JK, wengi hamjamwelewa!

JK, wengi hamjamwelewa!

Mzee Karibu Jamvini.

Sifa nyingi ulizoziongelea pengine zinakugusa wewe moja kwa moja Lakini hapa JF kuna two types of Groups.

Moja ni watu ambao ni very patriotic ambao wana nia ya kuona Tanzania bora , when they see anything that doesnt stand for the intrest of Tanzania they speak out and nothing will ever stop them.

Number two kuna watu ambao they are here for special intrest, Wako hapa kuwatetea wale wanaofanya madudu, kwasababu kwa njia moja au nyingine wanafaidi from hayo madudu.

Mheshimiwa bila kukuuliza maswali mengi ninaamini ulikwepo kwenye Dina ya Mheshimiwa Rais pale LA , na pale ndipo ulipoiuzia objectivity yako, Samahani but I think umeuza objectivity yako for a very cheap price yaani kitendo tu cha kuwa na mheshimiwa kwenye chumba kimoja, si kulaumu but watanzania wengi ndio walivyo.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anampinga mheshimiwa Rais kutafuta wawekezaji. Tunacho kiping ni kitendo cha Rais kuchota maji na kuyaweka kwenye pipa lililo toboka. Hauwezi kujaza pipa hata siku moja kama pipa lenyewe ulalo tia maji limetoboka na ndio maana hata kule kwetu uswahilini tunatumia common sense tukishajua hilo pipa limetoboka tunaweka cement chini ya pipa kwanza , na kuzuia kutu isilitoboe tena tunapaka cement pipa zima. Kwakufanya hivi it means hata mvua ya manyunyu inaweza kulijaza hilo pipa.

Mfano huu una maana ya kwamba mheshimiwa Rais inabidi asafishe nyumbani kwanza, leo hata akipata dola Billioni moja , wananchi masikini wataona milioni 10 tu zilizobaki zitaishia kwenye pipa lililotoboka/ufisadi , akisafisha na awafunge mafisadi wote na kuweka mazingira mazuri ya accountability ataweza kufanya any investment anayoipata na kuifanya as multiplier factor but now anapoteza mda na hata pesa kidogo tulizonazo.

Kama wewe ni mtu wa resorning hebu angalia. Kuwafunga mafisadi na kusafisha serikali kama yuko serious it only take three month which will save us alot of money . But hizo Investment unazosema wewe za kutengeneza movie Tanzania, planning and Implimentation yake it take three to four years which means JK atakuwa anakaribia kumaliza mda wake wa kipindi cha pili. Kwahiyo watu sio wanapiga kelele it all goest to time series and what is the priority ya Mheshimiwa and we as people we see that there is many can be done fast and efficiently to improve governmenment perfomance while we are waiting for those opportunities you talking about.

Watu wote walioko kweny Jamiiforums hawako Ulaya na Marekani there are prenty of them in Tanzania utagundua hivyo ukiangalia trend za uchangiaji, karibu sana jamvini but I think we will have more opportunity to exchange ideas and we will give you resorn on why we critical to the president and not otherwise.

Nakubaliana nawe 100%.Misaada mingapi tumeshapewa imeishia kuliwa kwa ufisadi, mfano wa karibu ni Ule wa wizara ya maliasili na utalii. If we really want changes and development, then we have to start working inside out...to clean the house first.Lazima tujue nini kinatakiwa kifanyiwe kazi kwanza na kipi kitafuata baadae. Leo hatuoni hayo..tunanunua radar, ndege ya rais, na mambo mengine kadhaa yasiyo na tija kwa watanzania wengi ila watu wachache. Nionanvyo, hakuna sababu ya kuzunguka dunia nzima kuomba misaada bila kujipanga vizuri kujua nini chakufanya na tufanye vipi. Hata kama tutapewa misaada kutoka kila upande, huu wizi na ukosefu wa uadilifu utazitapanya fedha hizo bila kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kama misaada inayoletwa inafanya vitu vinavyoonekana sidhani kama watu watakuwa na maswali mwngi ya kuuliza. Ninachojiuliza kila wakati ni hiki, hivi mbona misaada haileti maendeleo tunayokusudia?Kila kukicha ni kashfa tu na mwendo wa walio wengi kwenye maendeleo ni mdogo kuliko wa kinyonga.Lini Tutafika tunakokuta na misaada so far haijanishawishi bado kama ni njia muafaka ya kufikia hayo maendeleo
 
Wapendwa wana JF, mimi ni mara ya kwanza kuandika katika jamii hii.

Sikupendezwa na maelezo ya Ndugu Ambani Adnani Joseph kwa sababu hayana ukweli wa utafiti wa kina.

Ninachoweza kukiona ni kuwa mpendwa mwenzetu ametoa mawazo yake kama yeye ingawa amejitahidi sana kuonesha kuwa watanzania wote akiwemo yeye tunajadili ujinga, upuuzi, matusi na ukosefu mkubwa wa heshima kwa watu wengine. " Mpendwa Ambani Adnani Joseph kweli umetukosea heshima watanzania wenzako kwa kauli zako"

Nimeona hoja mbalimbali zailizotolewa hapo juu na watanzania wengine. Nakubaliana nazo ila ninaushauri ufuatao kwa ndugu yetu Ambani,

Fanya utafiti na uwe na uhakika ndo useme kwani,
1. Hizo blog za wakenya, waganda, waghana na south africa zina madudu mabaya ya ajabu na hawajadili ya maana kama tunayojadili watanzania. Ninao waganda, wakenya, Wanyarwanda, warundi wengi hapa China na wote wanatusifu sana kwenye blog zetu ukilinganisha na zao.
2. Wanaopinga ziara za kikwete nje ya nchi.... hawana mawazo kama yako. Wanaona kuwa anapiga hatua ya mbele wakati kuna mambo anatakiwa ayaweke sawa hapa nyumbani ndo atafute hao mabilionea. Asimwage hizo bilioni kwenye pipa lenye mashimo. (Elewa mada hapo)
3. Sina takwimu za mtanzania hata mmoja aliyejilipua kwa mabomu akiwa ughaibuni. Tunae mtanzania mmoja tu anayesadikiwa kuwa karibu na mtandao wa osama bin laden. Je, unauhakika kuwa watanzania walioko ndani na nje ni wajinga? Tupe data sahihi?

