Juma Nkamia, kauli yako kuhusu Mecky Mexime haijanifurahisha

Juma Nkamia, kauli yako kuhusu Mecky Mexime haijanifurahisha

Nkamia mburula tu huyu jamaa, mbona wakati akina kaburu na mwenzake Malinzi wanabadilisha kanuni ya kadi 3 za njano kwa mchezaji kuchagua mechi za kucheza mbona hakutia neno!??
 
Kama alitoa kauli hiyo nadhani aliteleza tu na ni vizuri kama ni muungwana akaomba radhi hadharani.
 
Nkamia katoa kauli hiyo baada ya kuulizwa maoni yake juu ya uteuzi wa Mexime.. Sasa maswala ya kadi 3 za njano yanakujaje hapa?.. Na kwani kuna mwandishi alimfuata na kumuuliza, akagoma kutoa mawazo yake.. Au alitakiwa aitishe press conference na kutoa tamko?
 
Ndio maana SA watu wanabomoa masanamu ya wakoloni wabaguzi maana wanavyoendelea kuyaona yanawaongezea uchungu. Huenda na hapa tukatumia mbinu zinazofanana na hizo pale wenye akili watakapoanza kujiuliza nani na nai walipataje uwaziri au nafasi za uongozi wa umma!
Kwani huyo kocha wa Ujerumani ana miaka mingapi mpaka anachukua kombe la dunia!?
 
Kwani kina Di mateo, Andre vila boaz ni watu wazima hao mbona wamefanya wonders......tatizo la kuwapa uwaziri watu wasiokua na mbele wala nyuma wanaishia kuropoka tu kama bata
 
Akihojiwa katika kipindi cha Jambo (TBC 1) cha leo tarehe 5/6/'15, waziri mwenye dhamana ya michezo nchini ametoa maoni yake kuhusu kocha msaidizi wa timu ya taifa, Taifa Stars- Mecy Maxime kuwa hafai kwa sababu bado mdogo, na kama angeulizwa yeye kuhusu kocha msaidizi angependekeza mtu kama Abdalah Kibadeni.

Kwangu mimi, naona hoja yake haina mashiko kwa kuwa kazi ya ukocha si ya kubeba matofali, bali ni ujuzi. Wapo kina Pep Guardiola ni vijana na wanafanya vizuri. Hata hao aliowataja yeye kuwa wanafaa wamekuwa makocha siku nyingi lakini sioni kigezo cha kuwapa timu ya taifa kwa kuwa hakuna jipya walilowahi kufanya hadi kustahili nafasi hiyo.

Namshauri waziri aache kufanya mambo kwa mazoea.

Mbona Na Wewe Ulichokiandika Hapa HAKIJATUFURAHISHA? Na Wewe Nakushauri Uache Kufanya Mambo Kwa Mazoea Na Ki POPOMA.
 
Sasa naanza kumuelewa Boko kwenye ule waraka wake aliposema makocha mbinu za kizamani,marefa na maamuzi ya kizamani,ligi ya mtindo wa kizamani,viongozi ubunifu wa kizamani...hakumalizia moja tu "mashabiki nao wakizamani"...kama ni ukongwe Kingunge anafaa kuwa Raisi wa Tanzania
 
Mhhhhh hapana labda nkamia naye alikuwa kajitoa ufahamu wakati akijibu swali hilo.
 
Basi apewe kingunge hiyo kazi maananadhani anamzidi hata huyo kibadeni....
 
Viongozi wa aina ya Nkamia ni mizigo kwa taifa maana hawajui hata vigezo kwenye vitu vya msingi!
 
Kama inshu ni Ujuzi;
Abdalah King Kibadeni ni kocha ambae yupo kwenye gemu tangu kitambo. Ameanza kufundisha soka mwishoni mwa miaka ya 80 ambapo Maxime alikua chekechea. Katika miaka yote hiyo amefundisha timu za vijana, timu za ligi kuu, timu ya taifa.. na pia anamiliki akademi yake mwenyewe.

Kama inshu ni Mafanikio;
Abdalah King Kibaden Mputa ni kocha pekee mzawa toka Tanzania mwenye mafanikio makubwa katika michuano ya Africa.. kwani aliifikisha fainali Simba Sc katika kombe la Shirikisho mwaka 1993. Amechukua kombe la chalenji jijini mwanza akiwa na timu ya taifa. Hapo sijataja idadi ya makombe ya ligi kuu, klabu bingwa africa mashariki aliyochukua.

Sasa kwa CV hii jamani, unapataje uthubutu wa kumlinganisha huyu "gwiji" Abdalah King Kibaden Mputa na "mwanae" Maxime??? Inabidi ujitoe akili ili ufanye mlinganyo huo.

Ni vyema Maxime alivyopata "shavu" la kuonja ukocha wa timu ya taifa.. ila ni kosa la jinai kusema Maxime ni bora kuliko Abdalah King Kibaden Mputa.

Mpeni Simba
 
Back
Top Bottom