john mnyika wa CHADEMA alipata Div ngapi?

john mnyika wa CHADEMA alipata Div ngapi?

Duuuh hii kali ya leo! Kila mtu basi angekuwa anapata DIV 1.....! unaweza kutoa statistics kwa unachokisema?

Mkuu umepotea!

unapanga bajeti ya uchaguzi nini na kukamilisha logistics za masanduku ya kura?

Kama uko ubungo please mjitokeze kwenye kampeni na kupiga kura kijana huyu aingie mjengoni
 
Wabongo tatizo letu ndilo hili hili, kuangalia sana paper credentials na superficialities, ndiyo mana watu mpaka leo wanaongelea electability ya Kikwete kwa sababu ni so called "handsome" despite Nyerere kuwapiga shule.

Rais Harry S. Truman wa US hakuwa hata na college degree,lakini aliliongoza taifa lake vizuri, wakati wa vita nevertheless. John Major naye kaenda kuwa PM wa Uingereza bila ya college degree, leo hii mtu usipokuwa na degree naamini unakuwa disqualified, sasa tutawapata wapi kina Evo Morales wetu? Ina maana mtu mwenye enterpreneurial genius kama ya Bill Gates hawezi kuwa rais bongo kwa sababu tu hana degree, kunawengine wanaona degrees/ academics zinawapotezea muda tu, nao wasiwe na eligibility?

Swala muhimu hapa ni track record, Mnyika kafanya nini katika miaka yake ya kazi CHADEMA. Naamini mwenyewe ni member humu anaweza kuja na waraka wa kujibu kuhusu kazi.Vitu hujulikana uzuri wake kwa matokeo ya kazi, sio kwa paper qualifications ambazo mwenyewe ushaanza kuzikandya kwamba papers zinaleak.

Uki dispute/ tarnish matokeo ya form four kwamba paper zinaleak, basi inamaana hata kwa papers za form six paper si kigezo.

Let's focus on kazi, amefanya kazi gani? Haya mambo ya papers papers Tanzania kuna papers bwana? Papers zenyewe hazina standars wala syllabus, akija Mungai anabadili vyake akija Sitta anapangua hivi, kuna papers huko bongo zaidi ya kukomoana tu?

Ndiyo nyie nyie anakuja tapeli kavaa suti kubwa anaongea "kizungu" kigumu, ananukia uturi maridadi, mnamfungulia milango yote anaiba kila kitu.

Akija an ascetic intellectual shabbili dressed anayeweza kuwasaidia mnamfukuza. Kila kitu watu wanaangalia the superficial, wanaona the shallow bila kutaka kujua the deep.


Mkuu mbona umeandika vitu vingi hata visivyohitajika hapa halafu kwa dharau naona unajaribu kuniwekea maneno ambayo sikuyasema.Hakuna aliyesema Mnyika hafai kuwa kiongozi kwavile alifaulu au alifeli sekondari.Bado sikusema kuwa kigezo cha uongozi Tanzania au ili kuwa kiongozi bora ni lazima uwe na shahada ya chuo kikuu.Isipokuwa mleta mada anataka kujua kama Mnyika alipata sifuri au la,tena akauliza ni muhimu?Sasa hiyo longolongo yako ya kina Truman nadhani ingekuwa vema kama ungemjibu muuliza swali wakati unamsifia Mnyika kuwa ni kichwa kwa vile alipata A zote kidato cha nne.
Wengine hatukubali mtu kuitwa kichwa eti kwavile alipata A zote kidato cha nne.Na si kwa Mnyika tu,ni kwa yeyote yule.Na kama Mnyika anataka kuwavutia wapiga kura kwa matokeo yake ya sekondari basi ni vema walau angetaja yote na si A zake za form 4 tu.
 
.....Na kama Mnyika anataka kuwavutia wapiga kura kwa matokeo yake ya sekondari basi ni vema walau angetaja yote na si A zake za form 4 tu.

Mnyika hajataka kuwavutia wapiga kura kwa matokeo yake ya sekondari .. bado unaendeleza mechi?
 
Yeye mwenyewe keshajibu kwanini mjadala usifungwe? Kwa sababu aliyeuliza alitaka kujua na mtuhumiwa keshajibu kwa maandishi,mchezo kwisha.
 