Nikushauri utuombe radhi.
 
Linganisha blogo na inteneti za Kitanzania na za Waafrika wengine nje ya Bara la Afrika. Angalia inteneti za Wakenya, Waganda, za Waghana, za Afrika Kusini. Watu wanajadili mambo ya maana ya maendeleo yao na kuchuana kikwelikweli kwa nguvu za hoja. Unapata mawazo na maoni adhimu na adimu, siyo matusi na ujinga.

Sisi tumebakia kwenye matusi na ujinga tu. Najua kuwa moja ya matatizo yetu makubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania waliokimbilia nje ni vijana waliokwenda kuzamia na kujilipua tu. Ni watu wasiokuwa na uwezo mkubwa wa elimu, ni watu wasiojua mambo isipokuwa uwezo wa kuvunja sheria za wanakoishi na kuwakimbia polisi. Hivyo haishangazi kuona kiwango cha chini cha mawazo katika inteneti za mawasiliano za Kitanzania.

Kagoda, Meremeta, Safari za nje zinazolipa fadhila kwa msafara, Kujuana makazini, kupeana ajira kindugu huku kote sio kuvunja sheria. Kuiba kura nk huu ndio utawala wa sheria na usawa.

Iko mifano mingi. Lakini angalia ujinga ambao umekuwa unaandikwa kuhusu ziara ya karibuni ya Rais Kikwete mjini Los Angeles, Marekani, ambako miongoni mwa watu wengine alikutana na nyota watengenezaji na wachezaji sinema kama vile Steven Seagal, Billy Zane na wengine.

ziara zake nyingi sana anakutana na nyota wengi, kama vile Kris taker, Boys 11 men nk nini wamefanya mpaka sasa kwa kutana nao, na wote hao hutoa ahadi hewa. na wajinga ndio mnaoliwa.

Wamejitokeza watu kwa kutumia inteneti za Kitanzania kumkejeli, kumdhihaka kama vile mkutano huo na nyota hao mabilionea hauna manufaa na kama vile mabilionea hawa ni watu wasiostahili kukutana na Rais.

Kwa sababu ameshakutana na wengi na porojo ni nyingi sana na kodi zetu zinaendelea kuliwa kwa safari zisizo na manufaa. Kwani hata wale wakulima msiowapenda sasa nao wanauelewa wa kotosha. Kikwete anakuja kuona miji na kusingizia anashawishi wawekezaji miaka mitano kaka imekwisha nani yuko Dar tangia aanze kuongea nao.

Ni ajabu kwamba mtu anaweza kuishi Marekani, ama nchi yoyote ya Ulaya, na bado akashindwa kujua uwezo umuhimu mkubwa wa watengenezaji na wachezaji sinema hawa.

Hawa siyo waosha masufuria, wanyanyua mizigo viwandani, ama waonya mabehewa ya treni kama tulivyo sisi wengi Watanzania tuliozamia nje. Hawa ni nyota. Ni matajiri wenye fedha nyingi kuweza kuwekeza katika nchi yoyote.

kwani kuwa nyota ndio uwekezaji?? Kama tu ndio unachokistaajabia basi utastaajibia mengi. Mwekezaji gani anaweza kuwekeza sehemu isiyo na hospitali inayofaa, barabara mbovu, urasimu narushwa iliyokithiri, maji kitim tim zaidi ya yote Umeme wa Richmond usio waka, sasa hiyo mitambo yenu ya sinema sijui mtatumia nishati gani, mwekezaji gani anaomba kuanza kazi ya uwekezaji kama hajafanya utafiti wa hali ya sehemu huu ni uongo usio na kifani. Walikuwa wanabarizi kama kawa.



Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.

Hii kali, $200mil.
Kama kweli bajeti ya sinema itakuwa $200mil kutokana uelewa wa wangu wa malipo ya kazi marekani na nchi nyingi zilizoendelea mishahara ndio yenye gharama kubwa sana kati ya 60% na 70% ya gharama zote.
Sasa unataka kusema kwamba wachezaji sinema watakuwa wamatumbi hivyo kuchota kitita chote cha bajeti ya sinema?
Je hii studia itakuwa ni kwa ajili ya nani ya watanzania au hollywood, je Tanzania soko letu la movie likoje na East afrika kwa ujumla?? Kaka hapa naona umeandika tu ili kujifurahisha kwanza bajeti ya movie $200mil kama ziko sio za hao jamaa zako.

Kazi kubwa ya Rais wa nchi yoyote ni kuvutia wawekezaji wenye fedha kwenda kuwekeza katika nchi yake. Mashindano ya dunia ya leo baina ya mataifa ni uwezo wa kuvutia wawezekezaji. Uwekezaji ndiyo unainua uchumi, na uchumi ndiyo uti wa mgongo wa nchi, siyo bla bla za matusi na ujinga wa kwenye inteneti.

Naam, sasa ili kuwavutia wawekezaji unatakiwa kufanya haya ya fuatayo.
Miundombinu imara kama barabara, maji, umeme wa uhakika, huduma za afya bora,mawasiliano yanayoendana na wakati, zidhibiti inflation.
Elimu bora kwa wananchi wako kwani kila mwekezaji anataka kuwa na wafanyakazi wenye uelewa mzuri. Ukifanya haya huhitaji hata kujua kiwanja cha ndege kama Rais hapo unamwacha kila waziri atangaze wizara yake kupitia balozi zetu nje. Na balozi za nchi husika ndani ya nchi yako.

Je siyo kweli kuwa kama itatengezwa sinema moja nchini na kuinufaisha nchi kwa kiasi cha dola milioni 200, basi nchi itakuwa imepata kiasi kikubwa zaidi kuliko kiasi chote kinachoingizwa nchini na Watanzania wote walioko nje?

