Jitahidi uwe unaenda haja kubwa mbali na nyumbani

ntuchake

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2024
Posts
408
Reaction score
1,549
Kukata gogo ni moja ya kutoa uchafu mwilini. Katika mambo ya kiroho kukata gogo ni moja ya kutoa mikosi, nuksi na majanga katika mwili wa binafamu. Kwa maana hiyo watu tunashauriwa usipendelee kunya nyumbani.

Jitahidi uwe unaenda kufanya haja kubwa sehemu tofauti ili kama unatoa mikosi, nuksi na majanga yaliyo mwilini uwe unayatolea mbali na sehemu unayoishi ili yasije kukurudia tena. Ukibanwa na haja kubwa usisubiri mpaka ufike nyumbani, tafuta chimbo utoe nuksi na mikosi mbali na nyumbani ili ujikinge mikosi uliyoitoa mwilini isikurudie.
 
wacha suala la mbali na nyumbani watu tuna vyoo chumbani ndo tuna kunya humo na hakuna nuksi tunapeta tu acha imani za kishirikina
 
Sasa hapo si inabidi utoe tumbo kabisa ulitupe mbali🤣maana ata ukinya bado yanakuwepo mengine- huu ni ushirikina kama ushirikina mwingine
 
Hii ni ilmu ahera ama ilmu duniya?
 
Haya mambo ukiya complicate unaweza ona maisha yetu ni meaningless. Kinyesi ni taka mwili tu ambazo hazihusiani na imani yoyote zaidi ya kuhakikisha unakuwa na afya nzuri
 
Wenye vyumba vya choo ndani inakuwaje ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…