Kuna jamaa yangu yupo Arusha alikuwa anaoa miezi kama miwili hivi iliyopita,huyu jamaa anafahamiana sana na Barnaba wa THT,akampigia simu akamwambia aende akapafomu yeye pamoja na Linah, siku ya harusi yake.Jamaa akawaambia ntawalipia tiketi ya ndege kwenda na kurudi wote wawili,na sehemu ya kufikia gharama zote zitakuwa juu yangu(bwana harusi).
Barnaba akahoji kuhusu malipo,jamaa akamwambia ntawalipa laki nne(400,000) kila mtu(linah+barnaba)=800,000
Mje ijumaa jioni mtafanya show jumamosi siku ya harusi jumapili mtaondoka,wakasema aina shida hiyo imekaa fresh.
Ruge akanasa habari,sijui kutoka wapi,ikabidi ampigie jamaaa wa Arusha(bwana harusi)na kuanza kumuhoji vipi mbona unawachukua vijana wangu bila kunitaarifu maswali mengi,sijui umeelewana nao shilingi ngapi?mara hivi mara vile,Mshikaji ikabidi amwambie ruge kuwa huyo barnaba ni kama family friend kwa hiyo mimi nimemuomba tu aje kwenye harusi yangu na sio kama ntamlipa wala nini,Ruge akazidi kukomaa na mshikaji,mbona nasikia kuna pesa mmeelewana kama laki nne kwa kila mmoja,jamaa akamwambia ndio,Ruge kusikia hivyo akasema sasa sikia utawapa laki mbili mbili tu laki nne zangu,alafu awana aja ya kupanda ndege watakuja kwa basi ijumaa asubuhi.
Mshikaji akaona ujinga pesa yakwangu alafu unipangie akaamua kuachana nao.
Huyu ndio ruge banaaa.
SWAHILI ORIGINAL WORLDWIDE