Watanzania walioko nje wanaingiza Tanzania zaidi ya $400 mil kwa mwaka statistics za 2006 sijui leo na kumbuka neno zaidi. Na hizi dola zinakwenda moja kwa moja kwa consumers kama unaelewa elewa na kama huelewi nitamwomba mchungaji akusaidie. sasa Kutokuona watanzania ni mbadala na $200mil ambayo hatakaa iwepo kwani hiyo ni bajeti na inaweza ikabaki bongo $1 mil na jasho kibao. Usisikie bajeti halafu ukashindwa kwenda details za hiyo bajeti. Je zinabakia ngapi tanzania?? Hata wakati wanasaini mikata ya barrics walitajiwa $billions wakazani zote zetu sasa wanachekwa ujinga, tarakimu zisitufanye kushindwa tumia akili na ubongo.

Sasa kejeli ya nini, ama tunajaribu, kwa mara nyingine, kuthibitisha ujinga wetu kama ambavyo tumezoea kujianika hadharani?

Nadhani hapa umetumia maneno yasiyofaa kabisa, sidhani kama JF kuna mjinga ila watu wanzibuana masikio na akili. Kama hujui mchango wa JF basi wewe ndio naona kidogo hayo uliyoyatumia yanakuhusu. JF watu wanaonyeshana mapenzi na nchi yao na jinsi ya kutatua matatizo yetu, huwa hapa watu hawahamaki kwani wote ni Watanzania. Huwa tunahoji je safari za mheshimiwa kweli zitalipa??? Tuwekee gharama ya safari zake zote kuanzia Kenya mpaka india, USA mpaka korea na nini alikileta kwa mafanikio ya safari hizi zaidi ya Porojo za kuombea kura. Sasa mnaleta mpya kwamba majuto anatengenezwa studio ya kisasa, hata bishanga naye atazaliwa upya na Ze komedy watapata ajira mpya kweli mtanzania ataweza igiza ndani humo??? ama ni kura tu.Wajinga kweli watakamtwa.

Isitoshe kama kweli tunaipenda nchi yetu kama ambavyo baadhi wanaandika kwa "uchungu mwingi" kuhusu maendeleo ya Tanzania kwa nini tusirudi nchini kwenda kushirikiana na wenzetu ambao wanahangaika usiku mchana kuiendeleza Tanzania.

watanzania wengi waliopo nje ni misaada mikubwa sana kwa familia zao, nchi inayosema imeajiri watu zaidi ya 85% kwenye kilimo. na kila mwaka kuna shida ya chakula. Ni hao watanzania walioko nje ndio wanaobadilisha vyoo vya gunia vya ndugu zao na kuweka milango, ndio hao angalau wanafanya ndugu zao na wajomba zao angalau kumaliza form 4 kwa kuwatumia ada. Ndio hao wanaowawezesha ndugu zao kununua aspirini. sasa wakirudi mtawapa nini, sio mtafanya familia zaidi ya laki kuwa masikini wa kutisha. Ndio hao walau wanatoa matumaini ya milo miwili badala ya mmoja na ndio sababu wanahasira sana na Safari za JK kwani ile ahadi yake ya maisha bora kwa Mtanzania imegeuka na kuwa maisha bora kwa kila fisadi.

Sisi tuko huko, tukicheza madisco na kunywa pombe, na tukiamka ni kuporomosha matusi kwa watu ambao wanapinda migongo katika kutafuta jinsi ya kuiendeleza Tanzania na ndugu zetu tuliowakimbia.

kaka nani anapinda mgongo, ni Rostam au Lowasa, ni Jk au Masha ni migongo ipi wamepinda au wameamua kunyanyua kitanda, Safari za kuwaogopa watanzania ndio kupinda migongo?? Ziko wapi za Kagoda, meremeta, tangogold, twintowers,nk au hawajui ziliko au liyumba ndio anayejua come on HR na fedha wapi kaka.?? nafurahi kwani siku zote ukweli huwa ni matusi mtasikia sana na tafuteni majina zaidi kwani kazi ndio inaanza.

Baadhi yetu hatuko honest. Ni wanafiki tu. Tunapenda kufaidi pande zote tukiongozwa na hadhithi ya chako ni changu, na changu ni changu.

Ni kweli kabisa Jakaya M Kikwete sio mkweli kwa watanzania kwani mika minne sasa maisha bora yamekuwa umasikini, utawala wa sheria umekuwa utawala wa kujana, jela ni za masikini na matajiri wote wanahaki. Ahadi zake zote zimekuwa uongo na mwisho kaamua kuishi marekani kwa kisingizio cha ziara.

Ndugu Ambani Adnani Joseph kama unanufaika na utawala huu wa kidhalimu tulia wewe tuache sisi tuliovitani tupambane na udhalimu. Usitutukane kwa kutumia lugha za kejeli, humu tunaandika na kuelimishana , najua nondo za huku ni kwa watu wazima tu kama una nepi kama yangu inabidi ugangamale la sivyo utachekwa ujinga
 
Last edited:
ambani ..karibu but umeongelea movie as if ndio immediate needs ya kuifanya nchi isonge...

As a nation ..we must have the agenda[priorities] and we expect our president to carry our agenda wherever he goes...do you think that rank top ten in our agendas....umeshasoma ilani yetu ya uchaguzi,...that is the voluntary contaract between voters and the gorvernment...and we expect our president to carry that along with his holly qouran or bible...and hata akikutana na mtu anataka kusaidia anajuwa kuwa kwenye ilani ni kitu gani bado!!!...........mwaka 2010 hatutamuuliza kwanini hajajenga HOLLWOOD hapa ..;;Tutataka kujuwa yake tuliyomtuma kwanza.....na hayo ya ziada kama yatafanyika ni kama bonus..tu!!!
Dah..! mkuu PM ilibidi ni log in ili nikushukuru kwa point hiyo hapo juu..! Obama alimuuliza unataka nikusaidie vp ili uweze kufanya lile uliloahidi sijui mkuu alijibu nini?

ukikaa na rais kikwete ni muongeaji mzuri ....anaweza kuongea usiku kucha ....na kwa wewe uliye hapo ukimsikiliza utafikiri kesho tu tanzania inakuwa newyork na .....lami itakuwapo hadi kijijini kwako....he talks dreams ..nadhani kama umepata wakati wa kukaa naye ..utashangaa hata kwanini watu wana m challange..!!...utekelezaji ndio tatizo....tunaye rais ambaye anajuwa vema matatizo ya watanzania .....ana nia ya dhati ya kuyatatua ...lakini hawezi na hana uwezo...he is idealist!! and neither practical nor capable!!!

