JK Vunja Baraza la Mawaziri-Mbowe

JK Vunja Baraza la Mawaziri-Mbowe

Serayamajimbo

Senior Member
Joined
Apr 15, 2009
Posts
191
Reaction score
38
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri kama njia ya kujipanga upya kukabiliana na ufisadi.
Rai hiyo imetolewa juzi na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kata ya Kwale, Pangani, mkoani Tanga.
Hata hivyo, Mbowe alisema haoni kama Rais Kikwete anaweza kuvunja baraza kwa nia hiyo kwani mafisadi wanaopaswa kushughulikiwa ni watu wake wa karibu, na ndio walifadhili kampeni zake za urais.
Mbowe alisema rais anapaswa kuwa mkali na kuwaondoa serikalini baadhi ya mafisadi ambao wamo katika Baraza la Mawaziri. Hata hivyo, hakuwataja majina mafisadi hao.
Alisema kosa kubwa la Rais Kikwete ni “kucheka na mafisadi”. Aliwataka Watanzania kukasirika na kuchukua hatua wakati wa uchaguzi mkuu ujao mwakani.
Wakati huohuo, jana chama hicho kimefanikiwa kuzoa wanachama 60 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) jirani na nyumbani kwa Mbunge wa Muheza, Harbert Mtangi.
Wanachama hao walijiunga na CHADEMA muda mfupi baada ya Mbowe kuhutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Misozwe.
Mbowe aliwaeleza wakazi wa Misozwe kuwa hakuna haja ya kumng’ang’ania mbunge huyo kwa kipindi cha miaka 10 hadi inafika wakati anajiona kama sultani wa kijiji.
Alisema hakuna haja ya kufunga ndoa na mbunge au chama na kama wanaona mbunge hawafanyii cha maana wana haki ya kuchagua mwingine tena wa kutoka chama makini cha CHADEMA.
“Ninyi watu wa Tanga mmefunga ndoa na CCM au mbunge? Mnakaa naye muda wa miaka yote hii na hafanyi mambo ya maendeleo halafu mmemng’ang’ania kujiita eti CCM wakereketwa na huku mkiwa na maisha magumu. Acheni kumfanya mbunge kama sultani,” alisema Mbowe.
Huku akishangiliwa na wananchi, Mbowe alitoa mfano kuwa kama kijiji kuna duka moja lazima muuza duka ataringa, lakini kama kuna maduka mawili mteja una uwezo wa kuchagua duka na kutoa mfano kuwa CCM ni sawa na duka moja, hivyo wanatakiwa kuongeza CHADEMA liwe duka la pili na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Grace Kiwelu, alieleza kusitikitishwa na kitendo cha Mtangi kuvuta umeme kutoka mjini na kuruka nyumba za wapiga kura wake na kuweka kwenye nyumba yake pekee. Alisema kitendo hicho kinaonyesha ni jinsi gani mbunge huyo asivyowajali wapiga kura wake.
 
