Juma Nature:Singeli ni muziki wa kihuni.

Wanaoiponda singeli ni wale wazee wote ambao ujana ushawapitia kando... Tuachen tuburudikr ki uswaz uswaz
 
Singeli ni mziki wa kiuni sawa nimekubali ila wauni wapo tangia yeye hajazaliwa na uho mziki utadumu kw kuwa wauni bado wanaongezeka na ndo miziki yao kitaa kila kukicha hainaga ushemeji tunakulaga
 
Mi mwenyewe huwa nahisi singeli ni upepo tuu utavuma na kuisha, tena imepata umaarufu kwa kuwa ilipigiwa promo na Efm, sasa na mawingu wakaidakia juu juu kwa kasi hawajui hata wanaipeleka wapi.
Singeli ina maisha mafupi kwa sasa
mimi huwa naushangaa sana, huwa siuelewagi kabisa, wenyewe wanadai wanataka kuupeleka next level ETI anga za kimataifa, yaani ni muziki wa mpito tuu kaama mayai ya kware na sifa zake yalipopotelea haijulikani.
 
Umeipa hadhi yake jf, watu ambao hawajui fasihi ndio wanauponda mziki huu. Kwa vile una hadhira yake utadumu... Kazikazikazi sholo mwamba anafanya Prof jay anafanyakazi, nawe jitume ufanye kazi....cheza kimabawa baharia wangu
 
Ananifurahisha na sura yake ya kitoto Japo ya kibangi, kwa hiyo ndyo kusema wakija wasanii studio kwenye Studio yake wakataka awarekodie singeri atawafukuza, hivi kwa week anakunja ngapi kwa mwezi je? Na bado yupo na mke wake yule wa nmb, vip Sinta kipindi kile aliporwa na nani? Wasanii legends msitake kick muziki ni ubunifu na kwenda na wakati wapeni wadogo zenu moyo, kuna kupanda na kushuka kwenye game, mbaya ni kuporomoka kama ilivyomtokea Mr Nice, wekeni akiba na kuwekeza mnavyokuwa mpo juu kimziki
 
anasahahu YEYE NDO ALIANZA NA HAKUNA KULALA!
hilo moja,
MCHIRIKU ULIKUFA LINI?
MNANDA JE?
of all the pipo JUMA NATURE wa temeke kujiona huu muziki sio karba yake?
 
mkuu, singeli ni jina la mtu, sio kama ulivyoelezea wewe, huyo mtu alikua anapenda sana kucheza hiyo tunayoiita singeli sasa hivi, alikua anafanya shows na kina sholo mwamba na man fongo( za kwenye vigodoro kipindi hicho kabla hawajapata majina kama waliyokua nayo sasa hivi) tuseme alikua mchezaji wao,sasa kwenye kuimba walikua wanamtaja sana 'kumpaisha' . kama "sijaona singeli" shika ukuta cheza singeli' sasa kutajwa tanjwa kwake sana ndo watu wakaanza kuuita huu mziki singeli.[emoji4]
 
Sio chura tena ni kifo cha mende .Kama Una geto onyesha funguo juu .
Hii mistari kuna uhuni hapo
 
Tatizo lingine lipo kwa mtu anaye uita mziki fulani ni wa kiuni yeye mwenyewe ni muhuni... sasa sijui huo muziki na yeye nani ana mshinda mwenzie?
 
Duh sasa tumwamini nani
 
Singeli itakufa kama mchiriku ,mduara,ngoma za daku na kigodoro.

Sioni kama utaishi huo mziki

Ni kama mmea uliota kwenye mchanga
Huo mchiriku unaoungelea, mwezi uliopita watu wMeperform white house USA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…