Joe Biden na Xi Jinping wakutana nchini Peru. Xi akubali kushirikiana na serikali mpya ya Trump

Joe Biden na Xi Jinping wakutana nchini Peru. Xi akubali kushirikiana na serikali mpya ya Trump

instagram

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,118
Reaction score
4,863
Rais wa China Xi Jinping amesema yuko tayari kushirikiana na serikali mpya ya Donald Trump kuhakikisha mpito mzuri katika uhusiano wa mataifa yao.

Xi alitoa kauli hiyo alipokutana kwa mara ya mwisho na Rais anayemaliza muda wake, Joe Biden, katika mkutano wa Asia-Pacific uliofanyika Lima.

Mkutano huo ulihudhuriwa huku kukiwa na wasiwasi wa vita vipya vya kibiashara na mvutano wa kidiplomasia pindi Trump atakapoingia Ikulu ya Marekani mwezi Januari. Xi alisema China iko tayari kudumisha mawasiliano, kupanua ushirikiano, na kusimamia tofauti na Marekani kwa lengo la kuimarisha uhusiano wao.

Biden, akielezea maendeleo ya uhusiano wao, alisema anajivunia kazi waliyoifanya pamoja, akisisitiza kuwa mashindano kati ya nchi zao hayawezi kuruhusiwa kugeuka kuwa mizozo.

Alibainisha kuwa, kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, wameonyesha inawezekana kuwa na uhusiano wa kiushindani bila kuingia kwenye migogoro.

Mkutano huo ulikuwa wa pili wa ana kwa ana kati ya Xi na Biden tangu mkutano wao wa kihistoria wa kutuliza mvutano uliofanyika California mwaka uliopita.

images (24).jpeg

My take:
Kweli ndiyo maana wenzetu wameendelea sana mkutano watu wazito kama hawa ila kila mtu kwenye meza ana kiti kinafanana bila kujali cheo na hakuna mabwana wakubwa wawili ambao wametengewa viti vyao vya enzi na ma AC yao peke yao ya kusimama jirani yao.

Ingekuwa ni nchi zetu za Africa zenye umaskini wa hela na teknolojia ungekuta hata mkuu wa kijiji ana kiti chake kireeefu zaidi kuwapita wenzake kwenye mkutano.

Source: MSN
 
Eti Xi jimping kakubali kushirikiana na serikali mpya ya Trump, 😁
Kwani ni lini china imekataa kushirikiana na serikali ya marekani?
Wachina ni jamii inayofanya kazi na yeyote sema wanakupokea vile unavyokuja. Ukija vizuri wanakupokea vizuri na ukija vibaya wanakupokea vibaya

Media za magharibi ziache kujitutumua
 
Confirmed; hakuna tena Vita kati ya China na Hong Kong iliokua inataka kujitenga. Hong Kong itaendelea ku report Beijing kama ilivo Zanzibar to Dodoma
 
Rais wa China Xi Jinping amesema yuko tayari kushirikiana na serikali mpya ya Donald Trump kuhakikisha mpito mzuri katika uhusiano wa mataifa yao.

Xi alitoa kauli hiyo alipokutana kwa mara ya mwisho na Rais anayemaliza muda wake, Joe Biden, katika mkutano wa Asia-Pacific uliofanyika Lima.

Mkutano huo ulihudhuriwa huku kukiwa na wasiwasi wa vita vipya vya kibiashara na mvutano wa kidiplomasia pindi Trump atakapoingia Ikulu ya Marekani mwezi Januari. Xi alisema China iko tayari kudumisha mawasiliano, kupanua ushirikiano, na kusimamia tofauti na Marekani kwa lengo la kuimarisha uhusiano wao.

Biden, akielezea maendeleo ya uhusiano wao, alisema anajivunia kazi waliyoifanya pamoja, akisisitiza kuwa mashindano kati ya nchi zao hayawezi kuruhusiwa kugeuka kuwa mizozo.

Alibainisha kuwa, kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, wameonyesha inawezekana kuwa na uhusiano wa kiushindani bila kuingia kwenye migogoro.

Mkutano huo ulikuwa wa pili wa ana kwa ana kati ya Xi na Biden tangu mkutano wao wa kihistoria wa kutuliza mvutano uliofanyika California mwaka uliopita.


View attachment 3154381


My take:

Kweli ndiyo maana wenzetu wameendelea sana mkutano watu wazito kama hawa ila kila mtu kwenye meza ana kiti kinafanana bila kujali cheo na hakuna mabwana wakubwa wawili ambao wametengewa viti vyao vya enzi na ma AC yao peke yao ya kusimama jirani yao.

Ingekuwa ni nchi zetu za Africa zenye umaskini wa hela na teknolojia ungekuta hata mkuu wa kijiji ana kiti chake kireeefu zaidi kuwapita wenzake kwenye mkutano.

Source: MSN
The bottom line says it all.
 
Kikao cha wababe wa uchumi, technolojia na takataka zote. Sijaona wa kufanana na mwijaku.
 
Confirmed; hakuna tena Vita kati ya China na Hong Kong iliokua inataka kujitenga. Hong Kong itaendelea ku report Beijing kama ilivo Zanzibar to Dodoma
Ujinga mtupu hakujawahi kuwepo kwa huo upuuzi unaoita vita kati ya China na Hong-Kong.

Na ni ujinga kufananisha taifa huru Zanzibar na masuala ya Hong-Kong eneo la China, sidhani hata historia ya Hong-Kong kwa China unaifahamu maana unafananisha vitu visivyo fanana.
 
Ujinga mtupu hakujawahi kuwepo kwa huo upuuzi unaoita vita kati ya China na Hong-Kong.

Na ni ujinga kufananisha taifa huru Zanzibar na masuala ya Hong-Kong eneo la China, sidhani hata historia ya Hong-Kong kwa China unaifahamu maana unafananisha vitu visivyo fanana.
Nani mjinga sasa kaka? Mimi au ule mzozo?
 
Back
Top Bottom