Job Ndugai: Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Pumb*vu za***k o
Sent using Jamii Forums mobile app
 
ukiamua kujitoa ufahamu unaandika pumba tu kutetea buku 7. Mkuu jaribu kushirikisha ubongo
 
Kuna watu wana roho mbaya Duniani sijawai kuona alafu watu kama hao juma pili wako kanisani au ijumaa wako msikitini

Ukiona Mtu anaenda kuoga maana yake anaenda kusafisha mwili dhidi ya Uchafu alionao Na hapaswi kumshangaa
 
Kina Ndugai na wenzie wanaoongoza mihimili mingine wamekosa ushauri mzuri wa kuendesha mihimili hiyo .

Sent using Jamii Forums mobile app

Jamaa ni mtaalamu wa kutega kwani kila vile anavyotega nao wanakuja kupita mulumule kwenye mitego yake yaani ni kama anawaambia nyuma geuka nao wanageuka ...mbele tembea nao wanaanza kutembea kama anavyotaka, Walishafunga mjadala wa shambulio lake leo wanamfuata kwenye makongomano yake huko anakopuyanga na kujibu tuhuma zake, Na hili naamini kabisa jamaa anataka asimamishiwe mshahara wake kwani hawatafuata taratibu ili maamuzi hayo yawe fimbo ya kuwachapa nayo na soon watafanya hivyo.
 

Anasimamishaje mshahara kabla hajajiridhisha na taarifa ya daktari kama kweli ameshakuwa fiti kurejea kazini?
Kwani spiker amepata taarifa mpya kuwa lisu ameruhusiwa kurudi TZ?
 
Kama hana cha kumliza interview zote za nini au leo kuja kugombea urais wakati mwenye chama yupo

Sent using Jamii Forums mobile app

Interview Ni haki yake kwani kavunja sheria gani? Kugombea uraisi ni uamuzi wake huyo mwenye chama hawezi kumzuia kugombea urais kwani sio lazima agombee kupitia cdm. Kwani Lowassa alipotaka urais na kukosa nafasi akiwa ccm ndio alikosa pengine pa kugombea?
 
Ipo sahihi

Yaani mpaka sasa hana hata ile report ya hospital ya Kenya kwa matibabu wala ya u Belgium.

Inakuwaje mwaka mzima hakuna report wala kuuliza hali ya mgonjwa kama mzima au amekufa, yule wamuonae voa ni kivuli, akipoa mtakimbia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni taarifa ninayompa Job Ndugai na wengine wote wenye mawazo mgando kama yake , kwamba huyu Tundu Lissu mliyeamua kumnyang'anya mshahara ( na zipo taarifa kwamba wiki ijayo mnamnyang'anya ubunge ) hana njaa wala tamaa ya hela taslimu , Lissu amehudumia kesi za wateja wake mahakamani kwa kipindi kirefu , ambapo taarifa zinaonyesha kwamba almost 95% amezihudumia kwa gharama ya bure kabisa huku akiwalipia mpaka nauli ya kwenda na kurudi mahakamani wateja wake hao

Lissu ambaye gharama za matibabu yake zinazidi mshahara ambao Job Ndugai ataupata tangu alipoanza kazi hadi atakapostaafu , kwa sasa ni Mtu wa kimataifa hawezi kamwe kudhalilika kwa kunyimwa mshahara unaolipwa kwa hela za madafu , hivyo basi juhudi zozote kutoka kwa watu walioshindwa kumuua kwa risasi , mabomu na uchawi hazitamkwamisha Mh Lissu , na zimeshindwa hata kabla ya kuanza , sana sana zinazidi kulidhalilisha bunge la Tanzania na kuondoa mashaka juu ya fikra kwamba linatumika na kutumikishwa na serikali , Matendo na kauli za Ndugai kuhusu Lissu ni sawa na kujionyesha yeye mwenyewe kwenye uso wa dunia kwamba hana utu na wala hajawahi kuwa nao , huyu Musukuma mtu aliyefeli mtihani rahisi wa darasa la 7 kutoa mwongozo ni mpango tu wa kiharamia wa kukamilisha mchakato wa kibunge ili kukidhi matakwa ya Ndugai na waliomtuma
 
