ni mhanga wa ukatili wa majumbani, naye akafanya hivyo lakini akiwa tayari ameshamkabidhi mtoto kwa ajili ya huduma. Lakini ajabu ni kwamba sisi sote tulikuwa tunafahamu kilichomtokea mtoto yule, tukio lililomtokea halikuwa cha kiasi hicho cha kumtia hali mbaya namna ile, hayo mambo ya kuvilia na kutapika damu yalikuwa yanashangaza sana.

Nilipomaliza kumwona mgonjwa nikaenda nyumbani na huko nikaeleza kwa wengine hali ya mtoto. Kesho yake, jumatatu, asubuhi nikiwa kazini nikapigiwa simu kuwa mtoto yule amefariki usiku, hivyo nyumbani kuna msiba. Jambo hilo likanishtua sana kwani sikutegemea kama lingetokea haraka hivyo, ndio mtoto yule alikuwa anaumwa lakini sikudhani kwa jinsi nilivyomwona siku ile basi angelifariki usiku wake. Wenyeji wa yale maeneo watakuwa wanaukumbuka msiba huu vema.

Msiba huo ulipelekwa nyumbani kwa wakina Bembela, maeneo ya Mbezi Mwisho, huko kwa wazazi wake. Wapangaji wote walihidhuria huo msiba isipokuwa bwana BIGI na familia yake. Hakuna aliyepata kuwaona mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. Baadae, kwasababu ya kutokuwepo ama kushinda nyumbani muda mrefu wa siku, nilikuja kupata taarifa kuwa maafisa wa polisi walifika pale nyumbani kuwahoji baadhi ya watu kuhusu kesi ile ya mtoto. Walihitaji kuonana na bwana BIGI na familia yake lakini hakuwapo hata mmoja, wakaomba mawasiliano ya hao watu lakini hamna hata mtu mmoja alokuwa nayo, wengine walidhani mimi ningelikuwa nayo kwasababu ya yale madhali ya kipindi kile kuja naye na pikipiki lakini hata mimi sikuwahi kuwa nayo, basi wakachukua namba ya mwenye nyumba kisha wakajiondokea.

Baadae mimi nikiwa nipo nyumbani naambiwa hayo yaliyotokea, ndipo simu yangu inaita akipiga mwenye nyumba. Bwana huyo akaniambia ametafutwa na polisi anatakiwa atoe taarifa za bwana BIGI na ubaya ni kwamba yeye hana chochote kwani hakuwahi kupeana makaratasi yoyote na yule bwana, aliniuliza kama ninayo namba yake nikamwambia sina, mimi nilimshafikishia BIGI ule ujumbe wake kuhusu mkataba muda mrefu tu hivyo sikufahamu kama muda wote huo hawakupata kuonana, basi yule bwana aka-panick sana, alihofia atawaambia nini polisi wakamwelewa na vipi kama BIGI hatopatikana tena?

Zilipita siku kadhaa, kama mbili au tatu hivi, baadae nikaja kusikia tetesi kwa watu kuwa mtoto yule marehemu kabla ya kukumbana na kifo chake aliendelea kulalamika akiwa pale hospitali ya kwamba maumivu yanamzidi na kumzidi. Ni kana kwamba aliendelea kupigwa na kupigwa lakini alokuwa anampiga haonekani. Zoezi hilo lilidumu kwa muda kidogo tu akapoteza maisha.

Tetesi hizo zilisambaa sana pale nyumbani na zikajenga hofu kubwa kumhusu bwana BIGI, wengine wakarejea kauli ya Bembela akiwa pale mlangoni mwa BIGI kuwa kauli hiyo imemponza, na wengine wakasema bwana huyo hatokuja kurejea tena pale alipokuwa anaishi, kwamba ametoroka baada ya kufanya tukio.

