Juma Njemba: Sangoma aliyeishi maisha ya peponi akiwa duniani

Juma Njemba: Sangoma aliyeishi maisha ya peponi akiwa duniani

Hii ndo nasikia leo Mwanalugondo alikuwa mke wa Juma Njemba Mwanalugondo alikuwa jirani yetu Igogo Mwanza Ila hajafa 2000 itakuwa 2002,alisifika kwa uchawi tulimuogopa mtaani hakuwa na kazi biashara Ila pesa anazo na kuvaa kanga mpya kila siku kwa mzee Mabruki analeta kupindiwa na mtoto wa Rashid Mwinuka, hii ya kuolewa na Juma ni mpya kwangu sababu bibi yangu Juma alikuwa kama kaka yake na Baba akimuita Juma Njemba mjomba Ila sijawahi kusikia kamuoa Mwanalugondo.
Mjomba maelezo yako ni kielelezo tosha kwamba Juma Njemba alikuwa anatisha .
Maana ana karibia miaka 20 chini ya ardhi lakini bado wamuogopa ..

Nilichoongea sijaongeza chumvi hata kidogo..Juma Njemba hakuwa MTU wa mchezomchezo ..Alikuwa hatari sana na suala la kuoa ameoa wanawake wengi sana wengi walikuwa wanaenda kilingeni kwake kama wateja na alikuwa akivutiwa nao tu basi wanakuwa wakeze..

Mke wa kwanza wa Juma Njemba ninae mfahamu Mimi aliitwa " Mkamiti Mwanalugondo" bibi wa kinyamwezi kutoka Urambo Tabora ambae na yeye alikuwa fundi kama mumewe ..Huyu alifariki akiwa mkoani Mwanza mwanzoni mwa miaka ya elfu mbili.. Huyu Mwanalugondo alikuwa anatoka kwenye familia ya kichawi pia...Yeye na babu yangu kizaa baba angu walizaliwa kijiji kimoja na mwaka mmoja 1918 ambao ndio mwaka aliozaliwa Juma Njemba ..

Alikuwa na wanawake wa Kirundi kibao, wanawake wa kiarabu ndio usiseme ..Mfano pale Nzega na Tabora mjini ana watoto wengi tu ambao amezaa na wanawake wa kiarabu.

Halafu jua kuwa Juma Njemba ni kikongwe rika la kina bibi fisi wa Mwanza..

Wanafunzi wake wengi ni watu wazima kwa sasa na wengi wao wamechuja kabisa wamebakiza uchawi tu wa kuumiza watu ..Nawajua wengi tu akina Athumani Balichako na Ali Zaidi hawa wapo kanda ya ziwa lakini hawana lolote kwa sasa .
 
Mjomba maelezo yako ni kielelezo tosha kwamba Juma Njemba alikuwa anatisha .
Maana ana karibia miaka 20 chini ya ardhi lakini bado wamuogopa ..

Nilichoongea sijaongeza chumvi hata kidogo..Juma Njemba hakuwa MTU wa mchezomchezo ..Alikuwa hatari sana na suala la kuoa ameoa wanawake wengi sana wengi walikuwa wanaenda kilingeni kwake kama wateja na alikuwa akivutiwa nao tu basi wanakuwa wakeze..

Mke wa kwanza wa Juma Njemba ninae mfahamu Mimi aliitwa " Mkamiti Mwanalugondo" bibi wa kinyamwezi kutoka Urambo Tabora ambae na yeye alikuwa fundi kama mumewe ..Huyu alifariki akiwa mkoani Mwanza mwanzoni mwa miaka ya elfu mbili.. Huyu Mwanalugondo alikuwa anatoka kwenye familia ya kichawi pia...Yeye na babu yangu kizaa baba angu walizaliwa kijiji kimoja na mwaka mmoja 1918 ambao ndio mwaka aliozaliwa Juma Njemba ..

