Juma Njemba: Sangoma aliyeishi maisha ya peponi akiwa duniani

Juma Njemba: Sangoma aliyeishi maisha ya peponi akiwa duniani

Kwa mtindo wako nacheka. Maana ili uelewe lazima uanze kusoma komenti yangu ya kwanza mpaka hii ninayoandika. Ili dhana zako zirekebike.

Kimantiki unaonekana unaamini kabla ya kuhoji waswahili wanasema kukubali kibubusa. Maana Huna na hautakuwa nalo la kumhoji mzee kachumvi. Ulishaamini sasa unapanga hoja zako kutoka kwenye chanzo ulichoamini kibubusa kwa kuhoji anaekipinga chanzo chako. Mithili ya wakili.

Baki hapo. Wajibu wangu nimeutekeleza.

Wajibu wako kama member wa familia yake kikweli umeutekeleza vyema sana, na popote alipo anaona hilo kwa namna ulivyo jitahdi kumtetea! Hata mimi ningefanya kama wewe, katika kumtetea mzazi wangu japo umeshindwa kijificha wewe ni nani wake, ningefanya same as you!

Hapo juu ya comment yako, yupo member mwingne amakuja kutoa ushuhuda kuwa, kipindi kinatangazwa kifo cha huyu mzee, misikiti mingi au karibu yote huko watu walishangilia.....kauli inayo endana na mtoa mada!
Baadhi ya maswali ulioshindwa kutufafanulia, ni kuwa inakuwaje malaika au mtakatifu wa aina yake akaogopwa kiasi hicho? Kwanini watu walishangilia? Kuna anaye shangilia kifo cha mtu aliye mwema na alie msaada kwa jamii au the opposite?

Kabla hujamaliza, ningependa uiandike tena tarehe yake aliokufa ili ikae kwnye rekodi humu mkuu!
 
Kuanzia katikati ya miaka ya themanini hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000 huko mkoani Kigoma aliishi " fundi " mmoja aliye julikana kwa jina la Juma Njemba.

Juma Njemba alikuwa MTU hatari sana katika masuala ya ulozi na alijikita zaidi katika kazi ya kuua watu kwa uchawi.

Sifa za Juma Njemba zilienea katika mji wa kigoma na nchi jirani za Kongo, Burundi na Rwanda.

Mamia ya watu kutoka sehemu mbalimbali walifurika kilingeni kwa Juma Njemba kwa ajili ya kazi moja tu ambayo ni kuwaua adui zao kwa kutumia uchawi wa Juma Njemba.

Kazi hii ya kuua watu kwa uchawi ilimtajirisha sana bwana huyu.

Kwa zaidi ya miaka ishirini aliyo Fanya kazi hii, Juma Njemba anakadiriwa kuwa amewauwa kichawi takribani watu elfu mbili na ushee ambao ni sawa na wastani wa karibu watu mia kwa mwaka

Juma Njemba alioa wanawake wengi sana .Anakadiriwa kuwa alioa zaidi ya wanawake 200 huku wengi kati yao akiwa anawaoa na kuwaacha na aliwaacha kwa sababu ndogo sana.

Kwa mfano akiwa anakula chakula halafu kikawa kimezidi chumv, au chai ikapungua au Kuzidi sukari au akatafuna jiwe kwenye wali basi mwanamke aliyepika chakula hicho atapewa talaka tatu papo hapo na wataliki wake wote walikuwa wanaishia kufa katika mazingira ya kutatanisha baada ya muda mfupi na walio bahatika kuishi basi waliishia kuwa vichaa au kuugua maradhi mazito kama vile kiharusi nakadhalika.

KATIKA HILO SABABABU YAKE ILIKUWA " WAKE ZANGU KWA MAISHA NINAYO ISHI MIMI SIWEZI KWENDA PEPONI..PEPO YANGU NI HAPA HAPA DUNIANI ..PEPONI HAKUNA WALI WENYE MCHANGA WALA ULIOZIDI CHUMVI..SITAKI KUPATA TABU YA AINA YOYOTE ILE HAPA DUNIANI NA YEYOTE ATAKAE NISABABISHIA TABU YA AINA YOYOTE ILE BASI NITAMFUTILIA MBALI..."

