Johnson Mashaka na mbio za Ubunge Ukonga

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2009
Posts
3,444
Reaction score
265
Vyanzo vyetu jijini Dar es salaam, vimethibitisha hali isiyo ya kawaida ambapo , Mwanaharakati John Mashaka amelivamia na kuliteka jimbo la UKONGA. Bw. John Mashaka ambaye yupo nchini kwa likizo, ameingiza magari matano, aina ya Landruiser 4X4 pamoja na kuweka kitita cha Dola za kimarekani karibia $350,000 kwa ajili ya kampeni yake. Hizi habari zimevuja kutoka ndani ya kamati ya kampeni

Bw. Mashaka, ameunda timu yake ya kutisha, ambayo imeundwa na wasomi kadhaa toka chuo kikuu cha Dar es salaam pamoja na wazungu Fulani wanaosadikiwa kuwa wamarekani ambao kwa pamoja wataendesha kampeni yak e kupitia Chama Cha Mapinduzi. Vile vile Bw. Mashaka ameonekana na hawa wazungu watatu ndani ya moja ya hayo magari yenye “tinted windows” katika kata ya Kinyerezi wakiongea na wananchi.

Kilichomtia Bw. John Mashaka jeuri ni uwezo wake wa kifedha na pia , kundi lake likiongozwa na mhadhiri mmoja “jina kapuni” kutoka chuo kikuu cha Dar, ilifanya utafiti wa siri kwa kipindi cha miezi sita na kugundua kwamba, kati ya wapiga kura 10 waliohojiwa jimboni kote, 7 hawatampigia kura tena Bw. Makongoro Mahanga, kutokana na kinachodaiwa kwamba Bw. Mahanga alitoa ahadi ambazo hazikutekelezaka.Vile vile Bw. Mashaka anasukumwa na wanasiasa wazito kutoka Chama tawala ambao wanamuona kama nyota chipukizi ambaye ataliokoa chama tawala, hasa kutoka katika kashfa ya ufisadi.

Habari hizi nyeti zimemfikia mbunge wa sasa wa Ukonga Mh. Milton Makongoro Mahanga ambaye ambaye ameingiwa na hofu kubwa na kulazimika kufanya kazi usiku na mchana ili kutetea jimbo lake hasa baada ya kusikia mambo ambayo Bw. Mashaka ameyafanya katika jimbo lake, hususan kumwaga karibia nusu Billioni na kutayarisha kamati yake ya kampeni inayotisha. Wiki iliyopita walionekana maeneo ya Ubungo plaza wanakofanyia vikao vyao

Ndugu wadau, kama kweli John Mashaka amejikita ulingoni, basi chachu mpya hasa ya mabadiliko nchini Tanzania imeanza kwa sababu uwezo wa huyu mtoto ni wa aina yake, kwa maana hiyo pamoja na Zitto Kabwe ambaye yuko upinzani, Chama tawala itakuwa na kichwa na kijana mwenye kipaji cha aina yake. Jimboni Ubungo nako yupo Nape Nauaye , Temeke January Makamba. Kwa maana hiyo Dar Es Salaam itachukuliwa na vijana. Swahiba wa John Mashaka, Dr. H Shayo wa Kule London naye yuko njiani kuelekea Moshi kwenye Kampeni

Je wadau, hii imekaaje? Hawa vijana watatu Mashaka, Shayo,na January ni Chachu mpya au nguvu ya Soda tu? Kama kweli watajitosa ulingoni, basi sura ya Tanzania itabadilika, kwa sababu uwezo wa kubadilisha nchi wanayo na ni majasiri kupambana na ufisadi, na nina uhakika Rais 2015 atakuwa mmoja wa hawa vijana watatu kama siyo Membe

Bila kusahau, ndugu yetu mwanakijiji vipi yeye anagombea wapi?
Tutawapa taarifa zaidi pale tutakapozipata…………………! Endeleeni kukaa mkao wa kula

UPDATE 1:

Hotuba ya John Mashaka:

 
Mmeanza yenu ya kuchafua vijana kwa visingizio vya pesa na madudu mengine.

Eti dola 350,000 ni propaganda tu, wewe umeziona hizo pesa?

Huwezi kufanya breaking news kitu ambacho huna uhakika nacho.
 