Mi nafkili ni mpiga soga mzuri na anaongea kile ambacho Watz wanataka kusikia hata kama haamini kwacho!
 
Last edited:
....Moja ya mawasiliano hayo ni matumizi ya blogo na inteneti.

Kama kuna kitu kinathibitisha ubora wa chini kabisa wa mawazo ya baadhi ya Watanzania, na hasa wale vijana waliokimbilia nje kwenda kuzamia ana kujilipua baada ya kwa wamepasua ama kutupa pasi za kusafiria za Tanzania ni aina ya majadiliano kwenye blogo na inteneti za Kitanzania

Kwanini kinachothibitisha ubora wa hali ya juu ya mtindio wa tafakuri kisiwe watu wanaojikomba kama wewe?Kila mtu kafika alipofika kivyake.Who knows kwamba nawe si mmoja wa hao unaojaribu kuwakandia (i.e. wazamiaji)?Lakini si vigumu kuelewa kuwa wewe ni mnufaika wa ufisadi,ndio maana umeweka busara kando,na kukurupuka kutetea for the sake ya kusikia sauti yako mwenyewe.

Siyo tu kwamba kinachojadiliwa wakati wote ni ujinga, upuuzi, matusi na ukosefu mkubwa sana wa heshima kwa watu wengine. Lakini pia kuna uongo na upotoshaji mwingi, mwingine ukiongozwa na mwelekeo wa kisiasa, mwingine ukiongozwa na ujinga wa kutokujua mambo.
Ujinga,upuuzi na matusi ni pamoja na kuwakosea heshima Watanzania mbalimbali wanaojitahidi kuwahabarisha wenzao kuhusu masuala mbalimbali yanayojiri ndani na nje ya nchi.Hivi Michuzi anaandika matusi,ujinga,upuuzi,etc?Mjengwa je?Haki-Ngowi?Hebu tuchukulie mfano wa blogs hizo tatu,kwa mfano tu,kisha tuthibitishie kauli zako za kilevi kuwa "kinachojadiliwa ni ujinga,upuuzi,matusi,nk".
Pia uzembe wa tafakuri umekufanya ushindwe kutambua kuwa asilimia kubwa ya blogs za Kitanzania zinaandikwa na watanzania walio ndani ya nchi,na nyingi kati ya hizo ni za picha kuliko uchambuzi.

Linganisha blogo na inteneti za Kitanzania na za Waafrika wengine nje ya Bara la Afrika. Angalia inteneti za Wakenya, Waganda, za Waghana, za Afrika Kusini. Watu wanajadili mambo ya maana ya maendeleo yao na kuchuana kikwelikweli kwa nguvu za hoja. Unapata mawazo na maoni adhimu na adimu, siyo matusi na ujinga.

Ulishazaliwa wakati baadhi ya blogs za wakenya zilipokuwa zinaendeleza ukabila kipindi cha vurugu za uchaguzi mkuu uliopita?I doubt if you were,and that suggests kwamba tunaweza kuwa tunapoteza muda kujadiliana na "mtoto mdogo"

Unapolinganisha vitu,ni muhimu uwe na mifano hai.Hicho cha muhimu unachokiona kwenye blogs za Kenya,Uganda,Ghana,etc ambacho hakipo kwenye blogs za Watanzania ni kipi hasa?Mgogoro wa kisiwa cha Migingo?Mapambano dhidi ya LRA na tuhuma dhidi ya M7 kuwa mkewe alimu-infect na kaugonjwa flani?Furaha ya Waghana kuwa nchi ya kwanza Afrika kuahidiwa ziara na Obama?


Sisi tumebakia kwenye matusi na ujinga tu. Najua kuwa moja ya matatizo yetu makubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania waliokimbilia nje ni vijana waliokwenda kuzamia na kujilipua tu. Ni watu wasiokuwa na uwezo mkubwa wa elimu, ni watu wasiojua mambo isipokuwa uwezo wa kuvunja sheria za wanakoishi na kuwakimbia polisi. Hivyo haishangazi kuona kiwango cha chini cha mawazo katika inteneti za mawasiliano za Kitanzania.
Mbona hata wewe ambaye "hukujilipua" unakabiliwa na tatizo hilohilo la kutoa hoja zisizo na kichwa wala miguu!Hivi ungekuwa umeelimika ungeweza kusema kitu kama "INTERNET ZA MAWASILIANO ZA KITANZANIA"?Ndio kitu cha aina gani hicho?Did you imply webforums (like JF),weblogs (like Michuzi's,et al) au websites za magazeti kama habarileo.co.tz?Internet za mawasiliano?Does that make any sense?Kwani kuna "internet" zisizo za mawasiliano,au za kujichua instead of mawasiliano?au za mawasiliano ya Kikenya,Kiganda,Kighana?

Iko mifano mingi. Lakini angalia ujinga ambao umekuwa unaandikwa kuhusu ziara ya karibuni ya Rais Kikwete mjini Los Angeles, Marekani, ambako miongoni mwa watu wengine alikutana na nyota watengenezaji na wachezaji sinema kama vile Steven Seagal, Billy Zane na wengine.

Kwanini walichaondika "hao" kiwe ujinga na unachoandika wewe kiwe "hekima"?Kwanini unakuwa mjinga kwa kutoheshimu uhuru wa mawazo ya mwenzako?JK mwenyewe amesema kuwa unapoishia uhuru wako ndio unapoanzia wa mwezio.Yaani unajikomba hadi unapingana na unayejipendekeza kwake?

Wamejitokeza watu kwa kutumia inteneti za Kitanzania kumkejeli, kumdhihaka kama vile mkutano huo na nyota hao mabilionea hauna manufaa na kama vile mabilionea hawa ni watu wasiostahili kukutana na Rais.

Ni ajabu kwamba mtu anaweza kuishi Marekani, ama nchi yoyote ya Ulaya, na bado akashindwa kujua uwezo umuhimu mkubwa wa watengenezaji na wachezaji sinema hawa.