Basi bwana, kama mchezo hivi, siku hiyo nikiwa natoka kazini na pikipiki, nikamwona bwana BIGI akiwa anashuka na begi lake mgongoni mwelekeo wake ni kule nyumbani. Sikujua kwamba ndo alikuwa anarejea nyumbani kutoka safari au alikuwapo tu hapa mjini, na kama anarejea kutoka safari mbona alikuwapo mwenyewe ingali pale nyumbani kwa maelezo ya majirani na polisi familia yake nzima haikuwapo? Au waliongea pasi na uhakika?

Nilimsalimu na kumtaka apande tumalizie safari yetu lakini alikataa, kabla ya kuachana nikamwambia anatafutwa sana na mwenye nyumba kuhusu swala lile la mkataba basi afanye namna wawasiliane, akaniambia anajua kila kitu, na anajua pia polisi wanamhitaji.

Baada ya hapo sikupata kuonana na bwana huyo kwa muda wa siku kadhaa, nilikuja kusikia polisi walionana naye na pia walimwona mtoto wake, yule mwenye utindio, lakini hamna cha maana na kikubwa kilichojiri. Kwa maneno ya yule shoga yake Bembela , maneno ambayo alipata kumwambia mke wangu, Bembela alikuwa amesafiri kwenda mkoani kuonana na mtaalam. Mwanamke huyo , yaani Bembela, hakupata kuwa sawa tena tangu tukio lile la mwanae na aliamini kabisa lina mkono wa mtu.

Lakini mbali na mwanamke huyo, hata mimi mwenyewe mke wangu hakupata kuwa sawa tena tangu siku ile. Hali ambayo ilikuja kupelekea hata baadae mimba yake kuharibika, hili ntakuja kulieleza hapo mbele, lakini punde kama siku chache mbele ya lile tukio, mke wangu alianza kuona siku zake pamoja na kuwa mjamzito.



***
Kalpana To yeye kitalembwa Antonnia PakiJinja
 
Mkuu ongeza japo moja aisee mwanzoni nilijua ile mifurushi big wanakunya ndani wanaenda kumwaga nikachukulia poa maana ilikua ndo zangu kipindi flan chuga maji kisoda bas ile mifuko laini ya zamani ilikoma. Kwangu ilikua kila ukiingia kunanuka puu mbaya sjui nlikua nawaza nn mbaya zaid akija mama yeyo nae anafanya yake tunamix tunavizia mtaa umepoa tunaenda kutupa nje mbali kidogo sitasahau mtego niliowekewa na kunaswa mpk nikahama saa kumi usiku sjui naenda wapi life la kukosa ela mtu unakuwa nusu mwehu
Dah....story yako nayo kali sana aisee[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787], najaribu kuvuta picha siku uliyonaswa ilikuwaje [emoji28][emoji28]...ebu pasimulie japo kidogo mkuu hapo kwenye mtego
 
Dah....story yako nayo kali sana aisee[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787], najaribu kuvuta picha siku uliyonaswa ilikuwaje [emoji28][emoji28]...ebu pasimulie japo kidogo mkuu hapo kwenye mtego
Ilikua balaa mkuu nilikimbizwa nikarushiwa fuko nlilotupa mgongoni likanibwaga nikachezea kichapo raia wamechukua simu saa mkanda viatu soks kila kitu na ela kwenye suruali wanalazmisha nikawape laki mbili home au nile mavi yangu tukaenda mpk home nimevaa niko hoi mpk atm enzi hizo karibu na fire kwa mguu wanatimba nyuma mie mbele nikawapa chao wanasema nenda nikianza kwenda wananilamba fimbo aloo nlitoka nduki magetoni kusanya kila kitu vingine nimeacha nikaanza kuhaha usiku kutafta nyumba kummbuka sina simu nimevimba kote aisee zilikua siku tatu chungu ule mtaa sijapita tena
 
