Joyce Ndalichako Atakiwa kujiuzulu, ni maafa kwa taifa

Joyce Ndalichako Atakiwa kujiuzulu, ni maafa kwa taifa

thatha

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2011
Posts
15,340
Reaction score
1,570
Salma Said


BAADHI ya wazazi ambao watoto wao wamefutiwa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne visiwani Zanzibar wanakusudia kulifikisha mahakamni Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kwa kutoa adhabu hiyo kinyume cha sheria.

Wazazi hao walitoa kusudia hilo mjini hapa jana katika wakati wa mjadala uliowashirikisha wadau mbali mbali wa sekta ya elimu na wanaharakati kujadili uamuzi wa Necta wa kuwafutia matokeo wanafunzi 3,303 kutoka Tanzania bara na Zanzibar na kuwazuia kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.
Ameir Hassan Ameir alisema pamoja na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya baraza hilo , kuna haja kwa wananchi visiwani humo kuitisha maandamano makubwa kupinga kufutwa kwa matokeo hayo na kushinikiza kuondolewa kwa dhabu dhidi ya wanafunzi.
Akipinga taarifa ya Necta kwamba mitihani hiyo imefutwa kwa sababu ya udanganyifu uliofanywa na wanafunzi, Ameir alisema baraza limeshindwa kuthibitisha udanganyifu huo na hivyo haliwezi kujiondoa katika kashfa ya kuvuja mtihani.
Alisema kushindwa kwa Katibu Mtendaji wa Necta, Joyce Ndalichako kutoa maelezo juu ya idadi na majina ya wananfunzi waliofutiwa mitihani kutoka kila upande wa Muungano, kumeibua hisia kwamba Tanzania bara imeandaa njama za kuua elimu elimu Zanzibar .

"Necta wanayo majina ya shule na namba za shule zote za Zanzibar , hivyo si kweli kwamba hawajui majina ya wanafunzi waliofutiwa mitihani," alisema Ameir huku akihoji uwepo finyu wa ushiriki wa Zanzibar katika muundo wa Bodi ya Wakurugenzi wa Necta.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati wa mjadala huo, bodi ya Necta ina wajumbe 14 na kati ya hao sita wanatoka upande wa Zanzibar .
"Sisi tuna uchungu na Zanzibar yetu, kuvuja kwa mitihani na watoto kufutiwa mitihani ni matokeo ya kero za Muungano. Adhabu ya miaka mitatu itawapotezea watoto wetu muda wa kusoma, Wazanzibari tuungane tulishtaki Necta," alisema.
Ali Hassan, Mkuu wa zamani wa Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja alisema ingawa Necta imeshindwa kutoa idadi ya wanafunzi waliathirika na uamuzi wa kufutwa matokeo, anaamini asilimia kubwa wanatoka upande wa visiwani wa Muungano.
Alisema maelezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Necta mbele ya mkutano na waandishi wa habari Februari 14 mjini hapa yanapaswa kusikilizwa tu na mtu asiyejua chochote na kuongeza kuwa kwa hatua hiyo: " Mama Ndalinacho amefeli astep down." Akiwa na maana aachie ngazi.

Faisal Mohamed, ambaye pamoja na Ali walisema ni miongoni mwa waathirika wa watoto wao kufutiwa mtihani alisema alivishambulia vyombo vya habari na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa alichoeleza kuwa kushindwa kuandika kwa kina habari za kashfa ya mitihani na kupokea kutoka Necta na kusaini taarifa bila kudadisi maelezo ya baraza hilo juu ya utata wa matokeo na hatua zilizochukuliwa dhidi ya wanafunzi.

Hata hivyo walalamikaji wote hawakueleza kusudio la kulishtaki baraza litatekelzwa kwa sheria, lakini walisema chini ya makosa ya jinai ni kinyume cha sheria kutoa hukumu ya jumla kwa kosa ambalo ni la mtu mmoja mmoja.
 
