Joseph Kibwetere and Ugandan Cult Mass Murder/Suicide


Huna imani hiyo na huumwi ndo maana wasema hivyo. Acha watu wapone, kufa kupo tu
 
Huna imani hiyo na huumwi ndo maana wasema hivyo. Acha watu wapone, kufa kupo tu

Unajua kwa nini Mungu alisema imani yako inaweza kuhamisha milima? Ni kwa sababu imani is such a strong thing which can either ruin you or help you depending on what you are believing in. Alijua kuna manabii wa uongo watakaokuja na ukiwaamini umekwenda na maji maana imani ni kitu kikubwa sana kama hutakuwa mwangalifu. Now, I am not saying babu ni nabii wa uongo kwa sababu yeye sio nabii bali ninaongelea imani ambayo inawafanya watu waende huko. Unaposema niwaache watu wapone unamaanisha kina nani? Ni nani aliyepona? Watu wa sukari na pressure ambao tunawasikia wakidai wamepona huku bado wanaendelea kutumia dawa za hospitali?
 

hapo kwenye RED Ni matokeo ya dhambi mkuu, na kila mwanadamu atakufa hata kama atakuwa mtakatifu kiasi gani kwa hiyo watu kufia Loliondo ni kitu cha kawaida kwa sababu babu hazui kifo yeye anatoa tiba.
 
Mimi ndio maana nawalaumu sana wana JF wengine maana si wastaarabu. Kmf. anayemtukana miss judith, mjinga, mara amechanganyikiwa! Hivi kweli, tukimpima thinking and reasoning capacity atamzidi Miss judith? Miss judith ametoa coments! Wewe jibu kwa hoja na sio matusi bwanaaa!! Try to be a great thinker. Great thinker hawezi kuongea ovyo kama huyu hata kama anampinga miss judith.
 
hapo kwenye RED Ni matokeo ya dhambi mkuu, na kila mwanadamu atakufa hata kama atakuwa mtakatifu kiasi gani kwa hiyo watu kufia Loliondo ni kitu cha kawaida kwa sababu babu hazui kifo yeye anatoa tiba.

Nakubali kifo ni matokeo ya dhambi ila sioni sababu ya watu kwenda kufia loliondo then tuone kuwa basi si wangekufa hata hospitali tu? Loliondo watu wanakufa, wanawekwa pembeni nje ya gari huku walio hai kwenye hilo hilo gari wakiendelea na msafara wa kusubiri dawa wanywe kwanza ndio wamrudie yule maiti wamlete hospitali hata kama zitapita siku mbili, jamani, seriously, kweli ni Mungu huyu huyu? Ni wapi kwenye Biblia ulishaona watu wanamsubiri Yesu au kina mtume Paulo wawaponye na katika kumsubiri wengine wakafa maana kulikuwa na umati mkubwa sana uliokuwa umemzunguka?
 
I hv my rule not to comment anything in threads that seems bogus, i broke it severaltimes, but nimegendua ni makosa. Kuna watu wanatuma threads za kijinga kwa makusudi fulani fulani yaliyo nyuma ya pazia. i wll stick to my rile. By miss Judith
 

Uko sahihi kabisa mkuu, wala hatutofautiani kimtazamo. Ndio maana nimependekeza tujadili namna ya kuweka utaratibu wa kuwatibu waliozidiwa ili wasifie kwenye foleni.
 
...MWANZONI NILITAKA KUMFANANISHA BABU NA SHUJAA WA VITA YA MAJIMAJI! Kwamba risasi zinapigwa zinabadilika kuwa maji.... Labda watasema babu anasingiziwa.."walinukuliwa baadhi ya watu wakisema "babu alisema maiti zitupwe hazitaoza katika eneo lile" wengine wakanukuliwa wakisema "anaekwenda na hirizi au kumjaribu babu hatoki salama kijijini Samunge!"
Napenda sana watu waendelee kwenda Kunywa Kikombe Kimoja Tu.... lakini mwisho wa siku midhali imeshasemwa "....dawa ya babu kwa sasa ni salama...>>>> ...ila ijulikane Wakenya na Waganda wanaendelea na utafiti wa dawa hiyo (ya miujiza!!!!) leo mwaka wa pili na ushei... miambili wamejitolea kufanyiwa majaribio... je maelfu waliosalia?
kwa hakika.... BABU HANA TOFAUTI NA KIBWETERE
 
Mkuu hao ndio great thinkers!! tunaowategemea WABOMOE HOJA NZITO NA KUJENGA HOJA IMARA!
Siwashangai, kwa sababu natambua ukomo wa weledi wao... wapo WAFIKIRIAJI WAPEVU JF lakini ni WACHACHE SANA.
Ukiona mtu anakimbilia kuita HOJA ya mwenzake PUMBA basi tambua uwezo wake wa kuchanganua mambo umekomea wapi!
Ndio maana unaona WENGI HAWACHANGII MAMBO YANAYOWAGUSA KUMOYO BALI YANAYOWAPENDEZA...
WANASAHAU KWAMBA, KUPAKANA MAFUTA NA KUSIFIANA NDIKO KULIKOTUFIKISHA HAPA TULIPO LEO....
Pole Tanzania!
 