Tupe chanzo cha habari yako. Magazeti ya udaku ndio huwa na vyanzo visivyo julikana. Je huu pia ni udaku?
 
Tatizo kama hau wadau wapo CCM basi hawana jipya watakaloliweza kulifanya ili kuiendeleza nchi hii ,wengi sana waliingia katika siasa wakiwa na roho na mioyo mikunjufu kabisa lakini ugonjwa uliomo ndani ya CCM ni wa kuambukiza ,hivyo kasi zao zitaishia kwenye mwongo wa mwanzo tu pengine hata zisionekane tena,na hao mazungu isije kuwa ni rasilimali wameekeza kwa huyo mbongo,na baadae watahitajia kulipwa kwa kupewa maeneo wafanye watakalo.Na pangu pakavu wahamishwe kwa mtutu wa bunduki.
 
Kama Mashaka atatumia kiasi cha fedha kilichotajwa kuhonga wapiga kura basi hana tofauti na mafisadi wengine. Hata tukikubali kuwa fedha ni kwa ajili ya kampeni, je Mashaka ni mjinga kiasi gani atumie kiasi kilichotajwa bila kutegemea kupata faida zaidi ya fedha aliyoitumia?
 
Ahahah!, Uwanja wa Porojo...Kweli Politics ni Dirty Game!...

Mmeanza kumchafulia Mapemaaa, Hii Ni Ishara ya WOGA! Kama Mbwa Koko,

B.
 
John Mashaka anatafuta kujiabisha tu . Kwanza zengwe pili atafunikwa akasemee kwenye Chama.CCM imezoea dhuluma hata aje nani ndani hawezi kubadilisha. Eti January Makamba . Huyu dogo si yuko Ikulu hata mail address hakuna ama uwezo wake utaanza kuonekana akiwa Bungeni huko Temeke ? Masikio hayazidi kichwa baba ana babwaja huo umakini wa kijana ni upi ? Nape ni opportunist hanisumbui kabisa . CCM ni ndoto bwana . Wazungu hao kama wako na mission ndiyo wao wnataka kumtumia kufanya biashara tu .Na Mashaka anakuja na mapesa ufisadi kabla hajaanza .
 
Bw. John Mashaka, kwa ushauri wangu, nadhani usiingilie sisasa kabisa. Heshima uliyonayo katika jamii inatosha. uwezo wako wa kibusara na kifedha unatosha, usiingie kwenye siasa. watakumaliza, watu kama wewe hawachelewi kutolewa nje.

Waachie wakina makongoro mahanga waendeleze libeneke lao la dirty politics. hata kama una nia, umri wako bado mdogo, subiri 2015 uwe rais moja kwa moja. ila Subiri Nyani Ngabu na Julious waamke wana majungu ambao kazi yao siku zote ni kuwaponda wengine, niaminie watashambulia kweli hizo hela ulizotoa.
 

Mkuu siku nyingine lete habari bila kuweka conclusion zako na ideas zako. Hapa naona tayari wewe ni sehmeu ya kampeni kwa hiyo unajaribu kutuvuta kwa hao jamaa zako.
 
Bahati nzuri kwa Dar yalipo makazi yangu ni Kipunguni-kitunda,na sijaona hata siku moja John Mashaka akishirikiana na sisi kweye suala la maendeleo;kwa ufupi kama kweli anakuja kugombea Ukonga na aje na "tutamnyoa" na hizo" hela zake!Kama suala ni mgombea kiana wapo wengi tu Ukonga na sio lzm awe John Mashaka ambaye umaarufu wake kwa wana Ukonga tunausikia tu kupitia blog ya Michuzi inayomtangaza kweli kweli!

Pia kama kweli ataleta Wamarekani kuja kumfanyia kampeni hapo atakuwa anavunja katiba,sheria mama za uchaguzi wa TZ zinakataza kabisa kwa mtu asiye raia wa tz kuhusika kwa lolote lile ktk uchaguzi wetu kama sisi ambavyo hatuingilii chaguzi za nchi zingine!