Akishavunja hilo baraza ndio CHADEMA inapata nini? Wapinzani wa Tanzania jamani wanasikitisha sana. Akivunja anapata sifa ya kuchukua hatua kisha anachaguliwa tena kwa kishindo. Elezeni sera za chama chenu. Hivi toka hawa jamaa wameenda Tanga mmesikia hoja yeyote zaidi ya kelele?
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri kama njia ya kujipanga upya kukabiliana na ufisadi.
Rai hiyo imetolewa juzi na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kata ya Kwale, Pangani, mkoani Tanga.
Hata hivyo, Mbowe alisema haoni kama Rais Kikwete anaweza kuvunja baraza kwa nia hiyo kwani mafisadi wanaopaswa kushughulikiwa ni watu wake wa karibu, na ndio walifadhili kampeni zake za urais.
Mbowe alisema rais anapaswa kuwa mkali na kuwaondoa serikalini baadhi ya mafisadi ambao wamo katika Baraza la Mawaziri. Hata hivyo, hakuwataja majina mafisadi hao.
Alisema kosa kubwa la Rais Kikwete ni “kucheka na mafisadi”. Aliwataka Watanzania kukasirika na kuchukua hatua wakati wa uchaguzi mkuu ujao mwakani.
Wakati huohuo, jana chama hicho kimefanikiwa kuzoa wanachama 60 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) jirani na nyumbani kwa Mbunge wa Muheza, Harbert Mtangi.
Wanachama hao walijiunga na CHADEMA muda mfupi baada ya Mbowe kuhutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Misozwe.
Mbowe aliwaeleza wakazi wa Misozwe kuwa hakuna haja ya kumng’ang’ania mbunge huyo kwa kipindi cha miaka 10 hadi inafika wakati anajiona kama sultani wa kijiji.
Alisema hakuna haja ya kufunga ndoa na mbunge au chama na kama wanaona mbunge hawafanyii cha maana wana haki ya kuchagua mwingine tena wa kutoka chama makini cha CHADEMA.
“Ninyi watu wa Tanga mmefunga ndoa na CCM au mbunge? Mnakaa naye muda wa miaka yote hii na hafanyi mambo ya maendeleo halafu mmemng’ang’ania kujiita eti CCM wakereketwa na huku mkiwa na maisha magumu. Acheni kumfanya mbunge kama sultani,” alisema Mbowe.
Huku akishangiliwa na wananchi, Mbowe alitoa mfano kuwa kama kijiji kuna duka moja lazima muuza duka ataringa, lakini kama kuna maduka mawili mteja una uwezo wa kuchagua duka na kutoa mfano kuwa CCM ni sawa na duka moja, hivyo wanatakiwa kuongeza CHADEMA liwe duka la pili na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Grace Kiwelu, alieleza kusitikitishwa na kitendo cha Mtangi kuvuta umeme kutoka mjini na kuruka nyumba za wapiga kura wake na kuweka kwenye nyumba yake pekee. Alisema kitendo hicho kinaonyesha ni jinsi gani mbunge huyo asivyowajali wapiga kura wake.
du hapa kuna utata ,,je hao wananchi wana kipato cha kuwawezesha kujiwekea umeme??
 
du hapa kuna utata ,,je hao wananchi wana kipato cha kuwawezesha kujiwekea umeme??

Ni wajibu wa mbuge huyo kuwawezesha wapiga kura wake wawe na uwezo wa kujikimu katika maswala muhimu ya kimaisha (basic needs) kama wananchi hawana uwezo huo nani wa kuwawezesha? (bulding capacity). Kwa kuwaruka wananchi wake na kupitisha umeme kwake tu inatuonyesha nini? utawala bora? kwa nini naye asiwe sehemu ya matatizo hayo aishi bila umeme ili atafute suruhisho kwa ujumla? kujiwekea umeme kwake na mkewe ndo maisha bora kwa kila mtanzania aliyoahidi wakati anaomba kura? au kukwepa majukumu yake?

Tumegundua tatizo moja tu la umeme, je mangapi aliyoyafanya bila kuwashirikisha wapiga kura wake (kuwaruka)? huu ndiyo uongozi bora siyo?
 
Ni wajibu wa mbuge huyo kuwawezesha wapiga kura wake wawe na uwezo wa kujikimu katika maswala muhimu ya kimaisha (basic needs) kama wananchi hawana uwezo huo nani wa kuwawezesha? (bulding capacity). Kwa kuwaruka wananchi wake na kupitisha umeme kwake tu inatuonyesha nini? utawala bora? kwa nini naye asiwe sehemu ya matatizo hayo aishi bila umeme ili atafute suruhisho kwa ujumla? kujiwekea umeme kwake na mkewe ndo maisha bora kwa kila mtanzania aliyoahidi wakati anaomba kura? au kukwepa majukumu yake?

