Jiwe la Almasi la tatu kwa ukubwa duniani lachimbwa Botswana

Jiwe la Almasi la tatu kwa ukubwa duniani lachimbwa Botswana

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Jiwe kubwa la almasi ambalo ni la tatu kwa ukubwa duniani limepatikana nchini Botswana, katika machimbo ya dhahabu ya Jwaneng yanayotajwa kuwa yenye utajiri mkubwa zaidi wa almasi duniani.

Jiwe hilo lenye ukubwa unaolingana na ngumi lina uzito wa karati 1,098. Thamani ya jiwe hilo inatarajiwa kutajwa ndani ya siku chache zijazo, lakini watafiti wa madini ya almasi wanakadiria kuwa litafikia thamani ya dola bilioni 2 (sawa na Tsh. trilioni 4 na bilioni 638).

Jiwe kubwa zaidi la almasi kuwahi kuchimbwa duniani lilikuwa Cullinan lililochimbwa mwaka 1905, likiwa na uzito wa karati 3,106.75. Jiwe hilo lilikatwa katika vipande ambavyo baadhi yake vinaunda vito vya thamani vya Malkia wa Uingereza (Crown Jewels)

Jiwe la pili kwa ukubwa, Sewelo, lilichimbwa mwaka jana likiwa na uzito wa kareti 1,758 na kununuliwa na Kampuni ya Fasheni ya Ufaransa ya Louis Vuitton.

Kampuni iliyochimba jiwe hili sasa, Debswana, inasema hilo ndio jiwe lake kubwa zaidi kuchimbwa ndani ya miongo mitano (miaka 50) iliyokuwa katika biashara ya uchimbaji.

0_BOTSWANA-MINING-DIAMOND.jpg

Rais wa Botswana, Mokgweetsi Masisi akiwa ameshika jiwe hilo. Picha: AFP
 
Hv wanatumia kwenye nini!?
 
Hv wanatumia kwenye nini!?
Almasi ni ngumu kuliko chuma na madini mengi, kwenye mohs scale score yake ni 10/10. Madini machache sana ni magumu kuliko Almasi, hivyo hutumika kupasua madini mengine, Almasi inapasua miamba, vioo, kwenye ujenzi inatumika kuchimbia, kwenye viwanda inatumika etc. Kifupi ni nyenzo muhimu sana kwenye kuchongea mambo mengine sababu ya ugumu wake.

Sababu ya uzuri na upatikanaji wake mdogo Almasi pia hutumika kwenye mambo ya urembo na utanashati.
 
Almasi ni ngumu kuliko chuma na madini mengi, kwenye mohs scale score yake ni 10/10. Madini machache sana ni magumu kuliko Almasi, hivyo hutumika kupasua madini mengine, Almasi inapasua miamba, vioo, kwenye ujenzi inatumika kuchimbia, kwenye viwanda inatumika etc. Kifupi ni nyenzo muhimu sana kwenye kuchongea mambo mengine sababu ya ugumu wake.

Sababu ya uzuri na upatikanaji wake mdogo Almasi pia hutumika kwenye mambo ya urembo na utanashati.
thank you
 
Almasi ni ngumu kuliko chuma na madini mengi, kwenye mohs scale score yake ni 10/10. Madini machache sana ni magumu kuliko Almasi, hivyo hutumika kupasua madini mengine, Almasi inapasua miamba, vioo, kwenye ujenzi inatumika kuchimbia, kwenye viwanda inatumika etc. Kifupi ni nyenzo muhimu sana kwenye kuchongea mambo mengine sababu ya ugumu wake.

Sababu ya uzuri na upatikanaji wake mdogo Almasi pia hutumika kwenye mambo ya urembo na utanashati.
Mngetuambia hasa kwanini bei yake ni kubwa hivyo yaani robo kilo tu ni trillion TSH.....
 
Mngetuambia hasa kwanini bei yake ni kubwa hivyo yaani robo kilo tu ni trillion TSH.....
Mix ya supply na Matumizi ndio inafanya iwe ghali.

Umeona Matumizi yake yalivyo mengi hivyo ina maana demand ni kubwa.

The Kuna kampuni inaitwa DE beers ambao wamehodhi Almasi nzuri, na Wana release kiasi kidogo sokoni hivyo sababu supply ni ndogo na Matumizi makubwa tena muhimu thamani nayo imekuwa kubwa.
 
Back
Top Bottom