Hawa siyo waosha masufuria, wanyanyua mizigo viwandani, ama waonya mabehewa ya treni kama tulivyo sisi wengi Watanzania tuliozamia nje. Hawa ni nyota. Ni matajiri wenye fedha nyingi kuweza kuwekeza katika nchi yoyote.

Nyota hao, kwa mfano, wanataka kwenda Tanzania kufungua Tanzania Studios ambazo zitakuwa za kwanza katika sub-saharan Africa kwa sababu studio pekee za kutengenezea na kucheze sinema kwa sasa ziko katika Afrika Kusini tu katika Bara zima la Afrika.

Ikichezwa sinema moja tu katika Tanzania kiasi cha watu 400 ama zaidi watanufaika moja kwa moja na utengenezaji wa sinema hiyo. Ukitilia maanani kuwa kila mtu ana familia ya wastani watu watano, unazungumzia watu 2,000. Hawa ni mbali na wale watakonufaika kwa namna nyingine nyingi zisizokuwa za moja kwa moja.

Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.

Tatizo lako ni fikra za kisisimizi,yaani ndogo kupita kiasi.Uchumi wa Tanzania haujaathiriwa kwa kukosekana studio za Wamarekani.Zinaweza kuja na zikafisadiwa just like migodi yetu ya madini inavyofisadiwa kila kukicha.
Kazi kubwa ya Rais wa nchi yoyote ni kuvutia wawekezaji wenye fedha kwenda kuwekeza katika nchi yake. Mashindano ya dunia ya leo baina ya mataifa ni uwezo wa kuvutia wawezekezaji. Uwekezaji ndiyo unainua uchumi, na uchumi ndiyo uti wa mgongo wa nchi, siyo bla bla za matusi na ujinga wa kwenye inteneti.
Kazi kubwa ya rais,kwa mujibu wa mjinga kama wewe, ni kuzurura kwa kisingizio cha kuvutia wawekezaji.Sasa umuhimu wa balozi zetu huko nje ni upi?TIC wafanye nini?Trade Centres zetu kwenye baadhi ya balozi zina kazi gani?Bodi ya utalii ifanye nini?

Kazi kubwa ya rais ni kuhakikisha serikali anayoongoza inatekeleza wajibu wake katika kuutumikia umma wa Watanzania.Tuna priorities nyingi mno kuliko hiyo aliyojipachika rafiki yako JK kuwa balozi wa utalii.Na hata kama hilo lingekuwa na umuhimu mkubwa,si ameshakuja hapo US mara kadhaa?Au anafuatilia utekelezaji?
Je siyo kweli kuwa kama itatengezwa sinema moja nchini na kuinufaisha nchi kwa kiasi cha dola milioni 200, basi nchi itakuwa imepata kiasi kikubwa zaidi kuliko kiasi chote kinachoingizwa nchini na Watanzania wote walioko nje?
Angalau hapa umetusaidia kubainisha kuwa wewe ni mweupe kiakili.Hebu tuambia hizo dola milioni 200 zinzvyoweza kuzalishwa na sinema moja!Ni kwenye mauzo (assuming Wachina na mitambo yao ya dvd feki Kariakoo "wameokoka na kuacha piracy"),fundraising au "malipo kwa Tanzania kukubali kuwa studio ya filamu hiyo"?


Sasa kejeli ya nini, ama tunajaribu, kwa mara nyingine, kuthibitisha ujinga wetu kama ambavyo tumezoea kujianika hadharani?
Kuna kejeli mbaya zaidi ya wewe kuwaita watanzania wenzako wajinga paipo uthibitisho wa msingi,and at the same time ukishindwa kutuonyesha kwanini nawe si tu mjinga,bali mjinga zaidi ya hao unaowakosea heshima?Na bora ungeficha ujinga wako badala ya kuuanika hadharani with your full name (pengine ukidhani kuwa ita-catch attention ya JK....FORGET IT.Kuna akina Salva wanaolipwa kwa kazi hiyo,kuna akina Muhingo Rweyemamu,Balile,etc wameshakuwahi.Eti Vision 2010!keep on dreaming,man!)
Isitoshe kama kweli tunaipenda nchi yetu kama ambavyo baadhi wanaandika kwa "uchungu mwingi" kuhusu maendeleo ya Tanzania kwa nini tusirudi nchini kwenda kushirikiana na wenzetu ambao wanahangaika usiku mchana kuiendeleza Tanzania.
Rudi kwanza wewe ambaye si ajabu kuja kwako hapo US ni matokeo ya ufisadi unaojaribu kuulinda,na ni mzigo kwa walipa kodi wa Tanzania.Kwani mlikuja pamoja na hao unaowataka warudi to an extent uwashupalie warudi nyumbani?
Sisi tuko huko, tukicheza madisco na kunywa pombe, na tukiamka ni kuporomosha matusi kwa watu ambao wanapinda migongo katika kutafuta jinsi ya kuiendeleza Tanzania na ndugu zetu tuliowakimbia.
Tabia yako ya ulevi sio kiwakilishi cha kila mtanzania aliye nje.Na hatuhitaji kujua kuwa ukishakunywa pombe "kwenye disco" unapoamka ni matusi mtindo mmoja!I'd advise you to get in touch with AA.
Kama kweli tunaijali nchi na ndugu zetu kwa nini tusirejee na kushiriki katika harakati za kuendeleza nchi, badala ya kila siku kushikilia kuwa tupewe dual citizenship? Tunataka urais wa Marekani, ama Uingereza, ama Canada wa nini kama tuna uchungu na nchi yetu ya Tanzania?
Mtanzania gani anataka urais wa Marekani,Uingereza au Canada?Najua ulitaka kusema uraia,lakini who knows,pengine ndio ushatoka kwenye disco....hahahaha!
Baadhi yetu hatuko honest. Ni wanafiki tu. Tunapenda kufaidi pande zote tukiongozwa na hadhithi ya chako ni changu, na changu ni changu.
Hiyo honest yako ni ipi?Au kwa vile umeweka jina lako halisi?That's not honesty bali ni mbinu zako zilizopita na wakati kwamba ukiweka jina lako hapo labda kuna fisadi ata-get in touch wakati tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu next year.If you are that honest ungetuambia bayana kuwa nawe si mnufaika wa huku na huko.Si ajabu kuwa jukumu la kukuleta huko US lilikuwa la mzazi wako lakini akafanya usanii na sasa jukumu hilo linabebwa na walipa kodi wa Kitanzania,same people unaowatukana hapa kuwa ni wajinga,wapuuzi na wasio na heshima.
Ambani Adnani Joseph

Mtanzania
– Los Angeles.

