JK atua Dar apokewa na Maandamano ya wana CCM

JK atua Dar apokewa na Maandamano ya wana CCM

Mwambieni basi mheshimiwa akazane kujifunza kiingereza hasa grammar na pronounciation. Nimemsikiliza leo CNN ana problem sana na haya maeneo. Itabidi amuombe Mkapa ampige msasa kidogo.

Duh! Ina maana muda wote huo aliokuwa waziri wa mambo ya nje bado tu lugha inampa shida?
 
Yaani swala la kenya ni dogo haliwezi kuchukua muda wa AU? Ati wao anashughulikia maswala ya maendeleo ya Afrika? Sasa ni maendeleo yapi ya Afrika watakayoshughulikia kama wataawaacha Waafrika walioko Kenya wauane wenyewe kwa wenyewe, wachomeane nyumba, na kuharibiana taratibu za maisha yao ?

Pumba kweli kweli hizi.
 
Yaani swala la kenya ni dogo haliwezi kuchukua muda wa AU? Ati wao anashughulikia maswala ya maendeleo ya Afrika? Sasa ni maendeleo yapi ya Afrika watakayoshughulikia kama wataawaacha Waafrika walioko Kenya wauane wenyewe kwa wenyewe, wachomeane nyumba, na kuharibiana taratibu za maisha yao ?

Pumba kweli kweli hizi.

Kweli kabisa Mkuu Kuchuguu, hizi ni pumba at 'its best'!
Utashughulikia maendeleo ya nani kama watu wanaostahili hayo maendeleo wanakufa?
Huu ni wehu wa hali ya juu?
 
(Samahani kama hii tayari iko kwenye threads zingine)

salamu za lipumba kwa jk


Taarifa ya Mhe Profesa Lipumba juu ya Uteuzi wa Mhe Jakaya Kikwete kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa AU

Kufuatia kuchaguliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Mheshimiwa Prof. Ibrahim Lipumba, ametoa taarifa ifuatayo:

“Nachukua nafasi hii kumpongeza kwa dhati kabisa Rais Jakaya Kikwete kwa heshima kubwa aliyopewa na viongozi wenzake wa nchi za Afrika waliyomchagua kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kwa mwaka huu wa 2008.

Chama Cha Wananchi (CUF) kimezipokea habari hizo kwa furaha kubwa na kinaiona heshima hiyo ni ya Tanzania na Watanzania wote kama Taifa bila ya kujali itikadi zetu za kisiasa. Hapana shaka kwamba kuchaguliwa kwa Rais Kikwete kuuongoza Umoja huo kutasaidia kuzidi kuipandisha chati Tanzania na kuitangaza kimataifa.......

Hii pia ni nafasi adhimu ya kukamilisha mazungumzo ya CCM na CUF ya kuupatia ufumbuzi wa kudumu mpasuko wa kisiasa Zanzibar ili kumpa nafasi Rais Kikwete ya kushughulikia vyema migogoro mingine ya kisiasa barani Afrika, ambalo litakuwa sehemu muhimu ya majukumu yake akiwa Mwenyekiti wa AU.

Namhakikishia Rais kuwa mimi binafsi na Chama cha CUF tutampa kila ushirikiano na msaada anaouhitaji katika kutimiza matumaini ya Waafrika wenzetu waliotuamini kuuongoza Umoja wa Afrika. Kwa mara nyengine tena, tunasema hongera Rais Kikwete.

DAR ES SALAAM
1 Februari, 2008

Mmh, Hizi sifa kwa mtu waliyemtarajia awe mgombea wao 2005 kama CCM wangemtema?😕🙁
 
nampongeza jk kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa au. inabidi ajitahidi ili katika kipindi cha mwaka mmoja awe angalau
amefanikiwa katika jambo moja la kibara (regional issue).

hivi kwa nini mwalimu jkn alikwepa uenyekiti wa oau katika
kipindi chote cha miaka 24 ya uraisi wake? nadhani jibu la hili
linaweza kutueleza undani wa uenyekiti wa au.
 
Wananchi wa Tanzania, walimpokea Lipumba na ni wananchi hao hao walimpokea Muungwana, sio kila ishu ni ya kuwa politicalization,

Kikwete kuwa mwenyekiti wa AU, ni heshima kubwa kwa Tanzania kama taifa, kama vile Lipumba kuwa UN, ni heshima kwa taifa letu pia,

Kama sisi JF hatuelewi hizi simple political facts, basi huko mtaaani hatuwezi kumsaidia mwananchi yoyote kama ambavyo lilivyo lengo letu hapa JF.

