*
MFULULIZO WA MASOMO YANAYOHUSIANA NA KUTAMBULIWA KWA MJI WA YERUSALEMU KAMA MAKAO MAKUU YA ISRAEL*
*✳SOMO LA 5⃣ :
VIASHIRIA VYA KUBOMOLEWA VYA MSIKITI WA AL-AQSA(DOME OF THE ROCK)✳*
* Na :
Shujaa Charles Mwaisemba*
*
KUBOMOLEWA KWA MSIKITI WA AL-AQSA(DOME OF THE ROCK)*
*ONYO KWA KWA WAKRISTO KUSHABIKIA KUPINGA ISRAEL*
* NGUVU ZA MAPINGAMIZI KUONGEZEKA KUTOKANA NA MUDA MCHACHE WA SHETANI ALIOBAKIZA KUFANYA KAZI DUNIANI*
* NINI WAJIBU WETU WA KUFANYA BAADA YA YOTE❓*
*1⃣ UTANGULIZI*
✍ Tukumbuke kuwa Mara baada ya Rais Donald Trump Kutangaza Kuutambua Mji wa Yerusalemu kama Makao Makuu ya Israel,Lakini hata Israel walikuwa na Sababu ya Kuhamisha makao yao Makuu Kutoka Telhaviv Kwenda Yerusalemu kwasabbu mambo mengi ya Muhimu Yapo Yerusalem Kama
i) Bunge la Israel lipo Yerusalem
ii)Makao ya Viongozi wa juu wa nchi yapo Yerusalemu
iii)Ofisi nyingi aa kiserikali zipo Yerusalem
Kwahiyo imekuwa ni makao yao makuu tangu mwaka 1950 kisheria yao,Lakini kusimama kutangaza ndio ilikuwa ni shughuli kubwa na ngumu ambayo ndiyo imetekelezwa na Taifa la Marekani.Ndio maana umeona Roho ya mpinga Kristo imesimama kwa nguvu kubwa,wote wenye roho hii ndio hawa wanapiga kelele kwasababu shetani ameshuka akiwa na ghadhabu nyingi akiwa anajua wakati wake upo karibu
Tukishakuyaelewa hawa tuendelee mbele na ikiwa hukufuatilia masomo yaliyopita basi wasiliana nami kwa namba nilizoandika mwishoni chini,Nitakupatia kuanzia mwanzo mpaka tulipofika
*2⃣
VIASHIRIA VYA KUBOMOLEWA KWA MSIKITI WA AL-AQSA(DOME OF THE ROCK)*
Kutangazwa kwa Yerusalem kama Makao yao makuu ya Israel,Kumeanza Kuonyesha viashiria vikubwa vya kuanza Kubomolewa kwa ule *Msikiti wa Dom of the Rock* Maana ndipo kulipokuwepo lile hekalu la Suleiman lililobomolewa kabla ya Israel kutawanywa kwenda kila kona duniani
Kumbuka Shauku yao Kubwa Israel si tu ilikuwa Kuipata Yerusalem yao bali hasa walitamani Kurudisha hekalu lao lililobomolewa mahali pale pale ulipokuwepo huu msikiti wa Al-aqsa,Hivyo Hilo Hekalu la 3 Suleiman lazima lijengwe tena hapo hapo
Maandiko yanasema Chukizo la Uharibifu litakaposimama hapo patakatifu (Chukizo la uhatibifu ni Mpinga Kristo) yaani atasimama hapo kulipo na hekalu.
Kwanini nasema viashiria vya kubomolewa huu msikiti upo tayari kuonekana ni kwasababu hivi tunavyozungumza Kwa Miaka mingi Vifaa vyote vya Ujenzi wa Hekalu vimekwishaandaliwa na vimeandaliwa kila kitu kuhusiana na hekalu hilo ambalo lazima lijengwe ndipo chukizo la uharibifu linalotajwa ambalo alizungumza Yesu Kristo alipokuwa anazungumza juu ya kuja kwake katika *MATHAYO 24:15-21* Aliulizwa juu dalili ya kuja kwake na ya mwisho wa Dunia *MATHAYO 24:1-3* Aliwaeleza kuwa hekalu kuwa litabomolewa
Dhiki kubwa inakuja baada ya kunyakuliwa kwa kanisa na huyu mpinga Kristo ndipo anatajwa atasimama kwenye hekalu hilo ambalo litajengwa baada ya huo msikiti wao wa Al-aqsa kubomolewa
Vifaa vyote vilishaandaliwa kabisa na Israel wameandaa kila kitu kama ilivyokuwa nyakati za suleiman,Zaidi sana wameandaa mpaka Mavazi ya Makuhani yote yapo tayari.
