Mkuu Mwiba, shida hapa ni umdebwedo wa Wazanzibari, wote wanataka kuwa viongozi na wale biriani ya kuku kila siku bila kufanyakazi! Unajua mtumwa wa jana akipata, ni kufuru tupu!
Huu ni ushirikiano wa ndovu (tembo) na panya! Sasa panya anadai mlo sawa na ndovu pamoja na kwamba mchango wake ni insignificant kwa maslahi ya ndovu! Akina Mwiba, mtapasuka msamba!
Ukweli ndio huo umishaelezwa ,sasa nyinyi endeleeni kuweka pamba masikioni mkiendela kubeza,kikao cha London ndio hicho kimeshapita,halafu wewe unaebeza mambo kufanyika London hivi umesahau hata yule mjanja mmoja alichukua chake mapema kule London ,yaani mna sahau za halaka sana ,siwashangai ,na hii kupasuka msamba sio WaZanzibar watakao pasuka bali hawa wanaowapigia kelele mafisadi maana hakuna la maana hata moja lililofanywa kama ni kina Lowasa ,jamani wao ndio wa mwanzo mbona hata hawana habari na hawa wengine si tumeshaona wapo uraiani kesho na kesho kutwa wanakuwa huru na fedha waliyokwiba ndio wataila bila kificho.
Kwani mnafikiri Zanzibar hakuna mafisadi ? Wapo wengi tu na fedha inaliwa ,kwani wakubwa wengi wamefungua mahoteli ya kitalii ya kisasa ,fedha wamepata wapi ?Lakini huu sio wakati wa kuwakurupusha ,wakati ukifika wataitwa kwa upole kabisa wajieleze na si kwa mahoteli yao bali kwa mahesabu yaserikali ambayo yatafanyiwa utafiti wa kina kabisa.
Tatizo ambalo WaTanganyika mnakumbana nalo ni kuwakurupusha hawa mafisadi wakati upinzani wenyewe haupo katika msimamo uliojengeka,yaani bado upinzani kwa Bara haujawateka wananchi wa kuaminika ambao wameshabwaga manyanga ya kuwa na CCM tofauti na Zanzibar ambako ukiwaamsha watu usiku kwenda kupiga kura basi CCM haishindi hata kwa robo ya kura na huo ndio ukweli ambao naamini kabisa kila mmoja wetu analijua hilo.
Uwajengee utakachowajengea Zanzibar hawaipigii kura CCM kwani wananchi wake walio wengi sana wameshachoka na utawala wa CCM,hilo lipo wazi na mtu anaeweza kufanya utafiti wa kweli na aende sio utafiti huu wa akina Nipashe,wengi wa hao CCM mnaowaona ni wabeba kadi tu kwa maslahi yao binafsi lakini ukienda kwenye kura anajua wapi pa kuipeleka kura yake japo ana uhakika kuwa majeshi na polisi wakisaidiwa na vyombo vya usalama vitabadilisha matorokeo lakini haipi kura CCM hata siku moja.
Kikwete ,Karume ,Pinda,Shein na wengineo wanalijua hilo kuwa CCM Zanzibar hawana ushindi ndio hapo alipowambia wananchi na wabunge wapinzani wachague watakapo lakini upinzani hautashika madaraka kwa karibu au hawatopata kuongoza kabisa.
Na wao wanaambiwa wajenge maendeleo,wapeleke umeme wafanye kila wanaloliona jema lakini CCM haitoshinda kwenye uchaguzi wowote,sasa hao ni wananchi ambao wanasema kwa uwazi kabisa,utawala wa CCM basi,miaka walioka madarakani imetosha waondoke.