Hey,mbona your name sounds like a Kenyan?mdogo wake Boniface Ambani wa Yanga?
 
Last edited:
thanks kishoka!!

Unazungumzia wenye pesa, nitakupa Upembuzi mwingine uutfakari. Nakuuliza hivi, kwa nini nchi yetu ilipokuwa ikikabiliwa na hali mbaya ya hewa ya kukosa mvua na kujulikana wazi tutakosa umeme, Rais Kikwete alipokuja Marekani miezi kadhaa kabla ya Tanzania kuingia mkataba na Richmond, kwa nini hakuomba Ikulu au Wizara ya mambo ya nje ya Marekani impigie krosi akutane na jamaa wa GE ambao wanatengeneza mitambo ya kuzalisha umeme na vifaa vya umeme?

Je si inafahamika wazi kuwa Tanzania tuna uhaba wa vifaa vya hospitali, mbona hajaomba kukaa chini na kina GE, Siemens, Phillips na wenginewe aingie mkataba wa bei nafuu tuuziwe kwa riba ndogo au bei poa vifaa vya kisasa vya hospitali ili kuachana na gharma za kupeleka watu nje ya nchi kwenda kufanyiwa MRI au CAT Scan?



Gaademu Ninkampupiism!
Nadhani, ni JK ambaye hajielewi, na sio sisi ambao hatumuelwi
 
KILA nchi na jamii inavyo vigezo vyake vinavyotambulisha ubora wa jamii hiyo na watu wake, ndani na nje ya nchi hiyo. Na Tanzania siyo tofauti katika ukweli huu.

Ni Kweli Kabisa

Vigezo hivyo viko vingi na kwa namna nyingi na tofauti. Moja ya vigezo vipya vilivyoibuka katika miaka ya karibuni ni teknolojia ya mawasiliano kwa njia ya kompyuta na matumizi yakee.

Piga Makofi

Mawasiliano hayo pia yako mengi na ya aina mbali mbali vile vile. Moja ya mawasiliano hayo ni matumizi ya blogo na inteneti.


Inaonekana hata hujui tofauti ya Blog na Internet, ila twende utaelewa tu maana uko JF, the Home of Great Thinkers


Kama kuna kitu kinathibitisha ubora wa chini kabisa wa mawazo ya baadhi ya Watanzania, na hasa wale vijana waliokimbilia nje kwenda kuzamia ana kujilipua baada ya kwa wamepasua ama kutupa pasi za kusafiria za Tanzania ni aina ya majadiliano kwenye blogo na inteneti za Kitanzania.

Internet ni Internet tu Hakuna ya Kitanzania wala ya Kikenya wala ya Kichina

Siyo tu kwamba kinachojadiliwa wakati wote ni ujinga, upuuzi, matusi na ukosefu mkubwa sana wa heshima kwa watu wengine. Lakini pia kuna uongo na upotoshaji mwingi, mwingine ukiongozwa na mwelekeo wa kisiasa, mwingine ukiongozwa na ujinga wa kutokujua mambo.

Punguza Jazba, Onyesha Ujinga, Upuuzi, Matusi na Wapi mtu amekosewa Heshima, Nadhani wewe ndio Umekosa Heshima kwa Kudhani kwamba kila aliyeko Nje Amejilipua


Linganisha blogo na inteneti za Kitanzania na za Waafrika wengine nje ya Bara la Afrika. Angalia inteneti za Wakenya, Waganda, za Waghana, za Afrika Kusini. Watu wanajadili mambo ya maana ya maendeleo yao na kuchuana kikwelikweli kwa nguvu za hoja. Unapata mawazo na maoni adhimu na adimu, siyo matusi na ujinga.


Naona huna info za kutosha, hivi umeshawahi kutembelea Mashada? Once again hakuna internet za wakenya


Sisi tumebakia kwenye matusi na ujinga tu. Najua kuwa moja ya matatizo yetu makubwa ni kwamba baadhi ya Watanzania waliokimbilia nje ni vijana waliokwenda kuzamia na kujilipua tu. Ni watu wasiokuwa na uwezo mkubwa wa elimu, ni watu wasiojua mambo isipokuwa uwezo wa kuvunja sheria za wanakoishi na kuwakimbia polisi. Hivyo haishangazi kuona kiwango cha chini cha mawazo katika inteneti za mawasiliano za Kitanzania.

Unapozidi kutumia neno Internet za Kitanzania unazidi kuonyesha Umaamuma wako. Too much speaking expose your ignorance kaka. JF watu wanashusha Nondo za kufa mtu hata Baba zako wanashinda huku kuchota Maarifa kaka


Iko mifano mingi. Lakini angalia ujinga ambao umekuwa unaandikwa kuhusu ziara ya karibuni ya Rais Kikwete mjini Los Angeles, Marekani, ambako miongoni mwa watu wengine alikutana na nyota watengenezaji na wachezaji sinema kama vile Steven Seagal, Billy Zane na wengine.

Ujinga gani umeandikwa?[/B]


Wamejitokeza watu kwa kutumia inteneti za Kitanzania kumkejeli, kumdhihaka kama vile mkutano huo na nyota hao mabilionea hauna manufaa na kama vile mabilionea hawa ni watu wasiostahili kukutana na Rais.


Mabilioenea? In TSH au USD?anufaa gani labda niendelee kukusoma may be utaayaanika hayo manufaa kwenye para za chini


Ni ajabu kwamba mtu anaweza kuishi Marekani, ama nchi yoyote ya Ulaya, na bado akashindwa kujua uwezo umuhimu mkubwa wa watengenezaji na wachezaji sinema hawa.

