Jorginho "The Pass Master", fundi asiyeimbwa

Jorginho "The Pass Master", fundi asiyeimbwa

Kiungo wa Kiitaliano mwenye asili ya Brazil, Jorginho anayekipiga katika klabu ya Chelsea amekuwa katika kiwango cha hali ya juu msimu huu.

Baada ya kuboronga kwenye msimu wake wa kwanza akiwa darajani, Jorginho wa msimu huu amekuwa mcharo sana. Amekuwa "anchor" katika mfumo wa uchezaji wa Chelsea. Licha ya kutokuwa na mwili mkubwa kama akina Pogba, amekuwa bora sana kwenye kupiga tackling, interceptions, assist na kuset tempo ya Chelsea pindi wanaposhambulia.

Kwa sasa namfananisha sana style yake ya uchezaji na Sergio Busquet. Ukimtazama Jorginho utaona mtiririko mzima jinsi Chelsea inavyocheza. Pamoja na yote hayo hasifiwi sana, kama wanavyosifiwa akina Abraham na Mason Mount.

Ni wakati wa kumpa credit zake Jorginho!
Huyu si ndo Chelsea walikuwa wanasema mtoto wa Sarri anabebwa kaanza lini kuwa pass master? maana huku kwetu kibanda umiza watu walikuwa wanamlilia kocha amtoe utadhani anawaskia... hapa ndo nazidi kuuamini ule msemo wanaokudharau siku moja watakusalimia kwa heshima
 
Ni moja ya watu wanaojua... Mwengine ambae pia ni pass master asieimbwa ni Cecs Fabregas yule jamaa anajua
 
Back
Top Bottom