Joto la sasa la Dar linaweza vunja rekodi

Trubarg

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2020
Posts
4,388
Reaction score
7,223
Habari wadau.

Joto la Dar sasa hivi linarange kati ya 33 • C hadi 35•C lakini unapata feeling ya 41•C kutokana na humidity.

Kwa kweli hali hii ni mbaya sana ambayo kama huna air condition iwe kwenye usafiri au nyumbani kwako kwako maisha yatakuwa ya taabu sana.

Tips muhimu za kuishi maisha ya hali hii ya joto ni pamoja na;

1. kunywa maji na vimiminika kwa wingi
2. Kuepuka kukaa kwenye jua moja kwa moja
3. Kuvaa nguo nyepesi

Hope TMA wataliongelea hili and hope hizotips zimesaidia
 
Kuvaa nguo nyepesi inaweza isiwe vizuri kwa mila na desturi zetu
 
Matajiri hawalii joto kali ,Nyie wengine endeleeni kuteseka Dar

Mtalimia meno
 
Mimi nilidhan shida iko kwenye hii nyumba mpya niliyohamia maana hata mvua inyeshe bado kuna joto.
Yani sasa hivi natumia unit almost 5 hadi 6 kwa siku maana mafeni na AC ndani ya nyumba zinawashwa muda mrefu.
Kumbe hata kwa wengine hivyo hivyo.
Kwa kweli hili joto ni balaa na sasa ilipaswa walau kuwepo baridi kidogo
 
Miaka ya myuma mwezi huu haukupaswa kuwa na joto
 
Huwezi washa fan na AC ukatumia unit 6 kwa siku. Huna AC dogo. Acha mbwembwe.
 
Mkuu unit 5 mpaka 6, yaani una mafriji, mafeni, ac bado unatumia unit 5, bado haujapiga pasi, na matumizi mengine, Mbona naona kama unatumia umeme wa bei rahisi mzee?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…