Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Huyo mkeo amepata mimba lini tena?mbona hakuna sehemu umeandika umemgegeda?yaani kumuingiza kwenye story jana tu leo ana mimba? Na hujasema kama uliwahi mgegeda.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hisia zangu zipo sahihi. Hii story umeitunga kizembe, sio kwa sababu haulipwi kuandika story humu basi ndio uje na uongo. Tuliza kichwa, leta story ya kweli, Kama huna pita kushoto
Umeandika ngapi za ukweli Hadi hivi sasa!?
 
Mambo kama hizi zilinifanya mimi nikaachana na story yangu ‘Nilivyokwenda South Africa bila kuwa na ndugu wala rafiki kule’

Watu humu wana ujuaji mwingi wakati mtu anaelezea story ya kweli ya maisha yake
Kumbe upo Mwamba
 
Baada ya kuulizwa mke sasa hivi kila sehemu unampachika. Ngoja nikukumbushe lingine, dada wa kazi(beki tatu) vipi? Maana ni ngumu sana wapangaji wote hao na familia hizo kusiwe na yoyote mwenye dada wa kazi
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 07




Nilitazama ndani ya kiroba kile pasipo kujali harufu yake kali iliyonifanya nizibe pua, ndani yake nikakuta nywele nyingi, sikujua ni nywele za nini na za wapi ila zilikuwa nywele ndefundefu za usinga, nguo zilizojifinyangafinyanga na nyama zilizokuwa zinatoa harufu … nyama ya nini hii? Nilijiuliza nikipekua, kidogo nikakutana na kichwa cha mbuzi, kichwa hicho kilikuwa na pembe fupi ambazo zimengushiwa uzi mwekundu, kukibinua kichwa hicho kukikagua na kukitazama vema mara nikasikia kitu kimedondoka mguuni pangu, nikapatwa na hofu kubwa, niliangaza upesi kwa tochi ya simu nikaona sarafu ya hamsini iko chini, sarafu hiyo ni mpya kama imetoka benki muda huu.

Niliichukua sarafu hiyo nikaiweka mfukoni kisha nikaendelea kupekuapekua kiroba kile kwa kijiti, nywele nyingi nisizozeielewa pamoja na manyoyamanyoya ambayo niliamini ni ya mbuzi yule yalijaa humo, kabla sijamaliza zoezi hilo nikasikia sauti za wanaume wakiwa wanateta, wanaume hao walikuwa wanakuja kutokea upande ule wa bar nilikotokea.

Nilitazama upande huo nikaona mwanga wa tochi ukimulikamulika, na pia nikasikia vishindo vya miguu vikisogea kwa upesi, basi haraka nikaona ni vema nikajificha kwani nikionekana hapo hakuna mtu atakayenielewa kuwa mimi ni mshuhudiaji tu, niliona hilo ni wazo bora kwasababu kama ningejaribu kukimbia ama kurejea katika njia yangu basi wangenikuta kabla sijafanikisha hilo na basi wangehisi kuna kitu kinaendelea na mimi humo korongoni.

Nikajibana nyuma ya mti nikatulia tuli niwezavyo, nikawasikia watu wale wakijongea na kujongea karibu huku wanaongeaongea, tochi yao kali inamulika hapa na pale, mwendo wao wa upesi sana.

Majamaa wale walipofika mahali fulani katikati ya korongo lile, katika kumulikamulika kwao huku na kule, wakamulika kile kiroba nilichokuwa nakipekua, nikamsikia mmoja akisema;

“Oya, nini kile?”

Nilitazama nikiwa hapo nyuma ya mti, nikaona kile kichwa cha mbuzi. Sijui akili yangu ilikuwa wapi, kumbe kile kichwa nilikitupia chini nikakiacha papo hapo, sasa kichwa hicho kilikuwa kimesimama chini kikitazamia kule njiani! Nikahamaki na moyo wangu. Niliogopa watu wale wasije kwa karibu kukitazama kwani wakifanya hivyo tu basi ningekuwa nimekwisha. Japo sikuwa kwa ukaribu mkubwa lakini uwezekano wa kuniona nilipojibana ulikuwa ni mkubwa pia.

Mwingine akamjibu mwenziwe: “Mbona kama kichwa cha mbuzi?” Walimulikamulika maeneo hayo ya karibu huku wakiwa wanaongeaongea kuhusu korongo lile, mimi akili yangu ikiwa inaomba tu wasije wakasogea upande wangu, muda si mrefu wakakata shauri wakaondoka kuendelea na safari yao, hiyo ndo’ ikawa ahueni yangu.