Ilikua balaa mkuu nilikimbizwa nikarushiwa fuko nlilotupa mgongoni likanibwaga nikachezea kichapo raia wamechukua simu saa mkanda viatu soks kila kitu na ela kwenye suruali wanalazmisha nikawape laki mbili home au nile mavi yangu tukaenda mpk home nimevaa niko hoi mpk atm enzi hizo karibu na fire kwa mguu wanatimba nyuma mie mbele nikawapa chao wanasema nenda nikianza kwenda wananilamba fimbo aloo nlitoka nduki magetoni kusanya kila kitu vingine nimeacha nikaanza kuhaha usiku kutafta nyumba kummbuka sina simu nimevimba kote aisee zilikua siku tatu chungu ule mtaa sijapita tena
Pole sana mkuu.....nadhani hukurudia tena huo mchezo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 09



KATIKATI ya usiku mke wangu alianza kuongea mwenyewe, mwanzoni nilidhani ni masikio yangu pengine yanasikia vibaya lakini nilipofungua macho kutazama nilibaini kile nilichokisikia kilikuwa ni kweli, mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa usingizini, maongezi ambayo kwa muda kidogo sikufahamu anachokimaanisha.

Kidogo, nikiwa namtazama na kumskiza, akakurupuka toka usingizini, aliponikuta namtazama akakurupuka tena zaidi kabla ya kutulia. Alikuwa ameparwa na hofu sana, macho ameyatoa akihema. Nilimuuliza ni nini kimemsibu lakini kabla hajaniambia kitu alinyoosha mkono wake kwenye swichi akawasha taa alafu akaniambia kwa kunong’ona, “kuna mtu mlangoni.” Akarudia tena akiwa amenishika mkono, “kuna mtu mlangoni.”

Nikatoka kwenda sebuleni kutazama, niliwasha taa nikaufungua mlango lakini huko sikuona kitu. Nilipogeuza uso kumtazama mke wangu nilimwona akiwa amesimama kwenye mlango wa chumbani ananitazama kwa macho ya hofu, nikamwambia hamna mtu hapa mlangoni wala koridoni kisha nikarejea naye chumbani, huko hakutaka tuzime taa abadan, alisema anaogopa sana.

Aliniambia alisikia mtu mwenye sauti kama ya kwake akiwa anagonga na kubisha hodi vilevile kama alivyokuwa anabisha hodi muda ule kwenye mlango wa BIGI. Alijaribu kuniamsha lakini sikuamka, punde kidogo ndo’ akasikia mlango unafunguliwa sebuleni.

Kwa kumtuliza, nikamwambia hiyo ni ndoto tu na jambo hilo ameliota maana alikuwa akilifikiria sana, cha muhimu apuuzie kisha alale hamna chochote kitakachotokea, kishingo upande akalala lakini akinisisitiza tena nisizime taa. Kama baada ya lisaa hivi akapitiwa na usingizi, lakini hakukucha mpaka asubuhi akawa anashtuka shtuka, si kwa kuota tena bali kwa uoga wake binafsi. Alikuja kulala kwa amani jua lilipomea.

Siku hiyo kama nilivyokuwa nimepanga, nilienda kumwona Tarimo kule hospitali, huko nikakutana na ndugu yuleyule ambaye nilimkuta siku ile kule Mwananyamala, ndugu huyo alikuwa pamoja na mke wa Tarimo, niliongea naye mambo kadha wa kadha kumhusu mgonjwa na nilipoona ni vema nikondoka zangu kurejea nyumbani. Nilipofika, hata sikupoa, nikapata taarifa kuwa mtoto wa Bembela, yule mwanamke mama ntilie, alizidiwa hoi bin taabani akafanya kuwahishwa hospitali ya Massana!

Yule jirani, mwanamke ambaye nilimdhania kuwa ni yeye ndiye alimpa maneno Bembela jana yake, alirejea majira ya jioni akitokea hospitali alipokuwapo na Bembela na mgonjwa akatuambia yale yaliyokuwa yamejiri, mtoto yule aliamka akiwa na homa kali tangu asubuhi na kutwa akilalamika mwili mzima unamuuma. Alimpatia dawa za kutuliza maumivu akidhani atapoa lakini kadiri muda ulivyoenda hakupata nafuu, ikambidi ampigie simu mama yake aje upesi waende hospitali. Maneno mengine aliyoyasema niliamini ni chumvi tu ya kwetu waswahili, sikuyatilia sana maanani mpaka pale kesho yake asubuhi mimi mwenyewe nilipopata kupitia hospitali ya Massana baada ya kupata upenyo mdogo kazini majira ya mchana, muda wa lunch. Hospitali hiyo haikuwa mbali na eneo ninapofanyia kazi, yaani hapo GOIG, hivyo haikuniwia ugumu kufika upesi kisha nikaendelea na mambo yangu mengine.

