Jokate Kidoti amwaga misaada kwa watoto yatima

Jokate Kidoti amwaga misaada kwa watoto yatima

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
JOKATE.jpg

Dar es Salaam. Mwanamitindo Jokate Mwegelo leo Ijumaa ametoa zawadi za Eid katika kituo cha yatima na wajane cha Ahbaabul Khairiya kilichopo Mwananyamala B, jijini Dar es Salaam.

Katika zawadi hizo Jokate alitoa mchele kilo 250, unga kilo 250, mafuta ya kupikia, mbuzi wawili na nguzo za watoto na wanawake.

Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi hizo, Jokate ambaye mwaka 2006 alishika nafasi ya pili katika Shindano la Miss Tanzania, amesema ameguswa kuwasaidia watu wenye uhitaji ili nao washerehekee Sikukuu ya Eid kwa furaha.

"Nikiwa kama mwanajamii nimeguswa na watoto hawa na akina mama nikaona si vibaya nikajikusanya na kutoa kidogo nilichonacho ili nao wafurahie sikukuu."

Mkuu wa kituo hicho, Ahmed Shebe ameshukuru kwa msaada huo na kuwataka wasanii wengine kuiga mfano huo.

"Ukiwasaidia wasiokuwa na uwezo Mungu anakuongezea maradufu, niwasihi wasanii kujitoa kwa ajili ya wanajamii na si kufanya matendo na matumizi ya anasa,"amesema Shebe.

Chanzo: Mwananchi
 
Huyu Dada atafute mume wa ndoa ...alidharauliwa sana na yake matamshi ya mama kariakoo na mwanae ....
 
Mbona kawa mweupe sana au na yeye sikuhz anajichubua eeh
 
Huyo mtoto huwa napenda sana kukaa naye kalibu st Peter siku za jumapili pale kwa pengo
 
Huyu Dada atafute mume wa ndoa ...alidharauliwa sana na yake matamshi ya mama kariakoo na mwanae ....
Angalia vizuri sura yake mkuu. Si wa kukaa na mme huyo.

Chunguza kwa kina sana sura yake itakupa tafsili halisi ya tabia yake.
 
Kampeni zimekatazwa hadi 2020 ...yeye kaamua kutoka kivinge.....aya bhana "hurusiwi kuongea ukiwa unakula"
 
Angalia vizuri sura yake mkuu. Si wa kukaa na mme huyo.

Chunguza kwa kina sana sura yake itakupa tafsili halisi ya tabia yake.
Much know;,,mwanamke akiwa na tabia iyo ni mtihani kukaa nae,, ila wanakuwaga mafaita kwenye kusaka pesa
 
Back
Top Bottom