Mabwana wale wakawa wameenda wakiwa wemeniachia funzo kubwa kwani nilihisi nimevuka sana mipaka na sikutakiwa kabisa kufanya yale niliyoyafanya. Vipi kama ningeonekana hapo na watu wakanishuku na kunidhuru kwa ulozi?

Nilitoka nikaenda nyumbani moja kwa moja, hakukuwa na kingine siku hiyo, nilijilaza na kwa msaada wa pombe nilizokunywa siku hiyo nikapitiwa na usingizi mapema ya saa saba, hiyo kwangu ilikuwa ni mapema maana si kawaida yangu. Kesho yake nikaendelea na mambo yangu mengine huku nikiwa najaribu kuona ratiba yangu itakuaje hapo karibuni ili nikapate kumtembelea bwana Tarimo kule Muhimbili.

Ikapita siku na masiku, bado sikwenda kumtazama mgonjwa, kila nilipojifaragua na ratiba ya kazi sikufanikiwa kabisa kupata upenyo hata weekend nilihisi uchovu, kiasi kwamba yule jirani niliyeagana naye kwenda pamoja hospitali akajiendea mwenyewe. Bwana huyo aliendea siku tatu tu baada ya siku ile ya Mwananyamala, mimi nikaapa mwisho wa wiki ijayo, yaani weekend nyingine inayofuata, haswa Jumapili, lazima nitaenda kumwona bwana yule kumjulia hali, kwahiyo kwa wakati wote huo nilikuwa naulizia tu na kupewa habari za mgonjwa toka kwenye vinywa vya watu wengine.

Nakumbuka vema, ilipofika siku ya Jumamosi, yani bado siku moja kwenda kumtembelea mgonjwa kama nilivyopanga, nikiwa nipo nyumbani pamoja na familia majira ya asubuhi, tulisikia tangazo la kipaza sauti likikatiza katika mitaa yetu, kwa mara ya kwanza nikadhani ni watu wa kuuza sumu za panya, mende, kunguni na viroboto maana nao siku hizi wamerahisisha kazi zao kwa vipaza sauti lakini kitambo kidogo tangazo hilo lilifika karibu nikalisikia vema, lilikuwa ni tangazo la kukumbusha kikao cha mtaa wa Mashuka, wito ukitolewa na mwenyekiti.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, kikao kilikuwa kinafanyika kuanzia saa kumi jioni kwenye kiuwanja fulani kidogo ambacho kilikuwepo upande wa kushoto mita chache tu tangu ukiacha njia pana iliyosakafiwa kama unatokea kituo cha Kontena kushuka zaidi kule Mashuka. Kiwanja hiko hakikuwa rasmi, kilikuwa kipo tu katika ‘saiti’ ambayo haikumaliziwa, nyumba fulani hivi ambayo ni kama ilitelekezwa kwa muda kidogo.

Agenda kuu ya kikao hiko ilikuwa ni kujadili kuhusu kumaliziwa kwa barabara ile ya sakafu tokea pale ilipokuwa imeishia, mbele kidogo ya geti la lile ghorofa la bweni la Saint Joseph, iende mpaka mwisho kabisa wa Mashuka, yani njia zima kusiwe na vumbi.

Tangazo hilo kwangu likawa ndo’ mara ya kwanza kulisikia lakini nilipouliza, ‘wife’ akaniambia ni siku ya tatu sasa linapita lakini kwasababu majira yake yalikuwa ni mchana, muda ambao mimi sipo home, ndo’ maana sikupata kulisikia.

Basi baada ya hilo tangazo, nilikaa hapo nyumbani mpaka majira ya mchana nikatoka kwenda Goba centre kwenye mnada. Siku ya Jumamosi kulikuwa na mnada hapo na mimi nilikuwa napendelea kwenda kwasababu ya kuchukua vitu vingi vya ndani kwa bei nzuri kuliko kuchuuza kidogokidogo.

Nilienda huko nikafanya kila kilichonipeleka, wakati wa kurudi, kama kawaida, nilipofika kituo cha Kontena nilishuka na barabara ile iliyosakafiwa kuelekea nyumbani kule Mashuka. Nilipomaliza barabara hiyo nikashika njia ya vumbi, kidogo mbele, pale kwenye kile kiwanja nikakuta tayari watu wameanza kusogeasogea, hapo pamewekwa viti kadhaa vya plastiki tayari kwaajili ya kikao.