Hapo hospitali nilimkuta Bembela akiwa na mwanae kitandani anampatia chakula. Mtoto huyo alionekana hana nguvu, amevalia khanga aliyoifunga shingoni na uso wake unaugulia maumivu. Mwanamke yule, yaani Bembela, akanieleza ya kwamba usiku wa kuamkia siku ile mwanaye alikuwa anasumbuka sana na ndotoni, na mara mbili alikurupuka akisema kuna mtu anampiga, mtu asiyemwona, kwa maelezo hayo akaamini mwanaye anaota yale yaliyotokea siku ile.

Asubuhi ilipowasili, aliondoka kwenda kuendelea na shughuli zake za kawaida, hakuona kama jambo lile ni ishu kubwa, lakini ajabu majira ya baadae ndipo alipigiwa simu na shoga yake akaambiwa hali ya mtoto imekuwa mbaya, aliporejea akamkuta mtoto amevimba na baadhi ya sehemu zake za mwili zimevilia damu, kama haitoshi homa yake ilipanda sana na tena anatapika damu mara kwa mara. Jambo hilo likamshtua maana mpaka anaondoka ile asubuhi hakupata kuona kama kuna cha ajabu kumhusu mwanaye.

Mtoto alipimwa ikabainika ana majeraha ya ndani, lakini pia maumivu yake makali, kwa mujibu wa daktari, hayakusababishwa na kitu kingine isipokuwa kipigo, swala hilo likafanya daktari amtake Bembela kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kwanza kwa kuhofia huenda mtoto yule alikuwa ni mhanga wa ukatili wa majumbani, naye akafanya hivyo lakini akiwa tayari ameshamkabidhi mtoto kwa ajili ya huduma. Lakini ajabu ni kwamba sisi sote tulikuwa tunafahamu kilichomtokea mtoto yule, tukio lililomtokea halikuwa cha kiasi hicho cha kumtia hali mbaya namna ile, hayo mambo ya kuvilia na kutapika damu yalikuwa yanashangaza sana.

Nilipomaliza kumwona mgonjwa nikaenda nyumbani na huko nikaeleza kwa wengine hali ya mtoto. Kesho yake, jumatatu, asubuhi nikiwa kazini nikapigiwa simu kuwa mtoto yule amefariki usiku, hivyo nyumbani kuna msiba. Jambo hilo likanishtua sana kwani sikutegemea kama lingetokea haraka hivyo, ndio mtoto yule alikuwa anaumwa lakini sikudhani kwa jinsi nilivyomwona siku ile basi angelifariki usiku wake. Wenyeji wa yale maeneo watakuwa wanaukumbuka msiba huu vema.

Msiba huo ulipelekwa nyumbani kwa wakina Bembela, maeneo ya Mbezi Mwisho, huko kwa wazazi wake. Wapangaji wote walihidhuria huo msiba isipokuwa bwana BIGI na familia yake. Hakuna aliyepata kuwaona mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. Baadae, kwasababu ya kutokuwepo ama kushinda nyumbani muda mrefu wa siku, nilikuja kupata taarifa kuwa maafisa wa polisi walifika pale nyumbani kuwahoji baadhi ya watu kuhusu kesi ile ya mtoto. Walihitaji kuonana na bwana BIGI na familia yake lakini hakuwapo hata mmoja, wakaomba mawasiliano ya hao watu lakini hamna hata mtu mmoja alokuwa nayo, wengine walidhani mimi ningelikuwa nayo kwasababu ya yale madhali ya kipindi kile kuja naye na pikipiki lakini hata mimi sikuwahi kuwa nayo, basi wakachukua namba ya mwenye nyumba kisha wakajiondokea.