Nyie wazenji, acha jaziba. Nawapa ushauri wa bure:
1. Thibitisha kama watoto wenu walifanya udanganyifu
2. Kama walifanya udanganyifu, Sheria inasemaje
3. Adhabu yake ni nini
4. Adhabu waliyopata inastahili kisheria-ndiyo iliyoainishwa kisheria
Then from there utafikia conclusion kama haki imetendeka. vinginevyo mtatumia jaziba na mtashindwa huko mahakamani.
 
ijumaa niliona kipindi cha kipima joto huyu mama alikuwa anahojiwa
tena alionyesha baadhi ya mtihani watoto walivyojibu ni aibu tupu, wamechora picha
mtoto wa form four mwandiko kama mtoto wa nursery school
wengine wameandika mistari
wapo waliojaza majibu ambayo hayapo, mfano chagua kati ya a,b,c,d wanafunzi, tena shule nzima wamechagua herufi O ambayo haipo.
kuna mwanafunzi ameandika kwenye answersheet kuwa baba yake ndo anamlazimisha kusoma

hao wazazi wengefuatilia maendeleo ya watoto wao toka shule ya msingi, wangekuwa bega kwa bega na walimu wo watoto wasingefeli.
na linapokuja swala la feki, pesa za kununua feki watoto wanatoa wapi?

unaposema ufinyu wa memba toka znz, hata wakiwa memba wa znz 10 ndo wawape alama za ufaulu wanafunzi hata kama wamefeli? hebu wagrow up na kutia msisitizo kwenye alimu na si kulilia upendeleo usio na mantiki
 
ijumaa niliona kipindi cha kipima joto huyu mama alikuwa anahojiwa
tena alionyesha baadhi ya mtihani watoto walivyojibu ni aibu tupu, wamechora picha
mtoto wa form four mwandiko kama mtoto wa nursery school
wengine wameandika mistari
wapo waliojaza majibu ambayo hayapo, mfano chagua kati ya a,b,c,d wanafunzi, tena shule nzima wamechagua herufi O ambayo haipo.
kuna mwanafunzi ameandika kwenye answersheet kuwa baba yake ndo anamlazimisha kusoma

hao wazazi wengefuatilia maendeleo ya watoto wao toka shule ya msingi, wangekuwa bega kwa bega na walimu wo watoto wasingefeli.
na linapokuja swala la feki, pesa za kununua feki watoto wanatoa wapi?

unaposema ufinyu wa memba toka znz, hata wakiwa memba wa znz 10 ndo wawape alama za ufaulu wanafunzi hata kama wamefeli? hebu wagrow up na kutia msisitizo kwenye alimu na si kulilia upendeleo usio na mantiki

wazenji,
Nawashauri vitu vyote mvipe uzito sawa, elimi ya dini na elimu ya dunia. Naamini hao waliofeli/waliofutiwa masomo ya madrasa wanayaweza sana. Ni kuweka juhudi pote pote!!! Msiwe na jaziba, tafuteni ukweli wa mambo, na mtapata amani.
 
ijumaa niliona kipindi cha kipima joto huyu mama alikuwa anahojiwa
tena alionyesha baadhi ya mtihani watoto walivyojibu ni aibu tupu, wamechora picha
mtoto wa form four mwandiko kama mtoto wa nursery school
wengine wameandika mistari
wapo waliojaza majibu ambayo hayapo, mfano chagua kati ya a,b,c,d wanafunzi, tena shule nzima wamechagua herufi O ambayo haipo.
kuna mwanafunzi ameandika kwenye answersheet kuwa baba yake ndo anamlazimisha kusoma

hao wazazi wengefuatilia maendeleo ya watoto wao toka shule ya msingi, wangekuwa bega kwa bega na walimu wo watoto wasingefeli.
na linapokuja swala la feki, pesa za kununua feki watoto wanatoa wapi?

unaposema ufinyu wa memba toka znz, hata wakiwa memba wa znz 10 ndo wawape alama za ufaulu wanafunzi hata kama wamefeli? hebu wagrow up na kutia msisitizo kwenye alimu na si kulilia upendeleo usio na mantiki

hiii 2011? au unasema kabala ya mapinduzi?
 