Mimi nikanyookea nyumbani kwanza kutua mizigo na kuoga kabisa, kisha nikarejea kujumuika na wale watu wa kwenye kikao. Nilikuta tayari wameshaanza.

Kuhusu ile barabara, nilichosikia kwa maneno ya mwenyekiti, ilikuwa ipo katika mpango wa kuendelea kujengwa kumaliziwa lakini changamoto iliyoibuka ni kwamba kuna baadhi ya makazi ya watu na hata pia magenge yamebana hifadhi hiyo ya barabara, haswa huko Mashuka kwa chini, na watu hao si kwamba wamevamia ama wametenda kosa, la hasha, yale ni maeneo yao kabisa kwa haki hivyo kikao kiliitwa ili pajadiliwe na ikiwezekana watu hao waombwe kutoa sehemu ndogo za maeneo yao kwaajili ya kukamilisha mradi wa barabara ile ilosakafiwa.

Kitendo cha serikali ya mtaa kukaa kimya muda mrefu bila kuiendeleza ile barabara, kuliibua minong’ono kwamba pesa iliyotengwa huenda ilishapigwa, kwasababu hiyo kikao cha kuweka mambo wazi kilikuwa ni muhimu.

Watu wakajadiliana na wakakubaliana, wengine waliokuwa wamiliki wa maeneo husika wakiwa pale, mwisho wa siku ikaadhimiwa mwenyekiti atatengeneza pendekezo rasmi na litafikishwa kwa walengwa, lakini wachache waliokuwepo pale wao waliridhia kabisa kugawa maeneo yao alimradi maendeleo yapite.

Baada ya swala hilo kumalizika mwenyekiti alitoa fursa kwa watu kuuliza ajenda zingine muhimu mbali na ile iliyojadiliwa, katika uwanja huo ndipo mjumbe akaibuka na yale ya kule korongoni juu ya namna gani watu wameligeuza kuwa dampo lisilokuwa rasmi. Mjumbe huyo alieleza kuwa korongo hilo limegeuka kuwa kero kubwa ya harufu kwenye baadhi ya maeneo kitendo ambacho ni hatarishi kwa milipuko ya magonjwa haswa kipindi cha mvua.

Swala hilo likaibua mengine, kuna wajumbe wakasimama na kuituhumu pia shule ya St. Joseph wakisema shule hiyo imekuwa ikielekezea uchafu wake wa machemba kule kwenye lile korongo. Punde chemba zao zinapojaa basi wanazifungulia kumwagia korongoni na ndo’ maana halijawahi kuonekana gari lolote la kunyonya maji machafu hapo shuleni tangu kuanza kwake kwa shughuli.

Basi swala hilo mwenyekiti akaahidi kulifanyia kazi lakini pia akapiga marufuku kwa mtu yeyote kutupa taka kule korongoni na endapo yeyote akikamatwa basi atawajibishwa. Katika kutimiza hilo, tena likijumuishwa na swala la wezi majira ya usiku wa manane ambalo kumbe lilishawahi kuongelewa kwenye vikao vya nyuma, mwenyekiti pamoja na wajumbe wakaazimia kuwe na ulinzi shirikishi katika maeneo yale japokuwa mimi mpaka naondoka kikaoni haikuelezwa wazi oparesheni hiyo itaanza rasmi lini.

Nilishika njia ya kurejea nyumbani, nikajikuta napatana na majirani wenzangu wawili wa kuongozana nao, majirani hao nao walikuwa katika kile kikao hivyo tuliongozana kwa pamoja tukiyajadili yale yaliyozungumzwa kikaoni, mwelekeo wetu ukiwa mmoja, hapo majira sasa yakiwa yanaelekea kuwa giza la saa moja.

Kufika getini tulipokelewa na sauti ya kilio cha mtoto, mtoto ambaye mimi sikumfahamu ni nani kwa sauti yake hiyo. Tuliingia ndani tukakuta wanawake wawili wakiwa wanahangaika na mtoto mmoja wa kike anayeishi humu ndani, mtoto wa kama miaka kumi hivi kwa makadirio, ambaye alikuwa analia kwa machozi mengi huku amejishika kichwa.

