Jobless mwenzangu, unafanyaje kupata nguvu mpya baada ya akili na mwili kuchoka na mapambano ya utafutaji maisha?

Jobless mwenzangu, unafanyaje kupata nguvu mpya baada ya akili na mwili kuchoka na mapambano ya utafutaji maisha?

mimi mtakatifu

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2019
Posts
248
Reaction score
539
Umeshatuma maombi ya kazi miezi mpaka unahesabu miaka lakini hupati kazi.

Unatafuta vibarua vya kujishikiza navyo inakuwa ni mtihani.

Unafanya kila kitu kujaribu kujinasua na mkwamo wa maisha ikiwemo mambo ya kiimani ila bado hupati matokeo. Uvumilivu, kupambana, ubunifu, experience, knowledge na kila kitu kinashindwa kukupa matokeo mazuri.

Sasa taratibu akili nayo inaanza kuchoka, ulikuwa unafanya application unakosa nguvu. Ilikuwa unazunguka door to door hiyo nguvu tena inakwisha. Mawazo mapya huna tena.

Watu wa kukubeba wamepotea wote. Unatamani upate idea mpya ya namna gani unajinasua ila kichwa hakina tena uwezo wa kufikiri kama zamani. Unaweza kaa siku nzima hujui cha kufanya unaenda mpaka mwezi ufanyi lolote sio kwa kupenda ila akili na mwili haviwezi tena kufanya kazi actively kama awali.

Kwa aliyewai kupitia hali hii alifanya nini ili ku-gain back zile energy za kupambana?

Motivation uliipatia wapi?
 
Just relax, vuta pumzi kwa na imani mambo yataa sawa, cha umuhimu tu ondoa mawazo epuka sana stress maana zitakupoteza kabisa ishi kama vile unamaisha teyar hata kama hauna just imagine... utakuja kunishukuru
 
I can feel unachokipitia but mafanikio kwanza yanaanza kwenye imagination. Hata ukiangalia waliofanikiwa watakuambia wali imagine kwanza watakavyofanikiwa na wakawa hivyo. So Lazima upige moyo konde ukiamini siku yako ya kufanikiwa ipo na imeeandikwa Apo ndo utapata energy ya kupambana. Lakini pia Kama ni mpenzi wa vitabu soma motivation books
 
Aisee cha kwanza tambua hiyo situation haupitii wewe peke yako, tuko wengi mkuu ila tunatofautiana kimtazamo akilini. Viko vingi ningeweza kukuambia lkn anza na hilo
 
Back
Top Bottom