wazenji,
Nawashauri vitu vyote mvipe uzito sawa, elimi ya dini na elimu ya dunia. Naamini hao waliofeli/waliofutiwa masomo ya madrasa wanayaweza sana. Ni kuweka juhudi pote pote!!! Msiwe na jaziba, tafuteni ukweli wa mambo, na mtapata amani.
hizo propagnda za wakiristo wa tanganyika. mbona hakuna waziri mzanzibar mkiristo lkn nchi ipo juuu kuliko kwenu kwenye wakiristo rushwa imejaa?
 
Salma Said

alisema Ameir huku akihoji uwepo finyu wa ushiriki wa Zanzibar katika muundo wa Bodi ya Wakurugenzi wa Necta.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati wa mjadala huo, bodi ya Necta ina wajumbe 14 na kati ya hao sita wanatoka upande wa Zanzibar .
“Sisi tuna uchungu na Zanzibar yetu, kuvuja kwa mitihani na watoto kufutiwa mitihani ni matokeo ya kero za Muungano. Adhabu ya miaka mitatu itawapotezea watoto wetu muda wa kusoma, Wazanzibari tuungane tulishtaki Necta,” alisema.

Hii ni 'kero' mpya ya Muungano. Inaashiria kwamba siku za mbele jambo lolote ambalo linafanywa kimuungano litakuwa linaleta utata tu, suluhisho ni kila upande u mind their own business, every business, tunakataa ukweli tu Watanzania, tunakataa ukweli, watu wamechoka na Muungano. Mimi naamini kwamba hata baada ya Katiba mpya, muundo wowote ambao utakuja baada ya Katiba mpya haitakuwa mwisho wa 'kero' za Muungano. Kila siku itakuwa kuongelea kero za Muungano, kero, kero, kero...

Lakini Zanzibar ni sehemu ndogo sana ya Tanzania (Zanzibar haijazi hata robo ya Mtwara!) lakini ina distract national agenda ya nchi nzima, inakula national attention ya nchi, ya nini?

Wanadai Zanzibar haina wajumbe wa kutosha kwenye bodi ya NECTA, na Wamakonde nao tudai equal representation kwenye bodi ya Wakurugenzi wa NECTA?

Na Wasukuma nao wakidai? I mean, kuna Wasukumu milioni 5 unusu, Wazanzibari milioni moja, nani ana haki ya kudai equitable representation kwenye bodi ya Wakurugenzi wa NECTA, Wasukuma au Wazanzibar? Wazanzibari kwani wao nani?
 
Kwani elimu nayo imo kwenye mambo ya muungano, imekuwaje Z'bar ikatafuta kusahihishiwa mitihani yao na Necta si wangesahihisha wenyewe?
 
hizo propagnda za wakiristo wa tanganyika. mbona hakuna waziri mzanzibar mkiristo lkn nchi ipo juuu kuliko kwenu kwenye wakiristo rushwa imejaa?

Kweli inawezekana, lakini jitahidi kwa nyanja zote
 
Si ajabu wanasiasa wakataka watafute umaarufu wa siasa hapa kwa kutaka kuwa na mambo ya uwakilishi kama hao wasio na kazi za kufanya wanavyotaka, wakumbuke hili ni eneo la taaluma liachwe lijiendeshe kitaaluma.
Chonde chonde wanasiasa p'se stay out of this!
 
ijumaa niliona kipindi cha kipima joto huyu mama alikuwa anahojiwa
tena alionyesha baadhi ya mtihani watoto walivyojibu ni aibu tupu, wamechora picha
mtoto wa form four mwandiko kama mtoto wa nursery school
wengine wameandika mistari
wapo waliojaza majibu ambayo hayapo, mfano chagua kati ya a,b,c,d wanafunzi, tena shule nzima wamechagua herufi O ambayo haipo.
kuna mwanafunzi ameandika kwenye answersheet kuwa baba yake ndo anamlazimisha kusoma

hao wazazi wengefuatilia maendeleo ya watoto wao toka shule ya msingi, wangekuwa bega kwa bega na walimu wo watoto wasingefeli.
na linapokuja swala la feki, pesa za kununua feki watoto wanatoa wapi?