Mtoto huyo nilipomtazama vema, kwa upande wake ule wa pili, alikuwa anavuja damu kichwani, juu kidogo ya sikio lake la kushoto. Mkono wake ulioshika hilo jeraha ulikuwa umelowa damu vidoleni.

Kabla sijafanya jambo, nikamwona ‘wife’ anakuja kwa kasi akitokea nyumba kubwa, amevalia khanga kiunoni na kifuani, akasema: “Hamna mtu ndani, yupo yule mtoto peke yake. Nimegonga na kuita lakini kimya, mlango ameufunga kwa ndani.”

Katika maongezi yalojiri hapo nikabaini kuwa yule mtoto wa BIGI ndiye aliyemjeruhi mtoto huyo kisha akakimbilia ndani na kujifungia, lakini zaidi katika maongezi hayo nikabaini kuwa mtoto yule wa BIGI kumbe hakuwa mtoto mzima kama wengine bali ana matatizo makubwa ya akili. Hata muda huo tukiwa tunazungumza na kumpatia huduma mtoto yule aliyejeruhiwa, yeye alikuwa dirishani akitutazama. Mimi nilimwona.

Lakini zaidi ya yote, nilijikuta napoteza yale yote niliyokuwa nayajenga kwaajili ya usalama wa familia yangu … si jingine bali jambo la kutokutaka kuwahusisha kwenye lolote lile kuhusu mwenendo wa yule jirani.


***

kazi ipo
 
Pole sana mkuu.....nadhani hukurudia tena huo mchezo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sikuwahi aisee kwanza najiuliza sana ilikuaje sjui ndo uyu big aliniroga nifanye undezi
 
Tupo wengi kumbe..mimi hata movie nione kiss naonaga ina ujinga na utoto🚮..thats why sipendi movies


Vipi na yule muheshiwa wako alipokuwa anaondoka Belgium airport alikuwa akila denda na mzungu, katika hali ile ulijisikiaje??, hukuzimia kweli?? 🤣🤣
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 09



KATIKATI ya usiku mke wangu alianza kuongea mwenyewe, mwanzoni nilidhani ni masikio yangu pengine yanasikia vibaya lakini nilipofungua macho kutazama nilibaini kile nilichokisikia kilikuwa ni kweli, mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa usingizini, maongezi ambayo kwa muda kidogo sikufahamu anachokimaanisha.

Kidogo, nikiwa namtazama na kumskiza, akakurupuka toka usingizini, aliponikuta namtazama akakurupuka tena zaidi kabla ya kutulia. Alikuwa ameparwa na hofu sana, macho ameyatoa akihema. Nilimuuliza ni nini kimemsibu lakini kabla hajaniambia kitu alinyoosha mkono wake kwenye swichi akawasha taa alafu akaniambia kwa kunong’ona, “kuna mtu mlangoni.” Akarudia tena akiwa amenishika mkono, “kuna mtu mlangoni.”

Nikatoka kwenda sebuleni kutazama, niliwasha taa nikaufungua mlango lakini huko sikuona kitu. Nilipogeuza uso kumtazama mke wangu nilimwona akiwa amesimama kwenye mlango wa chumbani ananitazama kwa macho ya hofu, nikamwambia hamna mtu hapa mlangoni wala koridoni kisha nikarejea naye chumbani, huko hakutaka tuzime taa abadan, alisema anaogopa sana.

Aliniambia alisikia mtu mwenye sauti kama ya kwake akiwa anagonga na kubisha hodi vilevile kama alivyokuwa anabisha hodi muda ule kwenye mlango wa BIGI. Alijaribu kuniamsha lakini sikuamka, punde kidogo ndo’ akasikia mlango unafunguliwa sebuleni.

Kwa kumtuliza, nikamwambia hiyo ni ndoto tu na jambo hilo ameliota maana alikuwa akilifikiria sana, cha muhimu apuuzie kisha alale hamna chochote kitakachotokea, kishingo upande akalala lakini akinisisitiza tena nisizime taa. Kama baada ya lisaa hivi akapitiwa na usingizi, lakini hakukucha mpaka asubuhi akawa anashtuka shtuka, si kwa kuota tena bali kwa uoga wake binafsi. Alikuja kulala kwa amani jua lilipomea.

