Utake ama usitake sisi kusema ni lazima tu mkuu na ukiona unakasirika basi ujue wewe si muungwana. Cheki haya:-
A.Mke kwenye intro unae lakini Stori ilivyoanza hukuwa nae (na ikapendeza uwe huna mke). Kuna waliotetea kwamba mke alitajwa kwenye geti limefungwa na Bonge huku ukiwa bafuni. Labda wenzetu hawawezi kusoma maana ulisema ulisogelea madirisha ya waliokuwa ndani (majirani) na mpaka jirani mwenyewe akakuona kabla hujagonga Wala kumwita sasa hapo mke yukwapi?
B.Umesema mke hakukuwA na sababu ya kumtaja maana hakukuwA na sehemu ya mojakwamoja ya yeye kuingia mapema ikaendana na stori. Wakati huohuo umesahau Kuna Stori kibao umezirefusha ambazo basins muunganiko wa mojakwamoja na stori. Mfano story za agenda za mkutano mpaka zilivyowasilishwa, Stori ya mama Bembela, na mifano mingine
C.Unalala kesho yake lakini hakuna hata mke kukuamsha kwenye usingizi mzito. Unatulia dirishani si chini ya nusu saa lakini hakuna hata mke kushtuka siku moja na kushangaa hata akakuuliza kulikoni. Hospital sijui zahanati mkitaka kwenda mke hakushiriki hata kunyanyua gauni la jirani yake lisiingie kwenye tairi ya pikipiki.
D.Bembela ni jirani yako lakini tena Bembela ni mtoto wa huyohuyo jirani yako. Halafu walikuwa wanazozana lakini kumbe kutoka ni Bembela kamleta mtoto apigwe na kwa Big hayupo aliyetoka sasa sijui alikuwa anazozana na nani. Mtoto wa big ulisema ni chizi like lakini hapo mwisho umetaja watoto kukaongezeka tena kama chizi wa pili ambapo umesema mkeo hakuwa akimjua vizuri kwakuwa alikuwa akifungiwa (au ni Mimi nimeshindwa kusoma na kuelewa labda).
E.Kwa macho ya wanawake lakini mkeo hakuweza kuona mke wa Big anavyokukata jicho. Hakuandalii maji, chakula, hakupokei, Wala hamuagani ukitoka. Tufanye hakuwepo kikaoni basi au alisafiri Kipindi chote Cha mauzauza. Una Kazi Fulani unamalizia kwa Laptop lakini... au basi!
Kuna mtu alisema kadiri unavyoirefusha Stori ndo unavyozidi kuiharibu, nimeamini nilipofika sehemu ya 8. Labda tu niseme wazi Mimi sinaga tabia ya kufuatilia maseason au mastori yenye episodes lakini hii ilinivutia kuifuatilia nikaisoma yote. Kusema ukweli ilipofika kwenye unaenda kilabuni kutafuta mbege nikaanza kukosa mvuto ila nikajikaza nikijua mbele itarudi itakuwa nzuri lakini kwa mpaka kufikia sehemu ya 8 niseme tu safari imenishinda nakung'uta matako naaga mashindano rasmi.
Mtanipa summury mtakaomaliza yote