Na wewe KWAMINCHI unajua unachokisema au unarapu tu na kungoja kutiliwa mziki ? Katika hati ya Muungano hakuna TANZANIA ipo Tanganyika na Zanzibar tu,sasa kujidai kuwa mumeitumbukiza Tanganyika ndani ya Tanzania huo ni wizi ,tena wizi wa kiini macho,ndipo pale mnapoambiwa kuwa kinachopewa serikali ya Muungano kigaiwe nusu kwa nusu hakuna huyu mdogo au huyu mkubwa,najua mtasema kuna mambo ya Muungano na yasio ya Muungano,na haya yasio ya Muungano hayamo katika Muungano haya ni ya Zanzibar tu, yaliomo kwenye Muungano hayo ni ya Zanzibar na Tanganyika,lakini ninyi mmeyaondoa yale ya Muungano na kuyafanya hayawahusu WaZanzibari hilo ni kosa !!! Maana kama hayawahusu WaZanzibari yatamuhusu nani ? Waziri wa Kilimo wa Tanzania au sio huyu anatakiwa awe na data za Zanzibar pia na akipewa matrector 50 ajue 25 yanakwenda Zanzibar lakini sivyo anasema Zanzibar wana wizara yao ya kilimo sasa hiyo ya Muungano ilikuwaje ikaitwa ya Muungano ,Muungano gani huo,au utanipeleka kwenye hati ya Muungano ?
Ndipo mkaambiwa kuwa Tanganyika mumejiingiza kwenye serikali ya Muungano na kujiita Tanzania ili kuiba ni wezi,na mnaendelea kuiba mpaka pale Tanganyika itakapopatikana hivyo fedha mnayopata na kupokea mishahara na kugawana mitambo na fedha za misaada zinazopata wizara za serikali mnakula na kulisha watoto wenu fedha ya haramu kwani kiasi cha fedha hizo ni za Zanzibar na Tanganyika ,kama umesoma hiyo attachment uneweza kuona namna wizi ulivyofanyika,ulaghai ulivyofanyika na barua za kutekeleza ili kuwepo na dhulma na fedha iliyoibiwa na BOT ni wizi tu hakuna jingine Serikali ya Tanganyika imejivalisha koti la Muungano na kuiba mapato ya Muungano kwa njia za hadaa na maneno mengi kama si wizi ni kitu gani,Muungano huu ni wa nchi mbili Nchi moja imejichomeka wapi ?Nani aliwapa ruhusa ya kujichomeka huko kama si kutaka kuiba ni kitu gani , ,wizmtwup !! Ni lazima iwepo Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanibar ya Zanzibar ipo ya Tanganyika iko wapi,tuamini kwamba haipo kwa misingi gani ? Mabadiliko gani yalioifuta Tanganyika ? Kama huku kujichomeka si kwa hila za kuiba kinachoingia kwenye Muungano ni nini ? Ni wizi tu hakuna jingine sasa wizi unafanyika kwenye Serikali ya Muungano hivi unafikiri Zanzibar haiathiriki na wizi huu ?
Muungano umechezewa na umevurugwa lakini hatukumsikia Kikwete akiwatisha wanaovuruga Muungano na badala yake amewatisha wanaotishia kuvuruga Mapinduzi ,hivyo huu Muungano kwa hapa ulipofikia si Muungano bali ni wizi ,wizi tu hakuna jingine ,kwani Zanzibar wakipiga mahesabu kama mnavyopiga nyie kuhusia na EPA na menginetele kinachopatikana ni wizi ,Serikali ya Zanzibar inaibiwa katika Muungano uliokuwepo ,fedha za Zanzibar zinazopotea zingeweza kuikwamua Zanzibar katika matatizo inayoyakabili, lakini serikali ya Tanganyika iliyojikita ndani ya Muungano inaiba fedha hiyo kwa maendeleo ya upande mmoja. Badala ya Zanzibar kuwa na Muungano na Tanganyika sasa imekuwa na Muungano na wezi unafikiri nani atakubali ,kila kitu kina mwisho kama mlivyodhamiria kuwafikisha mafisadi katika ulingo na kuwaweka kona ndivyo hivyohivyo Serikali fisadi ya Tanganyika ndani ya Tanzania itakavyofikishwa kwenye mahakama za kimataifa ,kesi ipo mbioni kufikishwa kunako husika.
Na na shangaa wale walioidai Tanganyika wakati ule wapo wapi au ndio tuamini kuwa wamekatiwa chao na kuonjeshwa fedhas za wizi zinazopatikana kwa kuibia Zanzibar ? Wapo wapi kama nawao walikuwa sio wezi waliokuwa hawapati mgawo ?