Pre GE2025 John Mnyika kapwaya sana Ukatibu Mkuu CHADEMA, nashauri aachie ngazi mara moja kwa heshima, itamsaidia zaidi kisiasa baadae

Pre GE2025 John Mnyika kapwaya sana Ukatibu Mkuu CHADEMA, nashauri aachie ngazi mara moja kwa heshima, itamsaidia zaidi kisiasa baadae

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
katiba si kipaumbele kwa sasa,

huenda tukacheki baada ya uchaguzi mkuu2025 :pedroP:
😂😂 kama kikwete, Magu na Mama sio kipaumbele😂 kitu kizuri Mungu atasafisha njia na kubaliza wale watakao itoa hii nchi mtaona matukio mengine mpaka kieleweke
 
😂😂 kama kikwete, Magu na Mama sio kipaumbele😂 kitu kizuri Mungu atasafisha njia na kubaliza wale watakao itoa hii nchi mtaona matukio mengine mpaka kieleweke
ushirikina unawapenda sana wasio na uelekeo,

wenye Imani thabiti na wenye malengo tunasonga mbele kwa Neema na Baraka za Mungu bila mbambamba yoyote 🐒
 
ushirikina unawapenda sana wasio na uelekeo,

wenye Imani thabiti na wenye malengo tunasonga mbele kwa Neema na Baraka za Mungu bila mbambamba yoyote 🐒


Mungu sio mshirikina ni kwa wale tu wezi tu ndiyo watafikiria hivyo. Mungu endelea kuisaidia hii nchi maana watu bado hawajielewi
 
Mungu sio mshirikina ni kwa wale tu wezi tu ndiyo watafikiria hivyo. Mungu endelea kuisaidia hii nchi maana watu bado hawajielewi
acheni kung'ang'ana na Imani potofu na ramli kama mnamtegemea Mungu sasa....

kuweni majasiri na wenye Imani thabiti, kwa Mungu hakuna kumbwelambwela kama mlivyo nyie 🐒
 
Nafasi ya uwakilishi, mathalani udiwani n.k inamfaa zaidi kuliko pale alipo sasa, halafu mbaya zaidi kuna uwezekano mkubwa akatoswa baada ya uchaguzi ndani ya chadema kumalizika baadae mwaka huu.

Kuliko kusubiri fedheha hiyo itakayo muathiri kisiasa, Busara imuelekeze kuachia ngazi kulinda heshima, hadhi na umarufu kidogo sana aliojipatia akiwa kwenye nafasi hiyo nyeti ya chama. aachie ngazi apate fursa ya kujipanga kuomba nafasi za uwakilishi hususani udiwani, na atabaki akiheshimika zaidi...

Kwakweli katibu mkuu chadema ni mnyonge mno aliezongwa na kuzingirwa na wenye sauti na nguvu ya pesa ndani ya CHADEMA, si Mnyika yule wa escrow tena kadhibitiwa vizuri sana right left and center na macatels ndani ya chama, hafurukuti bana, kapoaaa.

Ni katibu mkuu mwepesi mno, hana vibe tena, wala hamasa au haiba ya ukatibu mkuu, hana misuli, wala meno ya kimamlaka ndani ya chadema, utendaji wake umepoa mno, uko limited na unatambulika na kuheshimika kwa uchache sana ndani na nje chadema hususani kwenye matukio ya shari tu.

Ni kama vile kafungwa mikono na kuzubwa mdomo kisiasa, hawezi kung"aka wala kumbwekea yeyote ndani ya CHADEMA ila yeye anabwekewa sana kwamba hatoshi na hana ubavu pale CHADEMA.

Kadhibitiwa vizuri na waandamizi wenye nafasi nyingine ndani ya chadema, hafurukuti kabisaa, unaweza kusema naibu wake ndie ana nguvu, sauti uthubutu na ushawishi zaidi yake.

Katibu Mkuu wa CHADEMA ni mpweke sana ndrugu na kaka yangu John Mnyika. wema, woga na ustaarabu wake nadhani umezidi kiwango cha ukatibu mkuu, umemfanya awe si lolote si chochote CHADEMA. Awepo CHADEMA sawa, asipokuwepo nayo sawa. hana mipango, si mbunifu, si mjenga hoja tena Mnyika. yawezekana amekua mtu mzima, but amekua vibaya.

Nadhani aliililia nafasi ya ukatibu mkuu angali bado kijana mdogo, Lakini akiwa na matarajio makubwa na matokeo yake akakuta hali ni ndivyo sivyo. nadhani ameshindwa kabisaa kutengeneza chemistry na viongozi wengine waandamizi ndani ya chama, kitu ambacho kimemfanya awe mpweke mpaka sasa.

Akiacha ngazi sasa kwa heshima, huenda akawa na historia tukuka sana kwenye siasa za vyama na akaja kua kiongozi mwandamizi wa kisiasa mwenye nguvu na heshima sana huko mbeleni.

Kama kijana mtaalamu na mbobevu wa masuala haya ya siasa za Tanzania na hususani ndani ya chadema, namshauri kwa heshima, mungwana huyu rafiki yangu John J. Mnyika aachie ngazi mapema iwezekanavyo kadiri anavyoona inafaa.

Soma Pia:

Nafasi za uwakilishi mathalani udiwani zinamfaa zaidi, kuliko kuliko anachokifanya sasa hivi na hana sababu hata moja kusubiri kutoswa ndani ya chama chake wakati uchaguzi mkuu ukiwa umekwisha.
na kutoswa kwake kupo nje nje sana CHADEMA.

Ni muhimu kuamua na kuchukua hatua sasa, na kama sio sasa ni sasa hivi 🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Hongera kwa kumtakia mema, lakini kwa nini usimtabirie Uwaziri Mkuu au hata Urais badala ya udiwani?

Alishakuwa Mbunge na aliimudu sana hiyo nafasi. Labda umshauri Lissu akifanikuwa kuukwaa Urais amteue nafasi ya Uwaziri Mkuu!
 
acheni kung'ang'ana na Imani potofu na ramli kama mnamtegemea Mungu sasa....

kuweni majasiri na wenye Imani thabiti, kwa Mungu hakuna kumbwelambwela kama mlivyo nyie 🐒

Kila mtu ana imani yake wewe fuata Mungu wako na sio waachie watu na imani zao.
 
Hongera kwa kumtakia mema, lakini kwa nini usimtabirie Uwaziri Mkuu au hata Urais badala ya udiwani?

Alishakuwa Mbunge na aliimudu sana hiyo nafasi. Labda umshauri Lissu akifanikuwa kuukwaa Urais amteue nafasi ya Uwaziri Mkuu!
hata wewe unaweza kumtabiria na ikatosha, au huna imani?:pedroP:

halafu hiyo ya kusubiria dodo chini ya mnazi ndio ushirikina mbaya zaidi duniani...

uongozi kujipanga na kutafuta kwa bidii sana my friend, kwa ramli hutoboi, utasubiri sana....
 
Kuwa mwangalifu usije kufutwa hapa. Wewe endelea na uchawa wako badala ya kuweka weka maneno kwa Sr Members ambao ni founders
kwahiyo wanafuta watu kazi au? hebu elezea vizuri kwa kina kifupi kwa faida ya wadau gentleman..

kumbuka pia uoga wako ndio umaskini wako, vigezo na masharti kuzingatiwa :NoGodNo:
 
Back
Top Bottom