Siku hiyo kama nilivyokuwa nimepanga, nilienda kumwona Tarimo kule hospitali, huko nikakutana na ndugu yuleyule ambaye nilimkuta siku ile kule Mwananyamala, ndugu huyo alikuwa pamoja na mke wa Tarimo, niliongea naye mambo kadha wa kadha kumhusu mgonjwa na nilipoona ni vema nikondoka zangu kurejea nyumbani. Nilipofika, hata sikupoa, nikapata taarifa kuwa mtoto wa Bembela, yule mwanamke mama ntilie, alizidiwa hoi bin taabani akafanya kuwahishwa hospitali ya Massana!

Yule jirani, mwanamke ambaye nilimdhania kuwa ni yeye ndiye alimpa maneno Bembela jana yake, alirejea majira ya jioni akitokea hospitali alipokuwapo na Bembela na mgonjwa akatuambia yale yaliyokuwa yamejiri, mtoto yule aliamka akiwa na homa kali tangu asubuhi na kutwa akilalamika mwili mzima unamuuma. Alimpatia dawa za kutuliza maumivu akidhani atapoa lakini kadiri muda ulivyoenda hakupata nafuu, ikambidi ampigie simu mama yake aje upesi waende hospitali. Maneno mengine aliyoyasema niliamini ni chumvi tu ya kwetu waswahili, sikuyatilia sana maanani mpaka pale kesho yake asubuhi mimi mwenyewe nilipopata kupitia hospitali ya Massana baada ya kupata upenyo mdogo kazini majira ya mchana, muda wa lunch. Hospitali hiyo haikuwa mbali na eneo ninapofanyia kazi, yaani hapo GOIG, hivyo haikuniwia ugumu kufika upesi kisha nikaendelea na mambo yangu mengine.

Hapo hospitali nilimkuta Bembela akiwa na mwanae kitandani anampatia chakula. Mtoto huyo alionekana hana nguvu, amevalia khanga aliyoifunga shingoni na uso wake unaugulia maumivu. Mwanamke yule, yaani Bembela, akanieleza ya kwamba usiku wa kuamkia siku ile mwanaye alikuwa anasumbuka sana na ndotoni, na mara mbili alikurupuka akisema kuna mtu anampiga, mtu asiyemwona, kwa maelezo hayo akaamini mwanaye anaota yale yaliyotokea siku ile.

Asubuhi ilipowasili, aliondoka kwenda kuendelea na shughuli zake za kawaida, hakuona kama jambo lile ni ishu kubwa, lakini ajabu majira ya baadae ndipo alipigiwa simu na shoga yake akaambiwa hali ya mtoto imekuwa mbaya, aliporejea akamkuta mtoto amevimba na baadhi ya sehemu zake za mwili zimevilia damu, kama haitoshi homa yake ilipanda sana na tena anatapika damu mara kwa mara. Jambo hilo likamshtua maana mpaka anaondoka ile asubuhi hakupata kuona kama kuna cha ajabu kumhusu mwanaye.

Mtoto alipimwa ikabainika ana majeraha ya ndani, lakini pia maumivu yake makali, kwa mujibu wa daktari, hayakusababishwa na kitu kingine isipokuwa kipigo, swala hilo likafanya daktari amtake Bembela kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kwanza kwa kuhofia huenda mtoto yule alikuwa ni mhanga wa ukatili wa majumbani, naye akafanya hivyo lakini akiwa tayari ameshamkabidhi mtoto kwa ajili ya huduma. Lakini ajabu ni kwamba sisi sote tulikuwa tunafahamu kilichomtokea mtoto yule, tukio lililomtokea halikuwa cha kiasi hicho cha kumtia hali mbaya namna ile, hayo mambo ya kuvilia na kutapika damu yalikuwa yanashangaza sana.

Nilipomaliza kumwona mgonjwa nikaenda nyumbani na huko nikaeleza kwa wengine hali ya mtoto. Kesho yake, jumatatu, asubuhi nikiwa kazini nikapigiwa simu kuwa mtoto yule amefariki usiku, hivyo nyumbani kuna msiba. Jambo hilo likanishtua sana kwani sikutegemea kama lingetokea haraka hivyo, ndio mtoto yule alikuwa anaumwa lakini sikudhani kwa jinsi nilivyomwona siku ile basi angelifariki usiku wake. Wenyeji wa yale maeneo watakuwa wanaukumbuka msiba huu vema.

