Juma Mgunda usikubali kuwa kocha msaidizi , Uwezo wako ni mkubwa , tafuta timu uifundishe

Tatizo kocha hatafuti timu, bali anatafutwa. Hebu mshauri aende timu gani?
 

Ushauri wa wabongo bwana dah

Amekaa kwenye timu za chini kwa miaka mingapi?

Why haukumshauri wakati ametolewa cost ?
 
We si ndio ulimponda kuwa hana vyeti kipindi cha nyuma
 
Kaze ana leseni ya uefa pro. Lakini ni msaidizi wa Nabi. Mgunda ana caf A ya mwendo kasi (wiki moja karume stadium). Aende kufundisha simba queens
 
Kaze ana leseni ya uefa pro. Lakini ni msaidizi wa Nabi. Mgunda ana caf A ya mwendo kasi (wiki moja karume stadium). Aende kufundisha simba queens
Leseni ni kigezo cha ajira lakini achievement ndio criteria ya msingi huwezi kwenda kua msaidizi kwa mtu unae lingana nae au unamzidi utajifunza nini?

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Mshahara wa kocha msaidizi Simba au Yanga ni mkubwa kuliko kocha mkuu timu kama Coastal, Mtibwa, Mbeya City, Geita nk. Ndiyo maana Cedric Kaze yupo Yanga wakati ni level za kina Nabi
 
Ni kweli ana uwezo na CV kubwa, maana timu zote alizofundisha hazijawahi kukosa kombe au kuwa nje ya tatu bora kwenye ligi. Endelea kumshauri atafute timu nyingine.
 
Mbona nafasi yake Coastal Union ipo tu akitaka!! Lakini je Coastal Union wanamlipa Tsh ngapi kwa mwezi kama Kocha Mkuu na SSC wanamlipa ngapi kama Kocha Msaidizi? Kufundisha timu kwa ajili ya sifa kuwa wewe ni Koacha Mkuu huku huna hela mfukoni ni upimbi
 
Umemshauri kama vile Mgunda hajawahi kuongoza timu kama Kocha Mkuu kabla ya Simba.

Vyovyote itakavyokuwa sioni kama hata kama ana cha kupoteza, labda naye atangulize kiburi tu lakini kwangu kama hawatambughudhi kubaki hapo Simba kwa walau hata mwaka mmoja ni CV tosha kuliko kupata kazi ya kuifundisha Ruvu shooting au Dodoma Jiji.

Yeye ajichukulie kama vile yupo field...kufanya kazi na Mtu ambaye ameshazunguka Mataifa tofauti na kupata mafanikio anacho kikubwa cha kujifunza.

Ushauri wangu kwake "za kuambiwa achanganye na zake".
 
Simba inamlipa bei gani ? au mnababaika na jina tu ? hawa makocha wazawa wanakopwa ni balaa
 
huyu kocha mpya alipwe mshahara sawa na aliokuwa analipwa Mgunda siyo apewe mshahara mkubwa kwa kuwa yeye ni mzungu,tumeshakubaliana watanzania walipwe sawa na wageni,Fei Toto ametufungua macho sana!
 
Kinacho angaliwa ni pesa sio CV
 
Majungu si mtaji kuwa utatajirika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…