Hii ni taarifa ninayompa Job Ndugai na wengine wote wenye mawazo mgando kama yake , kwamba huyu Tundu Lissu mliyeamua kumnyang'anya mshahara ( na zipo taarifa kwamba wiki ijayo mnamnyang'anya ubunge ) hana njaa wala tamaa ya hela taslimu , Lissu amehudumia kesi za wateja wake mahakamani kwa kipindi kirefu , ambapo taarifa zinaonyesha kwamba almost 95% amezihudumia kwa gharama ya bure kabisa huku akiwalipia mpaka nauli ya kwenda na kurudi mahakamani wateja wake hao

Lissu ambaye gharama za matibabu yake zinazidi mshahara ambao Job Ndugai ataupata tangu alipoanza kazi hadi atakapostaafu , kwa sasa ni Mtu wa kimataifa hawezi kamwe kudhalilika kwa kunyimwa mshahara unaolipwa kwa hela za madafu , hivyo basi juhudi zozote kutoka kwa watu walioshindwa kumuua kwa risasi , mabomu na uchawi hazitamkwamisha Mh Lissu , na zimeshindwa hata kabla ya kuanza , sana sana zinazidi kulidhalilisha bunge la Tanzania na kuondoa mashaka juu ya fikra kwamba linatumika na kutumikishwa na serikali , Matendo na kauli za Ndugai kuhusu Lissu ni sawa na kujionyesha yeye mwenyewe kwenye uso wa dunia kwamba hana utu na wala hajawahi kuwa nao , huyu Musukuma mtu aliyefeli mtihani rahisi wa darasa la 7 kutoa mwongozo bungeni , ni mpango tu wa kukamilisha mchakato wa kibunge kwa matakwa ya Ndugai na waliomtuma
 

Serikali ya wanyonge!! endeleeni kunyonga tu ila jueni kuwa kila kitu kina mwisho, mimi mwenyewe na ushamba wangu ninajua aliyopitia tundu lissu hadi sasa, yeye mkuu wake hajui kivipi kama siyo unafiki? Tangu ameumia ni kipi mmefanya kuonyesha kuwa mmeguswa? mlitaka afe? nini mnaficha hadi mnachukia watanzania kiasi hiki? mmekosa utu kiasi kwamba mnamchukia mtu mwenye kutetea haki za wananchi wenu? Allaah awaongoze.
 
Ajavunja sheria ila njaa zinamsababisha kwenda kulia lia ughaibuni ila usijadanganye kwamba atampiga chini mwenye chama.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshahara analipwa mtu ambaye yupo kazini au nje ya kazi kwa sababu za msingi na kwa taarifa kwa anayemlipa mshahara.

Ni kweli Lissu inafahamika alipatwa na tukio la kinyama sana la kupigwa risasi ila haipendezi kusikia kuwa chama chake kwa niaba ya mhusika kilishindwa kumpa spika taarifa rasmi pamoja na taarifa za madaktari juu ya maendeleo ya Lissu alipo kwa ajili ya matibabu.

Kingine, kwa sasa Lissu ameonekana kuimarika kwa kiasi kikubwa, jambo ambalo kila mmoja wetu anapaswa kumshukuru Mungu kwa kuendelea kumpa neema ya uhai. Hivyo ikiwa amepewa muda wa kuwa nje ya hospital ilikuwa ni busara kwa Mhe Lissu kurejea nchini kwa ajili ya kuonana na familia yake, jamaa na marafiki zake kubwa zaidi wananchi waliompa ridhaa ya kuwawakilisha bungeni pamoja na wasamaria wema waliomchangia matibabu.

Angefika kusema asante, angefika angalau kwa muda huu mchache aendelee na uwakilishi wa wananchi wenzake pale bungeni mpaka hapo atakapohitajika kurejea hospitalini. Kinyume chake ameamua kufanya ziara za kuishutumu, kuishambulia na kuharibu taswira ya serikali yetu ya Tanzania katika nchi Ulaya na Marekani. Jambo hili halina afya kwake wala kwa chama chake.

Ni hatari kukubali kuichafua nchi yako sababu unalipwa au unataka kupata ushawishi kwa wananchi walio wengi. Huku ni kukosa uzalendo.

Namalizia kwa kushauri, dereva wake bado ni shahidi namba moja ambaye anaweza kulisaidia jeshi la polisi taarifa za msingi juu ya tukio hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Spika DHAIFU sana. Uwezo wake kiakili na kiuongozi ni finyu mno. Anaingia katika historia kama ni spika wa hovyoo haijawahi kutokea tangu Tanganyika ipate Uhuru. Ni aibu kubwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…