Na Jengo lile ujenzi wake sio kama tunavyojenga hivi sas kwa ujenzi aa kawaida,hivyo ingechukua Miaka Mingi kukamilika bali wameandaa kwa kutumia Technologia za kisasa kabisa yaani ile filimbi itakapolia,Ni kuta zinainuka,zinainuka,zinaungwa na kuungwa Kama unaunganisha vyuma,Ni kitu kinasimama tu kufumba na kufumbua kila kitu kipo mahali pale
Yaani sasa inangojea tu filimbi(Tangazo) na hichi ni kishiria kikubwa kwasababu huwa wanapata nguvu kuwa hapo ni kwao,hivyo wanaona pakishakuwa ni makao yao makuu basi wana haki ya kujua mji huu wanaufanyeje?Ndio maana unaona hawa wengine wanapiga kelele,Ndio maaana Palestina ndio wanaosema hii Yerusalem Mashariki ndio makao makuu ya nchi yao,itakayokuja‼
3⃣
ONYO KWA KWA WAKRISTO KUSHABIKIA KUPINGA ISRAEL
Sasa unapoona Tangazo la Mji wa Yerusalemu kutambuliwa kama makao makuu na Ikiwa wewe ni Mkristo ambaye unajua Neno,Unajua kuhesabu Miaka,Unajua Kusoma vitabu na kuhesabu miaka hupaswi kuwa upande wa mashetani bali utakuwa upande wa Israel(Katika unabii kuwa upande wa Israel ni kuwa Upande wa Mungu).Ukiibariki Taifa la Israel na wewe utabarikiwa,Iombee Amani Yerusalemu
Hivyo na wewe ukikurupuka na kuchukuliwa na na micoment ya watanzania ambao hawajui kupambanua kipi cha Mungu na kipi cha Shetani ambao hao hao ndio waliweza Kuchukuliwa na Babu wa Loliondo na kudai ni Mungu basi nawe utakuwa upotevuni maana siku zote wanashabikia vitu vya upande wa pili vya kishetani
Lakini hapa ndio tujue Miaka 70 imefika tayari ya taifa la Israel(14/5/2018) Asomaye na afahamu kuhesabu miaka na kujua jinsi tulivyo karibu kiasi gani na hili Chukizo la Uharibifu(Mpinga Kristo) ambaye atasimama muda si mrefu kwenye hekalu hilo litakalojengwa baada ya Msikiti kubomolewa
Unaweza kuona mbele yetu ni muda gani upo❓ Ni Muda mfupi sana ndugu yangu
Hakuna ajuaye siku wala saa lakini ni muda mfupi hapa,Chukizo la uharibifu litasimama katika hekalu ambalo maandalizi ya ujenzi wake upo tayari ndipo dhiki kuu inakuwepo, Na Kumbuka dhiki kuu ikiwepo ujue kanisa limekwisha nyakuliwa
⚠ Kwa hivyo chochote cha kufanya yote haya kutimia, kitakuwa na Upinzani sana,kutakuwa na matukio mazito mazito ya kupinga Tangazo hilo na mengineyo mengi Kama haya Maandamano ya Palestina ambayo yaliyokuwa yanaendelea mpaka sasa
4⃣
NGUVU ZA MAPINGAMIZI KUONGEZEKA KUTOKANA NA MUDA MCHACHE WA SHETANI ALIOBAKIZA KUFANYA KAZI DUNIANI
Kuanzia sasa na kuendelea tutaanza kuona matukio mengi ya Mapingamizi na kelele nyingi kutoka kila kona dhidi ya maamuzi hayo Kwasababu Shetani anajua Muda wake si mwingi kwasababu dhiki kuu ni Miaka 7,Na dhiki kuu ikiisha kanisa lililonyakuliwa na Yesu linakuja duniani na Yesu anatua kwenye mlima mzeituni mahali pale pale alipopaa wakati anaenda mbinguni, akiwa na Jeshi la watakatifu walionyakuliwa ambapo kutatokea vita inayoitwa *VITA VYA HARMAGEDONI* na baadae Utawala wa miaka 1000 wa Yesu Kristo dunia *(Ikiwa haujapata mfululizo huu matukio haya ya siku za Mwisho pia unaweza kuwasiliana nami nitakupatia)*