Wala Si Ajabu


Hawa siyo waosha masufuria, wanyanyua mizigo viwandani, ama waonya mabehewa ya treni kama tulivyo sisi wengi Watanzania tuliozamia nje. Hawa ni nyota. Ni matajiri wenye fedha nyingi kuweza kuwekeza katika nchi yoyote.

Wamewekeza nini Kwao?[/B]


Nyota hao, kwa mfano, wanataka kwenda Tanzania kufungua Tanzania Studios ambazo zitakuwa za kwanza katika sub-saharan Africa kwa sababu studio pekee za kutengenezea na kucheze sinema kwa sasa ziko katika Afrika Kusini tu katika Bara zima la Afrika.


Then?[/B]

Ikichezwa sinema moja tu katika Tanzania kiasi cha watu 400 ama zaidi watanufaika moja kwa moja na utengenezaji wa sinema hiyo. Ukitilia maanani kuwa kila mtu ana familia ya wastani watu watano, unazungumzia watu 2,000. Hawa ni mbali na wale watakonufaika kwa namna nyingine nyingi zisizokuwa za moja kwa moja.

Gadem


Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.


Dola milioni 200 ni kama bilioni 280 za kitanzania, Tumepoteza kiasi gani BOT, Kagoda, Meremeta na Wajomba zake


Kazi kubwa ya Rais wa nchi yoyote ni kuvutia wawekezaji wenye fedha kwenda kuwekeza katika nchi yake. Mashindano ya dunia ya leo baina ya mataifa ni uwezo wa kuvutia wawezekezaji. Uwekezaji ndiyo unainua uchumi, na uchumi ndiyo uti wa mgongo wa nchi, siyo bla bla za matusi na ujinga wa kwenye inteneti.

Hiyo ni kazi ya TIC

Je siyo kweli kuwa kama itatengezwa sinema moja nchini na kuinufaisha nchi kwa kiasi cha dola milioni 200, basi nchi itakuwa imepata kiasi kikubwa zaidi kuliko kiasi chote kinachoingizwa nchini na Watanzania wote walioko nje?


Watanzania Walioko Nje Wanaingiza Kiasi gani?


Sasa kejeli ya nini, ama tunajaribu, kwa mara nyingine, kuthibitisha ujinga wetu kama ambavyo tumezoea kujianika hadharani?


Nadhani wewe ndio umekuja kuanika Umaamuma Wako


Isitoshe kama kweli tunaipenda nchi yetu kama ambavyo baadhi wanaandika kwa “uchungu mwingi” kuhusu maendeleo ya Tanzania kwa nini tusirudi nchini kwenda kushirikiana na wenzetu ambao wanahangaika usiku mchana kuiendeleza Tanzania.

Onesha Mfano


Sisi tuko huko, tukicheza madisco na kunywa pombe, na tukiamka ni kuporomosha matusi kwa watu ambao wanapinda migongo katika kutafuta jinsi ya kuiendeleza Tanzania na ndugu zetu tuliowakimbia.


Pole sana kumbe Uko huko kazi kucheza Disco na Kunywa Pombe ukiamka unaporomosha Matusi

Kama kweli tunaijali nchi na ndugu zetu kwa nini tusirejee na kushiriki katika harakati za kuendeleza nchi, badala ya kila siku kushikilia kuwa tupewe dual citizenship? Tunataka urais wa Marekani, ama Uingereza, ama Canada wa nini kama tuna uchungu na nchi yetu ya Tanzania?

Acha Kulia lia


Baadhi yetu hatuko honest. Ni wanafiki tu. Tunapenda kufaidi pande zote tukiongozwa na hadhithi ya chako ni changu, na changu ni changu.

Wewe ndio Mnafiki kwa kujifanya huelewi Matatizo ya watanzania

Samahani hata sijakukaribisha Jamvini, Karibu sana
 
Huyu lazima ni zao la ufisadi na anaishi huko kwa mgongo wa mtandao wa mafisadi, hivi Tanzania kuna soko gani la kununua mafilamu ya kimarekani? hizi tu za kukopi za kariakoo watu zia washinda! eti nini....!? Yaani raisi wetu anatukejeli alafu huyu bwana amuunga mkono! unajiletea laana wewe! Yaani watanzania tunahitaji sana senema ee!?
 
Ndugu Mtanzania,
Nimeguswa mno na maelezo yako juu ya yanayoendelea nyuma ya pazia katika ziara za JK ambazo nyumbani zinapigiwa kelele nyingi mno na baadhi ya kambi zinazoona hazina umuhimu.

Nakuunga mkono kwa hoja yako kwa sababu JK ni kinara wa aina mpya ya uongozi wa hatamu za nchi kama ambavyo Barack Obama na mkewe wanafanya... Yaani kuuvuka mipaka kwa masilahi ya nchi.... na kuwagusa watu wa kawaida.... Je tunajua kwamba Obama amemuiga JK kwenda kula Gengeni Kariakoo wakati alipoenda yeye na makamu wake Biden walipovamia Fast Food kwa ajili ya Pizza???? na wakatoa tip kwa mwuuzaji..

Ninachowasihi wale wasio na subira au mwenye mawazo kinzani juu ya matunda ya ziara hizi wampe muda na matokeo yake tuyapime katika kipindi muafaka.

Yapo mengi tu yanayoendelea nyuma ya pazia ..mikutano yake na watendaji wakuu wa makapuni ya kimarekani ikiwemo Microsoft na IBM juu ya uwekeaji mitambo ya kisasa ya TEHAMA kwenye chuo Kikuu cha Dodoma ambacho kitapiku vyuo vikuu nchini ni jambo linalohitaji kufuatiliwa kwa hamu subira na kupewa muda kabla ya kuhukumu...
... JK pia anajua wakati muafaka wa kuvunja ukimya juu ya manufaa ya ziara zake..alishasema mara kadhaa na ataweka bayana wakati muafaka.... Waswahili hatutangazi jinsia ya mtoto kabla hajazaliwa.. TUSUBIRI SIKU YA KUZALIWA MTOTO TUTAJUA !!!!

