rip faza_nelly
JF-Expert Member
- Feb 19, 2018
- 5,749
- 7,038
Iko siku Ndugai atatembelea magongo na Lissu atadunda freshi tu.
Weee mjazeni upepo tu na lissu awezi kukataa pesa angekuwa hana shida angezirudisha pesa maana akuzifanyia kazi.Hivi mtu aliyeshinda mauti unaweza kumtisha na mshahara
Ama kweli Tundu Lissu anawanyima raha!Ni kweli jamaa anachukua malipo bila kufanya kazi..
Akiambiwa arudi kazini anadai anaumwa ila yupo busy kufuata Interview za TV miji Mbali Mbali duniani akialikwa Australia ataenda ila kwenda kufanya kazi bungeni hataki.
RIP. Kilangila.
spika na serikali wapanga figisu zingine kumkwamisha kijuku watume ndugu Tundu Lisu kwa kumyima haki yake mshahara.
Wananchi wote wapenda amani na wazalendo waaza harakati za kumchangia kilawezi 1000 ili ndugu Lisu aendele na matibabu na harakati za kuwapambania wanyonge mchango huo uta anza rasmi atakapo futiwa tu mshahara wake.
Tuta pambana kwa hali yoyote mpaka tufike
RIP x 100. Kilangila.Mtu hata aponyeke kifo mara kibao km fidel castro bado hofu ya kifo iko palepale. Naturally kifo ni hofu ya kila kiumbe hai. Imeumbwa hivyo
Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi kipindi kile hana ubunge aliishije?Bunge linazidi kujinasisha mtegoni.Wakibanwa watakataa huko mbeleni.
Alivyopona akawa anadhurura ughaibuni kama uyo?Ndugai ulivyoenda India kwa matibabu ukakaa zaidi ya miezi 3 je ulikuwepo bungeni na jimboni kwako? Ulisimamishiwa mshahara wako?
Umekataa kumtibu Haina shida ,lakini leo kudai report ya daktari ni uzwazwa mkubwa sana
Hahahahahah.Atalalamika tu na wa Tanzania hawatojari wataendelea na maisha kama kawaida tu
Kama tulivyo kimya kwa kifungo cha mbowe
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hili waliompiga.Tundu Lissu risasi wanajidhihirisha.wao.wenyewe kweupeee!Lissu kwasasa hana cha kupoteza, Mshahara kwake si kitu....
Yeye Ndugai kama Spika anapaswa kujua hali ya Lissu bila hata Lissu kumtaarifu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera wewe mzima ambaye huwezi kutembelea magongo............ Mungu akubariki kwa kuwa yeye ndio alitaka kutembelea hayo magongo.
Tuone sasa kama hawa makamanda uchwara watamchangia pesa ya kujikimu. Da'Mange mwenyewe ilibidi afunge akaunti yake gofundme.com baada ya makamanda kuuchuna.
Kama spika ndio kiongozi wa wabunge wote au ulijui hilo mkuu?Apewe taarifa ya daktari kama nani? Kwani yeye ndiye aliyempeleka? Kwani yeye ndiye aliyemlipia gharama za hospitali?
Dunia lazima ihabarishwe kuwa,Mpaka Muda huu ilitakiwa Katibu Mkuu wa Bunge ajiuzulu Kama aliendelea kumlipa Mtu Mshahara wakati hayupo eneo la Kazi Na Hakuna taarifa yoyote ya kimaandishi ya kutokuwepo kazini Na Sasa hivi anaonekana anazurura Kwenye Channel Za Kimataifa anachafua Nchi