Joaquim Chissano wins the the Mo Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership

wabongo bwana yaani jamaa walikuwa wanakesha kuomba dua MKAPA aiipate hiyo zawadi duh sio utani yote kwa sababu yy ni CCM angekuwa yy CHADEMA mngesemaje?

haya hongera chissano kupata zawadi.
 
infact Mkapa yupo kundi moja na kina Sani Abacha, Mobutu na wengine wanatofautiana tu amount walizoiba ila mionyo yao na tamaa zao zinafanana kabisa;

yebo yebo,
haya sasa majungu,hauwezi kumfananisha mobutu 9ngebe ya zabanga)na mkapa hata siku moja,yebo yebo acha chuki binafsi,

pamoja na wizi wa mkapa,mie bado naona kwa jicho na taswira kali ya kwamba Mkapa ndiye rais aliyejitahadi kuweka sera nzuri ya kuinua uchumi na maendeleo.Kina Jk ndio walikuwa wanamkwamisha pamoja na EL,ninaandaa ripoti kamili ili kuonesha kwanini namtetea mkapa na kwanini nasema Mkapa aliangushwa na timu ya wanamtandao..

ni mambo gani matano yebo yebo unafikiri Mkapa alikosea?

Kumfukuza Aliyekuwa mkurugunzi wa PPF mataka-Je akuzingatia maadili ya uongozi?

Kumlazimisha CDF wa kipindi kile Mbona je akuzingatia nidhamu ya jeshi?

Je suala la kuwaondoa Mawaziri walioboronga kipindi chake,Je akuzingatia utawala Bora??

Kuruhusu Kuanzishwa kwa tume ya haki za Binadamu na Utawala,Je Mkapa akuzingatia haki za Binadamu??

Kuhakisha hazina ya pesa ya kigeni inaongezeka,kuuongeza ukuaji wa uchumi ,je Mkapa akuzingatia kukua kwa Uchumi wa Tanzania??

Kuwezesha kujengwa kwa uwanj wa kisasa wa Taifa,Je mkapa AKuzingatia Maendeleo ya soka katika nchi yetu??

ujenzi wa barabara zote na mambo ya Mkukuta,Mkurabita,TAsaf,MMEM Je Mkapa alikuwa ataki maendeleo ya eleimu,afya na Elimu.??si alikwamishwa na watendaje

narudia tena hakuna mtu aliye perfect but Mkapa has done a lot to this country,
naomba kuwasilisha
 
Honestly, nampongeza Chissano and am happy kwa ushindi wake kuliko ungeenda kwa Fisadi ANBEM!

Hapo ndipo ulipo fikia fisadi Mkapa watanzania wenzio tunaomba na kufurahi ushindi uende hata kwa mtoka mbali kuliko wewe!!
 
ila heshima ya mkapa bado iko pale pale hata huko majuu
 
ila heshima ya mkapa bado iko pale pale hata huko majuu

His days in "good" fame are numbered. Mporonyoko wa umaarufu wa Mkapa umeshaanza kujionyesha waziwazi. Kushindwa kwake kuchukua tuzo ya Ibrahim MO foundation ni mfano mzuri.

Tusubiri tuone atakavyozidi kuaibika. Mtu huwezi kuwa very arrogant halafu ukawa unadunda tuuu...
 


Mheshimiwa sina sababu ya kuwa na chuki binafsi na Mkapa. Kitendo cha yeye kuwa president aliyepigiwa debe na Nyerere tena hatharani alishaniacha mbali sana...!!

Wewe unazungumzia mambo ambayo Mkapa ALIKOSEAkwenye Uongozi wake. Tafathali rejea post hii ya Mtanzania inayoweka bayana baina tofauti ya hoja:



Alamsiki
 
Hongera sana Mkapa nampongeza kwa kushindwa kwa kishindo sala za watanzania wanaomuamba aeleze alivyofisadi nchi zimefika.

Tunashukuru sana kamati ya mchakato imeleta mtu aliyetegemewa.
 
Ohhh now napumua...maana angepata Mkapa ingekuwa imeniharibia wiki yangu yote...Hongera Mwafrika wa Kike kwa kampeni yako...

Hongera Chisano...Hiyo zawadi si cha Mtoto...duh, sasa utakula kuku kwa mrija kisawasawa.

tehe tehe tehe!
 
Habari nilizopata punde zinasema aliyekuwa Rais wa Msumbiji Joachim Chisano ameibuka kidedea kwa kupata Tuzo ya Mo Ibrahim.
Soma


Source: http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7056159.stm
 
We unaishi chini ya mwamba nini...? Thread kibaoooo zimeanzishwa kuhusu hili ina maana wewe hujaziona? Au unataka kujaza nafasi tu?
 
Nadhani sasa atapata nafasi ya kujibu tuhuma. ALiogopa kujibu akijua kwamba atawapa ushahidi wa kumuengua, kumbe LA KUVUNDA HALINA UBANI... AMESHAVUNDA sasa hata Butiku rafiki yake amemtosa, Warioba alijaribu kuuma na kupuliza lakini MOYONI anajua ananuka. Mkapa rudi nyumbani ueleze UMMA ama uombe radhi na kurudisha mali zetu... vinginevyo pitia huko huko uende China ulikoandaa makazi ya dharura mambo yakiharibika
 
Hizo kibao ni za jana Ngabu! Na mshindi alikuwa bado kutajwa.
 
Hiyo panel iliyoteuliwa kuchagua ni vichwa vitupu..hakuna mbabaishaji pale. Wanawajua credits za marais waliokuwa candidates. Ila Chissano amemwacha mbali sana Mkapa, ukiachilia mbali umakini wake, masuala ya amani na uongozi uliotukuka; uchumi wa msumbiji ulikuwa unakua kwa kasi kubwa sana ukilinganisha na wa kwetu waliokuwa wanadai 6%. Chissano akiwa mmojawapo wa vijana wa mwalimu JKN alifuata kwa makini mafundisho ya yule mzee, tofauti na Mkapa ambaye alianza kumchafua roho baba yake mapema kwa kutapanya na kugawa mali za nchi hovyo kama issue ya NBC etecetera. Anyway amevuna alichopanda,alikuwa na nafasi nzuri ya kushinda kama asingeweka ubinafsi, kutokujali na dharau zake mbele.
 
mmh.. Nyani.. inabidi watu jamani waangalie kwanza kabla hujaposti Breaking News...
 
Halisi una maana kile kibanda cha Lushoto hakitoshi sasa amenunua kajumba huko Sanya.... (ya Uchina) maana ingekuwa Kisangara Juu ingekuwa kasheshe!
 
Nyani

"My Girl Gotta A Girlfriend
I just found out but..."

Tafadhali fafanua kidogo mkuu.

Thanks
 
Nyani

"My Girl Gotta A Girlfriend
I just found out but..."

Tafadhali fafanua kidogo mkuu.

Thanks

...my girl gotta girlfriend, I just found out but it's alright!
as long as I can be with her too..
it really is not a problem...
Cuz I'ma make it do what it do
Cuz having two chicks, it's better than no chicks...
I rather just join in, keep my girl, and the other one too.....
 


Nyani,

Makubwa hayo!
 

Alikula kiapo cha kulitumikia taifa kwa uaminifu sidhani kama kujilimbikizia mali, kufanya biashara ikulu na ubadhirifu wa hali ya juu ndio malipo ya uwajibikaji wake. Yani leo mtu kutimiza wajibu wak-e malipo ni UFISADI?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…