unaposema ufinyu wa memba toka znz, hata wakiwa memba wa znz 10 ndo wawape alama za ufaulu wanafunzi hata kama wamefeli? hebu wagrow up na kutia msisitizo kwenye alimu na si kulilia upendeleo usio na mantiki

Du kama kuna majibu kama hayo basi wazazi wa leo wanaotaka maendeleo ya wanao wana kazi ya ziada
 
chika kuitwa mzanzibar kuanzia leo ingawa mimi si mzenji na zenji sijawahi fika. Mtu ametekeleza majukumu yake ajiuzulu? kwa nini kama mnawaamini wanafunzi wenu msidai mtihani mwingine kwa eitha ku appeal baraza au kuandika barua kwa waziri wa elimu mkiomba watoto wenu wapewe mtihani mpya ili mmshike vizuri NDALICHAKO?

Akijiuzulu unadhani watoto wenu ndo watafaulu?
 
Nyie wazenji, acha jaziba. Nawapa ushauri wa bure:
1. Thibitisha kama watoto wenu walifanya udanganyifu
2. Kama walifanya udanganyifu, Sheria inasemaje
3. Adhabu yake ni nini
4. Adhabu waliyopata inastahili kisheria-ndiyo iliyoainishwa kisheria
Then from there utafikia conclusion kama haki imetendeka. vinginevyo mtatumia jaziba na mtashindwa huko mahakamani.

Kwanza hakuna sheria ya kuhukumu watu wote kwa kosa la mmoja. Pili anaehukumu ndio aonyehe hiyo adhabu kaitoa wapi na kwanini, sio anehukumiwa. Kuwa makini kidogo.
 
Du kama kuna majibu kama hayo basi wazazi wa leo wanaotaka maendeleo ya wanao wana kazi ya ziada

tena wana kazi kubwa sana, inabidi kufuatilia kwa ukaribu wa hali ya juu maendeleao ya wanafunzi. Imahine mwanafunzi anachora vikatuni kwenye karatasi ya majibu. na kwenye malezi yetu wazazi tuweke msisitizo wa elimu, watoto washike elimu. sio kutaka favours na kuzalisha mabomu ya baadae
 
hizo propagnda za wakiristo wa tanganyika. mbona hakuna waziri mzanzibar mkiristo lkn nchi ipo juuu kuliko kwenu kwenye wakiristo rushwa imejaa?

kuna wakristo na wanaojiita wakristo. wakristo ni wafuasi wa KRISTO kwa kila jambo, lakini wanaojiita wakristo, ni wale wanaotumia jina hilo, kwa mazoea tu, lakini ukiwaweka kwenye mizani hawana sifa.

Tanganyika kuna rushwa tena sana, nakubali lakini watanganyika sio watu wa kupenda upendeleo kama wazanzibar mlivyo shame on you.

mambo mengine mnatakiwa kuangalia,
1.je mna walimu wa kutosha kuanzia shule za msingi hadi sekondari?
2.walimu wanatekeleza majukumu yao inavyotakiwa?
3. wazazi mnakaa na watoto kuwasisitiza kujisomea au mnatilia mkazo kwenda baharrini kuvua saladini, kibua, chnagu, mkisi na wengine? (kipaumbele kinaamua nature ya matokea ya mwanao)
4. wanafunz wako serious na kitabu?

maswali haya yanaweza kuwajenga na sio kuwa walalamishi na kutaka upendeleo tu hapa
 
Kwani Ndalichako ndiye aliyefanya mitihani? Mfeli nyie mumsingizie Ndalichako?

ndalichako huyachakachua matokeo ya wanafunzi kwa Kikanda. Huyu mama ni janga la kitaifa
 
Back
Top Bottom