Huo ni ugaidi, si msingi wa jihadi, kujitoa muhanga ni kosa, kuua mtu asiye na hatiani kosa. Kufata dini kwa mihemko bila fikra huru lazima upotoke sehemu.
Lazima tu some dini.. Na hili ndilo la kwanza kwa mtume, alikazaniwa asome,
Vita ya kwanza mtume alipigana baada ya kuhama makkah ambao walikua wanakataza kuabudu, wanateswa, akahamia madina alikopata hifadhi, watu wa makkah hawakuridhika, wakawa wanawavizia njiani, wanapora misafara, choko choko haziishi, ndio mtume kuzichapa, sababu ya uonevu kuzidi.
Sasa wewe mtu unaswali kwa uhuru, unafanya kila jambo, jihadi ya nini.. Unakuta mtu wanakimbilia jihadi ila hata swala ambayo ndio nguzo kuu ya uislamu haifanyi... Mtu anakua brainwashed anapigana jihadi kumbe mzinifu, mzurumati.. Huu sio uislamu.
Enzi za mtume(nazungumzia himaya yake) kulikuwa na mayahudi, manaswara(wakristo) je aliwachinja, au waliishi kwa amani mradi tu hawavunji sheria za pale?
Kama mayahudi na manaswara ni wabaya mbona kulikuwepo sheria(ruhusa) kuwaoa hao watu wa kitabu(ahlul kitabu) mtu mbaya utapewa ruhusa umuoe.
Jihadi kubwa kabisa iliyobaki ni mtu na nafsi yake, labda kwa wale wanaoteseka na kunyanyaswa, hawa wana haki ya kupigana, kujitetea.