Alikuwa na wanawake wa Kirundi kibao, wanawake wa kiarabu ndio usiseme ..Mfano pale Nzega na Tabora mjini ana watoto wengi tu ambao amezaa na wanawake wa kiarabu.

Halafu jua kuwa Juma Njemba ni kikongwe rika la kina bibi fisi wa Mwanza..

Wanafunzi wake wengi ni watu wazima kwa sasa na wengi wao wamechuja kabisa wamebakiza uchawi tu wa kuumiza watu ..Nawajua wengi tu akina Athumani Balichako na Ali Zaidi hawa wapo kanda ya ziwa lakini hawana lolote kwa sasa ...
Balichako umenikumbusha mbali na baiskeli yake alikuwa anatuita mchumba akija nyumbani na madrasa tulisoma nyumbani kwake Kuna kipindi nilienda Mwanza nikaenda kumuona, walikuwa wanasema mchawi Ila sijawahi kuwa na uhakika Ila Mwanalugondo alikuwa hatari kwake ukienda yuko kizani, Ali Zaidi sijawahi kusikia sifa yake ya uchawi ndo na kusikia wewe, bado wapo hai yeye na Balichako Ila Kivuruga kafariki, Sheikh Mambosasa, Ibrahim Chake, juzi kati kafariki Cobra Igogo imeisha.
 
Balichako umenikumbusha mbali na baiskeli yake alikuwa anatuita mchumba akija nyumbani na madrasa tulisoma nyumbani kwake Kuna kipindi nilienda Mwanza nikaenda kumuona, walikuwa wanasema mchawi Ila sijawahi kuwa na uhakika Ila Mwanalugondo alikuwa hatari kwake ukienda yuko kizani, Ali Zaidi sijawahi kusikia sifa yake ya uchawi ndo na kusikia wewe, bado wapo hai yeye na Balichako Ila Kivuruga kafariki, Sheikh Mambosasa, Ibrahim Chake, juzi kati kafariki Cobra Igogo imeisha.
Sheikh Mambosasa amefariki?
 
Ndio hata 40 bado.
Don't tell me that u know what? Nimetembea Tanzania nzima kufanya tafiti kuhusu uchawi nimeenda sehemu zinazo sifika kuhusu uchawi Mwanza nilikuja hadi huko Igogo huyo Sheikh Mambosasa nilifanikiwa kukutana nae si ana binti Yake anaitwa Halima kitu kama hicho? Amefariki lini huyo Mzee? Alinisaidia mambo mengi Sana
 
Don't tell me that u know what? Nimetembea Tanzania nzima kufanya tafiti kuhusu uchawi nimeenda sehemu zinazo sifika kuhusu uchawi Mwanza nilikuja hadi huko Igogo huyo Sheikh Mambosasa nilifanikiwa kukutana nae si ana binti Yake anaitwa Halima kitu kama hicho? Amefariki lini huyo Mzee? Alinisaidia mambo mengi Sana
Yes Halima shombe shombe flani hivi tulisoma wote Madrasa kwa Mwalimu Chake, haya ulimjua Baba yake Kassim Swedi, Mzee Swedi alikuwa noma alitoka ujiji akaja Mwanza jirani na Mwanalugondo alikuwa anapunga majini kufichua mkoba wa uganga.
 
Don't tell me that u know what? Nimetembea Tanzania nzima kufanya tafiti kuhusu uchawi nimeenda sehemu zinazo sifika kuhusu uchawi Mwanza nilikuja hadi huko Igogo huyo Sheikh Mambosasa nilifanikiwa kukutana nae si ana binti Yake anaitwa Halima kitu kama hicho? Amefariki lini huyo Mzee? Alinisaidia mambo mengi Sana
24/12/2024 akazikwa 25/12/2025
 

Attachments

  • Screenshot_20250123-225450_1.jpg
    Screenshot_20250123-225450_1.jpg
    174.7 KB · Views: 2
Don't tell me that u know what? Nimetembea Tanzania nzima kufanya tafiti kuhusu uchawi nimeenda sehemu zinazo sifika kuhusu uchawi Mwanza nilikuja hadi huko Igogo huyo Sheikh Mambosasa nilifanikiwa kukutana nae si ana binti Yake anaitwa Halima kitu kama hicho? Amefariki lini huyo Mzee? Alinisaidia mambo mengi Sana
Umefikia wapi kwenye utafiti wako wa uchawi?..na ubatafuti nini haswa kwenye uchawi?
 