Tumegundua tatizo moja tu la umeme, je mangapi aliyoyafanya bila kuwashirikisha wapiga kura wake (kuwaruka)? huu ndiyo uongozi bora siyo?

sio kazi ya mbunge hiyo. huyo kiwelu aliyesema amewezesha nani kupata umeme huko kwao. Siasa za kitoto
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri kama njia ya kujipanga upya kukabiliana na ufisadi.
Rai hiyo imetolewa juzi na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara katika Kata ya Kwale, Pangani, mkoani Tanga.
Hata hivyo, Mbowe alisema haoni kama Rais Kikwete anaweza kuvunja baraza kwa nia hiyo kwani mafisadi wanaopaswa kushughulikiwa ni watu wake wa karibu, na ndio walifadhili kampeni zake za urais.
Mbowe alisema rais anapaswa kuwa mkali na kuwaondoa serikalini baadhi ya mafisadi ambao wamo katika Baraza la Mawaziri. Hata hivyo, hakuwataja majina mafisadi hao.
Alisema kosa kubwa la Rais Kikwete ni “kucheka na mafisadi”. Aliwataka Watanzania kukasirika na kuchukua hatua wakati wa uchaguzi mkuu ujao mwakani.
Wakati huohuo, jana chama hicho kimefanikiwa kuzoa wanachama 60 kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) jirani na nyumbani kwa Mbunge wa Muheza, Harbert Mtangi.
Wanachama hao walijiunga na CHADEMA muda mfupi baada ya Mbowe kuhutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Misozwe.
Mbowe aliwaeleza wakazi wa Misozwe kuwa hakuna haja ya kumng’ang’ania mbunge huyo kwa kipindi cha miaka 10 hadi inafika wakati anajiona kama sultani wa kijiji.
Alisema hakuna haja ya kufunga ndoa na mbunge au chama na kama wanaona mbunge hawafanyii cha maana wana haki ya kuchagua mwingine tena wa kutoka chama makini cha CHADEMA.
“Ninyi watu wa Tanga mmefunga ndoa na CCM au mbunge? Mnakaa naye muda wa miaka yote hii na hafanyi mambo ya maendeleo halafu mmemng’ang’ania kujiita eti CCM wakereketwa na huku mkiwa na maisha magumu. Acheni kumfanya mbunge kama sultani,” alisema Mbowe.
Huku akishangiliwa na wananchi, Mbowe alitoa mfano kuwa kama kijiji kuna duka moja lazima muuza duka ataringa, lakini kama kuna maduka mawili mteja una uwezo wa kuchagua duka na kutoa mfano kuwa CCM ni sawa na duka moja, hivyo wanatakiwa kuongeza CHADEMA liwe duka la pili na kutoa huduma bora kwa wananchi.
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Grace Kiwelu, alieleza kusitikitishwa na kitendo cha Mtangi kuvuta umeme kutoka mjini na kuruka nyumba za wapiga kura wake na kuweka kwenye nyumba yake pekee. Alisema kitendo hicho kinaonyesha ni jinsi gani mbunge huyo asivyowajali wapiga kura wake.

Mbowe ni mzungumzaji mzuri na ni mwanasiasa mwenye akili. Akiendelea na kampeni hizi nchi nzima zinaweza kufanikiwa kupata wanachama na hatimaye kujenga CHADEMA imara. Hata hivyo, kampeni za aina hii zinafaa ziende sambamba na elimu ya uraia kwa wananchi ili wajue haki zao za msingi, kuijua Katiba ya nchi yao na kujua kwamba Serikali inapaswa kuwajibika kwa wananchi.
 
Akishavunja hilo baraza ndio CHADEMA inapata nini? Wapinzani wa Tanzania jamani wanasikitisha sana. Akivunja anapata sifa ya kuchukua hatua kisha anachaguliwa tena kwa kishindo. Elezeni sera za chama chenu. Hivi toka hawa jamaa wameenda Tanga mmesikia hoja yeyote zaidi ya kelele?


Asante sana kwa kuliona hilo, ndio utagundua kuwa hivi vyama viko kwa ajili ya maslahi binafsi.

Mbowe na chama chake ndio walilitaja jina la JK katika list of shame, kuwa naye ni fisadi

Mbowe anajua fika JK kashindwa nchi hii na miaka hii minne hajafanya lolote juu ya mafisadi

Mbowe anajua fika kuwa Kikwete kaingia madarakani kwa fedha za EPA na ni fisadi mzuri tu

Mbowe leo hii anataka atuaminisje JK ni msafi, ila mawaziri wake ndio wabovu, same style with REDET,BBC na akina makamba

Hii statement imetolewa kujikomba kwa JK, na kama ndio hivyo mjue hakuna upinzania nchi hii, these are NGOs, unless nieleweshwe kivingine

Mbowe sorry to say this, achilia mbali matatizo ya chama chako na kubaka demokrasia, achilia mbali matatizo yako ya elimu, nashindwa kujua tukuweke wapi katika statement yako hii,this very statement!