Wakati huo wa miaka 1000,Shetani atakuwa amekamatwa na kufungwa kwa miaka hiyo hiyo 1000.Hivyo ile tu Kanisa linanyakuliwa kuna miaka 7 tu ya dhiki kuu,Na baada ya hapo shetani anakamatwa kufungwa miaka 1000
Hivyo Shetanj anajua haya,Anajua viashiria vyake kwa hiyo anapoona hatua hii inaanza na hii nyingine inaanza, kadiri inavyosogelea ni mapambano, ni vita vikali utaona dunia lote linakuja kwa nguvu zote,huwezi kutegeme kuona *Jumuiya ya nchi za ulaya* ikisapoti hili wakati hicho kinachofanyika ni cha kiMungu
Kumbuka hata hizo sarafu za Euro zina michoro ya 6⃣6⃣6⃣ zimewekwa pale,Na Jengo lao zima lina mavitu ya ajabu ajabu hivyo huwezi kutarajia sapoti ya jambo hili kuunga mkono kutambuliwa kwa Mji wa Yerusalem
Kinyume chake ndio utaona Mapambano na Maneno mengi ya kupinga uamuzi huo uliofanywa na Rais wa Marekani,Kwahiyo na wewe Ukiwa Upande huo wewe ni Mjinga,Hujui Neno wala hujui Wewe ni Nani❓Hujui hata kilichopo mbele yetu lakini unachukuliwa na siasa za wajinga katika nchi yetu na dunia kwa ujumla
5⃣
NINI WAJIBU WETU WA KUFANYA BAADA YA YOTE❓
Kwasababu hii tuukomboe wakati kwasababu tujue hatuna muda mwingi unaotusubiria,Kama hujafa basi siku ya mwisho kwa watu wote nayo haipo mbali *(Sisemi kuwa Yesu anarudi lini kwamba ni kesho au kesho kutwa bali ni bado kitambo kidogo Yeye hajae atakuja wala hatakawia)*
Sasa itakukuta Umefanya kazi gani ya Mungu❓ Tangu umeokolewa hutaki kujihusisha na kuwaleta watu kwa Yesu unadhani kazi hiyo ni ya Mchungaji wako au wainjilisti fulani❓ Unategemea kwenda kufanya kazi ya Mungu kanisani bali unachukuliwa na shughuli za dunia hii‼ .Itakushangaza Yesu atarudi atakuacha Ukiwaza kufanya mambo mengi ya kidunia bila kuwaza na kufanya kazi ya Mungu
Au Je itakukuta upo Safi kwenye maisha ya Utakatifu au Unachanganya masomo tu(Vuguvugu)❓ Je itakukuta unaliishi Neno hili hili❓ Maana ni Kanisa Takatifu tu ndiolitakalonyakuliwa *WAEFESO 5:25-27*
Ndugu yangu wewe ndio unayafahamu Maisha yako ya sirini,Ni kweli inawezekana unasali kanisani na unafanya hata huduma lakini maisha unayoishi unayajua sio ya usafi‼ Maisha yako yamejaa unafki,Unafanya dhambi sirini kwa makusudi eti unasema unatubu kimya kimya‼ Ndio maana maisha yako yapo vile vile hauoni tena ile furaha ya wokovu,Amani imepotea kabisa wala hufurahii Neno kama Mwanzo,Unaenda kanisani kama desturi na mazoea‼ Na Kwambia ndugu yangu hivyo ulivyo unaenda Motoni kama hujashtuka Ukaamua Kugeuka Leo na kuanza Upya Yesu anakuja kutunyakua ila wewe utaachwa kama utaendelea na maisha haya uliyo nayo ambayo umeshayazoe