Field Marshall ES,
Hakika mimi hukerwa sana na baadhi ya wachangiaji hapa JF. Hawana jambo jingine zaidi ya JK. Lolote linalotokea, wao kitu cha kwanza ni kutupa makombora kwa JK kana kwamba ni genge la kumshambulia Rais. Hata pale ambapo jambo ni la kweli lakini wao hulipindisha makusudi kabisa kwa sababu zao wanazozijua wao. Ninaungana na wewe kabisa kuwaasa hawa jamaa wajiangalie upya kwani wanajipotosha kwa kujijengea elimu ya ujinga. Ni vema wakaitumia JF kwa malengo yaliyokusudiwa si vinginevyo.

Napenda kuchukua nafasi pia kumshukuru Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Haruna Lipumba kwa taarifa yake nzuri ya kumpongeza Rais inayotupa matumaini kwamba sisi sote ni watanzania na pale ambapo pana maslahi ya taifa huongea kama watanzania bila ya kujali itikadi za vyama vyetu.
Nami mimi ninaahidi kama mwananchi wa Tanzania kumpatia ushirikiano mh Rais katika kipindi chake cha uongozi wa AU.
 
Itabidi amuombe Mkapa ampige msasa kidogo.

Did you mean you can "train an old ... new tricks" haya bwana!

So far it is not a big issue... JK jikite kwenye MKUKUTA na MDGs, na kuisaidia Africa,(hapa hakuna KPI ya kufahamu Kizungu, kifaransa, kichina,etc ni maisha bora tu!!!!) after all, si ndio tunataka Kiswali iwe lugha ya Africa...

Chapa kazi achana na hawa vijana wa shule za "FM Academia"
 
nampongeza jk kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa au. inabidi ajitahidi ili katika kipindi cha mwaka mmoja awe angalau
amefanikiwa katika jambo moja la kibara (regional issue).

hivi kwa nini mwalimu jkn alikwepa uenyekiti wa oau katika
kipindi chote cha miaka 24 ya uraisi wake? nadhani jibu la hili
linaweza kutueleza undani wa uenyekiti wa au.

Nyerere hakukwepa uenyekiti wa OAU. Ninavyokumbuka miaka ya 1983/84 au 1984/85 Nyerere alikuwa mwenyekiti wa OAU.
 
WaTanzania haya matusi haya sio mazuri kwenye jamii yetu... unless you are sure off... please don't utter these kind of words...

Kwetu Mwanakwerekwe watu wana hali kama ya pale Kipawa... kwa hiyo naona unatutukana...Yakhee... tutatoana mijino humu...

Kasheshe

Sikuwa na maana ya kutukana ndugu yangu jamii ya aina yeyote, ilikuwa katika kufikisha ujumbe wa watu wa maeneo ya karibu, nadhani utakubaliana nami watu wa Mwanakerekwe inakuwa ngumu sana kwenda uwanja wa ndege kupokea kiongozi.....watanzania tunasifika kuwa kisiwa cha amani...yakhe usinitoe meno tafadhani.bado napenda mifupa...
 
BAADA YA KUCHAGULIWA MWENYEKITI AU


MWENYEKITI wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Kikwete amekiri kuwa anakabiliwa na kazi nzito ya kusuluhulisha migogoro katika nchi kadhaa barani Afrika.

Akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Dar es Salaam, juzi usiku kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa J.K Nyerere, Dar es Salaam, mara baada ya kuwasili akitokea Addis Ababa, Ethiopia, alisema migogoro imekuwa chanzo kikubwa cha kurudisha nyuma maendeleo ya bara hili.

“Ninakabiliwa na kazi moja ngumu ya kushughulikia migogoro kwenye bara letu, imekuwa chanzo kikubwa cha kurudisha nyuma maendeleo yetu kila kunavyokucha,” alisema Rais Kikwete.

Alisema kazi aliyopewa ni ngumu, haiwezi kufananishwa na kazi ya urais wa nchi, lakini kwa kushirikiana na kamati mbalimbali za AU, wanaweza kufikia malengo waliyojiwekea.