Ukiachilia mbali mke wake wa kwanza na wa pili ambao aliwaoa wakati wa ujana wake kabla hajapata hiyo ilmu ya kuua watu kwa uchawi wake zake wote alikuwa anawaoa wakiwa bikira na alikuwa akiamini.wakeze hao walikuwa ni ma hurulain wake wa hapa DUNIANI.

Akimpenda binti yako basi anatuma tu ujumbe kuwa siku fulani atakuwa mgeni wako ambapo atakuja kumposa binti yako na hakuna mzazi ambae alikataa kumuozesha bintiye kwa Juma Njemba.Walio thubutu kufanya hivyo walikufa wao au binti zao au wote kwa pamoja..

MTU huyu aliogopwa kama Mungu..Wageni walio Tembelea katika kata aliyo ishi kwa sababu mbalimbali walikuwa wanaenda kuripoti na zawadi kwa Juma Njemba na wakati wa kuondoka walienda kumuaga kwa heshima zote.

Siku moja moja.alikuwa anapenda kuhemea soko kuu la pale Ujiji Kigoma.

Wafanyabiashara wa sokoni hapo walikuwa wakimuona walikuwa wakijipendekeza kwa kumuomba wampe bidhaa zao bure.

"Baba pitia hapa dukani kwangu uchukue walau kilo kumi za nyama baba ..Hii ni swadaka yangu kwako "

" Baba ukitoka buchani upitie hapa kilo 20 za mchele bill itakuwa kwangu" .Hayo ni maneno ya baadhi ya wafanya biashara wakijipendekeza kwa Juma Njemba.

Hata hivyo Juma Njemba alikuwa akikataa ofa hizo za nidhamu ya uwoga kwa kuwaambia kwamba yeye ana uwezo kuliko wao.

Ilikuwa ukimdhulumu MTU basi ataenda kulalamika kwa Juma Njemba halafu Juma Njemba atatuma ujumbe wa kukuita na ukifika atakwambia ulimpe deni lake.

Juma Njemba alifariki mwaka 2001. Waliokuwa NAE karibu wakati wa kifo chake wanasema kilikuwa ni kifo cha mateso makubwa sana..

Watu wa Kigoma waliposikia Juma Njemba amefariki walifanya sherehe kubwa sana.

Juma Njemba alifanya vituko na matukio Mengi sana ya kichawi ..Nikipata nafasi nitakuwa natupia kimoja baada ya Kingine ili watu waweze kujua
Tunasubili
 
Juma Njemba alikua ni zaidi ya mchawi na sidhani km kuna kiumbe wa level yake kwass hapa Tz,,tukiwa wadogo tulikua tunapita nje ya nyumba yake kwa kukimbia kwa hofu yake tu.

Tukiwa shule enzi hizo mtu akikuibia hata kalamu unampiga beat naenda kwa Juma Njemba anarudisha faster.

Na siku alokufa msiba wake ulitangazwa baadhi ya misikiti kgm ujiji kiukweli watu walifurahi baada ya kuhuzunika.

In short Juma Njemba alikua ni zaidi ya Juma Njemba
Hofu ya Simba ni kubwa na ya kutisha kuliko Simba mwenyewe..

Aghalabu, habari za wachawi zilituogopesha kuliko uhalisia wa mchawi mwenyewe alivyo. Mambo mengi tunayakuza pasipo na ushahidi.
 
Juma njemba ni kweli nami namfahamu , ila alikuwa haonyeshi ukatili , nachojua uganga alikuwa ana ufanya sana, sifa kubwa ya juma njemba ni uganga . mtu hatari ni yule mzee wa gungu baba yake na shuhuli ,,, maana mzee aliogopewa sana . ujiji inajulikana kwa uganga wa kiislamu zaidi .
 