Msiba huo ulipelekwa nyumbani kwa wakina Bembela, maeneo ya Mbezi Mwisho, huko kwa wazazi wake. Wapangaji wote walihidhuria huo msiba isipokuwa bwana BIGI na familia yake. Hakuna aliyepata kuwaona mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. Baadae, kwasababu ya kutokuwepo ama kushinda nyumbani muda mrefu wa siku, nilikuja kupata taarifa kuwa maafisa wa polisi walifika pale nyumbani kuwahoji baadhi ya watu kuhusu kesi ile ya mtoto. Walihitaji kuonana na bwana BIGI na familia yake lakini hakuwapo hata mmoja, wakaomba mawasiliano ya hao watu lakini hamna hata mtu mmoja alokuwa nayo, wengine walidhani mimi ningelikuwa nayo kwasababu ya yale madhali ya kipindi kile kuja naye na pikipiki lakini hata mimi sikuwahi kuwa nayo, basi wakachukua namba ya mwenye nyumba kisha wakajiondokea.

Baadae mimi nikiwa nipo nyumbani naambiwa hayo yaliyotokea, ndipo simu yangu inaita akipiga mwenye nyumba. Bwana huyo akaniambia ametafutwa na polisi anatakiwa atoe taarifa za bwana BIGI na ubaya ni kwamba yeye hana chochote kwani hakuwahi kupeana makaratasi yoyote na yule bwana, aliniuliza kama ninayo namba yake nikamwambia sina, mimi nilimshafikishia BIGI ule ujumbe wake kuhusu mkataba muda mrefu tu hivyo sikufahamu kama muda wote huo hawakupata kuonana, basi yule bwana aka-panick sana, alihofia atawaambia nini polisi wakamwelewa na vipi kama BIGI hatopatikana tena?

Zilipita siku kadhaa, kama mbili au tatu hivi, baadae nikaja kusikia tetesi kwa watu kuwa mtoto yule marehemu kabla ya kukumbana na kifo chake aliendelea kulalamika akiwa pale hospitali ya kwamba maumivu yanamzidi na kumzidi. Ni kana kwamba aliendelea kupigwa na kupigwa lakini alokuwa anampiga haonekani. Zoezi hilo lilidumu kwa muda kidogo tu akapoteza maisha.

Tetesi hizo zilisambaa sana pale nyumbani na zikajenga hofu kubwa kumhusu bwana BIGI, wengine wakarejea kauli ya Bembela akiwa pale mlangoni mwa BIGI kuwa kauli hiyo imemponza, na wengine wakasema bwana huyo hatokuja kurejea tena pale alipokuwa anaishi, kwamba ametoroka baada ya kufanya tukio.

Basi bwana, kama mchezo hivi, siku hiyo nikiwa natoka kazini na pikipiki, nikamwona bwana BIGI akiwa anashuka na begi lake mgongoni mwelekeo wake ni kule nyumbani. Sikujua kwamba ndo alikuwa anarejea nyumbani kutoka safari au alikuwapo tu hapa mjini, na kama anarejea kutoka safari mbona alikuwapo mwenyewe ingali pale nyumbani kwa maelezo ya majirani na polisi familia yake nzima haikuwapo? Au waliongea pasi na uhakika?

Nilimsalimu na kumtaka apande tumalizie safari yetu lakini alikataa, kabla ya kuachana nikamwambia anatafutwa sana na mwenye nyumba kuhusu swala lile la mkataba basi afanye namna wawasiliane, akaniambia anajua kila kitu, na anajua pia polisi wanamhitaji.

Baada ya hapo sikupata kuonana na bwana huyo kwa muda wa siku kadhaa, nilikuja kusikia polisi walionana naye na pia walimwona mtoto wake, yule mwenye utindio, lakini hamna cha maana na kikubwa kilichojiri. Kwa maneno ya yule shoga yake Bembela , maneno ambayo alipata kumwambia mke wangu, Bembela alikuwa amesafiri kwenda mkoani kuonana na mtaalam. Mwanamke huyo , yaani Bembela, hakupata kuwa sawa tena tangu tukio lile la mwanae na aliamini kabisa lina mkono wa mtu.

Lakini mbali na mwanamke huyo, hata mimi mwenyewe mke wangu hakupata kuwa sawa tena tangu siku ile. Hali ambayo ilikuja kupelekea hata baadae mimba yake kuharibika, hili ntakuja kulieleza hapo mbele, lakini punde kama siku chache mbele ya lile tukio, mke wangu alianza kuona siku zake pamoja na kuwa mjamzito.



***
Tivu kanyaga twendeeee
Boma liwanza
 
Back
Top Bottom