Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Unaona wivu sio?!
Ni hatari sana kwa kiongozi mkubwa kama huyu mwenye madaraka makubwa na ukaribu na watawala kuanza kulalamika kama wanywa kahawa wa vijiweni. Mbona kauli hii inaogopesha?
Kweli kabisa, ukiona MTU mkubwa kama huyo analalamika hii lazima iogopeshe, sasa kinachotakiwa watu wazungushe akili ili mambo yaende sawa,, !! " if you think hard enough, problems could always be solved "!!
 
Spika kama hutanii kua 2025 wananchi tuamue wenyewe nijambo jema nikushauri utusaidie kupaza sauti na mamlaka ulonayo kupata katiba mpya ambayo itatupa tume huru,yani nakwambia utaweka heshima kubwa ktk taifa hili,nimesema hayo kwakua wananchi tunatambua hii nchi tangu uhuru mnaongoza nyinyi ccm, kama kweli unataka watanzania wakuelewe simamia katiba yawalioba ujiwekee heshima.
 
Kuna watu walikuwa wanalaumu JPM kwa kukopa
Ghafla wamebadilika wanaunga mkono mikopo
Kwani jpm si alikuwa anasema HATUKOPI? SISI NI DONA KANTREE..MABEBERU WASITUTISHE...TUNAJENGA SGR,BWAWA KWA PESA ZETU...Leo imekuwaje?kumbe alikuwa anakopa?

TITAELEWANA TU
 
Thubutu!!!!!! Ukitaka kuona uzalendo wao upo wapi jaribu kugusia maslai yao kupunguzwa uone watakavyi kushambulia
 
Simbachawene na jeshi lake wasitoe kwenye reli kwa kulazimisha watumishi wa Mungu kukamatwa wakati serikali yao inalipa mpaka mr
 
Punguza kuwa Negative siku zote mkuu, wewe siku ukiigua ndugu na jamaa wakakuchangia ukapate matibabu wakikusema utajisikiaje.

Jaribu kutumia kichwa kufikiria sio kila kitu unaandika kwa kufikiria matako tu.
Imekuuingia hiyoo eeh .. Ndugai ni mnafiki mkubwa, kwani serikali imeanza kukopa leo ? Alikua wapi siku zote ? Sasa hivi ndio anapata nguvu ya kujitutumuaa.
Mbona vitu vingi tu vya serikali vilikua havipitishwi na bunge , yeye lilikuwepo tu pale Kama poyoyo.
 
Spika anahusika na kuongezeka kwa Deni la taifa kwa kuendeleea kuwalipa wabungu wasio na chama na inasikitish anavyolalama na Deni la taifa
 
Maneno ya Lissu yanazidi kutimia.
Mliwaona wapinzani adui kumbe ndio wanasaidia kuendesha nchi hii.
"Mkimaliza na sisi mtaparuana wenyewe kwa wenyewe"
Asante ATL.
Deni la taifa limeongelewa sana na kina Zito, Lema bado hatushtuki.
Hayo madarasa yanajengwa shule hazina maji safi na salama.
Waalimu wachache! Je madawati yapo?
Kuna mengi hapo. Na fedha hii inpigwa kwa kwenda mbele. Sio vijiji vingi vinapata hii pesa. Tuamkeni.
KATIBA KATIBA KATIBA NI MUHIMU KWA KIZAZI KIJACHO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…