Vision2010
Member
- May 28, 2009
- 7
- 0
KILA nchi na jamii inavyo vigezo vyake vinavyotambulisha ubora wa jamii hiyo na watu wake, ndani na nje ya nchi hiyo. Na Tanzania siyo tofauti katika ukweli huu.
Vigezo hivyo viko vingi na kwa namna nyingi na tofauti. Moja ya vigezo vipya vilivyoibuka katika miaka ya karibuni ni teknolojia ya mawasiliano kwa njia ya kompyuta na matumizi yakee.
Mawasiliano hayo pia yako mengi na ya aina mbali mbali vile vile. Moja ya mawasiliano hayo ni matumizi ya blogo na inteneti.
Kama kuna kitu kinathibitisha ubora wa chini kabisa wa mawazo ya baadhi ya Watanzania, na hasa wale vijana waliokimbilia nje kwenda kuzamia ana kujilipua baada ya kwa wamepasua ama kutupa pasi za kusafiria za Tanzania ni aina ya majadiliano kwenye blogo na inteneti za Kitanzania.
Siyo tu kwamba kinachojadiliwa wakati wote ni ujinga, upuuzi, matusi na ukosefu mkubwa sana wa heshima kwa watu wengine. Lakini pia kuna uongo na upotoshaji mwingi, mwingine ukiongozwa na mwelekeo wa kisiasa, mwingine ukiongozwa na ujinga wa kutokujua mambo.
Linganisha blogo na inteneti za Kitanzania na za Waafrika wengine nje ya Bara la Afrika. Angalia inteneti za Wakenya, Waganda, za Waghana, za Afrika Kusini. Watu wanajadili mambo ya maana ya maendeleo yao na kuchuana kikwelikweli kwa nguvu za hoja. Unapata mawazo na maoni adhimu na adimu, siyo matusi na ujinga.
Sisi tumebakia kwenye matusi na ujinga tu. Najua kuwa moja ya matatizo yetu makubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania waliokimbilia nje ni vijana waliokwenda kuzamia na kujilipua tu. Ni watu wasiokuwa na uwezo mkubwa wa elimu, ni watu wasiojua mambo isipokuwa uwezo wa kuvunja sheria za wanakoishi na kuwakimbia polisi. Hivyo haishangazi kuona kiwango cha chini cha mawazo katika inteneti za mawasiliano za Kitanzania.
Iko mifano mingi. Lakini angalia ujinga ambao umekuwa unaandikwa kuhusu ziara ya karibuni ya Rais Kikwete mjini Los Angeles, Marekani, ambako miongoni mwa watu wengine alikutana na nyota watengenezaji na wachezaji sinema kama vile Steven Seagal, Billy Zane na wengine.
Wamejitokeza watu kwa kutumia inteneti za Kitanzania kumkejeli, kumdhihaka kama vile mkutano huo na nyota hao mabilionea hauna manufaa na kama vile mabilionea hawa ni watu wasiostahili kukutana na Rais.
Ni ajabu kwamba mtu anaweza kuishi Marekani, ama nchi yoyote ya Ulaya, na bado akashindwa kujua uwezo umuhimu mkubwa wa watengenezaji na wachezaji sinema hawa.
Hawa siyo waosha masufuria, wanyanyua mizigo viwandani, ama waonya mabehewa ya treni kama tulivyo sisi wengi Watanzania tuliozamia nje. Hawa ni nyota. Ni matajiri wenye fedha nyingi kuweza kuwekeza katika nchi yoyote.
Nyota hao, kwa mfano, wanataka kwenda Tanzania kufungua Tanzania Studios ambazo zitakuwa za kwanza katika sub-saharan Africa kwa sababu studio pekee za kutengenezea na kucheze sinema kwa sasa ziko katika Afrika Kusini tu katika Bara zima la Afrika.
Ikichezwa sinema moja tu katika Tanzania kiasi cha watu 400 ama zaidi watanufaika moja kwa moja na utengenezaji wa sinema hiyo. Ukitilia maanani kuwa kila mtu ana familia ya wastani watu watano, unazungumzia watu 2,000. Hawa ni mbali na wale watakonufaika kwa namna nyingine nyingi zisizokuwa za moja kwa moja.
Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.
Kazi kubwa ya Rais wa nchi yoyote ni kuvutia wawekezaji wenye fedha kwenda kuwekeza katika nchi yake. Mashindano ya dunia ya leo baina ya mataifa ni uwezo wa kuvutia wawezekezaji. Uwekezaji ndiyo unainua uchumi, na uchumi ndiyo uti wa mgongo wa nchi, siyo bla bla za matusi na ujinga wa kwenye inteneti.
Je siyo kweli kuwa kama itatengezwa sinema moja nchini na kuinufaisha nchi kwa kiasi cha dola milioni 200, basi nchi itakuwa imepata kiasi kikubwa zaidi kuliko kiasi chote kinachoingizwa nchini na Watanzania wote walioko nje?
Sasa kejeli ya nini, ama tunajaribu, kwa mara nyingine, kuthibitisha ujinga wetu kama ambavyo tumezoea kujianika hadharani?
Isitoshe kama kweli tunaipenda nchi yetu kama ambavyo baadhi wanaandika kwa uchungu mwingi kuhusu maendeleo ya Tanzania kwa nini tusirudi nchini kwenda kushirikiana na wenzetu ambao wanahangaika usiku mchana kuiendeleza Tanzania.
Sisi tuko huko, tukicheza madisco na kunywa pombe, na tukiamka ni kuporomosha matusi kwa watu ambao wanapinda migongo katika kutafuta jinsi ya kuiendeleza Tanzania na ndugu zetu tuliowakimbia.
Kama kweli tunaijali nchi na ndugu zetu kwa nini tusirejee na kushiriki katika harakati za kuendeleza nchi, badala ya kila siku kushikilia kuwa tupewe dual citizenship? Tunataka urais wa Marekani, ama Uingereza, ama Canada wa nini kama tuna uchungu na nchi yetu ya Tanzania?
Baadhi yetu hatuko honest. Ni wanafiki tu. Tunapenda kufaidi pande zote tukiongozwa na hadhithi ya chako ni changu, na changu ni changu.
Ambani Adnani Joseph
Mtanzania
Los Angeles.
Vigezo hivyo viko vingi na kwa namna nyingi na tofauti. Moja ya vigezo vipya vilivyoibuka katika miaka ya karibuni ni teknolojia ya mawasiliano kwa njia ya kompyuta na matumizi yakee.
Mawasiliano hayo pia yako mengi na ya aina mbali mbali vile vile. Moja ya mawasiliano hayo ni matumizi ya blogo na inteneti.
Kama kuna kitu kinathibitisha ubora wa chini kabisa wa mawazo ya baadhi ya Watanzania, na hasa wale vijana waliokimbilia nje kwenda kuzamia ana kujilipua baada ya kwa wamepasua ama kutupa pasi za kusafiria za Tanzania ni aina ya majadiliano kwenye blogo na inteneti za Kitanzania.
Siyo tu kwamba kinachojadiliwa wakati wote ni ujinga, upuuzi, matusi na ukosefu mkubwa sana wa heshima kwa watu wengine. Lakini pia kuna uongo na upotoshaji mwingi, mwingine ukiongozwa na mwelekeo wa kisiasa, mwingine ukiongozwa na ujinga wa kutokujua mambo.
Linganisha blogo na inteneti za Kitanzania na za Waafrika wengine nje ya Bara la Afrika. Angalia inteneti za Wakenya, Waganda, za Waghana, za Afrika Kusini. Watu wanajadili mambo ya maana ya maendeleo yao na kuchuana kikwelikweli kwa nguvu za hoja. Unapata mawazo na maoni adhimu na adimu, siyo matusi na ujinga.
Sisi tumebakia kwenye matusi na ujinga tu. Najua kuwa moja ya matatizo yetu makubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania waliokimbilia nje ni vijana waliokwenda kuzamia na kujilipua tu. Ni watu wasiokuwa na uwezo mkubwa wa elimu, ni watu wasiojua mambo isipokuwa uwezo wa kuvunja sheria za wanakoishi na kuwakimbia polisi. Hivyo haishangazi kuona kiwango cha chini cha mawazo katika inteneti za mawasiliano za Kitanzania.
