Juuko Murshid haelewani na Benchi la Ufundi hasa Kocha Mkuu Joseph Omoga hivyo hana raha Kikosini na alichokifanya baada ya kuligundua hilo ni kumlazimisha Wakala wake amtafutie Timu ili Mkataba wake wa Simba SC ambao hata hivyo umekaribia kufikia mwisho ukifika tu awe free agent / player na aende zake huko ' Ng'ambo ' kujaribu bahati yake.
Kuhusu Beki Novatus Lufunga nadhani wengi wenu ni Mashabiki tu wa Mpira na siyo Wadau wa Mpira na hili ndilo limekuwa tatizo kubwa la Wapenda mpira wengi wa Tanzania.
Leo mnasema kuwa Beki Novatus Lufunga ni mbovu lakini hapo hapo mmesahau jinsi alivyoweza kucheza vizuri mechi karibia 10 za mzunguko wa Kwanza na ambazo kwa bahati nzuri Simba SC yetu ilishinda.
Kupwaya kwa Mchezaji kunatokana na mambo mengi ya ndani na hata nje ya Uwanja halafu kumbukeni kukosea kwa Mchezaji yoyote wa mpira ni kitu cha kawaida na ndiyo mnaambiwa kuwa mpira ni mchezo wa makosa.
Leo mnasema Novatus Lufunga anafungisha au anaharibu mbona juzi wakati Beki wetu Method Mwanjale alipofungisha tena ' Kizembe ' mno hadi Mshambuliji John Boko ' Adebayor ' akatulaza mapema wana Simba SC dhidi ya Azam FC hatukulalamika?
Jaribuni kuwa fair na msitawaliwe tu na chuki na mlivyo Wanafiki ni sisi sisi hawa hawa Mashabiki wa Simba kuna wakati tulikuwa ' tukimtusi ' na ' kumdhihaki Juuko Murshid lakini cha ajabu leo tena tumebadilika.
Nijuavyo Mimi ni kwamba Mabeki wote wa Simba SC ni wazuri na hawapishani sana Kiubora hivyo yoyote atakayepangwa atatekeleza majukumu yake halafu tujifunze kuheshimu Benchi la Ufundi hasa Kocha Mkuu kwani huo ndiyo Ueledi wenyewe halafu tujifunze vizuri mpira itusaidie kuwa Wachambuzi wazuri na wenye Tija.