“Kazi hii siyo kama kazi ya urais wa nchi, ni ngumu ambayo naamini kwa ushirikiano wa kamati zetu mbalimbali, ikiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya AU tunaweza kufikia yale tuliyojipangia,” alisema.
Alisema anakabiliwa na changamoto nyingi za kupambana na migogoro, ikiwemo ile ya Jimbo la Darfur nchini Sudan, mapigano ya waasi nchini Chad na mvutano wa suala la ushindi wa Rais Mwai Kibaki wa Kenya.
“Migogoro yote hii ni mikubwa, imesababisha tumesahau shughuli za maendeleo, yakiwemo ya kukuza viwanda na mambo mengine,” alisema Rais Kikwete.

Alisema AU inakabiliwa na kazi nyingine ngumu baada ya kundi la waasi kutaka kumuondoa madarakani rais wa Chad na kuwa jukumu hilo amekabidhiwa Rais wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi.
Alisema katika mkutano wa Addis Ababa, viongozi hao wamekubaliana kwa dhamira moja ya kuinua maisha ya wananchi wao na kuepukana na mapigano ya mara kwa mara.

Rais Kikwete alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa AU wiki iliyopita baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa umoja huo, Rais wa Ghana, John Kuffour kumaliza muda wake.
 
NAkubaliana naye kuwa kazi hiyo haiwezi kuwa sana na urais wa nchi...hoja ni kwamba anaiweza? waliposhindwa wenzake yeye ana mikakati gani ya kupaweza? au ndo mfupa uliomshinda fisi?

In the wake ya mambo yalivo nchini kwake mwenyewe...haoni kama huo urais ni kama kumtwisha mzigo mtu aliyelemewa tayari? Kitu gani kilimfanya 'kuukataa' Urais wa AU pindi alipochaguliwa 2005 na kuukubali kipindi hiki? what has changed?
 
Mtazamo wangu unanituma kutoshereheka na uenyekiti wa rais wetu huko AU.
Ili niwe clear, naomba nifahamishwe faida tuipatayo kwa kuwa mwenyekiti wa AU hasa kiuchumi na kiteknolojia.
Pili ni nani ambaye ana nguvu ya maamuzi ktk vikao vyao hao waheshimiwa. Maana tangu vuguvugu la ukombozi wa bara, sisi tumetumika huku tukiiacha nchi yetu fukara wa kutupwa. Lazima tuamke na kuhamasika ili kuweza kusonga mbele kama tunisia (utata), SA, misri na wengineo. Enzi za chenga twawala zimepitwa na wakati na sasa ushindi ni dk tisini na haijalishi how best you can play but how goals you can score and so on.

Watanzania tuache ulimbukeni wa kushabikia shabikia bali tukae na kufikiri what are the prior issues to tackle.

Hongera Mrisho Jakaya ila Am not proud until u create an opportunity for our country.
 
Mwambieni basi mheshimiwa akazane kujifunza kiingereza hasa grammar na pronounciation. Nimemsikiliza leo CNN ana problem sana na haya maeneo. Itabidi amuombe Mkapa ampige msasa kidogo.

Kazi kubwa sana hii,unaacha kuangalia mambo makubwa ya msingi na issues unaanza kusikiliza pronounciation.nani kasema tulimchagua rais kwa kupima kizungu chake?huo ni ukoloni wa kifikra.wapo viongozi wengi sana ambao wanatumia kingereza na bado kinawasumbua duniani.wapo mpaka wasioweza kabisa na bado ni marais bora kabisa.
 
Mtazamo wangu unanituma kutoshereheka na uenyekiti wa rais wetu huko AU.
Ili niwe clear, naomba nifahamishwe faida tuipatayo kwa kuwa mwenyekiti wa AU hasa kiuchumi na kiteknolojia.
Pili ni nani ambaye ana nguvu ya maamuzi ktk vikao vyao hao waheshimiwa. Maana tangu vuguvugu la ukombozi wa bara, sisi tumetumika huku tukiiacha nchi yetu fukara wa kutupwa. Lazima tuamke na kuhamasika ili kuweza kusonga mbele kama tunisia (utata), SA, misri na wengineo. Enzi za chenga twawala zimepitwa na wakati na sasa ushindi ni dk tisini na haijalishi how best you can play but how goals you can score and so on.

Watanzania tuache ulimbukeni wa kushabikia shabikia bali tukae na kufikiri what are the prior issues to tackle.

Hongera Mrisho Jakaya ila Am not proud until u create an opportunity for our country.


Mwenzako amepata kisingizio cha kukimbia nchi tena na tena huku akiiuza vipande kwa vipande. Watanzania wasipoamka watajikuta wakiwa watumwa kwenye nchi yao wenyewe!
 
Back
Top Bottom