Walijua Mh. Mnyika atachukua ubunge na mwizi wa kura kaamua kutogombea na sasa wanahaha angalau waligawe jimbo kwani wamegundua mkuu anakuja kwa kasi, huku ni kutafutiana ulaji pale wanapoona mambo yamewaharibikia kama wanavyotaka kufanya kuligawa jimbo la Zitto.
 

Kwa kumbukumbu zangu... kama nakumbuka sawa ... which if I remember correctly ...

Hizo ulizotoa ni taarifa za matokeo ya mitihani yote miwili, kidato cha nne na sita?

"Kama sikosei...sina hakika...kama nakumbuka...washashi nisahihisheni" zimesheheni kujengea msingi wa hoja ya kumwombea msamaha mtahiniwa ukitetea matokeo. "Kama nakumbuka vizuri," kama unakumbuka vibaya?

Umesema huna hakika na, yani hujui, maana ya daraja la kwanza nukta saba, halafu unatwambia kihitimisho kwamba alipata "A" tisa tumpe heko. Tusijekuwa tunamkejeli.

Unasema alipata alama "A" tisa, daraja la kwanza nukta saba, halafu unasema utashangaa akiwa na daraja sifuri. Si umeshadai alipata "A" tisa? Sasa mbona unaruhusu uwezekano wa daraja sifuri kama vile kuna daraja sifuri la "A" tisa? Jisome kabla ya kuharakisha kusomesha kwa "kumbukumbu za harakaharaka."

Umesema haijalishi kimaisha kuwa na matokeo mazuri au mabaya ya shule halafu papo hapo unajikita kumuombea msamaha ukitetea matokeo. Ukishataja "haijalishi" weka alama ya nukta papo hapo. Nukta.
 
Mkuu p53... much as i agree with you kwamba kuna watu wanapata mitihani na kuwa na scores wasizo-deserve, it is impossible kwa kilaza kupata 1 ya point saba form four hata akilala na mitihani wiki moja!!!

even the mediocre huwa wanaishia div 1 ya point 12-15 baada ya kukesha na pepa zao

Lets give each other credits where and when it matters most and in this case John deserves some credits

I am glad he is still our active member


De Novo salute mkuu!Wewe walau unaongea hali halisi na umeelewa naongelea nini.Anyway hata angepata div 3 anastahili hongera vilevile manake na yenyewe ni alama ya kufaulu!
 
De Novo salute mkuu!Wewe walau unaongea hali halisi na umeelewa naongelea nini.Anyway hata angepata div 3 anastahili hongera vilevile manake na yenyewe ni alama ya kufaulu!

ha ha ha ... hii dunia ya musa, pharao, kunta kinte, na haruni inafurahisha sana!
 
Mkuu mbona umeandika vitu vingi hata visivyohitajika hapa halafu kwa dharau naona unajaribu kuniwekea maneno ambayo sikuyasema.Hakuna aliyesema Mnyika hafai kuwa kiongozi kwavile alifaulu au alifeli sekondari.Bado sikusema kuwa kigezo cha uongozi Tanzania au ili kuwa kiongozi bora ni lazima uwe na shahada ya chuo kikuu.Isipokuwa mleta mada anataka kujua kama Mnyika alipata sifuri au la,tena akauliza ni muhimu?Sasa hiyo longolongo yako ya kina Truman nadhani ingekuwa vema kama ungemjibu muuliza swali wakati unamsifia Mnyika kuwa ni kichwa kwa vile alipata A zote kidato cha nne.
Wengine hatukubali mtu kuitwa kichwa eti kwavile alipata A zote kidato cha nne.Na si kwa Mnyika tu,ni kwa yeyote yule.Na kama Mnyika anataka kuwavutia wapiga kura kwa matokeo yake ya sekondari basi ni vema walau angetaja yote na si A zake za form 4 tu.

Na mimi sikusema kwamba umesema unachofikiri kwamba nimesema umesema.

Au ni maswala ya joka la mdimu?
 
Kama unaona kuwa hii ni ligi ya kombe la mbuzi, basi mimi naenda kununua njumu na jezi maana game ya kwanza ndio imeanza hivi.