Nikisema mjinga nitakuonea kwani unajua unachofanya, nikisema mpumbavu si kweli maana haukosei unalolitaka

you are opportunist!!! mjasiriamali nguli
 
- Akishavunja then awaingize kina nani? toka ashike power amevinja mara ngapi? Faida yake ilikuwa nini hasa?

- Wote waondoke mara moja, tuanze upya vunja vyama vyote vya siasa, marufuku wote waliowahi kuwa viongozi kugombea tena kwa mujibu wa sheria, tunaanza upyaa!

- Haya maviongozi hasa magoi goi ni reflection yetu wenyewe wananchi!

Respect.


FMEs!
 
Hongera Mbowe kwa kazi nzuri sana na kwa ajili ya kampeni zote Tanzania na pia yeye ni mzungumzaji mkubwa sana
 
Hongera Mbowe kwa kazi nzuri sana na kwa ajili ya kampeni zote Tanzania na pia yeye ni mzungumzaji mkubwa sana

Kazi ipi? tupe rekodi yake huyu kijana toka amekuwa mbunge na mpaka sasa. Alitoa hoja gani bungeni. Aliwasilisha hoja binafsi ngapi. Aliwasilisha miswada mingapi alipokuwa mbunge na kazi nzuri kafanya katika chama chake.

Be precise.
 
Asante sana kwa kuliona hilo, ndio utagundua kuwa hivi vyama viko kwa ajili ya maslahi binafsi.

Mbowe na chama chake ndio walilitaja jina la JK katika list of shame, kuwa naye ni fisadi

Mbowe anajua fika JK kashindwa nchi hii na miaka hii minne hajafanya lolote juu ya mafisadi

Mbowe anajua fika kuwa Kikwete kaingia madarakani kwa fedha za EPA na ni fisadi mzuri tu

Mbowe leo hii anataka atuaminisje JK ni msafi, ila mawaziri wake ndio wabovu, same style with REDET,BBC na akina makamba

Hii statement imetolewa kujikomba kwa JK, na kama ndio hivyo mjue hakuna upinzania nchi hii, these are NGOs, unless nieleweshwe kivingine

Mbowe sorry to say this, achilia mbali matatizo ya chama chako na kubaka demokrasia, achilia mbali matatizo yako ya elimu, nashindwa kujua tukuweke wapi katika statement yako hii,this very statement!

Nikisema mjinga nitakuonea kwani unajua unachofanya, nikisema mpumbavu si kweli maana haukosei unalolitaka

you are opportunist!!! mjasiriamali nguli

Kweli kiongozi wa "Chama mbadala" amechemka.

JK akivunja Baraza la Mawaziri watu wataanza kumsifia tena kwa sana tu, wakati siyo ishu, kwani kama kawa ataweka washkaji zake na watu wa RA na EL kwenye nafasi nyeti kama alivyofanya alivyovunja lile baada ya "kujiuzulu" kwa Lowassa.
Je JK ana nia thabiti ya kuondoa ufisadi? Atamgusaje RA? Si mmemsikia Chikawe anavyotafuta pretext ya kutowashtaki watuhumiwa badala ya kutafuta reasons za kuwakamata?
Dhamira ya kukomesha ufisadi haipo.

Akina Mbowe wanapaswa kumkosoa na kuelezea sera mbadala kwa wananchi bila kuchoka na kurudia tena na tena ili wananchi waendelee kuelewa.
Pia waelezee maamuzi mbadala ambayo wangeyatoa kama wangekuwa ndio wanaongoza Serikali.

Utendaji usioridhisha wa JK umetoa opportunity kwa viongozi mbadala ila hawajachukua opportunity hiyo kujieleza kwa wananchi, kwa lugha na mifano ambayo wananchi wataelewa.

Safari ya ukombozi ni ndefu, ila ni muhimu kusafiri.
 
Back
Top Bottom