TANZIA John Livingston Mwakipesile, Mbunge wa zamani wa Kyela afariki dunia

TANZIA John Livingston Mwakipesile, Mbunge wa zamani wa Kyela afariki dunia

Alituchelewesha sana. Chanjo tungeanza nazo mapema wazee hawa wangekuwa hai leo. Tunaendelea kupoteza watu leo kwa ajili yake.

Umenisoma ewe kajamaa?
Kwahiyo ujui nini kimemkuta aliyekuwa waziri mramba baada ya kuchanja
 
😂😂😂😂😂😂😂 Hiiiiii bagosha!

Kwani wewe ni mtalaamu mbobezi wa masuala ya afya?

Umelisikia tamko la serikali kutoka kwa wabobezi wataalamu wa afya kumhusu Gwajima?

"Atawajibishwa kwa vifo vyote hata vinavyotokea sasa kutokana na upotoshaji wake kuhusiana na chanjo."

Haiyumkiniki tamko hilo litawafuatilia wahusika wa upotoshaji wote hata kama wako Chato.


Serikali na wanaotuongoza wanapaswa wafahamu jambo moja la muhimu. Kuwasainisha watu waraka wa kujitoa muhanga ni jambo moja na vifo vitakapo kuwa vingi kutokana na chanjo " hatuombei hiyo itokee" kuzuia nguvu ya umma kutaka kujua kwa nini wapendwa wao wameuliwa na chanjo yenye walakini litakuwa jambo jingine.

Ikiwa chanjo itagundulika kuleta madhara kwa wengi " hatuombei" wajue umma utawageuka kuanzia wenye uwezo wa kupiga mayowe na vilio mpaka warusha mawe, wabeba marungu na mapanga na wabeba zana nyingine. Hili si jambo la kujiingiza mzima mzima bila ya kulitafakari mara kadhaa.

Wazungu hawa wanaotoa chanjo leo za msaada watawageuka hawanaga hasara hawa. Huangalia upande unao shinda. Anaye bisha angalie ya Afghanistan leo. Wametelekeza maelfu ya roho za wanajeshi wao walio poteza maisha kwenye vita vya ugaidi na vilema wa kumwaga, matrillioni ya dollari etc lakini sasa wameguka wanawaunga mkono Talliban walio waita magaidi na walea ugaidi duniani kwa kuwa achia waiangushe serikali kiulaini.
 
Kwahiyo ujui nini kimemkuta aliyekuwa waziri mramba baada ya kuchanja

Kwani wewe unaishi kisiwa?

"Waziri wa Zamani, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo agosti 17 akiwa anapatiwa matibabu regency hospital. Mramba alilazwa wiki mbili zilizopita kwa maradhi ya COVID-19.

Kifo chake kimesababishwa na Mshituko wa Moyo(Cardiac arrest)..."

Chanjo zilianza kutolewa wakati Mramba akiwa keshalazwa kwa covid 19.

Hata hivyo yamesemwa pia sana:

#COVID19 - Chanjo isiwe Siasa, Vigezo na Masharti vizingatiwe

Vigezo na masharti kwenye chanjo yanazingatiwa?

Au zoezi ni siasa tu zile zile za kutokea awamu ile?
 
Mramba ni strock imetokana na chanjo kugandisha damu

Acheni upotoshaji:

"Waziri wa Zamani, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo agosti 17 akiwa anapatiwa matibabu regency hospital. Mramba alilazwa wiki mbili zilizopita kwa maradhi ya COVID-19.

Kifo chake kimesababishwa na Mshituko wa Moyo(Cardiac arrest) .."

Mramba alilazwa kwa covid-19 kabla ya chanjo kuanza kutolewa. Bila kusahau:

#COVID19 - Chanjo isiwe Siasa, Vigezo na Masharti vizingatiwe

Cc: Elli M
 
Acheni upotoshaji:

"Waziri wa Zamani, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo agosti 17 akiwa anapatiwa matibabu regency hospital. Mramba alilazwa wiki mbili zilizopita kwa maradhi ya COVID-19.

Kifo chake kimesababishwa na Mshituko wa Moyo(Cardiac arrest) .."

Mramba alilazwa kwa covid-19 kabla ya chanjo kuanza kutolewa. Bila kusahau:

#COVID19 - Chanjo isiwe Siasa, Vigezo na Masharti vizingatiwe

Cc: Elli M
Basi sawa kumbe ni covid virus si covid chanjo sasa yeye alikuwa anangoja nini kuchanjwa siyupo ccm na umri wake zaidi ya 50
 
Vifo vimekuwa vingi sana, utasema tuko kwenye msimu wa Vita.
 
Basi sawa kumbe ni covid virus si covid chanjo sasa yeye alikuwa anangoja nini kuchanjwa siyupo ccm na umri wake zaidi ya 50

Ninakazia:

"Waziri wa Zamani, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo agosti 17 akiwa anapatiwa matibabu regency hospital. Mramba alilazwa wiki mbili zilizopita kwa maradhi ya COVID-19."

TANZIA - Waziri wa zamani, Basil Pesambili Mramba afariki dunia

Chanjo zimeanza kutolewa 3 August Marehemu akiwa keshalazwa kwa Covid-19 tayari.

Alaumiwe sana aliyetuchelewesha kupata chanjo hizi mapema.
 
Duniani tu wapangaji KILA mmoja anaenda kufa kwa wakati wake ukifika muhimu unaacha kipi duniani cha kumbusha Mungu akupunguzie adhabu kwa wema uliotendea waliohai.
 
Duh! huyu kocha wa corona united sijui anatumia formation gani haeleweki sijui 442 au 532 au total football kama sio 22222 yaani hasomeki aaagh
 
Ninakazia:

"Waziri wa Zamani, Basil Pesambili Mramba amefariki dunia leo agosti 17 akiwa anapatiwa matibabu regency hospital. Mramba alilazwa wiki mbili zilizopita kwa maradhi ya COVID-19."

TANZIA - Waziri wa zamani, Basil Pesambili Mramba afariki dunia

Chanjo zimeanza kutolewa 3 August Marehemu akiwa keshalazwa kwa Covid-19 tayari.

Alaumiwe sana aliyetuchelewesha kupata chanjo hizi mapema.
Nanda iwanja wa ndege kuna msiba wa jamaa kafariki baada ya chanjo hapo wafanyakazi wa air port wameingia hofu baada ya huyo jamaa kufa kama mimi muongo basi waandishi wa habari waliopo hapa waende kuuliza ,wewe uliwasikia wizara wakisema kuwa madhara ya kovidi yasijulikane kwa yoyote ni kampeni ya kitaifa
 
Back
Top Bottom