Baadae mimi nikiwa nipo nyumbani naambiwa hayo yaliyotokea, ndipo simu yangu inaita akipiga mwenye nyumba. Bwana huyo akaniambia ametafutwa na polisi anatakiwa atoe taarifa za bwana BIGI na ubaya ni kwamba yeye hana chochote kwani hakuwahi kupeana makaratasi yoyote na yule bwana, aliniuliza kama ninayo namba yake nikamwambia sina, mimi nilimshafikishia BIGI ule ujumbe wake kuhusu mkataba muda mrefu tu hivyo sikufahamu kama muda wote huo hawakupata kuonana, basi yule bwana aka-panick sana, alihofia atawaambia nini polisi wakamwelewa na vipi kama BIGI hatopatikana tena?

Zilipita siku kadhaa, kama mbili au tatu hivi, baadae nikaja kusikia tetesi kwa watu kuwa mtoto yule marehemu kabla ya kukumbana na kifo chake aliendelea kulalamika akiwa pale hospitali ya kwamba maumivu yanamzidi na kumzidi. Ni kana kwamba aliendelea kupigwa na kupigwa lakini alokuwa anampiga haonekani. Zoezi hilo lilidumu kwa muda kidogo tu akapoteza maisha.

Tetesi hizo zilisambaa sana pale nyumbani na zikajenga hofu kubwa kumhusu bwana BIGI, wengine wakarejea kauli ya Bembela akiwa pale mlangoni mwa BIGI kuwa kauli hiyo imemponza, na wengine wakasema bwana huyo hatokuja kurejea tena pale alipokuwa anaishi, kwamba ametoroka baada ya kufanya tukio.

Basi bwana, kama mchezo hivi, siku hiyo nikiwa natoka kazini na pikipiki, nikamwona bwana BIGI akiwa anashuka na begi lake mgongoni mwelekeo wake ni kule nyumbani. Sikujua kwamba ndo alikuwa anarejea nyumbani kutoka safari au alikuwapo tu hapa mjini, na kama anarejea kutoka safari mbona alikuwapo mwenyewe ingali pale nyumbani kwa maelezo ya majirani na polisi familia yake nzima haikuwapo? Au waliongea pasi na uhakika?

Nilimsalimu na kumtaka apande tumalizie safari yetu lakini alikataa, kabla ya kuachana nikamwambia anatafutwa sana na mwenye nyumba kuhusu swala lile la mkataba basi afanye namna wawasiliane, akaniambia anajua kila kitu, na anajua pia polisi wanamhitaji.

Baada ya hapo sikupata kuonana na bwana huyo kwa muda wa siku kadhaa, nilikuja kusikia polisi walionana naye na pia walimwona mtoto wake, yule mwenye utindio, lakini hamna cha maana na kikubwa kilichojiri. Kwa maneno ya yule shoga yake Bembela , maneno ambayo alipata kumwambia mke wangu, Bembela alikuwa amesafiri kwenda mkoani kuonana na mtaalam. Mwanamke huyo , yaani Bembela, hakupata kuwa sawa tena tangu tukio lile la mwanae na aliamini kabisa lina mkono wa mtu.

Lakini mbali na mwanamke huyo, hata mimi mwenyewe mke wangu hakupata kuwa sawa tena tangu siku ile. Hali ambayo ilikuja kupelekea hata baadae mimba yake kuharibika, hili ntakuja kulieleza hapo mbele, lakini punde kama siku chache mbele ya lile tukio, mke wangu alianza kuona siku zake pamoja na kuwa mjamzito.



***
Safiiii, Hongera, tunasubiri mwendelezo Mkuu.

Achana na wakosoaji wengine walifeli hicho kiswahili wanachojifanya kukifahamu.
 
Back
Top Bottom