Huwezi kuifanannisha familia ya Obama na wakina Kikwete kwa vigezo vyovyote vile! Obama ni Rais anayejua vipa umbele vya nchi yake na ndio maana hawezi kufanya ziara ya siku tisa nje kwa mara moja. Ukiangalia mkanda wa safari za Kikwete kwa mfano alipokutana na watu wa IBM, utaona body language ya wale jamaa kuwa walikuwa wanamuona juha; kitu ambacho ni aibu si kwake tu bali kwa nchi yetu. Wawekezaji hawawezi kuja kuwekeza nchi ambayo haina amani ya kweli, uhalifu na mauaji yakiwa yamekithiri! Put your house in order first and then the wawekezaji will troop in!
 
Ndugu Mtanzania,
Nimeguswa mno na maelezo yako juu ya yanayoendelea nyuma ya pazia katika ziara za JK ambazo nyumbani zinapigiwa kelele nyingi mno na baadhi ya kambi zinazoona hazina umuhimu.

Nakuunga mkono kwa hoja yako kwa sababu JK ni kinara wa aina mpya ya uongozi wa hatamu za nchi kama ambavyo Barack Obama na mkewe wanafanya... Yaani kuuvuka mipaka kwa masilahi ya nchi.... na kuwagusa watu wa kawaida.... Je tunajua kwamba Obama amemuiga JK kwenda kula Gengeni Kariakoo wakati alipoenda yeye na makamu wake Biden walipovamia Fast Food kwa ajili ya Pizza???? na wakatoa tip kwa mwuuzaji..

Ninachowasihi wale wasio na subira au mwenye mawazo kinzani juu ya matunda ya ziara hizi wampe muda na matokeo yake tuyapime katika kipindi muafaka.

Yapo mengi tu yanayoendelea nyuma ya pazia ..mikutano yake na watendaji wakuu wa makapuni ya kimarekani ikiwemo Microsoft na IBM juu ya uwekeaji mitambo ya kisasa ya TEHAMA kwenye chuo Kikuu cha Dodoma ambacho kitapiku vyuo vikuu nchini ni jambo linalohitaji kufuatiliwa kwa hamu subira na kupewa muda kabla ya kuhukumu...
... JK pia anajua wakati muafaka wa kuvunja ukimya juu ya manufaa ya ziara zake..alishasema mara kadhaa na ataweka bayana wakati muafaka.... Waswahili hatutangazi jinsia ya mtoto kabla hajazaliwa.. TUSUBIRI SIKU YA KUZALIWA MTOTO TUTAJUA !!!!

1. Huyu mtoto atazaliwa lini?? si baada ya miezi 9? sasa mpaka leo tangu ashike hatamu ni miaka mingapi? labda tusubiri mtoto wa tembo azaliwe.
2.Wawakilishi kazi yao nini? wazir wa mambo ya nje etc
3. Nafiki wewe unazungumzia MATUMAINI na IMANI zaidi face reality...au na wewe KADA?
 


Kiasi cha dola za Marekani milioni 200 zitaingia katika uchumi wa Tanzania kwa sinema moja tu kuchezwa katika Tanzania ambayo inayo mazingira mazuri ya kuchezea sinema.

Ambani Adnani Joseph

Mtanzania
– Los Angeles.

Thanks Vision 2010, naamini wewe siye Ambani Adnani Joseph, ila umem-quote tu, right??

Nachelea kuamini kwambahiyo movie itatuletea 200M USD, nimesoma somewhere kuhusu SlumDog Milionaire star kabaki kwenye slums na vilevile sijui uganda walipata dollar ngapi kwa movie ya Amin, na Mississipi Masala

Naomba kuelimishwa kidogo
 
Vision2010 swali kwako ni , katika siku nane za ziara ya Mhe , msafara wake umetumia kiasi gani cha fedha?
Was the visit worthwhile ? ie what did Tanzania as a country benefit?
Kwa mawazo yangu , ni kama vile alikwenda on holiday na hii imejumisha kutembelea IBM, Cisco , Stanford, etc. Next time labda atakwenda Disney Land!
Ni sawa na mtish akija Dar anapelekwa Mwenge na Mlimani.
 
Bwana Ambani kwa kutuhabarisha kuwa kazi kubwa ya rais ni kutafuta wawekezaji nje anatanabaisha kuwa hana tofauti sana na hao watanzania anaowaponda kuwa wana elimu ndogo!
 
kwanza nashangaa sana ..nimetembelea blog ya [mawasilianoikulu] naona wameipa lead hii story...nijuavyo mimi mtu yeyote anayeenda califonia ..lazima atembelee kwenye studios maarufu kama sony au universal studio...etc....i have beeen there ..na kuna watalii wengi...sana tu..,na hata ni jambo la kawaida sana kukutana na movie stars...pichani anaonekana jk akiwa ameshikana mkono na seagal...nadhani akajitambulisha ,..then akawakaribisha...wakajibu bila shaka!![watatoa jibu gani tena]

ni aibu sana kwa rais nzima wa nchi kwenda kutembea studios kama kina sisi tunapofanya tukiwa califonia...hakuna tofauti ....wengi wetu hata hizo picha na movie stars tulipiga[hawana hiyana unawaomba tu].......come on guys thats is being tooo low.......jk amejishusha sana .....

kuna aliyeongelea ..matokeo ya mkutano wa sullivan ambapo jk alitumia dola milioni 100 kuandaa [pamoja na zilizopigwa ..thats a new story]......hadi leo wale actors na african american in diaspora waliokuja pale ...kukimbia winter marekani ...wametuletea nini!!??
 
Vision2010 swali kwako ni , katika siku nane za ziara ya Mhe , msafara wake umetumia kiasi gani cha fedha?
Was the visit worthwhile ? ie what did Tanzania as a country benefit?
Kwa mawazo yangu , ni kama vile alikwenda on holiday na hii imejumisha kutembelea IBM, Cisco , Stanford, etc. Next time labda atakwenda Disney Land!
Ni sawa na mtish akija Dar anapelekwa Mwenge na Mlimani.


yeah aende desney land kutembea akirudi hapa atatudanganya kuwa ....ameahidiwa kujengewa mabembea pale mnazi mmoja na kidongo chekundu grounds.....
 
Back
Top Bottom