Yes Halima shombe shombe flani hivi tulisoma wote Madrasa kwa Mwalimu Chake, haya ulimjua Baba yake Kassim Swedi, Mzee Swedi alikuwa noma alitoka ujiji akaja Mwanza jirani na Mwanalugondo alikuwa anapunga majini kufichua mkoba wa uganga.
Halima kaolewa?..napenda shombeshombe
 
Nimesoma uzi wa Likud na pia wachangiaji wengine,nazaliwa nakuwa nilikuwa nasikia sifa za Juma Njemba kupitia kwa bibi yangu Maharusi Bint Juma Nyembo mzaliwa wa ujiji wahombo street alikuwa anamuita Juma Njemba kaka alikuwa akisimulia story za uganga wake akisema anauwa kwa wale waloenda kumaliza mtu unachagua aone jua lipi la kuchomoza au kuzama hata baba yangu watu walikuwa wakimkera utasikia wana bahati mjomba wangu Juma Njemba kafariki, ndugu wa uvinza na ujiji walikuwa wanaleta habari zake sasa hasali hafungi anasema yeye wa motoni,sijui kweli sikweli,Ila Baba yangu Mkubwa Juma Kambi alifanyiwa figisu kazini TRC Juma Njemba akamwambia mjomba usijali hicho kiti hatokaa mtu yoyote kila atakae kalia atakufa Babu Mzee Rajab Kapande akakataa hapana shemeji usifanye hivyo,naamini Story ya Likud Ina chumvi Ila Abu Hafizer naona moja ya watu wa karibu anasimama na kauli ya Mtume marehemu hasemwi kwa ubaya hakuwa saint alikuwa mganga wa kazi zote nzuri mbaya ndo maana aliogopwa Allah marehemu na kumswamehe.
 
Even dark of his, umeweka uwongo mwingi sana. Juma Njemba aliowa wake kwa dini ya kiislam, aliishi an wake wanne, akihitilafiana au kufiwa na mke aliongeza mke kwa kuoa mwingine. Hakudhulum mke wa mtu, alichumbia na kukubaliwa akaowa, alipokataliwa posa take hakuoa na hakudhuru mtu.

Pia umeandika kuhusu kuacha na kudhuru wenzi wake aliotalakiana nao, jambo ambalo si la kweli, mke wake wa kwanza akiitwa Bi. mtumwa bint Ali Saad, mwanamke huyu aliishi toka ujana hats kifo na mumewe na hawakujaliwa kupata mtoto.

Mke wake wa pili akiitwa Hawa bint Almas Msano mpaka leo anaishi Sengerema Mwanza amekuwa ajuza kwa umri wake alizaa nae bint aliyeitwa Asha.

Mke wa tatu sikumbuki jina lake lakini alizaa watoto wawili mmoja akiitwa Lwamba na Mwingine Mwamvua. Mwanamke huyu waliachana muda mrefu kwa mke huyu kurejea kwao Urambo ambako kaka yake alikuwa na uchumi hivyo aliamua kuachana na ndoa kuendelea kusimamia uchumi (pengine walikuwa na yao) lakini hakumuuwa wala hakukuwa na madhara, mama huyu kafa mwaka juzi 2016 Tanga Mjini.

Alimuoa pia mama wa kisenegal akazaa bint akiitwa Johari, mama Yule walitengana na hakumdhuru alifariki mwaka 2014 akiwa mtu mzima.

Alimuoa mwanamke mwingine akazaa nae mtoto wa kiume akiitwa Mwinyimbegu yupo mtu huyu pale Kigoma Ujiji na mama yake yu hai na hana madhara.