Iko mifano mingi. Lakini angalia ujinga ambao umekuwa unaandikwa kuhusu ziara ya karibuni ya Rais Kikwete mjini Los Angeles, Marekani, ambako miongoni mwa watu wengine alikutana na nyota watengenezaji na wachezaji sinema kama vile Steven Seagal, Billy Zane na wengine.
Wamejitokeza watu kwa kutumia inteneti za Kitanzania kumkejeli, kumdhihaka kama vile mkutano huo na nyota hao mabilionea hauna manufaa na kama vile mabilionea hawa ni watu wasiostahili kukutana na Rais.
Ni ajabu kwamba mtu anaweza kuishi Marekani, ama nchi yoyote ya Ulaya, na bado akashindwa kujua uwezo umuhimu mkubwa wa watengenezaji na wachezaji sinema hawa.
Hawa siyo waosha masufuria, wanyanyua mizigo viwandani, ama waonya mabehewa ya treni kama tulivyo sisi wengi Watanzania tuliozamia nje. Hawa ni nyota. Ni matajiri wenye fedha nyingi kuweza kuwekeza katika nchi yoyote.
Nyota hao, kwa mfano, wanataka kwenda Tanzania kufungua Tanzania Studios ambazo zitakuwa za kwanza katika sub-saharan Africa kwa sababu studio pekee za kutengenezea na kucheze sinema kwa sasa ziko katika Afrika Kusini tu katika Bara zima la Afrika.
Ikichezwa sinema moja tu katika Tanzania kiasi cha watu 400 ama zaidi watanufaika moja kwa moja na utengenezaji wa sinema hiyo. Ukitilia maanani kuwa kila mtu ana familia ya wastani watu watano, unazungumzia watu 2,000. Hawa ni mbali na wale watakonufaika kwa namna nyingine nyingi zisizokuwa za moja kwa moja.
Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.
Kazi kubwa ya Rais wa nchi yoyote ni kuvutia wawekezaji wenye fedha kwenda kuwekeza katika nchi yake. Mashindano ya dunia ya leo baina ya mataifa ni uwezo wa kuvutia wawezekezaji. Uwekezaji ndiyo unainua uchumi, na uchumi ndiyo uti wa mgongo wa nchi, siyo bla bla za matusi na ujinga wa kwenye inteneti.
Je siyo kweli kuwa kama itatengezwa sinema moja nchini na kuinufaisha nchi kwa kiasi cha dola milioni 200, basi nchi itakuwa imepata kiasi kikubwa zaidi kuliko kiasi chote kinachoingizwa nchini na Watanzania wote walioko nje?
Sasa kejeli ya nini, ama tunajaribu, kwa mara nyingine, kuthibitisha ujinga wetu kama ambavyo tumezoea kujianika hadharani?
Isitoshe kama kweli tunaipenda nchi yetu kama ambavyo baadhi wanaandika kwa uchungu mwingi kuhusu maendeleo ya Tanzania kwa nini tusirudi nchini kwenda kushirikiana na wenzetu ambao wanahangaika usiku mchana kuiendeleza Tanzania.
Sisi tuko huko, tukicheza madisco na kunywa pombe, na tukiamka ni kuporomosha matusi kwa watu ambao wanapinda migongo katika kutafuta jinsi ya kuiendeleza Tanzania na ndugu zetu tuliowakimbia.
Kama kweli tunaijali nchi na ndugu zetu kwa nini tusirejee na kushiriki katika harakati za kuendeleza nchi, badala ya kila siku kushikilia kuwa tupewe dual citizenship? Tunataka urais wa Marekani, ama Uingereza, ama Canada wa nini kama tuna uchungu na nchi yetu ya Tanzania?
Baadhi yetu hatuko honest. Ni wanafiki tu. Tunapenda kufaidi pande zote tukiongozwa na hadhithi ya chako ni changu, na changu ni changu.
Ambani Adnani Joseph
Mtanzania
Los Angeles.