Hakuna "siri" kuwa mitihani inavuja lakini hiyo siri haijafanya matokeo ya mitihani yawe feki kwa vile wajanja wachache walipata mtihani. Umeandika kaa vile una habari za ndani za wizi wa mitihani bongo hence swali langu kwako - matokeo yako nawe ni feki?

BTW - unamkumbuka aliyeandika hiki hapa chini?




Mimi sina habari zozote za ndani mkuu zaidi ya kufuatilia taarifa za kwenye vyombo vya habari.Sasa kwenye mazingira ya mitihani kuvuja hata credibility ya matokeo inakuwa ni ya mashaka pia.
Kwahiyo wewe Mkuu yanayoandikwa hapa JF yote unayachukulia ni ukweli?Mtu akisema ana PhD hapa wewe unaamini kweli anayo?Mtu akisema anafanya Masters wewe unaamini kabisa kuwa ni kweli?Mtu akiandika alisoma Azania wewe unaamini kabisa ni kweli?Jifunze kutokuamini yote unayosoma hapa JF mkuu.
 
Jifunze kutokuamini yote unayosoma hapa JF mkuu.

Ebana naomba niitumie hii line kama sahihi yangu hapo chini....maana ina akili nyingi sana kwa sababu kuna watu kweli wanaamini kama wanavyoamini misahafu wanachokisoma hapa JF
 
Mimi sina habari zozote za ndani mkuu zaidi ya kufuatilia taarifa za kwenye vyombo vya habari.Sasa kwenye mazingira ya mitihani kuvuja hata credibility ya matokeo inakuwa ni ya mashaka pia.
Kwahiyo wewe Mkuu yanayoandikwa hapa JF yote unayachukulia ni ukweli?Mtu akisema ana PhD hapa wewe unaamini kweli anayo?Mtu akisema anafanya Masters wewe unaamini kabisa kuwa ni kweli?Mtu akiandika alisoma Azania wewe unaamini kabisa ni kweli?Jifunze kutokuamini yote unayosoma hapa JF mkuu.
Kwahiyo JF kumejaa uongo mtupu?
 
Ahh hizi ndio hadithi ya sizitaki mbichi hizi.Kama kupiga A saba ni rahisi katika zama hizi za mitihani ku-leak mbona hatuzioni hizo As za kumwaga?Kumbuka,kupewa mtihani au kuuona mtihani kabla ya kuingia exam room hakumaanishi kichwa panzi atapata A.Sanasana ataepuka kupata Fs.Kwani umeambiwa kuona mtihani ni sawa na kuona majibu?

Tusimzungumzie yule kilaza kabisa asiyejiweza darasani.Chukulia kwa mfano mwanafunzi mwenye uwezo wa kupata div 3 bila kwenda tution wala kuona mtihani,basi kama atauona anaweza kupata A nyingi tu bila ubishi.Sasa tumuone huyu mtu aliyesomea 'shambani' bila kwenda tution wala kuona feki siyo kichwa kwavile hakupata A saba?Tumuone wa A saba aliyemaliza syllabus yote ya o'level kwenye tution akiwa ndiyo kwanza yuko kidato cha tatu halafu inawezekana akawa ameona mtihani eti ndiye kichwa?
 
Ebana naomba niitumie hii line kama sahihi yangu hapo chini....maana ina akili nyingi sana kwa sababu kuna watu kweli wanaamini kama wanavyoamini misahafu wanachokisoma hapa JF

Mkuu Nyani ruksa mkuu itumie!!
 
Na mimi sikusema kwamba umesema unachofikiri kwamba nimesema umesema.

Au ni maswala ya joka la mdimu?

Sasa usingeni quote basi.Vinginevyo ungejibu hoja at hand na siyo kuandika as if unajibu hoja ambazo nilizisema.
 
De Novo salute mkuu!Wewe walau unaongea hali halisi na umeelewa naongelea nini.Anyway hata angepata div 3 anastahili hongera vilevile manake na yenyewe ni alama ya kufaulu!
Hata kama alipata Div 0 to me it doesnt matter kama wewe p53 ulipata Div 1 with flying colours umelisaidia nini Taifa tunachoangalia ni performance katika uongozi wake ukianza kuchunguza matokeo ya mitihani ya viongozi hasa wabunge hutaamini macho yako
 
Back
Top Bottom