Ndugu yangu na wewe ambaye unasoma Ujumbe huu ambaye bado hujaokolewa au unajiita umeokolewa ila hauna badiliko la kweli la maisha,Kila siku unatubu ila upo vile vile,Unajikuta lile usilopenda kulufanya ndilo unalifanya na unalopenda kulifanya ndio hulifanyi‼Yaamkini unatamani Kumpendeza Mungu ila unashindwa unajikuta unaendelea katika dhambi‼ Unajifahamu wewe ni Mwenye dhambi wala unafki ndani yako,huu si wakati wa kujihesabia haki kwa dini zetu eti mimi dini Fulani,Yesu haji kunyakua dhehebu fulani au dini fulani bali anakuja kulinyakua kanisa takatifu❓ Je wewe ni Mtakatifu❓Huu ndio wakati wa Kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha nawe utapewa uwezo wa kushinda dhambi na kusamehewa dhambi zako zote na utakuwa sehemu ya watakaonyakuliwa
Je Wewe nawe ni Miongoni mwa wale waliokuwa wanampenda Mungu hapo mwanzo ila ilifika siku wakaanguka na kuacha wokovu na sasa upo mbali,unaishi maisha kama mtu asiyemjua Mungu❓ Sasa kwa somo hili Mungu amelileta kwako ili nawe usiachwe!Wewe ni mteule wa Mungu!Ni kweli shetani atataka kuwapoteza hata yamkini walio wateule ila hataweza kwakuwa watu kama ninyi ni wepesi kuisikia sauti ya Mchungaji wenu Yesu Kristo anapowaita.Kwa Ujumbe huu Mungu anakuita urudi kundini,Utubu nae atakupokea nawe utakuwa miongoni mwa watakaonyakuliwa muda mfupi Yesu akija‼ Ebu kumbuka ulipoanguka ukatubu,ukumbuke upendo wako wa mwanzo
▶Hivyo huu si wakati wa kuchanganya masomo,Lazima ujue viashiria hivi vinatupa kujua muda uliopo mbele yetu ni mfupi sana hatujui siku wala saa ila hatuna muda mrefu,Kinachowezekana kufanyika leo kisingoje kesho hivyo ikiwa unahitaji Msaada wowote Kati ya mambo niliyo yataja Ikiwa hujaokoka na unahitaji Uwezo huo wa kushinda dhambi na kukoka basi utawasiliana nami ,Vivyo hivyo ikiwa ulirudi nyuma na kuacha wokovu vile vile unaweza kuwasiliana nami kwa ushauri zaidi na maombezi ili tumalize safari kwa nguvu maana Mungu anaangalia umaliziaji si uanzaji
▶ Ikiwa Umeokolewa hakikisha unatafuta kanisa linalohubiri wokovu na kufundisha mafundisho ya utakatifu na wokovu kama hivi iki uzidi kuukulia wokovu na ujitambukishe hapo Kuwa umeokoka ila kama utahitaji Ushauri pia utawasiliana kwa namba zangu hapa chini
Mpaka kufikia hapa tumefikia Mwisho wa Mfululizo wetu wa masomo yanayohusiana na kutambukiwa kwa Yerusalem kama Makao makuu ya Israel,Natumai umejifunza Mengi mpaka kufikia hapa basi usiache kushare na kuwasaidia wengine ndani na nje ya kanisa ili nao wawe miongoni mwa watu watakaonyakuliwa siku ike Yesu akiwwa Mawinguni.Mungu akubariki kwa kufuatilia na ikiwa una swali au ushauri au lolote usisite kuwasiliana nami
*♨
Kwa mawasiliano zaidi,Ushauri au Maswali*
* Na: Shujaa Charles Mwaisemba*
*0712054498/0759420202*
www.facebook.com/charles.mwaisemba?__nodl
_stmwaisembac@gmail.com_