Mara siku moja akaja mzee wa heshima zake kapigilia kanzu na kofia ktk meza ya mama mmoja aliyekuwa akijishugulisha na kuuza samaki soko kubwa Ujiji. Kisha yule mzee akauliza kwa kumtaja jina la yule muuza samaki: wewe ndiye fulani (jina la muuzaji). Yule mama akaitikia ndiyo mimi baba. Yule mzee akaanza kulalamika huku akiondoka akisema watu wengine bwana huyu (fulani) sasa ana nini masikini, anatafuta riziki yake hapa. Yule muuza samaki akabaki anashangaa wakati yule mzee anaondoka huku akimlaumu aliyemsotea huyo mama.

Ndiyo watu wengine waliokuwa wakifanya biashara hapo wakamuuliza yule mama; unamjua huyo mzee? Yule mama akajibu simfahamu. Akaambiwa huyo ndiye JUMA NJEMBA. Yule mama akashikwa na khofu kubwa juu ya maisha yake ingawa mzee alikuwa tayari kapuuza kazi aliyokuwa kapewa.

Inaonekana kuna mtu alimfuata Juma Njemba ili ammalize huyo muuza samaki.
 
Wajibu wako kama member wa familia yake kikweli umeutekeleza vyema sana, na popote alipo anaona hilo kwa namna ulivyo jitahdi kumtetea! Hata mimi ningefanya kama wewe, katika kumtetea mzazi wangu japo umeshindwa kijificha wewe ni nani wake, ningefanya same as you!

Hapo juu ya comment yako, yupo member mwingne amakuja kutoa ushuhuda kuwa, kipindi kinatangazwa kifo cha huyu mzee, misikiti mingi au karibu yote huko watu walishangilia.....kauli inayo endana na mtoa mada!
Baadhi ya maswali ulioshindwa kutufafanulia, ni kuwa inakuwaje malaika au mtakatifu wa aina yake akaogopwa kiasi hicho? Kwanini watu walishangilia? Kuna anaye shangilia kifo cha mtu aliye mwema na alie msaada kwa jamii au the opposite?

Kabla hujamaliza, ningependa uiandike tena tarehe yake aliokufa ili ikae kwnye rekodi humu mkuu!
Third hand information ni hatari ukitumia Kama rejea kwa jambo usilolijua

misikiti ilishangilia

Ujiji si kijiji hata useme misikiti yote ilishangilia haya muulize
misikiti gani Ilishangilia

Unajua maana ya kushangilia?
 
Na hata aliesema wapo waliosoma, pia amedanganya tarehe yake na siku yake ya kufa!
Wake Mia 2
Aliua watu 2000
Aliishi Kama mungu
Aliishi Kama yuko peponi

Wakati zake akiichana nao hufa
Wakati mke wa Mzee njemba yu hai mpaka Leo
Kwako hizi si tatizo Kuliko Aliyekose utajo wa siku
 
Nakumbuka kina joti na mpoki ktk kipindi chao cha ze comed wakati bado wa eatv
Waliwahi kwenda kigoma na joti akaigiza kuwatisha wenzake kuwa amuogopi mtu kwani yeye yupo karibu na uyo mzee.
Hii inaonesha kuwa wakazi wa kigoma ujiji waliwaapa history ya huyo ndio maana wakamuigiza.
Huyo mzee inaonesha alikuwa mtu hatari.
Najaribu kuitafuta hicho kipande cha the comedy ktk YouTube kinakataa.
Nikifanikiwa nitakiketa humu
 
True kuna wazee walikuwa magwiji haswaa usipime,wazee wa kutundika koti hewani,
Hii niliambiwa walimfanyia Makamba alipoenda kule as RC..... Kisa akiwaambia waache kukaa kunywa kahawa wajishughulishe na kilimo... Nasikia Makamba akarudi kujiweka sawa, aliporudi tena kigoma akawaita ofisini kwake.. Wakawa wanarusha makoti yao badala yasimame yanaanguka... Ikabidi wasalimu amri waanze kujishughulisha.

Hebu nithibitishieni, ya Kweli Haya????
 
Ni kama Brand flanihivi...Mtu mmoja anajaribu kuiharibu na mtu mwingine anajaribu kuitetea, maana Njemba katumia miaka mingi kuitengeneza Brand yake na Familia yake, anapotokea mtu mmoja akaiharibu lazima moto uwake period!!
 
Back
Top Bottom