"Mwisho ni hii habari ya dola 350,000 na gari hizi zake za kifahari",Kwa maisha ya USA kujikusanya hadi kufikisha hela hizo na kununua magari hayo ni ngumu;anyway acha niamini kama anavyo vitu hivyo,lkn je vitamsadia kupata Ubunge wa Ukonga bila mtaji wa watu?
 

- Mkuu Malafyale heshima mbele sana mkuu, kumbe mkuu na wewe ni jirani unajua mimi mkuu nipo chini yako hapo Kinyerezi mkuu ukivuka reli tu njia ya kwenda Segerea, saafi sana sasa lazima tuhamishie hii elimu tunayoipata hapa JF mpaka huku jimboni kwetu saafi sana na tupo pamoja.

- Kwa leo sina comments na hizi habari za Mashaka, lakini in due time nitasema, kwanza ni jimbo langu anyways, ngoja niwasiliane na wazee wa jimbo kwanza and then nitasema tena loud and very clear, when the time is right.

Respect.

FMEs!
 
Kama kweli anataka ku-invest hizo dola laki 3.5 lazima aseme kwanza atazirudisha vipi. Hatuwezi tukawa tunafanya kazi ya kuwapigia kelele wezi na kuwakaribisha majambazi, au tukubali kununuliwa na majambazi.
Katika hali ya kawaida mtu mwenye dola laki 3 na 4x4 nne hata jiingiza kwenye "mchezo mchafu", aanze kwanza kwa ku-invest hizo dola kwenye jimbo hilo then tuone kama anawasaidia wananchi, otherwise ni kwamba anataka kuwanunua wananchi ili ajichotee
 

FMEs,Mkandara

Hii tabia kuwa ukiwa na hela basi unaweza kufanya lolote kwenye siasa za TZ lzm zikomeshwe na mwanzo wa ukomeshwaji huo utaanzia kwetu Ukonga!

Kwa leo sina mengi,nikitoka Kyela nitapitiliza kuongea na wazee na vijana pale Kwa njenje,kisha nizunguke kote hadi Kipawa;nisikie wazee na vijana wanasema nini!

FMEs na Mkandara kwa hili tuweke kando tofauti zetu,tunaweza kugswana kata za kuelemisha wapiga kura madhara ya kuifanya Ukonga kama jimbo la "majaribio"yaliyomkuta Mzee Rupia nahisi yatamkuta huyu kijana John Mashaka kwenye sanduku la kura!

Kuandika kizungu kwenye blog ya Michuzi ndiyo tiketi ya kuupata ubunge wa Ukonga?FMEs na Mkandara kwa vile mpo Dar watafuteni wadau kama akina Jerry Slaa kuwauliza wana maoni gani kwa hii issue!
 
Nilishatamka muda si muda mrefu uliopita humu ndani kuwa dude atakuwa ana lake jambo kutokana na historia na juhudi yake ndefu na kubwa ya kujibeza na kutafuta exposure ya dezo kwenye MICHUZI BLOG na hata mainstream media kama Daily News. Naona sasa pay-back time imekaribia, na kama Wamarekani wanavyosema, hamna msosi wa bure! Kaaz kwer kwer!
 
Haka kamjamaa ka-Mashaka kanachekesha kweli..nways time will tell/
 
Kuna habari nyingine huwa naona uchuro kuweka komenti zangu
 
If Mr. Mashaka really has enough money, I advice him to think of investing it somewhere else but not in politics. If he already has an investment, then he would rather think of expanding his current investment or in a completely different venture but not in politics. My professional competence and experience as a political analyst tell me that he has chosen a wrong place to invest his money. I am confident that Mr. Mashaka will loose horribly. To me and perhaps few of you, the reasons are rather obvious.
 
Kama kweli John Mashaka anatumia pesa kwenye kampeni hiyo basi he has spoilt himself and has been rejected outright. In the first place kamnunua michuzi kule kwenye blog yake. Huku nako wewe bwana umeshavuta chako. Vijana gani wazuri wanaengage into dirty politics? Watanzania tuwe waangalifu sana na hao wanaotaka kutumia vijisenti kuingia ktk madaraka. It implies kwamba wakishapata hizo nafasi watataka kurudisha pesa zao. If they have money and skill why don't they venture into business right away? They are just fishy! But I'm happy the community is slowly getting to know how to deal with such things. They won't and shouldn't agree to be bought/fooled!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…