Jorginho "The Pass Master", fundi asiyeimbwa

Jorginho "The Pass Master", fundi asiyeimbwa

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Kiungo wa Kiitaliano mwenye asili ya Brazil, Jorginho anayekipiga katika klabu ya Chelsea amekuwa katika kiwango cha hali ya juu msimu huu.

Baada ya kuboronga kwenye msimu wake wa kwanza akiwa darajani, Jorginho wa msimu huu amekuwa mcharo sana. Amekuwa "anchor" katika mfumo wa uchezaji wa Chelsea. Licha ya kutokuwa na mwili mkubwa kama akina Pogba, amekuwa bora sana kwenye kupiga tackling, interceptions, assist na kuset tempo ya Chelsea pindi wanaposhambulia.

Kwa sasa namfananisha sana style yake ya uchezaji na Sergio Busquet. Ukimtazama Jorginho utaona mtiririko mzima jinsi Chelsea inavyocheza. Pamoja na yote hayo hasifiwi sana, kama wanavyosifiwa akina Abraham na Mason Mount.

Ni wakati wa kumpa credit zake Jorginho!
70119652_741420976320520_7961963627824081084_n.jpeg
 
Penati anazopiga unajua kabisa huyu jamaa ana akili si za mchezo..Mimi Chelsea ila uliemfanisha nae ni habari nyingine yule
Busquet umri umeanza kumtupa mkono, kasi ya mchezo nayo imeanza kumuacha, hivyo kuibuka kwa watu kama akina Jorginho ni kama warithi wa nafasi yake hasa ile ya deeplying playmaker.
 
Bado tunahitaji Mtu kama Sesc Fabregas kwa final assists japo Joginho ni mzuri lakini bado hajafikia huo uwezo wa Sesc Fabregas.
 
Back
Top Bottom