1) Dawa ya babu wa Loliondo siyo IMANI ..............imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasioonekana - UKISHASHIKA KIKOMBE NA KUNYWA DAWA YA BABU - tayari umeshaiona hiyo dawa kwa macho na dawa ndio inakuponya sio IMANI yako. - Haina tofauti ya kunywa dawa za kawaida unazoona kwa macho.

IMAINI - katika uponyaji - ni unatamkiwa NENO la uponyaji - na unapona - hapo hakuna kikombe wala dawa unayoona kwa macho.

2) Hivi inakuwaje BABU aziweze kusogea hadi mahali panapofikika???? ibaki wachimbaji wake kwenda kuchimba dawa na wakasaidiwa kukodi magari ya kusomba hadi babu aliko??? Au Mungu amesema kituo kiwe hapo kijijini alipo tu???

3) Yumkini dawa hiyo inaponya na watu wanapata nafuu etc. lakini tukubali kuwa - na wengi watakufa pia - je wale wanaokufa wamejitayarisha je kukutana na Mungu wao wakati mawazo yao, mioyo yao iko kwenye KIKOMBE CHA DAWA YA BABU??

Mie nauliza tu - ni lazima tujue mbinu na hila za adui yetu. Hata kama dawa hiyo inaponya tuangalie tusimpe shetani nafasi kwa mazingira ya kupata dawa hiyo.

NA KAMA BABU HAWEZI KUHAMA ALIPO...............IKO SIKU anaweza kuyeyuka .... hapo ndipo kutakuwa kilio na kusaga meno ...............hapo nawaza tu jamani!!!:fear::fear::fear::fear::fear::fear::fear::fear::fear:
 

Haiingii akilini, magari yamepanga foleni kilometa 40 yakienda kwa mganga wa kienyeji Loliondo. This has happened only in Tanzania
 
haiingii akilini, magari yamepanga foleni kilometa 40 yakienda kwa mganga wa kienyeji loliondo. This has happened only in tanzania

watu wamezidiana kete ; wateja wanatoweka ugali umeingia tsunami roho mtakatifu wa akina maxi shimba yuko jobless ????
 
Haiingii akilini, magari yamepanga foleni kilometa 40 yakienda kwa mganga wa kienyeji Loliondo. This has happened only in Tanzania

Na kinachonishangaza ni jinsi wanavyotetea kuwa ni Mungu!!!! Yaani hawareason kabisa
 
Uko sahihi kabisa mkuu, wala hatutofautiani kimtazamo. Ndio maana nimependekeza tujadili namna ya kuweka utaratibu wa kuwatibu waliozidiwa ili wasifie kwenye foleni.

Sawa, but how? Wakati babu kashasema hiyo dawa ikitoka mahali alipo haitafanya kazi? Magari yamepanga foleni km 40
 
Habarini wana JF, Kuna mtu mmoja alifanya mambo ya kutisha kuliko Osama anaitwa Kibwetere. Aliangamiza watu wengi kwa moto kule Uganda. Napenda kujua kutoka kwenu kama huyu mtu alishakamatwa au anasakwa mpaka leo. Maana mambo aliyofanya ni mazito halafu ghafla dunia imekuwa kimya au ndio yale ya Mzungu mmoja sawa na waafrika 1,000?
 
Habari wana jf
nakumbuka mwaka 2000 kulikuwa na jamaa anaitwa kibwetere ambaye aliwachoma wafuasi wake kanisani huko uganda.
Je huyu mtu siku hizi yuko wapi? Kesi yake iliendaje maana nlikuwa bado mdogo katika kufuatilia!
Naomba mwenye taarifa amwage hapa kwa faida yangu na kwa wengine
nawasilisha!!!!!
 
alitokomea kusikojulikana na hazina ya kutosha
 
Hee! Inawezekana vipi? Au kuna mkono wa taasisi kubwa? Mtu asababishe mauaji kama yale kisha apotee bila kupatikana tena nchi kama ya uganda,Mbona Osama kadakwa? Au ndo tuseme yeye hana kosa?
 
hata mimi huwa najiuliza huyu jamaa aliishia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…