Alioa mwanamke wa kiha akiitwa Bora bint Maulid mungo mkuyu huyu kazaa nae watoto wanne. Wawili wa kiume wapo Dar Es salaam pale jiran ya Meeda Bar Sinza. Tena wapo na mama yao ambaye aliishi na marehemu mpaka kufa kwake. Na wawili wa kike mmoja ni mwalimu Mwanza na mwingine yupo huko Ujiji kwao.

Hivyo umeweka chumvi ya kutosha.

Lipo suala la kuuwa watu, lipo suala la uchawi nk tote uzushi.

Ila yupo aliandika hapa kuwa zama zile za ufanyaji wa biashara za magendo, mzee Yule alikuwa na ujuzi wa kukupa maandishi katika elimu yake ya kitabu na sio mti wala kizimba wala tunguri wala uchawi Bali ni katika uwezo wa elimu yake ya kitabu, basi utakuwa salama bila kukwaruzana na askari wala kukamatwa kwa Mali yako.

Ni hakika kuwa hakuna aliyekuwa akijipendekeza kwake, Bali aliheshimiwa mno, maana hakuwa akipenda waha na wamanyema kuonewa, maskini kuonewa, wanawake na watoto kuonewa hakupenda.

Siku moja akiwa darasani kwake akisomesha elimu zake, alitokea mama mmoja akamshitakia kuwa mwanafunzi wa huyu mzee akiitwa xxxxxxx Kamo (amekuwa marehemu),alikuwa akimtaka kimapenzi kwa lazima akisema anapata masomo yenye kuburi kubwa za Juma Njemba akikataliwa atamfanyia kisomo na kumdhuru.

Mzee Juma alimuondoa masomoni mtu huyu kwa tuhuma ile akisema elimu yake ni kinga kwa watu dhaifu kutokana na mabavu ya wenye nguvu.

Kesho nitasimulia kiss chake na Mkuu wa Mkoa Kannal Mahhawa aliyeonjeshwa joto la jiwe la elimu ya mzee huyu.

Pia nitasimulia kiss cha mtumishi mwenye dharau kwa wazee alivyoikimbia ofisi kwa kuona Simba.
Hiyo ya mahhawa natamani kuijua maana mmmmh
 
24/12/2024 akazikwa 25/12/2025
Innah Lilahi wa innahlilahi rajiun🙏🙏🙏

Poleni Sana wana Igogo. Huyu shekhe namfahamu sana yeye na watoto wake mmoja anaitwa Mohamed, Halima na Zai kama sikosei.

Nilizunguka Igogo yote kusaka uchawi na wachawi na nilifanya interview na mashekhe karibu wote wa Igogo plus watu maarufu kama akina Shekhe Sambamba hata huyo Kassim Sued pia nilisikia habari zake pia.
 
Yes Halima shombe shombe flani hivi tulisoma wote Madrasa kwa Mwalimu Chake, haya ulimjua Baba yake Kassim Swedi, Mzee Swedi alikuwa noma alitoka ujiji akaja Mwanza jirani na Mwanalugondo alikuwa anapunga majini kufichua mkoba wa uganga.
Kassim Swedi nilisikia habari zake lakini sikufanikiwa kuonana nae ila kwake nilionyeshwa. Kassim Sued alikuwa na Nini?
 
Don't tell me that u know what? Nimetembea Tanzania nzima kufanya tafiti kuhusu uchawi nimeenda sehemu zinazo sifika kuhusu uchawi Mwanza nilikuja hadi huko Igogo huyo Sheikh Mambosasa nilifanikiwa kukutana nae si ana binti Yake anaitwa Halima kitu kama hicho? Amefariki lini huyo Mzee? Alinisaidia mambo mengi Sana
Kuna uhusiano gani Kati ya uchawi na uisilamu maana naona majina ya hao wachawi yana element za uisilamu
 
Back
Top Bottom